Mchezo Mchafu: Kuna kina mama huwatuma mabinti kuingia vyumba vya wapangaji wa kiume, fumanizi la video hufanyika ni aidha utoe pesa ama unaenda jela

Mchezo Mchafu: Kuna kina mama huwatuma mabinti kuingia vyumba vya wapangaji wa kiume, fumanizi la video hufanyika ni aidha utoe pesa ama unaenda jela

Mtemi Eno

Member
Joined
Jul 10, 2023
Posts
37
Reaction score
148
Kuna mchezo mpya siku hizi kina mama hasa wenye nyumba za kupanga huwa wanawafundisha mabinti kujenga ukaribu na wapangaji wa kiume ili kuingia vyumbani mwao kuangalia tv, kuomba kuwafanyia usafi, kuomba kuingiziwa nyimbo au muvi, n.k. (mbinu kibao) sambamba na kuwafunza mitego ya kuwazuzua kimapenzi. vijana walengwa huwa ni wale wa chini ya miaka 30, wengi bado hawajakomaa vizuri kiutu uzima.

Mabinti hawa wanaotumika kama chambo wengi huwa shule zishawashinda ama watoro waliotukuka, Binti anaweza kuwa na miaka 16 lakini ni mtundu si kidogo, upole wake ni script tu, ashafundishwa akwambie ana miaka 19 akutoe uwoga ila siku ya fumanizi watasema ana miaka 14 na umemlaghai aache kwenda shuleni.

Mpango mzima unakuwa hivi, Kama umekuwa na msimamo hutegeki kimapenzi basi hutumia mbinu zingine kuingia chumbani, mfano binti anakuja kuomba maji ya kumezea panado kichwa kinamuuma, akinywa maji anaomba apumzike nusu saa anaomba apumzike, hapo ndipo mama mwenye nyumba anastua matapeli wenzie wawili watatu waje, wengine wanaleta kabisa mtendaji wa mtaa ama polisi ambao washanogewa na pesa za huu mchezo mchafu.

Wakiingia ndani humo wanarekodi video kwa simu, hupewi hata nafasi ya kujieleza kila mtu anasema umelala na binti mwenye umri chini ya miaka 18, utajitetea kwamba mlikuwa mnacheki tv au alikuwa kapumzika anaumwa lakini haitasaidia, utajitetea alikwambia ana miaka 19 utaoneshwa cheti (hata cha mchongo) kazaliwa 2007 kiufupi hapa upo ndani ya 18 zao!.

Hapo kuchomoka hakuna kiwango maalum, watakukadiria kulingana na hali yako ya uchumi na ufundi wako wa maneno, ila wengi huwa wanachapwa laki 5 hadi 8. Hapo watamalizana kimya kimya, inakuwa siri na ndio maana ni ngumu kukuta habari hizi hadi uwe na ukaribu na wahanga.

kijana hawezi kubaki hio nyumba atahama tu hata kama kabakiza kodi ya miezi minne, muendelezo wa upigaji huu unaendelea kwa wapangaji wapya.

Kwa watu wasio na shida na hela bali kisasi ama kukomoana hutumia mbinu hii kuwatupia vijana jela, kwa wengine binti akiwa mzigo nyumbani hii ndio njia ya ndoa ya mkeka.
 
Kuingiza Watu kwenye nyumba yako msio na uhusiano wowote au mkubwa nayo ni dalili ya kutojitambua.

Yaani MTU aje kuangalia Filamu kwako kwani hakuna mabanda ya TV au Mpira?
Au wewe uende ukaangalie Filamu Kwa jirani tena jinsia tofauti huo kama sio ushupeshupe ni nini?

Wengine kuingia kwenye majumba ya Watu ni ngumu. Halikadhalika ni ngumu Kwa MTU ambaye hatuna uhusiano mkubwa kuingia kwangu.
Ndio maana kuna Hotel, migahawa, Resort, beach, Lodge n.k.
 
Unadhani kuna watu wanaelewa (ga) basi?
Yn hao wamama na mabinti zao wanavyofanya naona ni sahihi kabisa, mana wanafanya kwa mwanaume ambaye hajitambui.

Wanaume mwenye akili timamu hawezi kumuingiza binti wa watu ety kuja kuangalia tv nk.

Na mpaka huyo binti afanye hvy inaonyesha hamna mahusiano nae ya kujuana sasa inakuaje unamleta watu hovyo kwenye nyumba yako.
 
Yn hao wamama na mabinti zao wanavyofanya naona ni sahihi kabisa, mana wanafanya kwa mwanaume ambaye hajitambui.

Wanaume mwenye akili timamu hawezi kumuingiza binti wa watu ety kuja kuangalia tv nk.

Na mpaka huyo binti afanye hvy inaonyesha hamna mahusiano nae ya kujuana sasa inakuaje unamleta watu hovyo kwenye nyumba yako.
#MazoeaYaliyozidiKiasi
 
Wakiingia ndani humo hupewi hata nafasi ya kujieleza kila mtu anasema umelala na binti mwenye umri chini ya miaka 18, utajieleza kwamba mlikuwa mnacheki tu tv, ulikuwa unamfundisha, ila wao wayakomaa umemlaghai binti mdogo
Acha mazoea na under-age.
Hangaika na wakubwa wenzako.
Mtoto chini ya 16 bado ni mtoto, usisingizie kisa kashindikana.
 
Ukigonga hodi mlangoni kwangu sikwambii karibu au ingia,ninakuja mpaka mlangoni nikiwa nimeweka uso wa punda wa dobi huwezi kupata ujasiri wa kuniambia eti unaomba kuingia kwangu kucheki muvi au kunisaidia usafi.
Sasa wewe mwanaume ukiona binti unaanza kujichekesha kama malaya kaona bia lazima upigwe matukio.
 
Ukigonga hodi mlangoni kwangu sikwambii karibu au ingia,ninakuja mpaka mlangoni nikiwa nimeweka uso wa punda wa dobi huwezi kupata ujasiri wa kuniambia eti unaomba kuingia kwangu kucheki muvi au kunisaidia usafi.
Sasa wewe mwanaume ukiona binti unaanza kujichekesha kama malaya kaona bia lazima upigwe matukio.
Hahahah yaani unaleta uswahili wako wa mkoa DSM![emoji23]
 
Siku hizi hata siwapi kazi ke kwa ofisi yangu ,Toka mlinzi ,cleaner mpaka mawakili it's a male zone ,Huwa na avoid instances za kijinga Kama hizi .
Kingine eti msichana anionbe Hela sijui hajala au amepotea au simu ampigie mamake amtumie nauli Huwa sifanyi .
Sitaki mind games nnzaoona siku hizi , usaidizi kwangu umeishia kwa jinsia yangu tu labda mke na watoto wangu wangu wa kike ,sawia pia ukipatana na wa kwangu ww mwanaume usimsaidie hata maji anitafute mie au ke wenzake .
Cheka na Ile jinsia nyingine utajipata kizimbani ukiuma Chuma
 
Siku hizi hata siwapi kazi ke kwa ofisi yangu ,Toka mlinzi ,cleaner mpaka mawakili it's a male zone ,Huwa na avoid instances za kijinga Kama hizi .
Kingine eti msichana anionbe Hela sijui hajala au amepotea au simu ampigie mamake amtumie nauli Huwa sifanyi .
Sitaki mind games nnzaoona siku hizi , usaidizi kwangu umeishia kwa jinsia yangu tu labda mke na watoto wangu wangu wa kike ,sawia pia ukipatana na wa kwangu ww mwanaume usimsaidie hata maji anitafute mie au ke wenzake .
Cheka na Ile jinsia nyingine utajipata kizimbani ukiuma Chuma
Uyaongeayo huyabahatishi. Umekwepa mishale mingi yaonekana. Umefundishwa na umefundishika.
 
Back
Top Bottom