Elections 2010 Mdahalo wa Dr Slaa Movenpick LIVE

Elections 2010 Mdahalo wa Dr Slaa Movenpick LIVE

Ngoja tusubiri watakavyotoka sisi m kesho manake Rais Mtarajiwa ameongea kwa kujiamini kabisa. Tutamsikia mzee anayelisha familia yake kwa propaganda bw(bi?) tembweleza.
 
tunamshukuru sana Dr Slaa ameweza kuchakachua vyema msimamo wa chadema kabla na baada ya uchaguzi
Ninavyo jua mimi Kuchakachua ni kubadilishabadili/kuangaunga, je hapo juu uliimanisha nini au hili neno maana yake nini?
 
Ukiwa msafi utanyoosha kidole kwa mafisadi. But ukiwa mchafu nomaaaaaaaaaaaaaaa.
 
Anaongelea nyumba za Tembe na Majani, mtu ananyumba imekaribia kuanguka lakini ameweka picha ya chagua kikwete, anashangaa sana.
Dr. ana data ya pesa ambazo CCm wamelipia mabango na hayajalipiwa ushuru, anasema kama haya yanawezekana kutapanya mabango nchi nzima, je elimu ya mtoto wako haiwezekani,

Kama unaweza kwenda kunywa chain a obama, kwa nini useme elimu bure haiwezekani?
Dr. anasema yuko tayari kula mihogo ikulu ila elimu iwe bure.
Anasema pesa ziko zimesambaa kote kwenye idara za serikali, kinachotakiwa ni uwajibikaji. Anasema kila mahali kuna uchafu, miezi ya kwanza ni kurekebisha na kurejesha uwajibikaji. Kwenye swala hili ametoa mifano kibao alipokuwa somewhere mawilayani.

Anataarifiwa kuwa zimebaki dakika saba, anatoa points za mwisho mwisho

Anawashukuru sana watanzania
Anawaomba radhi majimbo ambayo ameshindwa kufika leo kwa sababu ya wimbi zito
Anasema katika siku 71 ni vigumu kufika majimbo yote hata kwa kutumia helikopta, ila anawaomba wote kura zao.
Anasema yeye hataki kuona damu ya mtanazania inamwagika
Anasema Tanzania itakuwepo hata baada ya uchaguzi
Anasema kwa siku nane zilizobaki, ukipigwa kofi basi geuza la pili maana hautakufa
Anasema, ukitaka kumuumiza aliyekupiga, wewe mpuuze, inauma zidi ya kulipiza kisasi
Anamwomba kikwete awe makini, anasema vurugu zitaletwa na serikali, na polisi na watendaji wengine, ametoa mifano ya mwanza, ambapo hakulindwa na polisi, vijana wakajitokeza kumlinda.
Mwisho, anawaomba watanzania wote wampatie kura, Chadema ni Tumaini jipya, makofi kibaoooo, anasema tuanze mabadiliko pamoja

Anasema hataki kuona watu wanalala kwenye nyasi, na tembe; kwa kuondoa kodi katika vifaa vya ujenzi.
Anasema Elimu ya bure inawezekana, atalisimamia swala hilo ili vijana wetu wapate matumaini mapya,

La mwisho kabisa, kuna maswala yanamgusa mtanzania wa kawaida ambayo hawajayazungumzia kwa kuwa hawajafanya utafiti, ila watashughulikia ili watanzania wawe na maisha bora ya kweli.

Kwamba, maendeleo yaitakiwi yawe ya vitu bali ya watu.

Mwisho, Asanteni sana na poleni kwa Spell error, ni kwa sababu speed ya kuongea na kuandika ni tofauti.

Tuko pamoja,

MC
Mkuu bila kuomba radhi umetenda haki kabisa.
kwangu hakuna tv wala redio leo kwani umeme ulikwenda kitambooo. Nilikuwa online nakusoma na kusoma chat ya best wangu hapa alikuwa ananitumia aliyoyasema rais
 
kumbe ndo maana kinana alisema ushindi sio lazima
 
mmh.....kikwete anakazi ya ziada.Kwahii ya leo imemmaliza,natamani tungekuwa na uwezo wa kuisambaza copy ya debate hii kila mahali hasa vijijini waisikilize na watambue umakini wa chadema.........
CHADEMA OOOOYEEEE!
 
Hilo swali la mgombea mwenza kalijibu vizuri sana.. Aisee Dr Slaa ni kiboko! CCM Kwisha kazi....

nadhani vibaraka,makada na wadau wa thithiem kama vile thalma,ridhi,miraj,mkamb,jw,jeykey,na kinana wamepata heart attack baada ya kusikiliza mdahalo wa slaa,ile familia ya ikulu sijui iko katika hali gani now
 
JK ndo anapoona kuwa kuongoza nchi sio lelemama..unakutana na vichwa kama Dr.Slaa unategemea nini?
 
Dogo ananiambia home Ifakara watu wamelipuka kushangilia utadhani Asoamoah Gyan kasawazisha goli ile siku ya Ghana na Uruguay
 
Fabulous! What a performance!!!:thumb::thumb::thumb::thumb::thumb::thumb:!The future is open!
 
Malaria Suguuuuuuuuu uko wapi jamani hahahahahahahhhaaaa aibuuuuuuuu
 
kwasababu alijua kabisa haya mambo yatatokea

yaani naongea na dogo huku kijijini kwetu Ifakara ananiambia ile mdahalo kuisha watu wamelipuka kushangilia as if kuna mechi Taifa Stars imeifunga Spain
 
Dogo ananiambia home Ifakara watu wamelipuka kushangilia utadhani Asoamoah Gyan kasawazisha goli ile siku ya Ghana na Uruguay


home kwenu ifakara? duh nimesoma machipi high school yani unanikumbusha far kweli especialy siku kama ya leo ambayo tumemwona rais wetu live akizungumza na kujibu maswali kwa ushindi
 
malaria suguuuuuuuuu uko wapi jamani hahahahahahahhhaaaa aibuuuuuuuu

baada ya hii ya leo.....malaria sugu yuko kwa raj patel wanafanya mipango ya kuikimbia nchi mapema kabla ya 31/oct.....hawana chao kwa raisi wetu mpya baada ya muheshmiwa slaa kutangaza wazi bila chenga kwenye kitu itv na sio tbc ccm,msimamo wake juu wa wazandiki.........
 
Tupeni mambo jamani tuliombali tunawategemea sn ndg zetu wahabarishaji.
Mungu ibariki Tanzania,Mungu mbariki PhD Slaa & Development and Democratic Part(CHADEMA),
Chama makini na watu makini sn wanao jali maisha ya wa TZ.
 
Back
Top Bottom