Mchezaji gani aliyefariki ulikuwa unamkubali sana?

Mchezaji gani aliyefariki ulikuwa unamkubali sana?

Namkumbuka saana mshambuliaji hatari wa Gungu Rangers ya kigoma mbaluku kubaza huyu mwamba alifunga Goli 23 kwenye mechi 6 za ligi ya ng'ombe huko kigoma Alifariki mwaka 2008 huko Tanzania military academy (alijiunga na jeshi akafia mafunzoni)
 
Leo tuwakumbuke mafundi wa mpira ambao walikuwa wana uwezo mkubwa sana wakiwa dimbani enzi za uhai wao kabla ya kutangulia mbele ya haki.

Mimi naanza na huyu Said Nassoro Mwamba Kizota. Huyu jamaa mpira aliujua sana ila pia ubabe pia aliumudu mno. Toka anacheza mshambuliaji kisha baadae kurudi kucheza beki.

Enzi anacheza straika mabeki wengi walikuwa wanamuogopa, pia aliporudi kucheza beki, washambuliaji wengi wakawa wanamuogopa. Aliweza kucheza kwa kiwango cha juu sana kwa muda mrefu. Kama hujawahi kumuona enzi za uhai wake, anacheza kama anavyocheza Sergio Ramos.

Alijitengenezea sifa na umaarufu jinsi alivyomudu kumzuia mshambuliaji matata wa miaka hiyo, marehemu Majid Musisi wa Sports Club Villa kwenye klabu bingwa Afrika mashariki pale Kampla mwaka 1993 bila shaka.

Kwako wewe, ni mchezaji gani ulimkubali enzi ya uhai wake?
Lissu
 
Hamis thobias gaga
Ulikuwa kwenye akili yangu mkuu,,

Huyu jamaa hadi sasa sijaona mchezaji wa kitanzania,,
Kiungo wa aina yake..

--Mguu sumaku,,
--Pasi za macho,
--Mpira anahamisha upande mmoja kwenda mwingine.

Enzi zake akikutana na Athuman China wa yanga,,
Burudani kabisa dimbani..
 
Kwa soka la nyumbani ni hawa :
1.Edward Chumila.(Simba)
2.Said Mwamba 'kizota' (Yanga)
3.Hamis Gaga (Simba, Volcano, Yanga,)
4.Ramadhani Lenny (Simba)
5. Willy Mwaijibe (Simba)
6.Athumani Juma Chama (Yanga)
7.Joseph Katuba (Yanga, Simba)
8.Juma Mkambi Jenerali (Yanga)
9. Method Mogella (Simba, Yanga)
10. Seif Hassan Majebella ( Berlin FC, Temeke)
 
Nani anamkumbuka Machepe?mtangazaji wa radio Tz alisema haya pale alipofunga Simba against Yanga"Machepe anaichepea Yanga" ... alikuwa na umri mdogo , kipaji kikubwa lakini ndio hivyo mchezaji huyo aliyekuwa kipenzi Simba akapotea na kufariki mapema.
Duh sikujua kama Machepe ni marehemu.
 
Back
Top Bottom