Meya wa Moshi kuingia darasani kufundisha wanafunzi na kumsifia Rais Samia mbele ya wanafunzi ni sahihi?

Meya wa Moshi kuingia darasani kufundisha wanafunzi na kumsifia Rais Samia mbele ya wanafunzi ni sahihi?

Wizara ya Elimu popote mlipo , NAOMBA MKEMEE HIKI KITENDO HARAKA SANA KWANI NI KUDHALILISHA TASNIA YA UALIMU. HIVI KWANINI TUNARUHUSU HUU UJINGA UTAMALAKI? WIZARA YA ELIMU TOENI KAULI JUU YA HUU UJINGA.

Ukienda popote na ukafanya chochote hata nje ya utaratibu, ili mradi unamsifia rais basi ujue uko salama, hakuna yoyote wa kukugusa.
 
Wizara ya Elimu popote mlipo , NAOMBA MKEMEE HIKI KITENDO HARAKA SANA KWANI NI KUDHALILISHA TASNIA YA UALIMU. HIVI KWANINI TUNARUHUSU HUU UJINGA UTAMALAKI? WIZARA YA ELIMU TOENI KAULI JUU YA HUU UJINGA.
CCM ndivyo inavyoendelea kutuharibia nchi. Hayo yote kiherehere ili Rais amuone kama mchapakazi. Kupongeza kila kitu na kukihusisha na Rais. Mbatis emetwambia tuna tatizo la viongozi wengi kuwa mapunguani ktk nchi hii.
 
Huyu Meya dizaini namwonaga kama ana wenge flani.. Hivi hali msuba kweli?
 
Biology is a study of living things.
-Binamu
-Animal
-Mimea

Kupatwa kwa elimu.
Angalia alivyo jidhalilisha, hivi ndivyo siasa inavyoingilia shughuli za kitaalamu na kusababisha uharibifu. Mfano tu mwanafunzi akiulizwa swali: With examples what do you understand by the term biology? Halafu kwenye majibu ya mwanafunzi unakutana na mifano Kama:
-Binamu
-Animal
-Mimea
[emoji848][emoji848][emoji848][emoji848]
 
Huyu ni opportunist mkubwa kama nakumbuka alichangia kuongeza maambukizi ya uviko19 wakati wa Jiwe kwa kuzuia watu kuvaa barakoa ili kumfurahisha Jiwe. Anaalingalia upepo upande wenye maslahi kwake kisiasa.
 
Angalia alivyo jidhalilisha, hivi ndivyo siasa inavyoingilia shughuli za kitaalamu na kusababisha uharibifu. Mfano tu mwanafunzi akiulizwa swali: With examples what do you understand by the term biology? Halafu kwenye majibu ya mwanafunzi unakutana na mifano Kama:
-Binamu
-Animal
-Mimea
[emoji848][emoji848][emoji848][emoji848]
Sio hivyo tu mkuu,biology haihusiki na living things but also non living things, hapo meya kapotosha Sana,na mtoto huenda amekalili hivyo, mwisho wa siku lawama zinaenda kwa mwalimu
 
Hivi lile sakata lake na mkuu wa wilaya la milioni 25 za limo liliishaje
 
Huyu ana tuhuma kubwa akishirikiana na Sabaya zipo wazi

Anacho kifanya hapo ni kufukia kupata huruma litakapokuja kusanuka
 
Kwa nini afundishe? Alikuwa na lesson plan?
Moshiblog UpdatesView attachment 2087057
MOSHI: MICHANGO YAPIGWA "STOP" MASHULENI, MEYA RAIBU AINGIA DARASANI KUFUNDISHA BIOLOGY

Moshi Kilimanjaro


• Meya Raibu apiga marufuku michango mashuleni, adai walimu wakuu waache watoto wa Rais Samia wasome bila bugudha
• Awaonya wazazi wasiopeleka watoto shule kujiandikisha, adai wasiogope, Rais Samia amekwisha lipa ada yote
• Awapiga msasa wanafunzi wa kidato Cha Kwanza


Mstahiki Meya wa Manispaa Ya Moshi Ndugu Juma Raibu akiwa katika ziara ya kutembelea Madarasa yaliyojengwa Kwa ufadhili wa Fedha za Uviko 19 amezungumza na waalimu na wanafunzi akifafanua faida kedekede za ujenzi wa madarasa hayo.

Meya huyo amedai tayari Kwa asilimia kubwa ujenzi umekamilika na Madarasa hayo yameanza kutumika na yamekuwa msaada mkubwa katika Manispaa hiyo.

Amesisitisa walimu wakuu kuacha mara moja kuwarudisha nyumbani watoto kwa kisingizio Cha michango kwani Rais Samia amekuwa akitoa bilioni 28 Kila mwezi nchini kote kugharamia uendeshaji wa shule za serikali. Namnukuu
"Ndugu zangu walimu Kwanza niwapongeze Kwa kufanya kazi njema na bora sana ya kuwafundisha watoto wetu, lakini pili niwatake mwongeze bidii ili Manispaa yetu ipae zaidi na zaidi kielimu katika nafasi za kitaifa na tatu niwatake walimu wakuu kuacha mara Moja kuwarudisha mjumbani wanafunzi kisa michango kwani hela hizi zimeshalipwa na Rais Samia Kila mwezi Bilioni 28"

Lakini pia Mstahiki Meya huyo amewataka wazazi wote wa Manispaa hiyo kuwaleta na kuwaandikisha mashuleni watoto wote wanaopaswa kuanza shule za msingi na sekondari, kwasababu ni Elimu bila malipo. Namnukuu
"Watoto Waambie wazazi wote wawalete watoto waliobaki majumbani waje kupata Elimu ili iwe Mkombozi wa maisha yao na taifa Kwa ujumla na hivi sasa Elimu ni bila malipo kwani serikali ya Rais Samia inamaliza yenyewe Kila jambo"

Pia Meya amewataka wanafunzi hao kusoma Kwa bidii ili waje kulisaidia taifa siku za usoni, na Kwa msisitizo zaidi Meya huyo aliwafundisha wanafunzi wa kidato Cha Kwanza Somo la Baiolojia katika mada ya Utangulizi (Introduction of Biology).

MoshiBlog Updates
 
Ndio Maana nilisema, Watoto wangu kusoma hizi shule za Umma kwa level ya Primary na Sekondari ndani ya Tanzania hii.
Big No!! Oneni jinsi watoto wanaonewa.

Kwanza limsururu la watu wazima hivyo kuingia Darasani ni kuharibu tension ya Watoto na Walimu.

Na hautasikia popote Wizara ya Elimu au Tamisemi wakikemea hili.
 
Back
Top Bottom