Mfahamu Albert Fish, al maarufu kama The Brooklyn Vampire

Mfahamu Albert Fish, al maarufu kama The Brooklyn Vampire

Damaso

JF-Expert Member
Joined
Jul 18, 2018
Posts
3,978
Reaction score
6,739
Habarini za Jumatatu wakuu, natumaini mpo wazma wa afya na mnaendelea na majukumu yenu ya kila siku; Naomba niwatakie afya njema wote hasa wale wagonjwa mpate nafuu.

Kama ilivyo Kawaida yangu ya kupitia visa na mikasa mbalimbali ya kidunia na kuleta nyuzi zenye kuongea maarifa kuhusu mambo mbalimbali.

Hivyo leo Naomba nilete uzi huu maalumu kuhusu Bwana mkubwa Albert Fish, al maarufu kama The Brooklyn Vampire: Sehemu ya Kwanza.

Katika pita pita zangu nimepata kumsoma Huyu mzee aliyejipatia jina kwenye uwanja mchafu kidogo Ingawa maarufu.
Karibuni:

IMG_1628.jpg

Ilikuwa ni mwezi wa Novemba mwaka wa 1934, ambapo mtoto wa kike mwenye miaka kumi aliyekuwa anaitwa Grace Budd alipotea kwenye mazingira yenye utata sana. Mpaka mwezi huu wa Novemba; Grace alitoweka nyumbani kwako kwa zaidi ya Miaka Sita.

IMG_1630.jpg

Polisi na ndugu walijaribu kila namna iliyowezekana kufuatilia kesi hii bila kufanikiwa hata hatua moja. Lakini walipata mshangao mara baada ya Mama mzazi wa Grace kupata barua yenye ujumbe wa kutisha sana.

Ujumbe ule Ulitoa mwanga kwenye kesi hii Kwani ndani ya barua hiyo kulikuwa na maelezo kuwa mtoto Grace alikuwa amekwisha kufanywa msosi. Ingawa mwandishi wa barua hiyo hakuweka majina yake ila ndo alionyesha mwanga zaidi kwenye kesi hii.

IMG_1629.jpg

Ujumbe ule mkali na wenye kutisha ambao Mama yake Grace aliusoma; ulionesha na kuweka bayana kuwa kuna mwanadamu mwenye kupata dhamira na ladha ya nyama ya Binadamu mwenzake. Kwani ilijenga dhana Mbaya Kabsa ya kuwa mtoto Grace aliuawa kisha nyama yake kuchomwa mithili ya mishikaki ndani ya jiko la kuoka mikate.

IMG_1631.jpg

Je, Albert Fish ni nani:
Alizaliwa tarehe 19 mwezi Mei 1870 ndani ya Jiji la Washington, D. C ndani ya familia ya Bwana Randall pamoja na Bibi Ellen Fish. Alipatiwa majina ya Hamilton Howard Fish. Ingawa mpaka anaanza uhalifu wake alipewa majina kadhaa; mfano, the Brooklyn Vampire, the Werewolf of Wysteria, the Gray Man.

IMG_1632.jpg

Akiwa mtoto Mdogo Albert Fish alipatwa na ugonjwa wa akili ambao Ulikuwa unatembea kwa ndugu zake wengine pia. Historia ya familia yake ilikuwa inazungukwa na magonjwa ya akili mara nyingi. Kaka yake mkubwa aliwekwa chini ya uangalizi maalumu katika hospitali ya wagonjwa wa akili, wakati Mjomba wake alikutwa na ugonjwa wa mania. Mama yake Albert alikuwa na tabia ya kuona maluweluwe muda mrefu.
IMG_1633.jpg

Enzi za ujana wake alikuwa handsome kweli kweli lakini alikuwa anapambana na ugonjwa wa akili muda mrefu sana.
Baba yake Albert alikuwa na Miaka 75 wakati Albert anazaliwa; na Alifariki huku Albert akiwa na Miaka mitano tu. Bibi Ellen aliachwa kama mjane na hakuwa na uwezo wa kulea familia ya Watoto wanne akiwa peke yake. Hivyo aliamua kuwapeleka wakapate malezi kwenye kituo cha Watoto yatima al maarufu kama kuleana. Inasadikika kuwa huku ndiko Bwana Albert alipopata hamu ya kuona maumivu.

IMG_1634.jpg

Kituo cha kuleana cha St. John’s Home for Boys.

IMG_1635.jpg

Walezi na wahudumu katika kituo hiki mara nyingi waliwapiga Watoto na hata kuwafanya wapigane. Ingawa Watoto wengi waliishi kwa hofu ya maumivu; Albert pekee ndo alipendelea kuona vita na ugomvi.

Albert alipenda sana kujihusisha na matukio ya kumpa mtu maumivu na kufurahia matendo hayo.

Baadaye Mama Albert alifanikiwa kupona ugonjwa wake wa akili na alikuwa ameshakaa vizuri kiuchumi na kuweza kumlea mtoto wake. Mwaka 1880 alimuondoa kwenye kituo hicho; lakini madhara yalikuwa yamekwisha kukaa kichwani mwa Albert.

IMG_1636.jpg

Bwana Mdogo Albert Ali’s nyumbani Bado aliendelea na tabia na mazoea yale yake na alijenga urafiki na kijana mmoja jirani yao mwaka 1882. Kijana Huyu alimuingiza Albert kwenye michezo Michaud ya kupenda kula uchafu wa Binadamu ambayo kitaalamu hujulikana kama urolagnia and coprophagia, ambapo hujenga mazoea ya kunywa mikojo pamoja na kula kinyesi cha Binadamu.
Lakini hii ilimpelekea kuanza mchezo wa kufurahia maumivu katika mwili wake. Alijichoma sindano na kujiweka vidonda ili mradi tu afurahie maumivu.

Mwaka 1890, Albert akiwa kijana wa Miaka 20 alihamia jiji la New York na Hapo ndo alipoanza kushughulika na watoto rasmi.

IMG_1637.jpg

Picha ya X Ray ikionesha nyonga ya Bwana Albert ikiwa na sindano 29.

Albert alizidi kupenda kuona watu wakiwa kwenye maumivu; na punde tu baada ya kufika ndani ya jiji la New York alianza tabia ya ubasha kwa kuwaingilia kinyume na maumbile vijana kisha kuwatesa sana.

Mwaka 1898 Albert alifunga ndoa na Mwanamke aliyetambulishwa na Mama yake Albert; walipata Watoto Sita. Ila hakuwahi kufanya unyama wowote Watoto wake wala mke wake. Ingawa Albert alizidi kuwaingilia kinyume na maumbile vijana kama Kawaida.

IMG_1638.jpg

Mwaka 1910 Albert alianza mahusiano ya jinsia moja na Bwana Thomas Kedden. Lakini wakiwa na siku kumi tu za mahusiano; Bwana Thomas alifungiwa ndani kwenye nyumba kisha kuteswa na mateso makali sana.

Wiki mbili tu zilitosha kutoa mateso kwa Thomas; huku Albert akiuchezea mwili wa Thomas kisha kukata nusu kipande cha dhakari.

Mwaka 1917, Albert alianza kuonesha dalili za ugonjwa akili tena; na kupelekea mke wake kwenda kuolewa na mwanaume Mwingine. Hapo ndo alipozidi kujidhuru mwili wake. Alizidi kujichoma sindano kwenye nyonga yake.

IMG_1640.png
Mauaji ya Grace:
Mwaka 1919 kutokana na kupenda sana kutesa watu na kula nyama zao huko ndiko kulimpelekea kufanya mauaji haya na mengine. Huku wahanga wakiwa ni Watoto walemavu, Watoto wa mitaani pamoja na vijana wapenda vitonga.

Katika harakati za maisha, Familia ya Bwana Edward Budd ilihitaji mtu wa kufanya kazi ili apate pesa. Hivyo Albert akakutakana na tangazo hilo. Shabaha ya Albert ilikuwa ni kaka mkubwa wa Grace lakini baada ya kuona sura na umbo la Grace ndiko alipobadili mawazo na kuamia kwa Grace.

Alijenga ushawishi na kuwalaghai kuwa nyumbani kwake kuna sherehe ya siku ya kuzaliwa ya mpesa wake. Kwa muonekano wa nje ilikuwa vigils sana kwa familia ya Budd kumkatalia Albert hivyo walimruhusu aondoke na Grace. Na walipofanya hivyo hawakuwahi kumuona mtoto wao tena.

IMG_1639.jpg

Albert aliondoka na Grace huku mtoto wa kike akiwa mwenye tabasamu. Albert alimpeleka kwenye nyumba ile ile ambayo alipanga kumpeleka kaka yake Grace.

Kwa mujibu wa Barua aliyoituma kwa Mama wa Grace. Inadaiwa kuwa Albert alimkaba koo mpaka Grace akafariki kisha alimkatakata vipande ili niweke kwenye jiko la kuoka, na ilichukua siku tisa kumaliza mwili wote.

Je Polisi walitambuaje kuwa Albert Fish ndo mhusika na nini kiliendelea zaidi?

IMG_1641.jpg

Kwa sasa niishie hapa nitaendelea na sehemu ya Pili.

Asante sana

@Mshana Jr @daVinci XV @Lumumba na wengine [emoji120]

PIA SOMA
- Mfahamu Albert Fish, al maarufu kama The Brooklyn Vampire: Sehemu ya Pili
 
Duuu balaa asante sana mkuu kwa kushare,

Ila mtoa mada tunatishana sana!

(In Jiwe voices)
 
Karibuni Wakuu Tuendelee na visa vya Albert Fish. Hii ni sehemu ya Pili. Unaweza kupata sehemu ya Kwanza hapa: Mfahamu Albert Fish, al maarufu kama The Brooklyn Vampire: Sehemu ya Kwanza

Nitaendelea na Kisa cha mtoto Grace kukatwa vipande vipande kisha kupikwa kwenye jiko la kuokea mikate (oven). Kiufupi viungo vya mtoto Grace vilifanywa mfano wa Kuku Choma vile. (Samahani kwa Kutumia lugha hii).

IMG_1638.jpg



Barua ile aliyoituma kwa Mama Grace ilikuwa ni kwa ajili ya kujaza hofu ndani ya nyumba pamoja na familia ya Budd; lakini barua hii ndo ilikuwa kitu pekee kilichoanza kumchoma matatizo yake.

Karatasi iliyotumika kuandika ujumbe huo ilikuwa ni kipande cha karatasi kutoka kwenye ofisi moja kutoka jiji la New York. Polisi walikutana na kampuni kwenye ofisi hiyo nakuwahoji. Mwishoni walitambua kuwa kipande hicho kilitumiwa na kijana mmoja kutoka ndani ya kampuni hiyo hiyo.

IMG_1636.jpg


Ilisemekana kuwa kijana huyo Aliishi ndani ya chumba cha kupanga na jirani tu kulikuwa na nyumba ambayo Albert alipanga sehemu hiyo.

Polisi mara baada ya kuona kuwa Albert Fish anaonekana ndo Frank Howard, mtu aliyemteka mtoto Grace, basi Polisi waliamua kuweka mahojiano na mtu Huyu.

IMG_1639.jpg


Katika hali ya mshangao mkubwa sana; Frank Howard aligeuka na kuwa Albert Fish Halisi na kukiri kufanya kitendo hicho. Ijapokuwa katika mahojiano hawakudhania kuwa angeweza kufanya matukio hayo.

Alitoa taarifa kuhusu watoto zaidi aliowafanyia kitendo sawa na Grace.

Lakini ni Watoto watatu tu akiwemo Grace ndo wanachukuliwa kama wahanga.

IMG_1646.jpg


Mauaji mengine aliyofanya ni kwa mtoto Billy Gaffney mtoto wa Miaka minne tu. Mpaka Albert anakamatwa masalia ya mwili wa Billy.
Mwaka 1924 mtoto Francis McDonnell alinyongwa porini na Bwana Albert. Mwili wake ulikutwa ukiwa umenyongwa na suspenders zake. Na kabla Albert hajapewa adhabu yake ya kifo alidai kuwa ni yeye ndo alifanya tukio hilo.

Na alikuwa na dhamira ya kumtenganisha katikati ila alisikia sauti za watu zikisogea hivyo akakimbia eneo hilo.


IMG_1648.jpg


Adhabu ya kifo kwa Albert:
Kesi ya Bwana Albert Fish ilianza kusikilizwa machi 11 mwaka 1935; huku ikionesha kuwa ni wazi Albert hakuwa timamu. Mara nyingi alionyesha kutabasamu akiwa anajibu maswali.

Kesi hii ilitumia siku kumi tu na Albert kupewa adhabu ya kifo ya kiti cha umeme.

IMG_1649.jpg

Kabla ya adhabu yake kutekelezwa tarehe 16 Januari mwaka 1936; umma ulimuomba Jack Dempsey wakili wa Bwana Albert kuweka nyaraka za vifo alivyofanya Albert. Lakini wakili Huyu alikata katukatu huku alidai kuwa makaratasi hayo sio sahihi kusomwa na jamii.

NB: yameibuka makundi makuu mawili yenye kutoa maelezo kwenye suala hili:
1. Kundi la kwanza; linadai kuwa Albert alisumbuliwa na matatizo ya kiakili na afya yake ya akili haikuwa Vyema sana.
2. Kundi la Pili; hudai kuwa Albert aliingiwa na roho chafu ya kishetani tangu akiwa kituo cha Watoto yatima.

IMG_1628.jpg

Yote kwa yote Huyu Bwana mkubwa alikuwa ni hatari sana.
Naomba niishie Hapo leo mpaka Wakati Mwingine tena wanajukwaa.
 

Attachments

  • IMG_1647.jpg
    IMG_1647.jpg
    21.7 KB · Views: 9
  • IMG_1648.jpg
    IMG_1648.jpg
    43.8 KB · Views: 8
[emoji1545][emoji1545][emoji1545]mada zilizosheheni maarifa..nipo hapa kaka sibanduki
 
Aisee

Sikupata kabla, sjui kwanini labda ni kutokana na Kakabiliwa na Vimajukumu

Roho za kula nyama za watu na kutesa nimeziskia sana kwenye simulizi , mara nyingi roho hizo wanamiliki watu wanaoitwa wachawi...binadamu wa kawaida unatoa wapi hio roho

aisee kuna vingi vipya humo kwangu kuna maarifa hongera mkuu🙏
 
Back
Top Bottom