Mchungaji Eliona Kimaro wa KKKT Kijitonyama apewa likizo ya siku 60 na kutakiwa kuripoti Makao Makuu

Waumini wengi sana wa KKKT walitoka makanisa ya kilokole ya mwendokasi wakatejea kundindi Kijitonyama KKKT na wasio KKKT,

Sasa leo mnampiga Mchungaji ili Kondoo watawanyike?! [emoji848][emoji848]
 
Mchungaji kuhamishwa Usharika sio mgogoro,labda kama huyo mchungaji haendi sawa sawa na kiapo chake cha kichungaji, acheni upambe na mheshimu taratibu za Kanisa.
 
Kwa uelewa wangu hakuna mgogoro hapa.ila ni mtu na muajiri wake kuna mambo ya kuyaweka sawa.ni sawa na mwalimu mmoja akisimamishwa kazi kupisha jambo fulani litunzwe.Hapo utasema serikali ina mgogolo na waalimu?

Najua Watumishi wa Mungu hasa Maaskofu wana Hekima sana.Huwa wanajitahidi sana kulinda hadhi ya mtu.so wanajitahidi kudeal na mambo magumu kiungwana zaidi.Wasingependa na hawawezi kwenda kwenye media na kuelezea chanzo.Sababu huenda wakielezea chanzo mtaacha kumheshimu mchungaji wao
 
UNAPOSEMA AMENYOOKA UNAKUWA UNA MANA GANI? JE KWAMBA KANISA KKKT LINA MAMBO YSIYOFAA KATIKA JAMII MPAKA HUYO ANAONEKANA NDIYO MAMBO YANAYOFAA? YAANI HAPO NAONA KAMA UMELIPAKA MATOPE KANISA KUWA HALIFAI LABDA KAMA UTATUPA SABABU AU HUYO JAMAA AMENYOOKAJE
 
un
unamzungumzia aliyewahi kuwa Mchungaji mbezi beach kkkt?
 

Hii kitu ni kama copied mahali…
 
Sasa hata yasipoyumba so what? IMPACT YAO NI NINI? Msifanye vitu kwa mazoea, Kimaro na Mgogo wana injilisha kwa namna yenye kuleta mapinduzi, kimaisha na kiimani

Kuonekana You Tube ndio kuleta mapinduzi?. KKKT inajiendesha kwa mfumo wa dayosisi sio kwa mtu.
 
Mbona unapiga kelele mkuu ungeandika kwa font ya kawaida bado ungeeleweka.
 
Halafu wanabadilisha sala na kuziondoa nyingine kimya kimya, ila ukiwa na version za zamani za vitabu vya sala na kuhudhuria ibada muda wote unaushitukia mchezo!
Sema tu wazi Roman Catholic wanabadili sala ili wauze vitabu tutakuelewa ila tutafunga kwa ajili yako 😂😂
 
Mbona unapiga kelele mkuu ungeandika kwa font ya kawaida bado ungeeleweka.
Inategemea unatumia kifaa gani kusoma maandishi yangu, pia afya ya macho yetu inatofautiana.
 
Mchungaji kuhamishwa Usharika sio mgogoro,labda kama huyo mchungaji haendi sawa sawa na kiapo chake cha kichungaji, acheni upambe na mheshimu taratibu za Kanisa.
Taratibu za kanisa unamaanisha mapokeo, na utaratibu uliotungwa na wanadamu au unamaanisha msingi ulio kwisha kuwekwa na Yesu mwenyewe alisema hakuna atakaye weza kuvunja?.
 
Kma hazitaibuka tuhuma za kula waumini basi ntasimama na dayosisi ila zikiibuka tu ntasimama na Mch. Kimaro
 
Taratibu za kanisa unamaanisha mapokeo, na utaratibu uliotungwa na wanadamu au unamaanisha msingi ulio kwisha kuwekwa na Yesu mwenyewe alisema hakuna atakaye weza kuvunja?.
Kila taasisi ina taratibu zake, kama umeamua kutangaza neno la Mungu kwa kupitia kanisa la Roman Catholic utalazimika kufuata taratibu zao. Ni nini huelewi hapa?

Kama unataka usibanwe na taratibu za Kanisa kama taasisi, vua utambulisho wa kanisa na uanze kuubiri wewe kama wewe na sio kwa mwavuli wa kanisa.

Tumsifu Yesu Kristo!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…