Mchungaji Hananja: Wachungaji KKKT wakihoji vitendo vya viongozi kuuza Mali za kanisa, wanafukuzwa, asema na yeye alisimamishwa mwaka mmoja

Mchungaji Hananja: Wachungaji KKKT wakihoji vitendo vya viongozi kuuza Mali za kanisa, wanafukuzwa, asema na yeye alisimamishwa mwaka mmoja

KKKT haina tofauti na SACCOS ama kikundi cha vicoba.

Wana migogoro mingi ambayo haina tofauti na ile ya kwenye vyama vya siasa.

Wakati wa mgawanyo wa dayosisi ya Pare na Mwanga walimwagiana tindikali kinoma
Kungwi hueleweki kama nanii......
 
Mim sijaenda KKKT miaka karibu 10 sasa....Sadaka inapangwa kutoka juu, eti usharika huu mtoe kiasi fulani...basi hapo harambee za kijinga jinga tu.....ni wakati sasa wa maaskofu kutuachia kanisa
SAS wakiachia kanisa itaongozwa na nani kina kimaro ndio mnawataka waongoze kanisa ?

Tuwcheni ujinga Bado kijitonyama haijatetereka itaka sawa tu hz Ni siasa za kanisa tu

Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
 
Acha kumtukana Askofu Shoo.
Hapo amehusikaje ?
Malasusa ndiye anayehusika na Dayosisi ya Mashariki na Pwani na ndiye anayemsimamia Dr. Kimaro.

Kanisa la KKKT Lina katiba mbovu sana na ndiyo inayosababisha migogoro na wizi mkubwa ndani ya kanisa Hillo. Kanisa la KKKT ni Mali ya Maaskofu . Kila mmoja ana sharubu. Yaani Dr. Kimaro ni WA Malasusa na sio wa Dr.Shoo. Dr. Shoo Hana maamuzi yoyote juu ya Dr.Kimaro. Askofu mkuu alipaswa kuwa na mamlaka makubwa juu ya maaskaofu wote wa KKKT na kuweza hata kuwahamisha kwenye Dayosisi nyingine. Ndio maana Vitega uchumi vya KKKT vinakufa kila mahali Kwa sababu wengi sio waaminifu na hawana sifa za kusimamia miradi Hi hiyo

Kama anaitwa Askofu Mkuu ila hana mamlaka ni useless. Kama kweli Katiba iko hvyo kuna haja ya mabadiliko haraka
 
Mchungaji Hananja akihojiwa na Bongo5 (ingia YouTube, kaongea nusu saa nzima) ameeleza uonevu mkubwa wanaofanyiwa na viongozi wakuu wa kanisa, na anasema yeye aliandikiwa barua na kiongozi mkuu wa kanisa kumsimamisha kazi bila mshahara kwa mwaka mzima, bila sababu yoyote ile.

Hananja anasema alikataa barua ya kiongozi mkuu wa kanisa kwa kuwa si muajiri wake,

Hananja ameeleza kwamba kanisa linapitia maumivu makubwa kwa sababu ya unyanyasaji na roho mbaya sana, na visasi walivyonavyo viongozi wakuu wa kanisa Hilo.

Hananja ameeleza kwamba viongozi wakuu wako katika wimbi kubwa la kuuza viwanja vya kanisa, na wachungaji wanapohoji, wanafukuzwa na kunyanyaswa sana.

Kuna taarifa kwamba mchungaji Kimaro, kupitia Utumishi wake, kijitonyama imenunua viwanja vya mamia ya mamilioni, na kujenga majengo ya thamani kubwa, na kuna hisia kwamba wakuu wa kanisa wanataka kuviuza waweke Hela mfukoni.

Kanisa pia lilikuwa na hotel huko matema beach, hotel ambayo viongozi wakuu wa kanisa waliweka dhamana ili kupata mkopo wa mabilioni wa kujenga chuo kikuu, mkopo ulitolewa na fedha yote ikabebwa na wakuu wakanisa, benki walivyoanza kudai deni, wakuu wa kanisa harakaharaka wakatafuta mteja waiuze kwa bei ya kutupa. Mwaikali alipokataa hoteli isiuzwe, alitengenezewa zengwe na kufukuzwa kama mbwa, yaani askofu anafukuzwa kama mbwa na kulazwa rumande!

Pia yamekuwepo malalamiko kwamba shule za kanisa zinadorora, ada na fedha za wafadhili zimefanya wakuu wa kanisa wawe mabilionea wakiogelea kwenye fahari kuu. Na hata hospitali ya seliani Sasa ni mlango wa kuzimu, kwa kuwa haina huduma nzuri, na ukipelekwa pale, ni sawa na kusaini hati ya kifo
Wewe muongo!
Askofu Mwaikali alikuwa si mwaminifu kabisaa na wala usimtetee kujenga hija yako idiyo na miguu.
Ksulize Konde Dayosisi, Tshs 200 mil alizopewa Mwaikali kwa kuiuzia/kukodisha ofisi za Dayosisi Tukuyu zilienda wapi?
Kuna sharika Rungwe zilimpatia zaidi ya Tshs 60m ili wanunue mashamba ya miti Iringa, alikula hizo.
Nakushauri mtoa mada usikurupuke kwa mifano isiyo na tija.
 
Wewe muongi!
Askofu Mwaikali alikuwa si mwaminifu kabisaa na wala usimtetee kujenga hija yako idiyo na miguu.
Ksulize Konde Dayosisi, Tshs 200 mil alizopewa Mwaikali kwa kuiuzia/kukodisha ofisi za Dayosisi Tukuyu zilienda wapi?
Kuna sharika Rungwe zilimpstia zaidi ya Tshs 69m ili wanunue mashamba ya miti Iringa, alikula hizo.
Nakushsuri mtoa mada usikurupuke kwa mifano isiyo na tija.
Tutaliondoa kanisa mikononi mwa wahuni
 

Mapashkuna ya Dr Rev Kimaro
 
Kwamba tuhuma alizopewa mtu kama Dr Munga zote zilikuwa za kupika ili viongozi wa kanisa waibe viwanja?



Too good to be true! Wengine wanavuna walichopanda wenyewe.
 
Acha kumtukana Askofu Shoo.
Hapo amehusikaje ?
Malasusa ndiye anayehusika na Dayosisi ya Mashariki na Pwani na ndiye anayemsimamia Dr. Kimaro.

Kanisa la KKKT Lina katiba mbovu sana na ndiyo inayosababisha migogoro na wizi mkubwa ndani ya kanisa Hillo. Kanisa la KKKT ni Mali ya Maaskofu . Kila mmoja ana sharubu. Yaani Dr. Kimaro ni WA Malasusa na sio wa Dr.Shoo. Dr. Shoo Hana maamuzi yoyote juu ya Dr.Kimaro. Askofu mkuu alipaswa kuwa na mamlaka makubwa juu ya maaskaofu wote wa KKKT na kuweza hata kuwahamisha kwenye Dayosisi nyingine. Ndio maana Vitega uchumi vya KKKT vinakufa kila mahali Kwa sababu wengi sio waaminifu na hawana sifa za kusimamia miradi Hi hiyo
Mimi ni MKKKT na hicho ukichosema kuhusu katiba ni ukweli mtupu na nmekuwa nikisema kila siku.

Angalia mfano yule Bagonza wa karagwe jinsi alivyo na mapembe!

Yani KKKT ni moja lakini humo ndani ina vipande vingi balaa.
 
Mim sijaenda KKKT miaka karibu 10 sasa....Sadaka inapangwa kutoka juu, eti usharika huu mtoe kiasi fulani...basi hapo harambee za kijinga jinga tu.....ni wakati sasa wa maaskofu kutuachia kanisa
Dah blaza hatuchekani
 


Mchungaji Hananja akihojiwa na Bongo5 (ingia YouTube, kaongea nusu saa nzima) ameeleza uonevu mkubwa wanaofanyiwa na viongozi wakuu wa kanisa, na anasema yeye aliandikiwa barua na kiongozi mkuu wa kanisa kumsimamisha kazi bila mshahara kwa mwaka mzima, bila sababu yoyote ile.

Hananja anasema alikataa barua ya kiongozi mkuu wa kanisa kwa kuwa si muajiri wake,

Hananja ameeleza kwamba kanisa linapitia maumivu makubwa kwa sababu ya unyanyasaji na roho mbaya sana, na visasi walivyonavyo viongozi wakuu wa kanisa Hilo.

Hananja ameeleza kwamba viongozi wakuu wako katika wimbi kubwa la kuuza viwanja vya kanisa, na wachungaji wanapohoji, wanafukuzwa na kunyanyaswa sana.


=====

Kuna taarifa kwamba mchungaji Kimaro, kupitia Utumishi wake, kijitonyama imenunua viwanja vya mamia ya mamilioni, na kujenga majengo ya thamani kubwa, na kuna hisia kwamba wakuu wa kanisa wanataka kuviuza waweke Hela mfukoni.

Kanisa pia lilikuwa na hotel huko matema beach, hotel ambayo viongozi wakuu wa kanisa waliweka dhamana ili kupata mkopo wa mabilioni wa kujenga chuo kikuu, mkopo ulitolewa na fedha yote ikabebwa na wakuu wakanisa, benki walivyoanza kudai deni, wakuu wa kanisa harakaharaka wakatafuta mteja waiuze kwa bei ya kutupa. Mwaikali alipokataa hoteli isiuzwe, alitengenezewa zengwe na kufukuzwa kama mbwa, yaani askofu anafukuzwa kama mbwa na kulazwa rumande!

Pia yamekuwepo malalamiko kwamba shule za kanisa zinadorora, ada na fedha za wafadhili zimefanya wakuu wa kanisa wawe mabilionea wakiogelea kwenye fahari kuu. Na hata hospitali ya seliani Sasa ni mlango wa kuzimu, kwa kuwa haina huduma nzuri, na ukipelekwa pale, ni sawa na kusaini hati ya kifo

Zaidi soma: Mchungaji Eliona Kimaro wa KKKT Kijitonyama apewa likizo ya siku 60 na kutakiwa kuripoti Makao Makuu

Kwani hii kkkt ni ya malasusa? Ni wakati sasa waumini wamsusie kanisa abaki yeye na familia yake.

Watu mngejua siri ya haya makanisa mngeokoa mipesa yote mnayowachangia ili waishi maisha ya kifahari
 
Back
Top Bottom