Mchiriku: Hisani Musical Club (Gari Kubwa)

Mchiriku: Hisani Musical Club (Gari Kubwa)

Naomba nikuweke sawa kaka mkubwa. Huyu KICHEKO w E-fm ambae kwa sasa yupo clauds, sio kicheko wa gari kubwa (HISANI). Wakati hisani wanapiga nyimbo zao enzi hizo kicheko huyu wa genge la singeli alikuwa mtoto mdogo sana. Wale hisani walikuwa wanapatikana mwananyamala wakati kicheko na dogo mfaume wote watoto wa temeke. Kicheko kazaliwa mikoroshini temeke. Hakuwahi kuimba mnanda. Hisani walikuwa dizain kama ya watu wazima kipindi hicho sasa angalia Age ya kicheko sasa hv ni viwili tofauti. Wakati jamaa wanatamba hata huyu marehemu omary omary, Allah amrehemu alikuwa bado mdogo vile vile. Wakati kicheko na omary omary bado ommy ni mkubwa. Hisani walishakuja maeneo ya tandika bandari enzi hizo parifurika watu ikawa historia, katika harakati za kuburudisha likatokea timbwili si unajua tena masela , ilikuwa balaa show ikafa watu walipotea na raia kama wawili walidedi. Hao waliodedi walikuwa masela waliochukuliana demu maana hiyo piga yake balaaa sijui silaha walizipigilia viunoni! Braza wangu alirudi hom na kandambili moja.
Kwani kuna watu wanajua Kicheko wa mchiriku ndio huyo wa E-fm?,doooh!.
 
Malumbano na zogo kubwa Katika Basi lile,
Kati ya kondakta na Bwana mgambo yule,
Kondakta anadai nauli yake hee,
Na mgambo anataka kupanda bure anadai Yeye ni chombo cha dola,
Kondakta akaja juu akasema haiwezekani kupanda bure hee,
Nimeruhusiwa na jeshi la magereza,
Nimeruhusiwa na jeshi la polisi,
Kupanda buree nmeruhusiwa na chombo cha dola.
×2
Nyimbo hii wenye Chaukucha(watoto wadogo waliokomaa vichwa),lakini wengi wanaitambulisha vibaya kwamba ni ya Jagwa.
 
Hisani walileta mapinduzi makubwa sana kwenye mchiriku

Na laiti Mkapa asingeupiga marufuku basi sasa hivi mchiriku ungekua zaidi ya bongo flavour
Hisani ndio waasisi wa mnanda,wameutoa kutoka kwenye Chakacha.
 
Hiki kisa ni cha kweli kabisa. Said Kipaka alikuwa mwizi wa hatari na anaogopeka kishenzi Temeke yote mpaka Buguruni. Alikuwa anaishi pale Temeke Sokota. Kuna siku alienda kuiba maeneo yale Wananchi wakala nae Kona kufika pale Sokota avuke barabara kuelekea upande wa shell akagongwa na Gari,alipogongwa tuu Wananchi wakammaliza Kwa Moto. Hata alipokufa yeye wakabaki wengine kwenye familia yao kuendeleza wizi,Kabwe akashika usukani. Dah longtime sana yale maisha ya uswazi plus mchiruku yalikuwa so excited aiseee.

Sent using Jamii Forums mobile app
Wakati Mwembe Yanga biashara ya machungwa inatamba,mameza kama yote.
 
I hope someone angetengeneza documentary ya historia ya muziki wa mchiriku
Mimi niko mbioni kufanya hivyo,kwani nina historia iliyoshiba ya mziki huu na nawajua watu wengi waliokua ni wadau wakubwa ambao wanaweza kunirekebisha nikoseapo.Halafu naupenda mziki huu.
 
Mimi ninayo ila nashindwa kuapload humu, nitumie namba ya WhatsApp nitakutumia. Halafu kuna WhatsApp group la Mchiriku lipo ukitaka utaunganishwa, huko utapata kila unachotaka kuhusu Mchiriku.
Naomba uniunge what's up group la mchiriku, 0713963812
 
Upitie tena huu wimbo na utamsikia mwimbaji akisema hivi hii ni sauti ya chaukucha family eh,watoto wadogo waliokomaa kichwa kutoka kulekule kwa kopa,hii ni ishara kuwa nyimbo hii haikuimbwa na jagwa bali ni nyimbo ya chaukucha family na huu wimbo huyu mwimbaji(Igosh) anawapiga dongo jagwa kutokana na ugomvi uliomfanya ahame jagwa muzik(dege la jeshi) na kuhamia chaukucha family
Nalog off
Yap,hongera kwa kuwaweka sawa .Marumbambano na zogo kubwa(Kondakta)wenyewe ni Chaukucha,kundi lililoimarishwa na maprofesheno waliojitoa Jagwa baada ya kurumbana.Humu zimepigwa dumbaki kali sana na za kuchezeka.
 
Wimbo wa ajali ya kibada nani aliimbiwa?

Ni kweli wasanii wa mnanda waligongwa na gari walikuwa waporaji?
Washkaji karibuni maskani
Lakini msione kimyaa
Said dabani hamumuoni
Amefariki dunia kwa ajali ya gari
Ambayo imetokea buguruni
Said dabani kaacha majonzi
Hata kwa mzazi mwenzie
Pili mama Ali amebaki analia
Said dabani kaacha majonzi
Kwa kisia babu na fikiri fika enock wa mbeya na magomba wanalia
Saidi Dabani kaacha majonzi
Kwa bwana tondo na bwana Ema uvuruge na omar wanalia
Na siri ya mungu kubwa siri haeleweki sifahamu safari hii nani atatangulia kama mimi bwana ommy au wewe bwana tondo .
 
Washkaji karibuni maskani
Lakini msione kimyaa
Said dabani hamumuoni
Amefariki dunia kwa ajali ya gari
Ambayo imetokea buguruni
Said dabani kaacha majonzi
Hata kwa mzazi mwenzie
Pili mama Ali amebaki analia
Said dabani kaacha majonzi
Kwa kisia babu na fikiri fika enock wa mbeya na magomba wanalia
Saidi Dabani kaacha majonzi
Kwa bwana tondo na bwana Ema uvuruge na omar wanalia
Na siri ya mungu kubwa siri haeleweki sifahamu safari hii nani atatangulia kama mimi bwana ommy au wewe bwana tondo .

Naskia kuna wanamuziki wa mnanda vibaka ambao walikuwa wanalala barabarani magari yakisimama wanayapora siku hiyo huko Kibada Kigamboni dereva alisimamishwa lakini hakusimama akawagonga wote wakafa,jamaa akawaimbia huo wimbo wa Ajali ya Kibada

 
Bangusilo tutimke, masela tutimke... Moody boy tutimkeee.. Kitambo. Ila sasa hivi Jagwa wanapiga mpaka kwenye stage za Ulaya. Mambo yamebadilika aha.
Mkuu huu wimbo unaitwaje?naupenda sana ila sijajua jina lake
 
Unaitwa Beach Boy na umeimbwa na Marehemu Omary Omary akiwa na bendi ya Atomic na sio Jagwa.
Ahsante mkuu,ila nimeutafuta mtandaoni sijaupata,Kama unao nauomba,mimi jagwa ndio bendi yangu pendwa so nikajua wameimba wao
 
Mimi bhana naomba kujua hawa waliokuwa wanatajwa kwenye nyimbo za jagwa walikuwa na cheo gani kwenye bend,
1.Kamongo Manja(Manjalino)
2.Jolijo
3.Saidi Misape
4.Bonge mzito
4.Baba Dullah
 
Back
Top Bottom