Uchaguzi 2020 Membe anaweza kutuvusha upinzani kuliko Lissu

We ni ccm, hili suala nadhani halikuhusi! Hapa tunataka kujadiliana wapinzani tu,
Membe tuvushe upinzani 2020
 
Wewe utakuwa ni li-ccm, malizaneni na mwenyekiti wenu huko lumumba. Hapa ni upinzani tu
Twende na Membe 2020
Naona Liumumba mna taka kuwapangia upinzani baada ya nyie kuandaa fomu moja
 
Wewe sio CDM na hujawahi kuwa. Membe ndio mgombea pekee tunayemuhitaji upinzani
Ndugu yangu mimi ni CDM damu! Nasema kuwa tutashinda na wasitutangaze, tutafanya nini? ndiyo hoja yangu
 
Sikiliza, Lissu yupo vizuri lakini hana ushawishi kuliko Membe. Lissu bado wakati wake
Sasa hivi twende na Membe
Membe ni chaguo lako wewe na nani??
Kama unamtaka mpeleke Lumumba awe mgombea mwenza wa jiwe!!
Safari hii hatuyumbi tunakuja mazima mtaipatapata!!
Lissu for Presidence. Period!!
 
Una chuki binafsi na Membe. Membe ndio karata turufu kwa upinzani, na tupo tayari kumpatia nafasi, hutaki kalale
Tanzania itakuwa chini ya kwa zaidi ya miaka 50 ijayo,ndio ukweli ingawa unauma!!huwezi kumtenganisha Membe na CCM!!!UPinzani ukiingia kwenye tego hilo basi
 
Sikiliza, Lissu yupo vizuri lakini hana ushawishi kuliko Membe. Lissu bado wakati wake
Sasa hivi twende na Membe
Lissu hana ushawishi labda kijijini kwenu, Tanzania hata mtoto ndogo anamjua Lissu.
Huyo Membe anajuljkana na wana CCM.
Hiyo karata ya jokeri ya Membe tumeisha ishutukia, once biten shy!!
Peleka mtu wenu CCMb CUF au NCCR agombee huko, CDM a big NOOO!!
 
Sikuona hata mpinzani aliyejiandaa kwenda ikulu nafuu hata halima mdee yuko serious kidogo.

Uchaguzi unafika ndo kila mtu anataka urais.

Upinzani mme experience kugoma full time kugoma, bungeni almost muda wenu wote mko nje mnagoma.

Mtahimili kuibeba dola au ndo mkiudhiwa mtakimbilia ulaya kulia lia huko na kuitelekeza nchi.

Anzeni kukomaa ili miaka ijayo muaminike.
 
Tuliza akili bro, huyu jamaa ni jasusi na ana mbinu zote za kuwezesha upinzani kushinda uraisi mwaka huu. Ni karata turufu


Mbinu za umafia na wizi kweli anazo , jaribuni kumchukua mafia hilo utakuwa ndio mwisho wenu
 
Hakuna mtu yyte anayetoka CCM kupewa dhamana na upinzani bado hatujawa wapuuzi kiasi hicho boss
 
Huo ni utopolo. Labda kama kuna chama kitakubali kujidhalilisha kwa kumpa nafasi hiyo lakini siyo upinzani kwa ujumla wake.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…