Elections 2010 Mdahalo wa Dr Slaa Movenpick LIVE

Elections 2010 Mdahalo wa Dr Slaa Movenpick LIVE

kwa maana hiyo mbowe asahau uwaziri mkuu maana yeye labda atakuwa mbunge wa hai au sio aidha zito asahau uwaziri wa madini!!!!!!

Logic ni kwamba waziri sio lazima awe mbunge na sio mbunge hatakiwi kuwa waziri.
Ndo nilivyoelewa.
 
Swali la Lwaitama kuwa awaondoe hofu wazee yeye akiwa kama mwanachama mfu wa CCM.
Mzee mgomvi huyu
 
mmh.....kikwete anakazi ya ziada.Kwahii ya leo imemmaliza,natamani tungekuwa na uwezo wa kuisambaza copy ya debate hii kila mahali hasa vijijini waisikilize na watambue umakini wa chadema.........
CHADEMA OOOOYEEEE!
Jamani vijiji vya sasa bongo si kama vile vya 2005. Watu wanauelewa mkubwa sana na wana TV kwa wingi baada ya madish kupungua bei.
Isitoshe kwa sasa hivi wana sisi m wenyewe wanamkubali kiasi kwamba hata huko vijijini wanapiga kampeni wenyewe kwamba achaguliwe Dr Slaa.
 
kwa maana hiyo mbowe asahau uwaziri mkuu maana yeye labda atakuwa mbunge wa hai au sio aidha zito asahau uwaziri wa madini!!!!!!

Swala la kuteua waziri asiye mbunge ni sawa kabisa kwani unaondoa ile conflict of interest itakayotokea baina ya kuwa mtendaji wa serikali na mtunga sheria na mwanasiasa hivyo hilo litasaidia kuondoa ukungu tulionao wa mawazo ya kisiasa kuingilia utendaji wa serikali.
 
Mdahalo umefanyika na DR kama ningekuwa judge ningempa 90%. Amejibu maswali vizuri sana na ametangaza sera za chadema kwa utulivu bila jazba. Mungu tunakushukuru kwa uliofanya na tunaomba uendelee kuwa nasi katika siku zilizosalia. watanzania mmemsikia Dr akielezea namna atakavyotekeleza ahadi zake kwa ujasiri ,anamaanisha ,
 
Naona jamaa wa kijani wameanza kuja, wanataka kumsaidia Mkwere kupangua hoja za Dakta.
 
Hivi kule kwa Blog ya Michuzi unaweza kuta mambo bomba kama haya yanawekwa wazi hivi? Hasa mdahalo huu uliokuwa ukiendelea? Ebu wapenzi wa michuzi naomba maoni yenu!
 
hivi kule kwa blog ya michuzi unaweza kuta mambo bomba kama haya yanawekwa wazi hivi? Hasa mdahalo huu uliokuwa ukiendelea? Ebu wapenzi wa michuzi naomba maoni yenu!

ukiona jf wamewacha kupost kupitia you tube huu mdahalo wa slaa ujue slaa ameboronga sana!!!
 
Kwa wale ambao hatukuona ITV baada ya umeme kutatika mtatusaidiaje tumuone rais wetu Slaa wa awamu ya 5? Je kuna redio au TV ambayo itarusha marudio ya mahojiano ya rais Dr Slaa?

Tunaomba wanaohusika watusaidie tumwone au kumsikiliza rais Slaa, redioni au kwenye TV. Tunampenda Rais wetu Dr. wa ukweli Slaa.
 
Dr Slaa amezungumza vizuri sana. Kwa yeyote yule mwenye mapenzi ya kweli na Tanzania na alibahatika kuangalia kipindi kile ni lazima ampe kura Dr Slaa, vinginevyo mtu huyo haitakii mema nchi yetu. Nilikuwa nimekaa na wadada wawili ambao wote kabla ya mdahalo kuanza walisema kura zao watampa Kikwete na wabunge wa CCM hata kabla ya kipindi kuisha walikuwa wamebadili mawazo na kusema kwamba kura zao watampa Dr Slaa na wagombea ubunge wa chadema. Hongera sana Rais Mtarajiwa Dr Slaa, hongera sana chadema kwa kuwa makini sana katika kampeni zenu zilizowawezesha kuzikonga nyoyo nyingi za Watanzania.

Well, Kuzungumza sio kuongoza... kuongoza ni zaidi ya kuwa na nia... kama kuna mtu alikuwa na nia nzuri huku duniani alikuwa JK 2005... but you all know....

Kuna mengi sana ameyajibu vizuri kama debate lakini practically mmhhh... only people who know how to lead will understand... otherwise washabiki wa JK in 2005 they have just got another one to shabikia...
 
Mie nimefurahia jinsi Dokta alivyokuwa anatoa Broad issues za msingi kuelezea vision yake.

Ni tofauti na ukimsikiliza Mkwere, yeye anatumia muda wote kudanganyia project ndogondogo ntaleta bomba la maji, ntaleta meli, ntajenga zahanati. Mambo hayo si issues za kampeni ya urais, ni mambo ya bajeti.

Dokta amenikumbusha zile kampeni za akina Obama, na juzijuzi za kina Cameron an Cleg. Tunataka hivyo Mgombea Urais tupe vision yako.

Well done Dokta, umevuna kura nyingi leo!!!
 
Back
Top Bottom