Membe: Musiba na Mchange anayewatuma kunichafua kwanini hamnipeleki mahakamani? Kama mnaweza kunirekodi mmeshindwa nini kutoa huo ushahidi

Membe: Musiba na Mchange anayewatuma kunichafua kwanini hamnipeleki mahakamani? Kama mnaweza kunirekodi mmeshindwa nini kutoa huo ushahidi

Membe tulia. Ulitaka Serikali ijibu uzushi ?
kati yako na membe nani anajua serikali? mkitumwa uliza vizuri: je, ikitokea njiani tukakutana na shushushu mbobezi na mwanadiplomasia nguli ( lavlov like) tufanyeje? unauza sura?
 
Anaandika Bernard Membe.
Rondo- Lindi.

Watanzania Wenzangu! Nawasalimia! Kwa siku tatu mfululizo magazeti ya makuhani wa fitina na unafiki Musiba na Mchange na wenzao wamekuwa wakinishambulia kwa uchochezi wa sintofahamu iliyotokea kuanzia Alhamisi tarehe 17 Octoba siku ambayo Mhe Rais ameondoka Lindi kuelekea Dar hadi Jumapili ya tarehe 20. Mimi nipo Kijijini kwangu Rondo kwa mwezi mmoja sasa.

Ni nini hicho nilichokisema au kukiandika kwenye mitandao ya kijamii? Kwa kuwa mawasiliano yangu yote nayafanya kwa simu yangu ambayo inasikilizwa na kudukuliwa, naviomba vyombo vinavyohusika vitoe hadharani mazungumzo na maandishi yangu ili watu wasikie, wasome na wanihukumu. Napenda niuhakikishie umma kuwa Mimi sikuwa mjinga! Nilijua kuwa nikisema au kuandika vibaya, wabaya wangu wataninyooshea vidole.

Sikuingia kwenye mitego yao hiyo. Mimi kama Watanzania wote wenye akili za kawaida nilishangazwa sana na ukimya wa Serikali huku damage na rumours zikiwa zimetanda kote nchini bila kuzitolea maelezo kwa siku 3 mfululizo! Mhe. Rais ni kiongozi wa Umma. Inapotokea sintofahamu au upotoshaji wowote ule, ulikuwa ni wajibu wa Msemaji wa Ikulu au wa Serikali kukanusha na kuweka mambo sawa kama wanavyofanya siku zote.

Vinginevyo wale wenye akili za mbilikimo na makuhani wa unafiki wanachukua mwanya huo kutunga ya kwao ili kumfurahisha Mhe. Rais. Good governance requires quick response to rumours. Rumours left unattended damages governance! Narudia! Naviomba vyombo husika vitoe hadharani nilichokisema au kupost kwenye mitandao ili nihukumiwe na Wananchi wenyewe na sio na Wabwekaji wa Taifa.

Ben Membe.
Rondo- Lindi.View attachment 1241102View attachment 1241103
Hili JITU lipo SMART kichwani hadi linatia hasira. Yani linatupa MAWE kwa Mkulu kupitia kwa wabwekaji wa taifa.
 
muwe mnafanya utafitikwanza bila kulopoka tu. et trason ni kwa rais wa nchi tu...

treason
trēzən]

NOUN

high treason (noun) · high treasons (plural noun) · treasons (plural noun) · petty treason (noun) · petty treasons (plural noun)
  1. the crime of betraying one's country, especially by attempting to kill the sovereign or overthrow the government.
    "they were convicted of treason"
    synonyms:

    treachery · lese-majesty · disloyalty · betrayal · faithlessness · perfidy · perfidiousness · duplicity · infidelity · sedition · subversion · mutiny · rebellion · high treason · Punic faith
    antonyms
    :

    allegiance · loyalty
Wewe ni bogus kweli unafikiri ki-academically sana umekwenda ukabeba general definition ya treason. Mimi naongelea definition according to our Penal Code wewe vuvuzela!!
 
Membe arudishe tu mabilion ya Watanzania aliyopora kutoka libya

Jamhuri ikiamua kumshitaki atafilisika


Pia sio vizuri kuwatumia vijana kubweka mtandaoni kuisema serkali

Tuendelee kumuunga mkono mh Rais Kwa uchapa kazi
Huyo unaetaka tumunge mkono yuko wapi mbona hatumuoni ktk Tv
 
Sikubaliani na Membe.

Ilichokifanya serikali nadhani ndicho kilikuwa sahihi.

Kwamba, tetesi za kijuha na kipumbavu, ni vyema kuzipuuza kwa maneno lakini pia kuzijibu kwa vitendo ndani ya muda mzuri.

Rais kujitokeza na kuendelea kufanya kazi zake, lilikuwa ni jibu murua kabisa kwa majuha wote walioshiriki kutunga na kueneza uzushi wao.

Hivyo ndivyo inavyotakiwa.

Msemaji wa serikali akianza kujibu kila aina ya uzushi, kufanya hivyo ni kuubariki na kuuhalalisha uzushi huo. Serikali itafanya hivyo kwa mangapi? Maana uzushi na uongo ni sehemu kubwa sana ya hii mitandao ya kueneza na kujazana ujinga.

Safi sana serikali. Safari hii mmetenda vyema.

Mhhhh mtu mwenyewe alivyokuwa sura utadhani alilala kwenye barafu
 
From jasusi mbobezi to mtu wa kujibizana mitandaoni...maisha yanaenda kasi sana.
 
Kile kiwanda chenu cha kupika majungu na upotoshaji kimebaki uchi sasa,tupu zenu nje
Kusingiziwa kufa kwa magonjwa yenu mnalalamika wiki nzima lakini nyie kukusudia kuua kwa kupiga risasi 38 kwa mtu mnaona kawaida na mnakataza watu hata kumuombea? Mnashangaza kweli
 
Sikubaliani na Membe.

Ilichokifanya serikali nadhani ndicho kilikuwa sahihi.

Kwamba, tetesi za kijuha na kipumbavu, ni vyema kuzipuuza kwa maneno lakini pia kuzijibu kwa vitendo ndani ya muda mzuri.

Rais kujitokeza na kuendelea kufanya kazi zake, lilikuwa ni jibu murua kabisa kwa majuha wote walioshiriki kutunga na kueneza uzushi wao.

Hivyo ndivyo inavyotakiwa.

Msemaji wa serikali akianza kujibu kila aina ya uzushi, kufanya hivyo ni kuubariki na kuuhalalisha uzushi huo. Serikali itafanya hivyo kwa mangapi? Maana uzushi na uongo ni sehemu kubwa sana ya hii mitandao ya kueneza na kujazana ujinga.

Safi sana serikali. Safari hii mmetenda vyema.

Sometimes mtetee vinavyoteteeka....

Mr President anazushiwa ugonjwa na si ugonjwa tu bali MAUTI kabisa na kweli kwa siku tatu mfululizo akiwa hajulikani aliko (kitu ambacho si kawaida yake) unasema ni kitu ambacho hakikupaswa kuchukuliwa hatua yoyote ku - calm situation????

Si hiyo tu bali katika hizo siku tatu "when he was missing", kulitokea kwa kukatisha ziara yake ghafla tu akiwa huko Lindi/Mtwara akiwaacha wananchi waliokuwa wanamsubiri huko dismayed, yet unasema ni hali ya kawaida na serikali haina sababu ya kutolea maelezo hali hiyo?? Really?

Membe is absolutely right 100%.

Iko shida serikalini whether we like it or not. Na kama ilikuwa ni mbinu yao ya kupotezea kitu fulani wanachojua wao, then they totally lost their calculations...!!
 
Anaandika Bernard Membe.
Rondo- Lindi.

Watanzania Wenzangu! Nawasalimia! Kwa siku tatu mfululizo magazeti ya makuhani wa fitina na unafiki Musiba na Mchange na wenzao wamekuwa wakinishambulia kwa uchochezi wa sintofahamu iliyotokea kuanzia Alhamisi tarehe 17 Octoba siku ambayo Mhe Rais ameondoka Lindi kuelekea Dar hadi Jumapili ya tarehe 20. Mimi nipo Kijijini kwangu Rondo kwa mwezi mmoja sasa.

Ni nini hicho nilichokisema au kukiandika kwenye mitandao ya kijamii? Kwa kuwa mawasiliano yangu yote nayafanya kwa simu yangu ambayo inasikilizwa na kudukuliwa, naviomba vyombo vinavyohusika vitoe hadharani mazungumzo na maandishi yangu ili watu wasikie, wasome na wanihukumu. Napenda niuhakikishie umma kuwa Mimi sikuwa mjinga! Nilijua kuwa nikisema au kuandika vibaya, wabaya wangu wataninyooshea vidole.

Sikuingia kwenye mitego yao hiyo. Mimi kama Watanzania wote wenye akili za kawaida nilishangazwa sana na ukimya wa Serikali huku damage na rumours zikiwa zimetanda kote nchini bila kuzitolea maelezo kwa siku 3 mfululizo! Mhe. Rais ni kiongozi wa Umma. Inapotokea sintofahamu au upotoshaji wowote ule, ulikuwa ni wajibu wa Msemaji wa Ikulu au wa Serikali kukanusha na kuweka mambo sawa kama wanavyofanya siku zote.

Vinginevyo wale wenye akili za mbilikimo na makuhani wa unafiki wanachukua mwanya huo kutunga ya kwao ili kumfurahisha Mhe. Rais. Good governance requires quick response to rumours. Rumours left unattended damages governance! Narudia! Naviomba vyombo husika vitoe hadharani nilichokisema au kupost kwenye mitandao ili nihukumiwe na Wananchi wenyewe na sio na Wabwekaji wa Taifa.

Ben Membe.
Rondo- Lindi.View attachment 1241102View attachment 1241103
Vikaragosi vya watawala vinamuogopa sana Membe !
 
mkewe anajua yuko wapi?
ungekuwa nyumba ndogo yake ungejua yuko wapi.
Akisha kubali cheo kile mahali alipo sio siri tena! Sasa mnamficha kwa nini?
Ngojeni walete uzushi tena kuwa yuko GAMBOSHI anatibiwa ndio mtakapo imba "hauwezi kushinda....." hadi sauti ikauke.
 
Kuna kila sababu ya kuanza kuamini kuwa hii nchi inaongozwa na waganga wa kienyeji na ushirikina.....

Mtu anakatiza hotuba kimiujiza ujiza tu na ktk mazingira ya kama kichawi hivi akiwa jukwaani akihutubia wananchi na kwa sababu iyo hiyo anakatiza ziara nzima bila maelezo....

Anawaacha watu/wananchi waliokuwa wanamsubiri katika maeneo mengine dismayed na bado kuna watu wanatetea kuwa haina haja kwa serikali kutoa maelezo kwa umma kuhusu kilichompata Rais hadi kukatiza ziara???

Then Rais ktk mazingira hayo hayo anapotea kwa siku tatu. Haikujulikana yuko hospitali gani wala kwa babu mganga gani wa jadi kama aliugua ghafla iwe ni ugonjwa wa kawaida au usio wa kawaida....

Nyuma unavuma uvumi mkubwa unaozua taharuki nchi nzima kuwa Rais ni mgonjwa na wengine wakisema amekufa, yet tunaona ni jambo la kawaida tu lisilohitaji maelezo ya serikali yenyewe??

Mmh, sijui kama tunafikiri vyema!
 
Kwa hiyo membe unavyosema akili za mbilikimo unamaanisha hawana akili watu wa hivo aisee we ni mbaguzi wa hatari na mchochezi katika taifa hili lea wajukuu uongizi kwa sasa ushau
Ndiyo maana nasubiri uhakikisho kuwa habari hii imeandikwa na mwenyewe!!!!Ama wanamzushia.
 
Back
Top Bottom