Uchaguzi 2020 Membe: Kuhusu suala la urais hilo halina mjadala, nitajitosa na nitashinda

Uchaguzi 2020 Membe: Kuhusu suala la urais hilo halina mjadala, nitajitosa na nitashinda

Mbwa kala mwanae...hasa ule upinzani wa ndani ndio umeanza rasmi. Hebu chadema na AcT tuachieni uwanja tutifuate. Huu mtifuano hatutaki kugombelezewa....mtuache jameni.
 
Bernard Kamillius Membe waziri wa zamani wa Mambo ya nchi za Nje na uhusiano wa kimataifa, anazidi kukoleza mbio za kuwania urais katika uchaguzi mkuu wa 2020 ndani ya chama cha Mapinduzi CCM. Anaripoti Yusufu Katimba.

Taarifa za hivi karibuni zinasema Membe ambaye alikuwa waziri kwa miaka minane ya utawala wa Jakaya Kikwete, ameapa kujitosa katika kinyang'anyiro cha kumpinga rais wa sasa John Pombe Magufuli.

"Kuhusu suala la urais hilo halina mjadala tuombe Mungu niwe mzima. Nitajitosa na nitashinda." Amenukuliwa mwanasiasa huyo akiwaeleza baadhi ya wafuasi wake wa karibu ndani ya chama hicho.

Amesema, "Katika hili siwezi kurudi nyuma na hayupo anayeweza kunishawishi kurudi nyuma. Nitagombea, nitajitosa katika kinyang'anyiro hicho kwa kuwa nina kila sababu ya kufanya hivyo."

Kupatikana kwa taarifa kuwa Membe amepanga kujitosa katika mbio za urais 2020, kutaweza kumaliza mining'ono kuwa kwa muda mrefu kiongozi huyo amekuwa akiendesha mikakati yake kimya kimya ya kumkabili Magufuli ifikapo 2020.
Mh Membe popote ulipo, tambua una KURA yangu tayari.

Kazi kwako....
 
Mbwa kala mwanae...hasa ule upinzani wa ndani ndio umeanza rasmi. Hebu chadema na AcT tuachieni uwanja tutifuate. Huu mtifuano hatutaki kugombelezewa....mtuache jameni.
Sisi zetu kuni tu
FB_IMG_1563969418216.jpeg
IMG-20190731-WA0004.jpeg
 
Self-explanatory.

Naona jamaa anaendelea tu kuwakata watu maini. Watajuuuta kumchokonoa!


View attachment 1173321
Inaudhi kupita kiasi kwa wahusika, kuhusu 'vijimambo' vya namna hii vinavyochokonoa chokonoa, lakini haviumi vya kutosha kujibu mapigo.
Utaanzia wapi kujibu mapigo ya uhakika kwa 'vimaneno' kama hivi! Unabaki tu unaumia ndani kwa ndani.

Hii ni mikakati ya ajabu sana!
 
Tunaisubiri kwa hamu 2020 tujinywee juice ya maembe
Nalog off
 
Kwa kuwa huyu jamaa ashawahi/bado ni kachero si dhani kama hii shauku alionayo ni halisi. Napata mashaka sana asijekuwa yupo kazini tu.
 
Kuna tukio litamtokea uyo jamaa atapotea mazima kwenye ulimwengu wa siasa za Tanzania na itabaki historia.

Tokea aanze kukubali sauti ni yake kuna kitu anakitafuta ila akili nyingi wameshamstukia ndio maana hamna mtu ndani yq chama anabishana nae.
 
Huyu mzee sidhani kama ana akili sawa sawa kwa sasa. Kwanza umri wake tu unasuggest anapitia serious mental condition ya midlife crisis.

Ukisikia uzee kuja vibaya ndio hivi sasa. Hizi ndoto za mchana, badala akae na wajukuu zake afurahie maisha anaanza upuuzi.

Ndio. Maana life expectancy ipo chini Tanzania sababu watu wakifika umri unaotakiwa wawe na utulivu wao ndio wanaanza fujo.
 
Huyu mzee sidhani kama ana akili sawa sawa kwa sasa. Kwanza umri wake tu unasuggest anapitia serious mental condition ya midlife crisis.

Ukisikia uzee kuja vibaya ndio hivi sasa. Hizi ndoto za mchana, badala akae na wajukuu zake afurahie maisha anaanza upuuzi.

Ndio. Maana life expectancy ipo chini Tanzania sababu watu wakifika umri unaotakiwa wawe na utulivu wao ndio wanaanza fujo.
Akili zimeanza kuwa siyo sawa baada ya kusema anagombea urais?
 
Kuna la ajabu hapo mpaka usiamini, huoni juzi kakiri kuwa sauti iliyodukuliwa ni ya kwake? Kama ameweza kukiri yale atashindwa kuzungumza hayo? Ukweli ni kuwa kuna wanaccm wengi hawaridhishwi na namna Magufuli anavyoongoza chama chao na nchi kwa pamoja kwani kajigeuza kuwa mkubwa kuliko chama na nchi. Sasa huyo Membe anachofanya ni kumuonyesha kwamba yeye sio mkubwa kuliko chama au nchi, hivyo yuko tayari kupambana naye ili kumuonyesha hana madaraka zaidi ya hayo anayopaswa kuwa nayo.

Mimi ninaamini Membe hawezi kuwa rais mzuri, lakini huyu wa sasa sio mzuri pia. Na pia tulishatoka kwenye kuongozwa kwa vitisho na kusujudia viongozi. Sasa hivi tunataka kiongozi anayeheshimu wananchi sio anayeogopwa na wananchi kisa anapandikiza hofu. Kama ni maendeleo tungeweza kuyapata hata chini ya wakoloni, lakini uhuru wetu ulikuwa na maana kuliko maendeleo ya wakoloni.
''KAMA NI MAENDELEO TUNGEWEZA KUYAPATA HATA CHINI YA MKOLONI, LAKINI UHURU WETU ULIKUWA NA MAANA KULIKO MAENDELEO YA WAKOLONI''
ahsante sana!
 
Miundombinu inajengwa kwa kodi za wananchi na sio hisani au mshahara wa rais. Hivyo miundombinu itajengwa na yoyote hata kama nchi itakuwa haina rais kwani mipango ya nchi ipo tayari.
We jamaa ujue una akili sana! YANI UMEJUA KUNITENGENEZEA SIKU YANGU !
LIMEBARIKIWA TUMBO LILILOKUZAA!
 
Nimekutana nayo mahali
 

Attachments

  • Screenshot_20190806-142552.png
    Screenshot_20190806-142552.png
    39.7 KB · Views: 29
Magufuli anatufaa sana kwa sasa. Ninatamani ashinde kwa kishindo na aendelee na uongozi. Wanaotaka kugombea siwapingi maana ni haki yao kwa mujibu wa katiba. Lakini kwa mtazamo wangu kwa sasa tunamhitaji mh. Magufuli kuliko hao wengine.
 
Back
Top Bottom