Mercedes Benz C- Class

Mercedes Benz C- Class

Salaam Wakuu wangu, natumaini wote mko vema na mnaendelea salama na ujenzi wa Taifa Tanzania.

Natumaini Kama si wote basi baadhi yenu mnauzoefu na ujuzi japo kwa kiasi fulani juu ya vyombo vya moto {hapa nimelenga zaidi magari}

Wandugu mimi ni mpenzi wa Gari aina ya Gari aina ya Mercedes Benz C- Class sasa wakuu naombeni ushauri juu ya hii gari:-

1} Changamoto zake katika uendeshaji/umiliki
2} Utunzaji
3} Utumiaji wa mafuta

Na pia kama kuna kingine tujuzane kwa faida ya wote wenye ndoto hii.

Asanteni wakuu.

C class ni model ya benz ambayo hazina mambo mengi na ni ya mtumiaji wa kawaida hata gharama zake zinakuwa sio juu sana,
Hiyo ni c class W203,zinaanzia 2003 hadi 2006,
Zinakuwa na engine ya 4 petrol,(M111 or M271) cc 1990 hadi 2000,
Kuna zenye engine ya v6(112) c230
Na kuna yenye engine ya diesel
Ila kukushauri chukua ya petrol 4cylinder.

Utuzaji ,inahitaji kuzingatia service na kuonana na fundi kila unapoona tatizo au warning light,
Vilevile spare zake kwa sasa sio ghali maana hii model zipo nyingi

Kwa engine ya 4 hainywi mafuta kabisa,kwa kifupi hii gari iko poa sana


Sent from my iPhone using Tapatalk
 
C class ni model ya benz ambayo hazina mambo mengi na ni ya mtumiaji wa kawaida hata gharama zake zinakuwa sio juu sana,
Hiyo ni c class W203,zinaanzia 2003 hadi 2006,
Zinakuwa na engine ya 4 petrol,(M111 or M271) cc 1990 hadi 2000,
Kuna zenye engine ya v6(112) c230
Na kuna yenye engine ya diesel
Ila kukushauri chukua ya petrol 4cylinder.

Utuzaji ,inahitaji kuzingatia service na kuonana na fundi kila unapoona tatizo au warning light,
Vilevile spare zake kwa sasa sio ghali maana hii model zipo nyingi

Kwa engine ya 4 hainywi mafuta kabisa,kwa kifupi hii gari iko poa sana


Sent from my iPhone using Tapatalk
Asante sana mkuu FUNDIBENZ..
 
ni machine nzuri, C class kuna zenye cc 2500 na zenye cc1800. ulaji wake wa mafuta ni wa kawaida sana. ikifika muda wa service uandae kama 400,000/= service yake sio ya kumwaga oil tu.
I recommend this car for you.
 
ni machine nzuri, C class kuna zenye cc 2500 na zenye cc1800. ulaji wake wa mafuta ni wa kawaida sana. ikifika muda wa service uandae kama 400,000/= service yake sio ya kumwaga oil tu.
I recommend this car for you.
Service ya 400,000 bado una-recommend?
 
Back
Top Bottom