MENGI aamua kuwabana wazushi

Halisi

JF-Expert Member
Joined
Jan 16, 2007
Posts
2,802
Reaction score
614
Nimekutana na taarifa iliyotolewa leo na wakili wa Mwenyekiti Mtendaji wa IPP Reginald Mengi, siku moja baada ya gazeti la Tazama kuandika habari na makala zenye muelekeo wazi wa chuki na jazba za wazi.

 
Last edited by a moderator:
ukitinga kwenye siasa tinga na dhambi zako zote na ujue jinsi ya kujitetea
 
Hili la zamani mbona.. yaani watu hata hawakumbuki habari hiyo iliandikiwa hata magazetini.? well, wanajitahidi kujaribu lakini.
 
Na nakumbuka ilitolewa maelezo ya kutosha kiasi kwamba watu wote walilizika hata waliotoa pesa walilidhika kuwa Bwana Mengi hausiki
 
ukitinga kwenye siasa tinga na dhambi zako zote na ujue jinsi ya kujitetea

Mkuu,

Hapo Mengi ametinga kwenye siasa zipi? Anagombea cheo gani?

Tatizo hapo ni Mengi kupigana dhidi ya ufisadi. Najua Mengi kama mfanyabiashara kuna makosa amefanya lakini bado yeye kwa Tanzania ni nafuu mno ukilinganisha na hao wanaotuibia kila siku.
 
Mafisadi watatafuta kila njia ya kumchafua Reginald Mengi kwa kuwa vyombo vyake vya habari vimewaanika vilivyo. Mwisho wa sikuu uongo unagonga mwamba tu. Pole ndugu yetu Mengi. Tuko nawe katika kukuombea ili wasikudhuru kwa chochote. Mungu akulinde kama tuilindavyo mboni ya jicho.
 
Unless sikuyaelewa vizuri maelezo ya mwanasheria ya Mengi lakini ilivyo ni kwamba hakukuwahi kuwa na hiyo NGO na hata pesa haziwahi kuombwa kutoka UNAIDS na wala benki statement haikuwa ya kweli. Kwa hiyo hapa kila kitu kilikuwa ni cha kupika ili kuharibu jina la Mengi. Cha kushangaza hawa jamaa wa TAZAMA waMeibuka upya na suala ambalo liliwahi kutolewa maelezo na likafungwa.

Ni siri iliyo wazi kuwa hawa wanatumiwa na mafisadi kupunguza kasi ya Mzee kupiga vita UFISADI. Wamekwama na tena kwa aibu kubwa!
 
Kwa kweli nashangaa sana jinsi hiyo makalana habari ilivyoandikwa kishabiki na jinsi walivyosahau hata kwamba suala hilo lilifikishwa hadi polisi kwa dci \manumba baada ya UNAIDS na NBC kukerwa na watu walioghushi
 
Kwa kweli nashangaa sana jinsi hiyo makalana habari ilivyoandikwa kishabiki na jinsi walivyosahau hata kwamba suala hilo lilifikishwa hadi polisi kwa dci \manumba baada ya UNAIDS na NBC kukerwa na watu walioghushi

Hao inabidi wachunguzwe, inaelekea wanawajua waliotekeleza mpango huo
 
Kwa kweli nashangaa sana jinsi hiyo makalana habari ilivyoandikwa kishabiki na jinsi walivyosahau hata kwamba suala hilo lilifikishwa hadi polisi kwa dci \manumba baada ya UNAIDS na NBC kukerwa na watu walioghushi

ebanae! hayo ndo mambo ya Karamagi et al., hilo gazet la TAZAMA TANZANIA linamilikiwa na Karamagi. Mafisadi wameanzisha magazeti haya kwa lengo la kujisafisha na kuwachafua wengine. kazi ipo!
 

Tuko pamoja katika hili.Hizi habari zishatolewa maelezo ya kutosha siku nyingi,inaelekea baadhi ya magazeti yanaanzishwa kwa malengo ya kuwachafulia majini watu.Tazama kila mara wanatoka na habari ya kumchafua Mengi!!!!!!!!!!!!!!!!.
 
mmh... mimi nadhani kifanyike kikao cha mafisadi ili kuwapa maelezo ya jinsi ya kupambana na wale wanaowaudhi kwani mbinu zao bado ni dhaifu sana. Mengi haitaji kwenye Baraza la Habari yeye awafungulie mashtaka mahakamani, na kuwadai fidia ya Bilioni 30 (akinigawia .005% ya kiasi hicho kwa ushauri huu haitakuwa na ubaya). Pamoja na hayo hilo gazeti pia liandike kwa maandishi makubwa yale yale kuwa "Tumechemsha kuhusu Mengi" ili awasamehe deni hilo!
 
Kwa kweli nashangaa sana jinsi hiyo makalana habari ilivyoandikwa kishabiki na jinsi walivyosahau hata kwamba suala hilo lilifikishwa hadi polisi kwa dci \manumba baada ya UNAIDS na NBC kukerwa na watu walioghushi


Kwa nini asilipeleke mahakamani moja kwa moja kwa kuandika habari ya uongo? huko MCT ni kupotezeana muda tu dawa ya watu kama hao ni kwafikisha kizimbani mara moja na kuomba mahakama ifungie gazeti hadi kesi iishe
 


Duh...kaka kumbe naona tumefikiri sawa apo!
 
Huyu Mzee anachemsha sasa....anashindana na MWEHU Charles Charles!!! Dawa yao hawa ni kuwadharau tu....kwanza gazeti lenyewe haliuziki na wanunuzi ni wajinga wenzao tu ambao wamejichokea....
 
Cha kusikitisha ni kwamba kiwango cha uandishi kilichoonyeshwa na Tazama kimeanza kuzoeleka, na tunaelekea kwenye udaku na ujinga; hawakufanya upembuzi kabisa kwa wanachokiandika... au labda wameamua kufanya hivyo ili ku-divert public attaention kwa sasa.

On a positive note; Ngalo kafanya cha maana, kaanzia kunakotakiwa (kwenye baraza lao), haya mambo ya mahakama kwa sasa in most cases ni uptezaji wa muda na ishara ya corrupt legal system ambayo everyone can run to (especially kama anajua kuna mwanya fulani). Naamini wataishia hapo maana Tazama wameandika utumbo mtupu.

Kizuri zaidi ni jinsi mafisadi wanavyoshuka hadhi mpaka wanafikia kufukua makaburi kutafuta cha kusema kuhusu Mengi, wanatapatapa na mifano ni mingi... sio wale tuliokuwa tumewazoea wakiwa na confidence, wide smiles everywhere na authority, wamerudi kuwa na kauli kama za watu waliofumaniwa na kukumbushia ya zamani ku-justify upuzi wao

The more these fisadis write utumbo, the better for our nation because they are just reducing themselves to size

"Say No to Fisadis"
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…