Menelik II: Mtawala wa kiafrika aliyekomesha ukoloni wa wazungu

Menelik II: Mtawala wa kiafrika aliyekomesha ukoloni wa wazungu

zitto junior

JF-Expert Member
Joined
Oct 7, 2013
Posts
20,537
Reaction score
31,729
Habari za asbuhi wana jukwaa moja kwa moja niende kwenye mada husika.

UTANGULIZI
Mfalme menelik II a.k.a Dagmawi sahle maryam menelik alikuwa mtawala wa Ethiopia kati ya 1889 hadi 1913 ambapo alianza kama mtawala wa eneo la shewa kuanzia 1866-1889. Alizaliwa mwaka 1844 na kufariki mwaka 1913 na inaelezwa alitoka kizazi cha uzao wa Queen of sheba (Makeda) na Mfalme suleiman. Menelik II alikuwa na uwezo wa kuongea lugha 7 ikiwemo kiingereza,kifaransa na kiitalia pia inaelezwa alikuwa msomi wa masuala ya usimamizi wa fedha(Finance) na ndio maana aliweza kuwekeza kwenye hati fungani huko marekani na kuwekeza kwenye migodi ya wabelgiji. Pia katika utawala wake alikuwa kwenye ndoa mara 3 ingawa hakuwahi kupata mtoto kwenye ndoa zote tatu lakini alizaa watoto nje ya ndoa na wote walikuwa mabinti.
images (40).jpg


UMAARUFU WAKE
Mfalme Menelik I anakumbukwa zaidi kwa kupambana na ukoloni wa kizungu katika nchi yake ambapo toka ashike madaraka mpaka anaondoka wazungu walishindwa kabisa kuitawala Ethiopia maana kila wakijaribu walikutana na nchi yenye dola kamili na kujitambua hta wakashindwa kujipenyeza na walipojaribu kuvamia walikutana na kipigo kikali. Pia menelik II anakumbukwa kwa kuitanua ethiopia hata kufikia mipaka kama iliokuwa nayo ufalme wa kush wa zamani uliofahamika kama Axum/Aksum.

VITA YA ADOWA
Kati ya mambo makubwa anayokumbukwa Menelik II ni vita ya Adowa ambapo Italia ilipokuwa amekuja Afrika kuchukua makoloni baada ya mikutano ya Berlin aliiteka somalia na Eritrea na hivyo alitaka na kuiteka Ethiopia ili kupanua utawala wake Afrika.

Italia ikaandaa Jeshi la watu 18,000 viliojipanga kwa brigedi 3 huku Ethiopia ikiwa na wanajeshi wenye uweledi,mafunzo na nidhamu zaidi ya 70,000 na viliongezeka hadi 120,000 vikiongozwa na ma Ras mbalimbali akiwemo mwanamama shujaa Taytu Betul ambaye aliongoza vikosi vya kutoka kaskazini akisaidiwa na kina Ras Makonnen na wengineo.

Usiku wa February 29 1896 vikosi vya Italia viliingia ndani ya Ethiopia katika eneo la Adowa hivyo waethiopia walipopata taarifa wakawazingira milimani wakiwasubiri kuwapa kipigo cha mbwa koko!!!
adwa-260x300.jpg


Brigedi ya Albretone kilikuwa cha kwanza kushambulia ila kilikutana na mizinga ya kutoka urusi iliotumiwa na jeshi la Ethiopia iliowadhoofisha sana na hata msaada ulipotoka kwa brigedi zingine za Italia chini ya Arimondi haukusaidia na maelfu walichinjwa pale huku Albertoni akikamatwa.

Brigedi ya mwisho kuleta msaada, chini ya Dabormida ilikuwa njiani kuja adowa ila majeshi ya kabila la Oromo chini ya Ras Mikael walimzunguka pande zote na kutoa amri wazungu wote wachinjwe kwa upanga na wote akiwemo Dabormida walikatwa vichwa!!!

Kufikia saa 6 mchana vikosi vyote vya Italia kikiwemo cha baratieri kule Mlima bellah vilisambaratishwa na wengi kujisalimisha kiufupi ndio vita iliishia hapa kwa kipigo kikali kwa wazungu.

MAFANIKIO
Tukiachana na vita ya Adowa pia Menelik I alijenga treni ya kisasa kutoka Ethiopia hadi Eritrea, Pia mfumo wa benki ulianza kwenye utawala wake bila kusahau umeme,magari na mfumo wa simu za mawasiliano yote haya Ethiopia walikuwa nayo kipindi bado nchi karibu zote za Afrika tulikuwa tupo gizani tukiuzwa utumwani!!!

UTUMWA
Menelik II hakupendezwa na biashara ya utumwa na katika wakati wake alikuwa akikushika unafanya biashara hii ya utumwa adhabu ilikuwa kukatwa mikono na chuki hii ya biashara ya utumwa ndio ilimchochea zaidi kuchukia ukoloni wa wazungu hapa Afrika akiwa tofauti na watawala wengine wakafrika walioona sawa kuuza waafrika wenzao utumwani.

HITIMISHO
Kupitia mfalme Menelik I Afrika tunapata fundisho kwamba maendeleo hayaletwi na mkoloni tu au misaada ya wazungu ndio maana Menelik II licha ya kuwakataa wakoloni ila bado aliweza kulinda uhuru wa nchi yake na kuwapa maendeleo ya kisasa bila kusubiri mzungu alete misaada na mikopo ya kinafiki, hili liwe somo kwa viongozi wa kiafrika kwamba tukiamua Afrika tunaweza kuwa bara la kuogopeka na lenye ushawishi kama alivyokua Menelik II hadi kupelekea nchi za wazungu kujaza balozi zao pale

Naomba kuwasilisha
menelik-ii-4.jpg
 
Last edited:
He was a real Hero of Africa..
Ila inatokana pia na misingi iliyoachwa na vizazi vilivyopita, kutokana na Historia yao pia toka vizazi na vizazi.

Alikua Rastafarian?
Hapana kufikia wakati anafariki Rastafarian movement haikuwa imeanza sababu ilianza wakati wa utawala wa haille selassie ambaye ndio aliitwa Ras Tafari ila huyu alikuwa muorthodox na ndoa zake zote za nyakati tofauti alifunga kanisani.
 
Hapana kufikia wakati anafariki Rastafarian movement haikuwa imeanza sababu ilianza wakati wa utawala wa haille selassie ambaye ndio aliitwa Ras Tafari ila huyu alikuwa muorthodox na ndoa zake zote za nyakati tofauti alifunga kanisani.
Siku zite nilidhani Menelik slikuwa ni rastafarai
Umetutoa tongotongo wengi
 
He was a real Hero of Africa..
Ila inatokana pia na misingi iliyoachwa na vizazi vilivyopita, kutokana na Historia yao pia toka vizazi na vizazi.
Ni kweli vizazi vilichangia maana unarithishwa maarifa ya utawala kutokea enzi za makeda na suleiman ni lazima tu alikuwa amepikwa vya kutosha kutawala ufalme mkubwa kama ule sio sisi huku hatuaandai viongozi mtu anakurupuka tu huko aliko anataka ubunge na Urais.
 
Hapana kufikia wakati anafariki Rastafarian movement haikuwa imeanza sababu ilianza wakati wa utawala wa haille selassie ambaye ndio aliitwa Ras Tafari ila huyu alikuwa muorthodox na ndoa zake zote za nyakati tofauti alifunga kanisani.
Naam mkuu nimeon alipelekwa kanisani japo alizikwa bila kutangazwa kifo chake.
Mkuu mbona imani ya Rastafarian inasemekana imeanza kitambo kabla ya H.Selasi
 
Italy mbona walikuwa na jeshi dhaifu tu hao hata Kinjeketile Ngwale angewapiga.

Ethiopia ashukuru Mungu aiseee angekutana na wajukuu wa Adolf Hitler mbona huyo Menelik kichwa chake kingekuwa makumbusho ya Munich sahivi.

Mjerumani mkatili sana
Hahahhaha mkuu hawakuwa wadhaifu kihivyo kumbuka walitoka kumtandika eritrea na somalia ambao ni majirani kabisa wa Ethiopia.... Sema tu walikutana na jeshi lililojipanga ila wangekutana na jeshi aina ya kinjekitile ngwale mbona Italia wangemkata kichwa Menelik II
 
Ni kweli vizazi vilichangia maana unarithishwa maarifa ya utawala kutokea enzi za makeda na suleiman ni lazima tu alikuwa amepikwa vya kutosha kutawala ufalme mkubwa kama ule sio sisi huku hatuaandai viongozi mtu anakurupuka tu huko aliko anataka ubunge na Urais.
Nimesoma Artcle ya House of Solomon wanasema kua hakuna ushahidi kua Menelik katokea kwenye Bloodline ya King Solomon. Is that true?
 
Naam mkuu nimeon alipelekwa kanisani japo alizikwa bila kutangazwa kifo chake.
Mkuu mbona imani ya Rastafarian inasemekana imeanza kitambo kabla ya H.Selasi
Kama ilikuwepo basi kwa jina jingine ila unaposema RAS TAFARI ni jina la kuzaliwa la Mtawala Haille Selassie ni sawa na CCM na TANU kwamba huenda kulikuwa na imani ya kama hyo lakini haikuitwa Ras Tafari sababu Ras Tafari imeanza kuitwa hilo jina miaka ya 1940 baada ya Haille Selassie kupambana na waitalia chini ya Benito Mussolini kwenye vita kuu ya pili ya dunia

Ngoja nimuite nyabhingi atupe nondo zaidi
 
Nimesoma Artcle ya House of Solomon wanasema kua hakuna ushahidi kua Menelik katokea kwenye Bloodline ya King Solomon. Is that true?
Kunaweza kusiwepo ushahidi wa moja kwa moja ila ile bloodline ndio ilikuwa inatoa watawala wa Ethiopia kwa miaka mingi hadi kufikia kwa Haille Selassie sasa sidhani kama waethiopia na uwekaji rekodi wote huo washindwe kutunza usahihi wa hili jambo.... Ingawa kutunza kitu kwa miaka 3000 sio rahisi ila bado kuna uwezekano kuwa ukoo ule ulikuwa bado unatambuliwa vizazi na vizazi
 
Huu Uzi unatosha kabisa kumwambia trump sasa basi.

Kinachotuumiza waafrica ni mapokeo, yaani wenye nafasi zao wapo kupokea tu hawataki kujiamini waaminiwe. Nimewahi kuwaza jf ilivo na hoja nzuri za kufundisha hivi hatuwezi kumchagua mmoja kisha tuanzishe chama ambacho kitaongoza nchi??? Naamini maendeleo yatakuja bila mzungu. Mshana Jr waziri wa sayansi[emoji122]

Nawasilisha
 
Kama hujafika. Anza na Misri kwanza, kisha nenda uyahudi/Israel hafu ndo uje Ethiopia ili kupata sequence nzuri ya matukio.
Misri nishafika Mkuu ,kuna Uzi humu wa Farao Tut,nilitaka kuweka pics lkn nikaona si poa ,bado Israel na Ethiopia, Israel nitaenda kupitia ziara /hija za kanisa katoliki tayari fungu lake lipo ,Ethiopia ndio naanza mkakati wa kwenda huko
 
Kunaweza kusiwepo ushahidi wa moja kwa moja ila ile bloodline ndio ilikuwa inatoa watawala wa Ethiopia kwa miaka mingi hadi kufikia kwa Haille Selassie sasa sidhani kama waethiopia na uwekaji rekodi wote huo washindwe kutunza usahihi wa hili jambo.... Ingawa kutunza kitu kwa miaka 3000 sio rahisi ila bado kuna uwezekano kuwa ukoo ule ulikuwa bado unatambuliwa vizazi na vizazi
Maybe wazungu wanapindisha pia. Wanasema blooodline ya Solomon imevunjika takriban mara mbili hadi kufikia 13Century ilikua ishasambaratika.
 
Misri nishafika Mkuu ,kuna Uzi humu wa Farao Tut,nilitaka kuweka pics lkn nikaona si poa ,bado Israel na Ethiopia, Israel nitaenda kupitia ziara /hija za kanisa katoliki tayari fungu lake lipo ,Ethiopia ndio naanza mkakati wa kwenda huko
Hongera sana mkuuu nenda Israel then Ethiopia ikikupendeza zaid nenda na Vatican. Utakua umetalii na kifaham karibu robo tatu ya ustarabu/Tamaduni/historia ya dunia.
 
Back
Top Bottom