Lazima heshima iwepo kwa viongozi wa serikali vipi kuhusu viongozi wa dini wao hawastahili heshima
Sawa mama Bashite tumekusikiaSalaam humu, nina hasira sana na Gwajima...
Laiti, mm ningekuwa RC Makonda, saa hizi Gwajima angekuwa maabusu and behind unknown bars..
Serikali, kamateni huyu mchungaji feki, mmemlea sana, kaota mapembe, akijua yuko juu ya state.. Iweje Gwajima, anamchafua Mkuu wa Mkoa, Makonda kwa kiwango hiki, na asikamatwe? With immediate action, kamateni mhuni mchungaji feki, iwe funzo la milele..
HATUWEZI kuwa na mchungaji mhuni mhuni kuchafua viongozi wa serikali kutumia kanisa lake . I wish ningekuwa RC Makonda, sitanii, Gwajima ungejuta, kamata huyu mhuni haraka.. Aaaaarrghh
Haiwezekaniki mchungaji feki huyo kumchafua RC kiasi hiki, no way, no how, not acceptable, lazima lazima heshima iwepo kwa viongozi wa serikali ikibidi kwa lazima, Who is Gwajima? Mandate ya kuchafua kiongozi wa serikali anapata wapi? I was offline for 2 weeks, namuona Gwajima anaachiwa kucheza hovyo, piga ndani huyu mhuni mkubwa, ww Gwajima ww, jua wazi hauko juu ya serikali, na serikali inakujua ww kuliko unavyojijua, acha ujinga mara moja.. Aaaarrghh
Huyo siyo askofu bro trust me. Alipewa na nani kwani. Alijipachika mwenyewe kama ambavyo na wewe unaweza kujiita askofu kuanzia leoNjaaa zako zitakuuuaa...bashite alete vyeti hicho tu... Akuanzae mmalize tulifundishwa hivyo..bashite alisema mwenzie anauza dawa...mwenzie kajibu bashite kanunua vyeti....bashite kasepa no vyeti no nn..
Big up askofu
Nenda UDSM kaulizie; Hii ya Gwajima ni fake from the fake fakes! Kibaya zaidi ni mtu wa Mungu kuendelea kujiita DR. Wakati Taasisi iliyompa hiyo " Honorary PHD" Haitambuliki popote! Mamlaka zote za Afrika Kusini Haziitambui hiyo Taasisi Feki.
Kuna cheti cha div 0?Nadhani anayo matokeo ya shule aliyosoma BASHITE akapata zero, Pamoja na vyeti vya MAKONDA.
Hawa ni watu wawili tofauti.
Nadhani atajibu hii asikute naye alibashite, Pasco njoo huku ujibu hizi tuhumaPascal Mayala haeleweki, ila nae atuambie alikopitia elimu yake mpaka anapata digrii. Make mimi Mayala nimeanza kumsikia anaandika habari wakati hana digrii.......sasa atuambie alikuwa mwandishi vipi wakati hana digrii......na ameipataje digrii yake hapo baadae. Hizi elimu za kuunga zina shida sana.
Cheti hakuna ila matokeo yapo.Kuna cheti cha div 0?
amesema ana cheti tumuelewe nani kati yenu.Halafu matokeo ya NECTA yapo online,kelele zote hakuna aliweza kuyabandika humuCheti hakuna ila matokeo yapo.
Imani na sheria ni vitu viwili tofauti sana. Kama yeye kwenye Imani yake anaamini ni cheo kikubwa zaidi ya urais why wewe uone kasema uongo? Mind you hajasema kikatiba yeye ni zaidi ya rais, but he meant is at peace with what is doingWanabodi,
Manabii wa Uongo na Tutawatambuaje?.
Kwa sisi waumini wa dini ya Kikristo, tunayemwamini Bwana wetu Yesu Kristo, kabla hajapaa mbinguni, alituhusia kuwa "kutajitokeza manabii wa uongo, ambao watahubiri neno na kutoa mapepo kwa jina langu lakini sii wangu". Wanafunzi wake wakamuuliza, "Jee tutawatambuaje?", Yesu akawajibu, "Mtawatambua kwa matendo yao".
Mchungaji Dr. Josephat Gwajima ni Nabii wa Kweli au Nabii wa Uongo?.
Hii ni thread ya swali kumhusu Mchungaji wa Kanisa la Ufufuo wa Uzima, Mchungaji, Dr. Josephat Gwajima, Jee ni Mtumishi wa Mungu wa Kweli?!, ni Nabii wa kweli au ndio wale manabii wa uongo aliowazungumza Bwana wetu Yesu Kristo?.
Akiwa katika mimbari, madhabahuni, mbele ya Mungu na wana kondoo wake, badala ya kuihubiri Injili na neno la Mungu lenye uzima na lenye kujenga upendo, amani na mshikamano miongoni mwa jamii, yeye anahubiri siasa kwenye nyumba ya ibada, tena mahubiri juu ya chuki dhidi ya binadamu mwingine hadi kumuita "huyu kiumbe"!.
Japo ni kweli Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mhe. Paul Makonda alimdhalilisha Mchungaji Gwajima kwa kumtaja kujihusisha na madawa ya kulevya, jee namna ambayo Mchungaji Gwajima, anavyomzungumzia Mkuu wetu wa Mkoa, ndivyo Bwana Yesu alivyofundisha namna ya kuwashughulikia wale walio tukosea?. Yesu alifundisha mtu akikupiga kibao shavu la kushoto mgeuzie na la kuume. Adui mpende. Samehe saba mara sabini. Vipi kuhusu Baba Mchungaji Gwajima kumuishi Bwana Yesu kwa maneno na matendo? .
Jee Maneno na Matendo ya Mchungaji Gwajima ni Kama Yesu, ni ya KiMungu?.
Swali ni jee huu ndio utendaji wa watu wa Mungu, kuwatakia wenzao mabaya?, kuwazushia uongo mchana kweupe tena madhabahuni kwenye mimbari ya Mungu?!. Yesu alitufundisha, "tumpe Kaisari yaliyo ya Kaisari, na tumpe Mungu yaliyo ya KiMungu, kwanini Mchungaji Gwajima, analeta ya Kaisari mezani kwa Bwana?!. Jee huyu Mchungaji Gwajima, ni mchungaji wa Mungu au ni wa mungu?. Mchungaji Gwajima kama mtu wa Mungu wa kweli, anaweza kweli kusema uwongo kama ule madhabahuni kwa Bwana?!. Jee huyu ni mchungaji wa kweli anayemtumikia Mungu wa kweli, au ndio wale wachungaji aliyewasema Bwana wetu Yesu Kristo kuwa "kutajitokeza manabii wa uongo, ambao watahubiri neno na kutoa mapepo kwa jina langu lakini sii wangu". Wanafunzi wake wakamuuliza, "Jee tutawatambuaje?", Bwana Yesu akawajibu, "Mtawatambua kwa matendo yao".
Jee kwa matendo kama haya, kuna kitu chochote cha kutambua?.
Mchungaji Gwajima ni Nabii wa Mungu, au nabii wa mungu?.
Japo nimewahi kushiriki Ibada kwa Mchungaji Gwajima, naomba mimi nisiseme kitu bali msikilize mmoja wa waumini wake ambaye pia ni mwanachama mwenzetu hapa jf.
Kwa ushuhuda huu mtaona tuhuma unga kwa Mchungaji hazikutolewa na Makonda kwa wivu wa helicopter au vita vya Jimbo bali Makonda alipewa majina na akayaanika.
Paskali
Jumatatu Njema.
Paskali
Cheti hakuna ila matokeo yapo.
Hayo ni ya kwako. Mimi sio mpenzi wa udaku.Matokeo ya kuzaa na Flora Mbasha au