BARD AI
JF-Expert Member
- Jul 24, 2018
- 3,591
- 8,826
Raia wa China Li Naiyong amefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu , akikabiliwa na kesi ya uhujumu uchumi yenye mashtaka sita likiwemo kuisababishia Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), hasara ya zaidi ya Sh221 milioni.
Naiyong amesomewa mashtaka yake leo, Februari 15, 2023 na Wakili wa Serikali, Yusuph Aboud mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Pamela Mazengo.
Akimsomea mashtaka yake, Aboud amedai kuwa kati ya Agosti 13 hadi Oktoba 22, 2022, katika Hoteli ya Hongkong iliyopo Kariakoo, Wilaya ya Ilala, aliingiza vifaa mbalimbali vya mawasiliano vya kielekroniki bila kuwa na leseni.
Wakili Abood amedai pia katika tarehe hizo mshitakiwa huyo alisimika na kusimamia mitambo ya mawasiliano ya kielekroniki bila kuwa na leseni kutoka TCRA.
Vilevile mshtakiwa huyo kwa nia ovu, alitumia mawasiliano kwa kutumia vifaa hivyo vilivyounganishwa katika njia ya mawasiliano kwa lengo la kupokea na kutoa mawasiliano, bila ya kuwa na leseni.
Shtaka la tano, mshitakiwa huyo anadaiwa kuendesha mitambo hiyo ya mawasiliano kwa lengo la kupokea na kusambaza mawasiliano kimataifa, pamoja na kufanya matumizi mabaya ya vifaa hivyo kwa nia ya kukwepa makato, kwa kupokea na kusambaza simu za kimataifa bila leseni.
Shtaka la sita, katika tarehe hiyo kwa vitendo vyake hivyo, aliisababishia serikali na TCRA hasara ya Tsh. Milioni 221,163,600.
Upande wa mashtaka wamedai kuwa upelelezi wa kesi hiyo bado haukamilika hivyo wanaomba tarehe nyingine kwa ajili ya kutajwa.
Hakimu Mazengo alitoa masharti ya dhamana dhidi ya mshtakiwa huyo ambayo yamemtaka mshtakiwa kuwasilisha fedha taslimu Sh 110,581,800 au mali isiyohamishika yenye thamani hiyo.
Pia mshtakiwa huyo ametakiwa kuwa na wadhamini wawili mmoja awe ni mtumishi wa Serikali.
Mshtakiwa ameshindwa kutimiza masharti ya dhamana na hivyo kurudishwa rumande hadi Machi Mosi, 2023 itakapoitwa kwa ajili ya kutajwa.
Naiyong amesomewa mashtaka yake leo, Februari 15, 2023 na Wakili wa Serikali, Yusuph Aboud mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Pamela Mazengo.
Akimsomea mashtaka yake, Aboud amedai kuwa kati ya Agosti 13 hadi Oktoba 22, 2022, katika Hoteli ya Hongkong iliyopo Kariakoo, Wilaya ya Ilala, aliingiza vifaa mbalimbali vya mawasiliano vya kielekroniki bila kuwa na leseni.
Wakili Abood amedai pia katika tarehe hizo mshitakiwa huyo alisimika na kusimamia mitambo ya mawasiliano ya kielekroniki bila kuwa na leseni kutoka TCRA.
Vilevile mshtakiwa huyo kwa nia ovu, alitumia mawasiliano kwa kutumia vifaa hivyo vilivyounganishwa katika njia ya mawasiliano kwa lengo la kupokea na kutoa mawasiliano, bila ya kuwa na leseni.
Shtaka la tano, mshitakiwa huyo anadaiwa kuendesha mitambo hiyo ya mawasiliano kwa lengo la kupokea na kusambaza mawasiliano kimataifa, pamoja na kufanya matumizi mabaya ya vifaa hivyo kwa nia ya kukwepa makato, kwa kupokea na kusambaza simu za kimataifa bila leseni.
Shtaka la sita, katika tarehe hiyo kwa vitendo vyake hivyo, aliisababishia serikali na TCRA hasara ya Tsh. Milioni 221,163,600.
Upande wa mashtaka wamedai kuwa upelelezi wa kesi hiyo bado haukamilika hivyo wanaomba tarehe nyingine kwa ajili ya kutajwa.
Hakimu Mazengo alitoa masharti ya dhamana dhidi ya mshtakiwa huyo ambayo yamemtaka mshtakiwa kuwasilisha fedha taslimu Sh 110,581,800 au mali isiyohamishika yenye thamani hiyo.
Pia mshtakiwa huyo ametakiwa kuwa na wadhamini wawili mmoja awe ni mtumishi wa Serikali.
Mshtakiwa ameshindwa kutimiza masharti ya dhamana na hivyo kurudishwa rumande hadi Machi Mosi, 2023 itakapoitwa kwa ajili ya kutajwa.