Meya wa Jiji la Dar es Salaam, Isaya Mwita Meya anyang’anywa gari, ofisi yafungwa. Adai kuwa yeye bado ni Meya halali

Wakuu hivi haya MAJIBWA , Ma - CCM tunakwamia wapi?
 
Acha uzushi hizo ni tuhuma feki zimetengenezwa na makonda ili wapate kumng’oa madarakani, hizi ni mbinu za kishamba kijinga sana na haziwezi kuongeza ndege viwanda na kuleta maendeleo
 
Jana nimesikia Waitara akimkoromea Mbowe kutokutumia pesa huko Hai na akampa madaraka mkuu wa wilaya kuzitumia pesa za mfuko wa jimbo hilo.

Tuliona Ofisi ya Bunge ikimpa rais Mipesa kibao kwamba haikutumika, tumeona Dr. Mpango akiyakoromea makampuni yasiyoleta gawio, viongozi wa hayo makampuni watafute kazi zingine.

Tumemsikia na kumuona Dr. Mpango akilalamikia Tanzania kupunguziwa misaada ya wahisani, hadi kusababisha baadhi ya miradi kutokutekelezeka na mingine kusuasua.

Na mara kadhaa tumemsikia rais Magufuli akitafuat pesa kokote humu ndani hadi kuwakumbusha wakurugenzi kubuni njia zingine za mapato.

Sasa leo nimeshangaa, Eti moja ya makosa ya Meya Mwita ni kutokutumia Bil 5.8 zilizotoka kwa Kisena.

Ikiwa tunashida na tunatafuta pesa kila kona kwanini hilo liwe kosa kwa Meya badala ya kumpongeza na kuzichukua zikafanye kazi kwingine?

Tatizo liko wapi hadi iwe hivyo kwa Meya Mwita?

Mgogoro wa UDA na jiji uliisha au bado upo, na kama upo au kesi iko mahakamani kwanini hiyo pesa itumike? na kama mgogoro uliisha kwanini haikutumika?
 
Anamuomba Rais Magufuli aingilie kati wakati suala lake lipo Mahakamani, aendelee na taratibu za kimahakama
 
Kutokutumia pesa za wananchi ni kuwanyima wananchi maendeleo,kuwanyima wananchi maendeleo ni kosa. Mengine sijui mkuu.

macson
 
Hizo bilioni 5.8 zingejenga madarasa mengi sana na kufanya watoto zaidi ya 5000 kuingia masomoni hapo Dar.Huyo meya ni wa kufurushwa mapema
 
Hizo bilioni 5.8 zingejenga madarasa mengi sana na kufanya watoto zaidi ya 5000 kuingia masomoni hapo Dar.Huyo meya ni wa kufurushwa mapema
 
Kwa wale wa Isidingo hiyo style ya kumchomoa Meya tunaiita ,"SECHABA MATHABANE STYLE" au "MOTHUSI FIGISU".

Fungeni mikanda kwelikweli maana yajayo GE yanasikitisha.
 
CCM wanataka kurejesha mfumo wa chama kimoja
ok kwa hiyo hata kama wameona amefanya ubadhilifu wamwachie tu sababu ni wa chama cha upinzani eeeh...s.tt..u.p..i.dd
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…