Membe: Sikushangazwa kufukuzwa. Niliendelea kusimamia nia yangu kugombea Urais 2020. Mwenyekiti na Katibu wameratibu mimi kufukuzwa

Hivi kweli Membe anaamini alikuwa tishio kwa JPM ndani ya CCM?

He can’t be serious.
Ni kweli hakuwa tishio ila alithubutu kutema mate mahali patakatifu. Kule kuthubutu kusema; I will challenge you ilitosha kumwambia what you are doing is not good. Sasa nnani mwingine amethubutu?? Hakika; Zidumu fikra sahihi za m/kiti
 
Hilo ni bomu la ccm la kisiasa kwa UKAWA kama walivyokuwa lowasa na sumaye
Wala siyo bomu. Wewe huoni sisiemu kilivyopata tabu kushindana na Lowasa? Kilikuwa katika hali mbaya sana 2015 kiasi cha kupoteza majimbo mengi na mgombea wao JPM akapata ushindi mdogo katika historia ya chaguzi za vyama vingi. ccm wanajuana wenyewe na ukiwapambanisha wanakomoana balaa. Maalim Seif ni CCM wa zaman unaona anavyohofiwa Zenj kule? Mengine ya kurudi ccm huo ni uchumia tumbo wa kawaida kwa wanasiasa wa tz bara maana kuna wakati njaa inahama kutoka eneo lake la asili na kukaa kichwani na unakuta politician anatoa maamuzi mabovu balaa.
 
Media ni silaha muhimu sana kwenye propaganda

Jr[emoji769]
Ni kweli ila hastahili kupata attention yote hii. Analazimisha kukubalika. Ukiondoa hapa JF na twitter, huko kwa wapiga kura hakuna mwenye habari naye, wala hutosikia akitajwa kama anayeweza kushinda nafai ya Urais majina tunayokutana nayo ni mengine kabisa.
 
Oohhoo!!kumbe ni ndoto binafsi !! NIkajua yuko driven na spirit ya utumish kuwatumikia watanzania.
Sasa kwenye ndoto yako ww mzee, je ndoto zetu sisi na za taifa zina reside wapi????
 
Membe unachelewaa

Tuna hasira na hiyo kima
 
Magu mwenyewe anasema BWM kwake ndiyo kila kitu, bika yeye asingefika hapo alipo. Hata hiyo nafasi yake ni mipango yake, usitegemee akamtupa
 
U know nothing bro. Hao uliowataja ukijua visa vyao hata wewe ungekuwa Meko ungewatumbua vizuri tu... Huyo Mwandosys alikuwa akipita mitaani yeye ni kupond tu Rais hajamaliza hata miezi 6 ameanza kumchafua mitaani
Kumchafua rais ndio kupoje ?
 
Membe kamwe hawezi kuwa Rais wa nchi hii,mchezo walomfanyia Lowassa na yeye kafanyiwa. Yeye kakatwa jina kwa kufukuzwa kwenye chama. Magufuli ndo CCM kwa sasa.
Kitu CCM mnajivika upofu ni kutojua tu..
Jinsi gani Watanzania wanahitaji mbadala wa hiyo dikteta uchwara..

Yani Membe akicheua tu... Tunalala nae.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…