Mdada katendwa kabakia haamini kama ni yeye ...

Mdada katendwa kabakia haamini kama ni yeye ...

FirstLady1

JF-Expert Member
Joined
Jul 29, 2009
Posts
16,789
Reaction score
5,401
Huyu mdada ni jirani yangu..

Alikuwa na ka mtindo fulani kila siku anamsifia husband wake ooh ndoa yangu ni imara na ni kama paradise ndogo
Mme wangu hawezi kurudi saa mbili usiku kama waume zenu wanavyofanya nashangaa mie.!
Akitoka kazini moja kwa moja home
Nawahurumia nyie waume zenu kurudi home saa tano..sita ,akiwahi sana saa nne mnawezaje haya maisha ..?
Sifa nyingi zilimiminika kwa huyu dear husband
..Mama mmoja wa makamo alikuwa mara nyingi akimwambia temea mate chini mdogo wangu,
Haya mambo omba mungu aendelee kumtunza mmeo
LOL sasa limezuka la kuzuka
Ghafla mme kaanza kurudi saa mbili eti ooh nilikuwa na washikaji
Ikaenda saa sita kulikuwa na vikao vya dharula kazini nisamehe my wife
Ikafikia sasa anarudi asubuhi ooh nilikuwa night shift siku hizi nimekuwa potential sana kazini wife
Ghafla picha ya mrembo mmoja kwenye screen ya simu..oops
Simu inakumbatiwa wakati zamani ilikuwa inakaa popote pale
Mara trip za hapa na pale zikaendelea

Vunja kazi mzee kamtakia wife Mie bila kumuoa huyo dada wa kwenye screen ya simu nitajiua ..makubwa ……
***Based on true story ****
Jamani tuendelee kuwaweka kwenue maombi wenza wetu
Tuziombeee ndoa na familia zetu
Amani itawale daima

Nawakilisha

FL1- Mama Mwenye Nyumba
 
FL1, pole yake! ila pia fundisho, ni kama uwe na mtoto wa kike ndani, halafu we kutwa kunanga majirani wenye watoto wa kike vicheche, wallah huwa yanarudi hapa hapa duniani, vyako vinakuwa si vicheche tena, bali nungunungu!
 
Duh...kwa hiyo solution ni nini?
Wapeni waume zenu mapenzi msiwabanie ila mkiombwa mchezo mmbaya kataeni kwani mtaharibiwa tu na kukimbiwa
 
duuu.. m simwamini wangu hata siku moja...hahahaa pole yake huyo mtu...wanaume bana hta kama cheating ni nature inabidi tuibue na sisi cheating ni ATIFISHO mambo gan haya.
 
makubwa haya mambo ya kusifia sifia ovyo ni vyema kukaa kimya na kumshukuru mungu kwa yote
Hii ndoa yangu ni paradise ndogo hii naona sasa inamtokea puani
Apige goti chini na kuomba mungu
 
Nilishawahi kusema hapa wakati fulani kwamba wanawake wengi wanaumia kwenye ndoa kwa sababu ya kuwasifu waume zao kwa mashoga kupita kiasi, si vibaya kumsifia mumeo kwa mashoga lakini pale yanapotokea mabadiliko kama haya usione aibu kusema umeshindwa na kuangalia mustakabali wako upya, kila mtu ameoa au kuolewa kwa utashi wake na hamna sababu ya mahusiano yenu au ndoa yenu kushikiliwa na majirani, marafiki au ndugu, kama yamekushinda bwaga manyanga anza maisha mapya, mambo ya kuanza kuwaza eti,...... "hivi majirani, ndugu au marafiki watanionaje?" yamepitwa na wakati, ndoa ni yako na sio ya kwao, anayeumia ni wewe na wala sio wao, na kama wakikuzodoa kwa kukusimanga wakikwambia ........ "kiko wapi ulichokuwa ukiringia...." Wao haiwahusu kwani wao wana maisha yao na wewe una maisha yako, kama alikuwa na tabia nzuri ni wakati ule,.......... Sasa kama amebadilika na kuwa na tabia za kiasherati wewe ufanye nini.......? Mtu hukuzaliwa naye tumbo moja, amelelewa kwao na wewe umelelewa kwenu, mmekutana ukubwani, kisa cha kutoana roho kwa sononi na msongo wa mawazo ni nini....!?
Kila mtu anaweza kuchukua ustaarabu wake kwani huo sio mwisho wa maisha.... na maisha ni popote, hata kama ukisemwa au kusengenywa na mashoga thamani yako iko pale pale wala haiondoki, ni wewe tu unayeweza kuiondoa kwa kujishusha na kujiona dhalili mbele ya binadamu wenzio..............
 
FL1,

Mpe pole sana huyo dada. Bahati mbaya ni too late ila huu wimbo unamfaa sana!!



Babu DC!!!
 
Last edited by a moderator:
Nilishawahi kusema hapa wakati fulani kwamba wanawake wengi wanaumia kwenye ndoa kwa sababu ya kuwasifu waume zao kwa mashoga kupita kiasi, si vibaya kumsifia mumeo kwa mashoga lakini pale yanapotokea mabadiliko kama haya usione aibu kusema umeshindwa na kuangalia mustakabali wako upya, kila mtu ameoa au kuolewa kwa utashi wake na hamna sababu ya mahusiano yenu au ndoa yenu kushikiliwa na majirani, marafiki au ndugu, kama yamekushinda bwaga manyanga anza maisha mapya, mambo ya kuanza kuwaza eti,...... "hivi majirani, ndugu au marafiki watanionaje?" yamepitwa na wakati, ndoa ni yako na sio ya kwao, anayeumia ni wewe na wala sio wao, na kama wakikuzodoa kwa kukusimanga wakikwambia ........ "kiko wapi ulichokuwa ukiringia...." Wao haiwahusu kwani wao wana maisha yao na wewe una maisha yako, kama alikuwa na tabia nzuri ni wakati ule,.......... Sasa kama amebadilika na kuwa na tabia za kiasherati wewe ufanye nini.......? Mtu hukuzaliwa naye tumbo moja, amelelewa kwao na wewe umelelewa kwenu, mmekutana ukubwani, kisa cha kutoana roho kwa sononi na msongo wa mawazo ni nini....!?
Kila mtu anaweza kuchukua ustaarabu wake kwani huo sio mwisho wa maisha.... na maisha ni popote, hata kama ukisemwa au kusengenywa na mashoga thamani yako iko pale pale wala haiondoki, ni wewe tu unayeweza kuiondoa kwa kujishusha na kujiona dhalili mbele ya binadamu wenzio..............
umenikuna haswa! umeongea ki.com haswaaaaaaaa! kudos babu mtambuzi!
 
FL1, pole yake! ila pia fundisho, ni kama uwe na mtoto wa kike ndani, halafu we kutwa kunanga majirani wenye watoto wa kike vicheche, wallah huwa yanarudi hapa hapa duniani, vyako vinakuwa si vicheche tena, bali nungunungu!
cacico mdada kabiki amechanganyikia ila duniani kweli kuna mambo ya ajabu sana
Nikiwaza huyo mmewe wa ndoa leo anamtamkia bila kumuoa fulani najiua
Wakati unasema hayo hukumbuki watoto,mke ,na ndugu zako
Inashangaza sana
 
Last edited by a moderator:
Nilishawahi kusema hapa wakati fulani kwamba wanawake wengi wanaumia kwenye ndoa kwa sababu ya kuwasifu waume zao kwa mashoga kupita kiasi, si vibaya kumsifia mumeo kwa mashoga lakini pale yanapotokea mabadiliko kama haya usione aibu kusema umeshindwa na kuangalia mustakabali wako upya, kila mtu ameoa au kuolewa kwa utashi wake na hamna sababu ya mahusiano yenu au ndoa yenu kushikiliwa na majirani, marafiki au ndugu, kama yamekushinda bwaga manyanga anza maisha mapya, mambo ya kuanza kuwaza eti,...... "hivi majirani, ndugu au marafiki watanionaje?" yamepitwa na wakati, ndoa ni yako na sio ya kwao, anayeumia ni wewe na wala sio wao, na kama wakikuzodoa kwa kukusimanga wakikwambia ........ "kiko wapi ulichokuwa ukiringia...." Wao haiwahusu kwani wao wana maisha yao na wewe una maisha yako, kama alikuwa na tabia nzuri ni wakati ule,.......... Sasa kama amebadilika na kuwa na tabia za kiasherati wewe ufanye nini.......? Mtu hukuzaliwa naye tumbo moja, amelelewa kwao na wewe umelelewa kwenu, mmekutana ukubwani, kisa cha kutoana roho kwa sononi na msongo wa mawazo ni nini....!?
Kila mtu anaweza kuchukua ustaarabu wake kwani huo sio mwisho wa maisha.... na maisha ni popote, hata kama ukisemwa au kusengenywa na mashoga thamani yako iko pale pale wala haiondoki, ni wewe tu unayeweza kuiondoa kwa kujishusha na kujiona dhalili mbele ya binadamu wenzio..............

Sawa ila sasa huyo mwanamke alikuwa anajimwagia misifa kwa watu ili iweje?

Hata wakimsimanga kwa sasa sitamuonea huruma!! Kama angechukulia mambo yake na mume wake kivyake vyake, kwa sasa angekuwa na mambo kidogo tu ya kumshughulisha....Ila sasa inabidi aanze kuhangaika na jinsi ya kudeal na hao majirano aliokuwa anawakoga....Malipo ni hapa hapa duniani!!

Babu DC!!
 
Duh...kwa hiyo solution ni nini?
Wapeni waume zenu mapenzi msiwabanie ila mkiombwa mchezo mmbaya kataeni kwani mtaharibiwa tu na kukimbiwa
Saint Ivuga kwani tunawanyima nini wakiomba ?ila wakishaonja huko nje ndo matatizo yanaanza ..
Kuna kaka mmoja huwa anasema jamani mie nikioa mke wangu ruksa kuniwekea Libwata maana haka ka tabia niliko nako sijui kama nitakaacha....
 
Last edited by a moderator:
duuu.. m simwamini wangu hata siku moja...hahahaa pole yake huyo mtu...wanaume bana hta kama cheating ni nature inabidi tuibue na sisi cheating ni ATIFISHO mambo gan haya.
Vaislay huyu baba ukimuona na vituko vyake ni vitu viwili tofauti kweli maisha hayatabiriki...
 
Last edited by a moderator:
Nilishawahi kusema hapa wakati fulani kwamba wanawake wengi wanaumia kwenye ndoa kwa sababu ya kuwasifu waume zao kwa mashoga kupita kiasi, si vibaya kumsifia mumeo kwa mashoga lakini pale yanapotokea mabadiliko kama haya usione aibu kusema umeshindwa na kuangalia mustakabali wako upya, kila mtu ameoa au kuolewa kwa utashi wake na hamna sababu ya mahusiano yenu au ndoa yenu kushikiliwa na majirani, marafiki au ndugu, kama yamekushinda bwaga manyanga anza maisha mapya, mambo ya kuanza kuwaza eti,...... "hivi majirani, ndugu au marafiki watanionaje?" yamepitwa na wakati, ndoa ni yako na sio ya kwao, anayeumia ni wewe na wala sio wao, na kama wakikuzodoa kwa kukusimanga wakikwambia ........ "kiko wapi ulichokuwa ukiringia...." Wao haiwahusu kwani wao wana maisha yao na wewe una maisha yako, kama alikuwa na tabia nzuri ni wakati ule,.......... Sasa kama amebadilika na kuwa na tabia za kiasherati wewe ufanye nini.......? Mtu hukuzaliwa naye tumbo moja, amelelewa kwao na wewe umelelewa kwenu, mmekutana ukubwani, kisa cha kutoana roho kwa sononi na msongo wa mawazo ni nini....!?
Kila mtu anaweza kuchukua ustaarabu wake kwani huo sio mwisho wa maisha.... na maisha ni popote, hata kama ukisemwa au kusengenywa na mashoga thamani yako iko pale pale wala haiondoki, ni wewe tu unayeweza kuiondoa kwa kujishusha na kujiona dhalili mbele ya binadamu wenzio..............
Mtambuzi umeongea maneno mazuri na yenye hekima sana ikiwa na maana inatupasa tujitambue na tujue tunahitaji furaha maishani mwetu,,umenigusa moyoni barikiwa
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom