Meneja wa Uwanja wa Benjamin Mkapa, Gordon Nsajigwa atumbuliwa, Sasa kupangiwa Majukumu mengine

kama kisa cha kufukuzwa ni hicho sawa... lakini mamlaka imkanye pia yule shabiki wetu wa YANGA anayeingia na njiwa uwanjani... ule ni unyanyasaji na utesaji wa wanyama, haufai hata kidogo
uko sahihi kaka naitafuta ile clip
 
Msifiche ukweli kisingizio jeneza wakati mnajua manara aliwezaje kufanya kazi siku hiyo ya 6 na wao Kama wasimamizi wapo?
 

Simba wamponza Meneja Uwanja wa Mkapa,​



WAZIRI wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mohamed Mchengerwa leo tarehe 9, 2022 amemuagiza Katibu Mkuu wizara hiyo, Dk. Hassan Abbasi kumpangia majukumu mengine Meneja wa Uwanja wa Benjamini Mkapa, Godon Nsajigwa kwa kushindwa kusimamia matumizi ya uwanja huo. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Hatua hiyo imekuja ikiwa ni siku moja imepita baada ya Klabu ya Simba kuadhimisha sherehe za kilele ya Siku ya Simba ‘Simba Day’ na kuibu mjadala kuhusu baadhi ya burudani zilizotolewa na wasanii waliolikwa na klabu hiyo.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa kwa umma na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, John Mapepele imesema Meneja huyo anapangiwa majukumu mengine kwa kushindwa kusimamia matumizi endelevu ya Uwanja wa Benjamini Mkapa.

Dk. Abbasi akieleza utekelezaji wa agizo hilo, amesema tayari taratibu zimekwishaanza za kupangiwa majukumu mengine nna nnafasiuo hiyo inatarajiwa kusazwa mara moja.



Itakumbukwa kuwa katika tamasha hilo la Simba Day lililofanyika jana Jumatatu tarehe 8 Agosti, 2022, msaani wa Bongofleva, -Khalid Ramadhani Tunda maarufu kama Tunda Man aliingia katika uwanja wa Benjamini Mkapa akiwa amebebwa katika jeneza pamoja na msalaba uliokuwa na maneno ya dhihaka kwa watani wao wa jadi Yanga yaliyosomeka “Kifo cha Utopolo.”

Staili hiyo ya Tundaman kuingia katika tamasha hilo, imebua mjadala na kuwaibua baadhi ya viongozi wa dini akiwamo Askofu Msaidizi wa Jimbo Katoliki la Bukoba, Methodius Kilaini ambaye mapema leo amelaani kitendo cha klabu hiyo ya Simba kumruhusu msanii huyo kutumbuiza kwa kutumia msalaba na kufanya dhihaka.

Kitendo hicho Askofu Kilaini amesema ni “dharau na kufuru kubwa kwa waamini wakristu na wote wanaoamini walikombolewa katika msalaba huo.
 
Si ni sanaa tu, mbona tunaingilia burudani kwa mambo ambayo sio tangible na ni imani tu, kuna mtu hapo amepata hela kutengeneza hizo jeneza, kuna muuza chuma na midumari, muuza mba, msafirishaji, na wote probably wanalipia leseni zao serikali inapata kipato apo, Serikali yenyewe imefanya nini ? Kuajiri haiwezi kazi ni kukandamiza juhudi kwa kuwaza kama zama za Roma, tunapaswa kuwaza nje ya Box seeing the bigger picture.
 
Huyo msanii ni muislam! Kwann wasitumie imani za kiislam??
 
Halafu sijui ni kwa nini wasanii wa kiislam hupenda sana kutumia maudhui ya kikristo kufanya upumbavu wao!

Si angebebwa kwenye yale majeneza yao ya msikitini wanayotumia kubebea marehemu wao, halafu angewachukua wapambe wake wenye kanzu na barakashia, na makobazi miguuni!
 
Vyoo ni vichafu sana na maji hakuna,swali mamlaka haikuona kabla ya mechi?Na alishindaga meneja bora wa uwanja🤔
 
Huyo msanii ni muislam! Kwann wasitumie imani za kiislam??
Nani alisema kwamba jeneza ni dini ? Hata Yesu alizikwa kwa sanda kwenye pango bila jeneza, hizo ni tamaduni za kizungu tu zisitufanye tufarakane.
 
Jeneza kuingizwa uwanjani na msanii kunauhusiano Gani na Team ya SIMBA? Ni sawa na msanii kuingia uwanjani kwa kamba, akidondoka team nayo inahusukaje? Hilo ni manjonjo ya Msanii tu.
 
... haya matimu ya nchi hii hayajawahi kuwa na akili; bure kabisa.
 
Jeneza kuingizwa uwanjani na msanii kunauhusiano Gani na Team ya SIMBA? Ni sawa na msanii kuingia uwanjani kwa kamba, akidondoka team nayo inahusukaje? Hilo ni manjonjo ya Msanii tu.
Umesahau Gigy money aliwaponza Wasafi wakafungiwa
 
Mashindano ya Afcon yafanyike Tanzania kwa viwanja gani mlivyonavyo? Hako kauwanja kamoja?
 
Viongozi wote wa simba na wale walioigiza hilo tukio ni waislamu kwanini hawajaigiza kiislamu?

Bi chaunabe apigwe fine
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…