Mchungaji Gwajima ni Mtumishi wa Mungu wa kweli au? Asema Uongo. Adai yeye ni zaidi ya Rais

Mchungaji Gwajima ni Mtumishi wa Mungu wa kweli au? Asema Uongo. Adai yeye ni zaidi ya Rais

Bila ujasiri wa huyu jamaa, watu wengi wangesotea sero, maana yule jamaa alishapanga mpaka awamu saba
 
Haiwezekani amuite Mkuu wa Mkoa kiumbe...ni kosa kubwa sana
Kosa kubwa kivipi, binadamu, wanyama wote waliopo duniani, nchi kavu na majini, miti pamoja na mimea yote ni viumbe.., bashite is no exception.
 
Dini ni kweli inakataza kulipa kisasi kwani inasema kisasi kulipiza ni kazi ya Mungu mwenyewe. Gwajima ameingia kwenye ubinadamu zaidi na kumwacha Roho wa Mungu pembeni. Kwani yeye ilitakiwa amwombe Mungu aingilie kati kuonewa kwake naye angejidhihirisha na kuchukua hatua azijuazo yeye Muumba. Pia kunawakati huwa yupo sahihi kwani kazi ya watumishi wa Mungu ni kukosoa na kukemea pale haki inapopotoshwa au kudhulumiwa. Pia nivyema makonda akaweka vyeti vyake hadharani kwani taaluma sio siri ili kukata mzizi wa fitina.
 
Hivi kati ya watumishi wa Mungu, Gwajima naye ni mmojawapo? Hata kama kakosewa kama anavyodai, je yeye neno la kusamehe huwa linampita pembeni? Au akisoma Biblia vifungu vinavyohusu kusamehe huwa vinafutika? Huwa anawafundishaje waumini wake kuhusu somo la msamaha?

Mathayo 6:14-15 Kwa maana mkiwasamehe watu makosa yao na Baba wenu wa mbinguni atawasamehe ninyi bali msipowasamehe watu makosa yao wala Baba yenu hatawasamehe makosa yenu."

Waefeso 4:32 "Tena iweni wafadhili ninyi kwa ninyi, wenye huruma ninyi mkasameheane kama na Mungu katika kristo alivyowasamehe ninyi."

Mathayo 18:21-22 "Kisha petero akamwendea akamwambia Bwana ndugu yangu anikose mara ngapi nami ni msamehe? hata mara saba? Yesu akamwambia sikwambii mara saba bali hata saba mara sabini."

1 Wakorintho 13:4, 5. “Upendo ni wenye ustahimilivu na wenye fadhili. Upendo hauna wivu, haujigambi, haujivuni, haujiendeshi bila adabu, hautafuti faida zake wenyewe, hauchokozeki. Hauweki hesabu ya ubaya. Haushangilii juu ya ukosefu wa uadilifu, bali hushangilia pamoja na kweli. Huhimili mambo yote, huamini mambo yote, hutumaini mambo yote, huvumilia mambo yote.”
Umenukuu vifungu vya biblia vizuri kabisa. Ila tafsiri unayotaka kuambatanisha navyo inaniogopesha. Kuwa mkristo sio kuja kutetea uovu kwa kigezo cha upendo. Sio kunyamazia ubaya fulani eti usionekane una hasira. Ukristo sio kuogopa kufunua vyeti feki eti usionekane huwezi kusamehe.

biblia inasema mtu akikosea akaja kuomba msamaha" msamehe. Awali kabisa gwajima alisema daudi aombe msahama kabla chungu hakijapata moto zaidi. Daudi akakausha. Sasa mkuu unaponukuu habari ya msamaha bila mwombaji kuhitaji msamaha una maama gani? Sisi tunafundishwa kwamba Mungu ni wa rehema tukiziungama dhambi zetu, je usipotubu, Mungu anawezaje kukusamehe?

Namalizia kwa kile kiitikio chetu "wacha maneno weka vyeti"
 
Ukweli ni kwamba sijawahi mwamini huyu mwinjilisti. Imani yangu kwake ilitoka pale alipokuwa anamshauri Rais magufuli kuwa ajitoe ndani ya ccm na urais wake na kujiunga na chama kingine. Angewezaje kkuvua uanachama na kubaki na urais?
Lakini pia katika hili sakata lake na mh.makonda,mara ya kwanza alisema makonda alimaliza kidato cha nne pale pamba sec.na akapata zero,juzi anasema kuwa alifukuzwa,ukweli ni upi? Anatueleza pia kwamba ana cheti cha daudi bashite na kwamba ana zero,kama kweli makonda alihitimu mwaka 2000, Mimi nilihitimu 2001,div.0 walikuwa hawapewi vyeti.gwajima kakipata wapi?
Kwakeli gwajima anaongea sana,na amepata washabiki wengi,ila Mimi simwamini kwakuwa tangu nianze kumsikiliza nimekosa kumwelewa hasa kwenye mwendelezo wa story zake,na uelewa wako juu ya mambo ya kawaida.
Ni maoni yangu tu.
 
Suluhisho ni kwa mkuu wa mkoa kutoa vyeti vyake tu hlf wote tutamdharau Gwajima, atoe hata kadi ya kliniki iliyoandikwa Paul basi mchezo utakuwa umeisha, vingine askofu ataendelea kuwa shujaa!
 
Ushujaa wa askofu hautatokana na makonda,ushujaa wake itategemea jinsi anavyowaandaa kondoo wake kwa haki na kweli ili kuurithi uzima wa milele.
 
Kama ww haumuani Gwajima. je ww unauona ukweli ni upi hususu Bashite au Makonda?
 
Gwajima na Makonda nani Haaminiki? nani mbabaishaji na anaeshindwa kuthibitisha ukweli.
 
Ukweli ni kwamba sijawahi mwamini huyu mwinjilisti. Imani yangu kwake ilitoka pale alipokuwa anamshauri Rais magufuli kuwa ajitoe ndani ya ccm na urais wake na kujiunga na chama kingine. Angewezaje kkuvua uanachama na kubaki na urais?
Lakini pia katika hili sakata lake na mh.makonda,mara ya kwanza alisema makonda alimaliza kidato cha nne pale pamba sec.na akapata zero,juzi anasema kuwa alifukuzwa,ukweli ni upi? Anatueleza pia kwamba ana cheti cha daudi bashite na kwamba ana zero,kama kweli makonda alihitimu mwaka 2000, Mimi nilihitimu 2001,div.0 walikuwa hawapewi vyeti.gwajima kakipata wapi?
Kwakeli gwajima anaongea sana,na amepata washabiki wengi,ila Mimi simwamini kwakuwa tangu nianze kumsikiliza nimekosa kumwelewa hasa kwenye mwendelezo wa story zake,na uelewa wako juu ya mambo ya kawaida.
Ni maoni yangu tu.
Unaonaje bashite nae atoe vyeti then upigilie kabisa msumari kwa Gwajima kutomkubAli kabisa hebu mshauri iko kitu bwana bashite
 
Aisee kumbe wengine mmesoma kw kukariri,kwani akiwa na result slip si ni cheti pia?
Nyinyi mnawajua watumishi wote wanaosali kwa gwajima je kama wamempelekea ushahidi huo wa kuprint hata kama ni document sio cheti?pascally wewe nina wasi wasi utakuwa ni mhanga kama daudi bashite.
Result slip ya nini wakati MTU kapate divisheni ziro,sufuri au 0? Hakuna kitu kama hicho.
 
Wanabodi,
Manabii wa Uongo na Tutawatambuaje?.
Kwa sisi waumini wa dini ya Kikristo, tunayemwamini Bwana wetu Yesu Kristo, kabla hajapaa mbinguni, alituhusia kuwa "kutajitokeza manabii wa uongo, ambao watahubiri neno na kutoa mapepo kwa jina langu lakini sii wangu". Wanafunzi wake wakamuuliza, "Jee tutawatambuaje?", Yesu akawajibu, "Mtawatambua kwa matendo yao".

Mchungaji Dr. Josephat Gwajima ni Nabii wa Kweli au Nabii wa Uongo?.
Hii ni thread ya swali kumhusu Mchungaji wa Kanisa la Ufufuo wa Uzima, Mchungaji, Dr. Josephat Gwajima, Jee ni Mtumishi wa Mungu wa Kweli?!, ni Nabii wa kweli au ndio wale manabii wa uongo aliowazungumza Bwana wetu Yesu Kristo?.

Akiwa katika mimbari, madhabahuni, mbele ya Mungu na wana kondoo wake, badala ya kuihubiri Injili na neno la Mungu lenye uzima na lenye kujenga upendo, amani na mshikamano miongoni mwa jamii, yeye anahubiri siasa kwenye nyumba ya ibada, tena mahubiri juu ya chuki dhidi ya binadamu mwingine hadi kumuita "huyu kiumbe"!.

Japo ni kweli Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mhe. Paul Makonda alimdhalilisha Mchungaji Gwajima kwa kumtaja kujihusisha na madawa ya kulevya, Makonda alipewa tuu list yenye majina na kazi yake ilikuwa ni kuwataja tuu, aliyemtaja Gwajims ni muumni wake mtiifu, koss ls Makonds ni lipi?!.

Jee namna ambayo Mchungaji Gwajima, anavyomzungumzia Mkuu wetu wa Mkoa, kwa ubaya na kumsingizia uongo, ndivyo Bwana Yesu alivyofundisha namna ya kuwashughulikia wale walio tukosea?!. Yesu alifundisha mtu akikupiga kibao shavu la kuume mgeuzie na la kushoto. Adui mpende. Samehe saba mara sabini. Vipi kuhusu Baba Mchungaji Gwajima kumuishi Bwana Yesu kwa maneno na matendo? .

Jee Maneno na Matendo ya Mchungaji Gwajima ni Kama Yesu, ni ya KiMungu?.
Swali ni jee huu ndio utendaji wa watu wa Mungu, kuwatakia wenzao mabaya?, kuwazushia uongo mchana kweupe tena madhabahuni kwenye mimbari ya Mungu?!. Yesu alitufundisha, "tumpe Kaisari yaliyo ya Kaisari, na tumpe Mungu yaliyo ya KiMungu, kwanini Mchungaji Gwajima, analeta ya Kaisari mezani kwa Bwana?!. Jee huyu Mchungaji Gwajima, ni mchungaji wa Mungu au ni wa mungu?. Mchungaji Gwajima kama mtu wa Mungu wa kweli, anaweza kweli kusema uwongo kama ule madhabahuni kwa Bwana?!. Jee huyu ni mchungaji wa kweli anayemtumikia Mungu wa kweli, au ndio wale wachungaji aliyewasema Bwana wetu Yesu Kristo kuwa "kutajitokeza manabii wa uongo, ambao watahubiri neno na kutoa mapepo kwa jina langu lakini sii wangu". Wanafunzi wake wakamuuliza, "Jee tutawatambuaje?", Bwana Yesu akawajibu, "Mtawatambua kwa matendo yao".
Jee kwa matendo kama haya, kuna kitu chochote cha kutambua?.
Mchungaji Gwajima ni Nabii wa Mungu, au nabii wa mungu?.
Japo nimewahi kushiriki Ibada kwa Mchungaji Gwajima, naomba mimi nisiseme kitu bali msikilize mmoja wa waumini wake ambaye pia ni mwanachama mwenzetu hapa jf.

Kwa ushuhuda huu mtaona tuhuma unga kwa Mchungaji hazikutolewa na Makonda kwa wivu wa helicopter au vita vya Jimbo bali Makonda alipewa majina na akayaanika.
Paskali
Jumatatu Njema.
Paskali
Asante sana Paskali,
Pamoja na kwamba si kubahatiwa kusoma kwa umakini mkubwa mwanzo mwisho wa andiko lako lenye uchambuzi wa kina, hoja moja ni dhahiri hata mimi ninamuunga mkono Mchungaji Gwajima. Kiongozi wa kweli wa kiroho ni zaidi ya rais wa nchi. Wakati rais anaweza kuwabagua watu kwa ajili ya maslahi ya chama chake , kiongozi wa kiroho hawezi akawa na "hawa ni wangu na hawa sio". Wakati rais anaweza kuwateua wateule wake kwa kuwafahamu tu na kulipa fadhila kwa au kumpingia kura au kumsaidia kupandisha ngazi fulani huko nyuma, kiongozi wa kiroho anawaona watu wote ni sawa.

Na kwa marais wa siku hizi, wenye chuki na watu, visasi nk. nidhahiri kuwa kiongozi wa kweli wa kiroho ni zaidi ya rais. Na kuna wakati nashawishika kuaamini kuwa hata baba wa familia anayejitambua anazo sifa za ubora kuliko hawa marais wa siku hizi. Baba wa familia hawezi kutengeneza njama miongoni mwa watu wake. Hana upande.
 
Kama kwa kufichua vyeti vya Daudi Bashite ndiyo unamuita Nabii wa uongo, acha awe na mimi binafsi ndiyo nitazidi kumpenda na Jumapili nitaenda pale kanisani kwake kusali
 
Back
Top Bottom