Mchezaji gani aliyestafu ungependa arudi uwanjani

Wanakwambia Kombe la Dunia la mwaka 1974, katika mechi ya Fainali, Uholanzi dhidi ya Mwenyeji Ujerumani Magharibi, kombinesheni ya Neeskes na Cruyff inawafanya Uholanzi kupata goli pasipo mchezaji yoyote wa Ujerumani kugusa mpira.

Ila Wajerumani wakafanya kitu flani ambacho hata Waholanzi hawakutegemea, Hapa ndipo ule usemi wa " Never underestimate the Germans " ulipokuja. WAJERUMANI wakasawazisha na kupiga la goli la Ushindi na kubeba ndoo yao.

Ila Wadachi hawana bahati kabisa, maana miaka minne baadae walipoteza tena Fainali kwa mwenyeji Argentina lakini safari wakiwa bila staa wao Cruyff ambaye aligoma kwenda kwenye michuano hiyo kutokana na sababu za kisiasa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…