Megastructures mlizozipinga zimeibadili taswira ya Tanzania, mlikurupuka kumkosoa Rais Magufuli

Megastructures mlizozipinga zimeibadili taswira ya Tanzania, mlikurupuka kumkosoa Rais Magufuli

naona unavyojitaidi kuitetea serikali utadhani anko anapitia kusoma comment za kila mtu hapa

natetea ama nasema ukweli? we kama unasubria serikali utasubiri sana! na uendelee kusubiri ivo ivo
 
natetea ama nasema ukweli? we kama unasubria serikali utasubiri sana! na uendelee kusubiri ivo ivo
au wewe ndio jiwe mwenyewe naona unatuenjoy tu hapa jf
Mimi lazima niisubiri serikali sababu wao walizunguka nchi nzima wakituambia watatupa ajira sasa inakuaje Leo waanze kugeuka vitu walivyotuaidi wenyewe
 
Magufuli bus terminal ni ya kisasa zaidi. Kuwa nje ya mji sio sababu kuwa haina ubora wa kimataifa.

Hizo kevel tatu sio sababu ya kuwa ya kisasa kama Magufuli bus station
Sikushangai. Wakati wa kampeni za uchafuzi mkuu kuna mtu alisema Arusha itakua kama California, Tanzania itakua kama ulaya. Sasa tumeshaipita SA, pengine Mungu akijalia mwaka mmoja au miwili ijayo tutaifikia Ulaya. Lakini usisahsu waalimu bado wanasubiria laptop na wanakijij wanasubiria milioni 50.
 
Sikushangai. Wakati wa kampeni za uchafuzi mkuu kuna mtu alisema Arusha itakua kama California, Tanzania itakua kama ulaya. Sasa tumeshaipita SA, pengine Mungu akijalia mwaka mmoja au miwili ijayo tutaifikia Ulaya. Lakini usisahsu waalimu bado wanasubiria laptop na wanakijij wanasubiria milioni 50.
Endelea kusubiri nao sisi tunapanda mpunga.
 
Magufuli bus terminal ni ya kisasa zaidi. Kuwa nje ya mji sio sababu kuwa haina ubora wa kimataifa.

Hizo kevel tatu sio sababu ya kuwa ya kisasa kama Magufuli bus station
Level tatu si kea maana ya ghorofa , kwa maana ya kukutanisha mabasi , taxi rank pamoja na metro rail underground , mind you upande mwingine kuna ile treni ya umeme .

Watanzania tuna tatizo kubwa la exposure , kama kweli umewahi kufika park station halafu ulinganishe na stendi ya mbezi basi ,una tatizo kubwa.
 
Leta picha za Jo'burg Park station na hizi Magufuli stations tufanye comparison kabla hatuja endelea na mjadala
Achana na lijinga hilo hata Jo'burg Jiji analisikia tu halijafika na kama lina picha ya hiyo Station litakuwa limeokota jalalani Manzese. Wenzetu wanabomoa Bus Stations mijini kupisha matumizi mengine kwa sababu usafiri wa Mabus umepitwa na wakati wala masoko mijini wameachana nayo miaka mingi wao ni Supermarkets hata gari utapata, Shopping Centres, Malls na unafanya shopping ukiwa umetulia nyumbani. Badala ya Mabus wenzetu ni Treni za kisasa kama Bullet za Japan na China, TGV za Ufaransa, ICE za Ujerumani, Maglev na nyingine nyingi zote hizi spidi zao sawa na za Bombardier za Magufuli. SGR siyo ya Kisasa ila nchi za EAC ziliamua kuwa na Gauge moja kubwa kuliko zilizopo na spidi yake ya maili 100 kwa saa ni karibu sawa na ya gari lako binafsi. Watanzania wengi wanaangalia Chato iliyo kama Ulaya basi wanalinganisha na chochote kinachojengwa popote kwingineko nchini na kuona ni mafanikio makubwa ya kuigwa duniani.
 
Manispaa ya ubungo itakuwa inapata bil 7+ kwa mwaka kupitia Magufuli bus terminal, unadhani hazitamsaidia mwananchi wa kawaida? Au unakaririshwa kukosoa tu?
Una uhakika zitaenda kumsaidia mwananchi wa kawaida, au zitatumika kumalizia ujenzi wa Ikulu yenu ya kifahari kwa ajili ya PK mtarajiwa?
 
Megastructure sio za mtu inabidi zijengwe kwa kuzingatia long term plans na city master plan inasemaje na mahitaji kwa wakati husika..., unaweza ukajenga kitu kikawa a white elephant...

Kwahio ujenzi wote mkubwa lazima uzingatie michango ya wadau / wataalamu na wahusika wa pande zote sio mmoja tu kuamua najenga hiki au kile..... Mpaka sasa kama nchi tungekuwa tuna long term na short term plans za nini kinajengwa na wapi na kwa faida ya nani Tangia Enzi za Mwinyi hawa viongozi kazi yao ni kutekeleza tu....

Sio kiongozi atakayekuja sababu anatoka Gamboshi aamue kwamba mji uhamie Gamboshi (kabla hajamaliza muda wake tupate kiongozi wa Ukara) na yeye aamue ujenzi wake...., Kwa precedence hii tunaweza tukawa na nchi ya unfinished projects
[emoji38][emoji38][emoji38][emoji38][emoji38]Eti kiongozi wa ukara.
Kwani mkuu zile flyovers,sgr na stendi mpya ya mbezi zinanufaisha watu wa gamboshi na ukara peke yake
 
1) serikali ni kampuni ya kuhudumia wananchi, inategemea mapato ili itoe huduma kama kampuni zingine tu!
2) Tegemea kuona maskini wengi zaidi miaka ya mbele, unless watu watakapoamua kupata elimu!
3) jinsi tunavoenenda, yawezekana wananchi wengi wakaingia kwenye umaskini mkubwa sna unless serikali ifanye umafia! dunia sasahv ni nchi moja mtu anaweza kwenda kufanya kazi au kuanzisha biashara kokote duniani!

kama basi dunia imekua this remote na wananchi bado wanalilia serikali basi tuna safari ndefu sana kutoka kwenye huu umaskini, yaani imefika hatua kuna mtu kama bezoes ana utajiri wa $200B sawa sawa na uchumi wa tanzania miaka minne! meanwhile mtanzania kama wewe bado umelalia malalamiko serikali ivi una akili kweli wewe?
Dawa inayo wafaa nyinyi ni mapinduzi tu. Hakuna namna. Hamuwezi kutuumiza mtaani kwa kisingizio cha kujenga hiyo miundombinu yenu.
 
serikali its for the people ila haina uwezo wa kuajiri nchi nzima, na hakuna serikali duniani inaweza kuajiri nchi nzima, infact kodi tanzania its only 18% and what your expecting ni kuajiri nchi nzima? akili unazo timam?

--- Dunia inaelekea kwenye kitu kinaitwa decentralised systems, meaning mifumo isiopitia serikalini mfano kwenye monetary kuna kitu kinaitwa block chain, izi haziwi controlled by any government mfano bitcoin, je tukisha decentralise kila kitu utamtupia nan lawama zako?
Ndiyo haiajiri watu wote ndoana tabaka la wanaostahili kuajiliwa nchini ni asilimia 10 ya watu wote
Meaning illiterates na ambao hawajasoma Tanzania ni wengi Sana. Hiyoa asilimia 10 haiwezi kushindikana kuajirika. Sema siyo kipaumbele Cha jpm. Kipaumbele chake ni kuona watu wanakufa lakini barabara zinajengwa
 
Wapinzani wa Tanzania wanakasumba mbaya sana. Wao kila jambo ni kukosoa tu.

Wakiona serikali inajenga shule,hospital, barabara au stendi ya mabasi wao ni kukosoa tu.

Nimeshuhudia mabadiliko makubwa sana kwenye miji yetu tangu JPM awe rais.Naweka baadhi ya mifano. Nilishuhudia mkoa wa Singida ukipata stendi mpya ya kisasa iliyogharaimu bil 12 +.

Pia tumeshuhudia stendi mpya ya kisasa jijini Dodoma na soko kubwa la kisasa la Ayubu Ndugai. Stendi mpya ya mabasi ya Magufuli ni ya kutiliwa mfano. Maana ni zaidi ya Johanesburg park station.

Wapinzani tokea JPM aingie madarakani mlikuwa mnakosoa na kumdhihaki kuw ni mzee wq kupenda Megastructures. Je, sasa hamuoni zilivyobadili taswira ya taifa letu? Hamuoni kuwa ni kaendeleo makubwa na miundo mbinu ya kisasa ambayo itaongeza mapato kwa taifa?

My take; Tusipende kukosoa kila kitu,hata mradi wa JNHPP ukikamilika itakuwa ni Megastructure inayotusaidia.
Wanakuja kukupinga mkuu
 
Back
Top Bottom