Meli kubwa ya mizigo yashindwa kukwamuliwa katika Mfereji wa Suez kwa siku ya tatu

Meli kubwa ya mizigo yashindwa kukwamuliwa katika Mfereji wa Suez kwa siku ya tatu

Sijazifatilia kwa miaka ya karibuni ila upo mwaka tulikutana na meli ya ukubwa huo Hong Kong na dock ya Singapore mabaharia mnabaki mnashangaa tuu imebeba contenna utadhani viberiti...
Hii iliyokwama Suez ina uwezo wa kubeba ngapi chief.
 
Hii ishu italeta msongamano wa Meli na tujiandae kwa uhaba wa baadhi ya bidhaa.
 
Ishaso
Inatakiwa wawaite Wanorway hiyo kitu ni dakika chache tu wanaitoa. Walitaka kuitoa Kusik ile nyambizi ya Puttin akaona ni kudhalilika
Ishasogezwa hiyo pembeni ngoma zinapita hizo tug zina nguvu kama nyati zilikua karibu nane ngoma lazima isogee wakati dock inasogezwa na tatu tuu.
 
Kwa 40ft huwa zinapungua mpaka 12,000 boxes ila twenty ni 20,000 boxes kwa meli nyingi kubwa haiwezi kubeba idadi ya 40ft na 20 ft sawa
Inabeba 20,000 TEU's hizi ni 20 ft ina maana kama ni 40ft zinakuwa 10,000. Haiwezi kuwa 12,000.
 
Hapa nimekuelewa maana kuna meli kubwa sana za mafuta huwa zinakuja na kuishia kule kigamboni ambapo tpa wana pipe yao ya kunyonya mafuta kuyaleta huku pwani......ilo dude pale halipiti
Fikiria basi siku likaja halafu likakwama kuanzia kule wavuvi wanakoegesha madau yao mpaka kule meli za Bakhresa zinakopakia abiria wake.Sijui itakuwaje siku hiyo.Safari zote kwenda Kigamboni itabidi zipitie Kurasini kwa miezi kadhaa mpaka waje mabeberu kuikwamua.
 
Anavyosema imepewa uwezo wa kuingiza meli kubwa anamaana ya kuwa Meli kubwa inaingia na inaishia baharini kwenye mkondo wa maji makubwa,kisha inakuja meli yetu ndogo inapakua mzigo kisha unaenda kushusha bandarini,ndivyo uelewa wangu huo
Hapo gharama inaongezeka au inapungua ?
 
Ni changamoto kweli.Safari hii kimbunga cha mchanga inaonekana kimechangia kujaza kifusi ndani ya Suez.Wapunguze jeuri na kupitisha bidhaa haramu.Mwenyezi Mungu akikasirika anaweza kuufukia mfereji wote kwa dakika moja tu ikawa kama zamani.
Nguruwe za mchina na heineken za mholanzi zinapita hapo
 
Shughuli ya kuondoa meli kubwa ya mizigo iliyokwama katika mfereji wa Suez nchini Misri na kuziba njia kwa vyombo vingine vya maji kupita imeingia siku ya tatu hii leo bila mafanikio yoyote.

Jitihada za kugeuza meli yenye uzito wa tani 220,000 na urefu wa mita 400 iliyopewa jina Ever Given inaendelea leo baada ya mapumziko mafupi usiku, huku shughuli hiyo ikihofiwa kuchukua wiki kadhaa ikiwa uamuzi wa kupakua makontena yote yaliyopo kwenye chombo hicho utafikiwa kabla ya kukigeuza.


Kukwama kwa meli hiyo katika mfereji wa Suez kumesababisha mrundikano wa vyombo vingine vya maji zaidi ya 150 katika bahari ya Mediterania na Bahari ya Shamu vikisubiri kukwamuliwa kwa Ever Given.

Meli hiyo iliyosajiliwa nchini Panama inayoendeshwa na kampuni ya Taiwan ilipoteza mwelekeo katika mfereji huo kutokana na upepo mkali uliofikia mwendokasi wa kilometa 50 kwa saa na kuifanya kuegama upande hivyo kuziba njia kwa vyombo vingine vinavyopita katika mfereji huo.

Mfereji wa Suez hupitisha hadi meli 50 kwa siku, na takriban asilimia 12 ya safari zote za baharini hupitia katika mfereji huo. Baada ya maboresho yaliyofanywa na serikali ya Abdel-Fattah al-Sisi mwaka 2015, mfereji huo uliweza kupitisha meli kubwa zaidi duniani, ikiwamo Ever Given yenye uwezo wa kubeba makontena 20,000 kwa wakati mmoja.

Kuendelea kuzuiwa kwa mfereji huo kunamaanisha kuwa bidhaa za chakula, mafuta na bidhaa za viwandani zinashidwa kupitishwa kutoka mataifa ya Ulaya kwenda Mashariki ya Mbali na kutoka Mashariki ya Mbali kwenda Ulaya. Mbali na changamoto za kiuchumi, uwepo wa meli iliyokwama baharini kunaongeza hatari ya kiusalama kutokana na kuongezeka kwa matukio ya uharamia katika nchi za Mashariki ya Kati katikati ya mzozo baina ya Iran na Marekani.

View attachment 1734064

Chanzo: The Guardian
419910_76c83468dde8183507f05dcc6a86025e.jpg
 
Back
Top Bottom