Mchoraji Katuni, Optter Fwema mahakamani leo

Kigogo mwenyewe siku hizi anavyowatukana chadema baaada ya lissu kukataa ushauri wake wa cdm kuingia msituni anadhani yameisha kumbe jamaaa bado wana hasira naye
 
Hii kesi wanaenda kujidhalilisha tena mahakamani. Katuni imechorwa mwanamke anachezea maji nyuma yake Kuna jamaa ameandikwa neno KIWETE mgongoni hapo unaweza kutoa kila aina ya tafsiri.

Hii wanapoteza muda na kumsumbua kijana wa watu.
Sio mama ni mtoto mwenye shida ya "mdomo wa sungura"
 
Katuni haina shida yeyote! Tafsiri yako ndio shida! Huwezi kuadhibiwi kwa tafsiri ya mwingine, sina uhakika kama sheria zetu zinaruhusu!
 
Hii picha ina tafsiri kubwa sana. Naomba tutafakari hapa kwa pamoja.

1. Dishi lina bendera ya Tanzania na lina maji. Hapa anawakilisha nchi ya Tanzania na watu wake.

2. Mwenye nguo nyeusi ni mzazi na mwenye kilemba ni mtoto. Huyo mtoto anachezea maji ndani ya dishi. Hapa inaeleweka zaidi.

3. Maji yanakanyagwa na mtoto mwenye kilemba pamoja na mtu wa nguo nyeusi. Yaani hapa sheria za nchi zinasiginywa/kukanyagwa.

4. Mtu wa nguo nyeusi anawaambia wananchi watulie nchi inaongozwa vizuri. Hapa anawatoa hofu wananchi ya kuwa kila kitu kipo pouwa kabisa, hivyo waondoe maulizo na mishangao.

5. Wananchi wameshika vichwa vyao. Inaonekana wananchi hawamuelewi kabisa huyo mtu, yaani wanashangaa na kujiuliza bila ya majibu yoyote.
 
Na kuna sauti imepunguzwa hadi mwisho.
 
Mkuu unaonaje upewe nafasi kwenye jopo la wanasheria wanaomtetea mtuhumiwa...kama kawaida hii kesi inaenda kuwadhalilisha zaidi mapolisi!
 
Mwenye nguo nyeusi ki KIWETE how can they prove otherwise in court
 

Mkuu hii ikukumbushe nawewe mtuhumiwa mtarajiwa mwenzangu kwamba,kabla sheria haijaonyesha makali yake kupitia mahakama,basi utakuwa umeshachoka sana.

Chunga sana njia zako,ohooo.
 
mkuu hii ikukumbushe nawewe mtuhumiwa mtarajiwa mwenzangu kwamba,kabla sheria haijaonyesha makali yake kupitia mahakama,basi utakuwa umeshachoka sana.

chunga sana njia zako,ohooo.
Ndio maana watu weusi tunaonekana kama tuna laana!Ni kutesana tu bila sababu za msingi!
 
CCM kila siku kesi hivi mtajenga nchi lini?
 
Wapuuzi sana hawa wakati mwingine, kazi ni kuzushia na kudhalilisha watu tu!
Usiwaze kama wale askari wa kitengo cha cyber ambao anachotafsri ndo kinakuwa kesi ya mtandao kiongozi huwezi kuwa na wanaokupongeza tu saa 24 lazima wapo wanao kukosoa kwa haki ama kukuonea wanakupa changamoto za kujiangalia ...watu wanampinga na kumdhihaki Mungu Mwenye wafuasi wengi Sembuse kiongozi wa nchi ?
 
Kuna issue inazungumzwa kwamba katika msimu huu wa 6, ole wako umguse Msoga utapewa meno ili uyasage
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…