Mfahamu Hussein Shekilango, aliyepewa barabara Dar (Bamaga - Urafiki) kutambua mchango wake kwa Taifa

Mfahamu Hussein Shekilango, aliyepewa barabara Dar (Bamaga - Urafiki) kutambua mchango wake kwa Taifa

Alikuwa waziri wa nchi ofisi ya waziri mkuu na alifariki 1980 akitokea Entebbe Uganda, na ndege iliangukia Arusha, unaweza kusearch Hussein Shekilango nafikiri unaweza kupata data zaidi.
Akiwa na Kilumanga. ..baba yake Chabaka Kilumanga
 
I thought this was a serious question........ipo kona ya jokes kuleee ama ndio miafrika?Au udumavu?
Stanting huenzia utotoni na madhara huonekana ukubwani!

Lishe Bora ni Bora kwa ustawi wa taifa,,
 
Nimepata sikia Msasani ni jina la Musa Hassan so likafupishwa/unganishwa na kuwa Musa Hassan
 
Huku tunapoenda naona unanilazimisha kukukosea heshima

Kwa sababu iam brave enough sitofanya hivyo

Endelea na hekaya zako

Mimi nipo namsoma Shakespeare hapa ,Hekaya zako nasoma nikiwa sina cha kufanya kupoteza muda hivyo kuniwekea picha zako hazisaidii unapoteza nguvu bure

Umekosewa wapi heshima ? Hebu jiheshimu ,wazazi wangu hujui walipo wewe na hujui walivyo nilea ,kama unataka tuende personal iam good at that too

Eleza kwanini kwenye hekaya zako hujawahi kuongelea Zanzibar kutokuwa na rais Mkristo


Huwezi kujibu kwanini Zanzibar hakuna Rais mkristo ila kila siku uko na Nyerere na Uislamu ,oh uhuru ,oh bibi Titi alikuwa sijui nani ,oh Mama Maria Nyerere alikuwa sijui na duka la mafuta taa Magomeni ,Mwanae Andrew akakataa mama yake hakuwa na duka hilo

Kama sio hekaya hizi ni nini ?

Endelea na Hekaya zako

Mimi nimemaliza
Yamakagashi,
Kama kunivunjia adabu hilo ushalifanya na ndiyo imetufikisha hapa kwa mimi
kukuonyesha kuwa nayaweza pia.

Kuhusu Shakespeare labda nikutahadharishe jambo.

Nimefanya fasihi Cambridge Examination 1970 na katika hayo ya Kiingereza
ikutoshe kuwa nimetoka na First Class Merit Pass English Oral yaani mtihani
wa kuzungumza Kiingereza.

Katika moja ya vitabu nilivyotahiniwa ni Shakespeare.
Sasa acha hayo maneno ya Shakespeare wa kutishwa na Shakespeare si mimi.

Nimefanya English Elocution ''passage,'' yangu kutoka kwa Shakespeare ''Julius
Caesar.''

''Into what dangers would you lead me Cassius...''
Malizia wewe...

Hili la kwanza la pili mimi niko katika jopo la waandishi wa Oxford University
Press, Nairobi wanaoshughulika na usomeshaji wa lugha ya Kiingereza kwa shule za
msingi Afrika ya Mashariki.

Nishaandika vitabu viwili katika mradi huo kimoja kwa shule za msingi na kingine
kwa ajili ya shule za sekondari na vitabu vyote viko katika mtaala Kenya.

Nakuwekea hapo chini toleo la kwanza na la pili la moja ya kitabu changu:

20140104_205335.jpg


the%20torch%20on%20kilimomanjaro.jpg


Mohamed Said: OXFORD UNIVERSITY PRESS WATOA TOLEO LA PILI LA "THE TORCH ON KILIMANJARO" KITABU CHA WATOTO CHA MWANDISHI MOHAMED SAID

Kwa hiyo mimi si wa kutishwa na mambo ya Shakespeare tafuta mtu mwingine lakini
si Mohamed Said.

Njoo na hiyo unayoita, ''personal,'' nakukaribisha.

Ungekuwa wewe mama yako kakufunza adabu hiyo adabu mimi ningeiona katika kauli
yako.

Wewe unasema mimi naandika hekaya.

Umenitukana kuwa mimi ni mwandishi wa hekaya.

Nimezunguka duniani kwingi nikahadhiri historia ya Tanganyika katika vyuo vya kutajika na nimekuwekea ushahidi usome.

Ungekuwa na akili na adabu ingekutosha kujua kuwa umekosea na ngalau hata kama
usingenitaka radhi basi ungerudi na adabu zako kamili.

Unazidi kudhihirisha umbumbu wako licha ya kukuelekeza kuwa hilo suala lako la rais
Mkristo Zanzibar ni kichekesho, ungekuwa na akili ungefanya utafiti niliokushauri.

Badala yake umerudi tena na upuuzi ule ule.

Lakini nitakujibu swali lako kwa kuwa wewe huna uwezo wa kujua jibu la swali ulilouliza.

Rais wa nchi na jamii katika nchi yeyote iliyokuwa koloni inachukua uongozi katika nchi
kwa kushiriki katika siasa za ukombozi.

Umepata kuona au kusoma popote pale au angalau kusikia kuwa katika vyama vya
ukombozi Zanzibar, Hizbu, ASP na baadae Umma Party kama kulikuwa na kiongozi Mkristo wanapigania uhuru wa visiwa hivyo?

Au umepata kumuona Mkristo yeyote Zanzibar aliyekuwa na nguvu za kisiasa kiasi
aweze kugombea kuingoza nchi?

Mwisho kumbe lililokuchoma ni historia ya Ali Msham na duka la mafuta la Mama
Maria
Nyerere.

Kwani wewe ulipata kumsikia Mshume Kiyate katika historia ya TANU na historia ya
Nyerere kabla mimi sijamtaja?

dRI92Wy52vZELRmwqQbgZvtY6fjqAGp_GsKC1nwC9D2dAjXOmwLxFJtWLerfPTm5WOPG_N_N7tNsArsJ5OnSBwKRrk1iaONhXSvk4j4X1F-teVD4lhh8WBFM_IXCOp_b58FqnmSCKukcKcZ4W4IoSyj4fBnrJYb9463ZcYG_eV01bd1FFs5HULE57yNBDJVpfn7jkn_VIiK_hGAEPd6QBR3fpnXgix9ndGvtn3hA5xYVeW6ibkLIGlfq_62aDUSUBgiOPwhNMwId-M_rRWobR5t1dzVz2nvjsowP1ZuI7bKpvdZe8qkhVh_FQBn2hdRvITfJL37vgS6YGQ3xTXFqBxQ12e11Q_q4yPhxwSVO4eduXp91uxrCQ6-5OdRdz6qGjn3kZzwtlHS3JLB4CVK1f-Fb7r7D829ws4kejf2VdFJjKGL5F4ouQJ71SjofFqBaQC2UhXAg66j-TvJyQjE0SQulJV4kgrNBElnCnMJCTPWb3NTIYJAAZHFBPmoITcXepOV3F8NPr9oH4bDo2IhkBFKbj0vVjG2EwC_uyXlr3WXQoYmEHZ0tg6-66SbJikY3jTtdSznmGKRc8HYGrRUFv7H_vHlhsj6D361wfPNh6pQHnr8z=w360-h480-no

Mshume Kiyate na Nyerere 1964

Tuseme kwa kuwa hakupata kutajwa popote ndiyo Mshume Kiyate hakuwepo?
Mshume Kiyate alikuwapo na alikuwa rafiki mkubwa sana wa familia ya Nyerere.

Halikadhalika Mama Maria katika harakati za kupigania uhuru wa Tanganyika na yeye
alishiriki kama walivyoshiriki wazalendo wengine na akakumbaana na dhiki kama
zilizowapata wazalendo wengi katika TANU.

Hii biashara ya mafuta Mama Maria Nyerere aliifanya pia Mtaa wa Mchikichi
karibu na nyumba ya Mwalimu Bahia.

Huyu Mwalimu Bahia mimi ni shangazi yangu.
Mshume Kiyate, Ali Msham na Mwalimu Bahia si ''hekaya.''

Hawa walikuwapo na walishirikiana na Mwalimu Nyerere
bega kwa bega katika kupigania uhuru wa Tanganyika.

DSCN1793.JPG


Kulia Ali Msham aliyekaa ni Mwalimu Julius Nyerere 1955
 
Yamakagashi,
Kama kunivunjia adabu hilo ushalifanya na ndiyo imetufikisha hapa kwa mimi
kukuonyesha kuwa nayaweza pia.

Kuhusu Shakespeare labda nikutahadharisha jambo.

Nimefanya fasihi Cambridge Examination 1970 na katika hayo ya Kiingereza
ikutoshe kuwa nimetoka na First Class Merit Pass English Oral yaani mtihani
wa kuzungumza Kiingereza.

Katika moja ya vitabu nilivyotahiniwa ni Shakespeare.
Sasa acha hayo maneno ya Shakespeare wa kutishwa na Shakespeare si mimi.

Nimefanya English Elocution ''passage,'' yangu kutoka kwa Shakespeare ''Julius
Caesar.''

''Into what dangers would you lead me Cassius...''
Malizia wewe...

Hili la kwanza la pili mimi niko katika jopo la waandishi wa Oxford University
Press wanaoshughulika na usomeshaji wa lugha ya Kiingereza kwa shule za
msingi Afrika ya Mashariki.

Nishaandika vitabu viwili katika mradi huo kimoja kwa shule za msingi na kingine
kwa ajili ya shule za sekondari na vitabu vyote viko katika mtaala Kenya.

Nakuwekea hapo chini toleo la kwanza na la pili la moja ya kitabu changu:

20140104_205335.jpg


the%20torch%20on%20kilimomanjaro.jpg


Mohamed Said: OXFORD UNIVERSITY PRESS WATOA TOLEO LA PILI LA "THE TORCH ON KILIMANJARO" KITABU CHA WATOTO CHA MWANDISHI MOHAMED SAID

Kwa hiyo mimi si wa kutishwa na mambo ya Shakespeare tafuta mtu mwingine lakini
si Mohamed Said.

Njoo na hiyo unayoita personal nakukaribisha.

Ungekuwa wewe mama yako kakufunza adabu hiyo adabu mimi ningeiona katika kauli
yako.

Wewe unasema mimi naandika hekaya.

Umenitukana kwa kuwa mimi si mwandishi wa hekaya na nimezunguka duniani kwingi
nikahadhiri historia ya Tanganyika katika vyuo vya kutajika na nimekuwekea usome.

Ungekuwa na akili na adabu ingekutosha kujua kuwa umekosea na ngalau hata kama
usingenitaka radhi basi ungerudi na adabu zako kamili.

Unazidi kudhihirisha umbumbu wako licha ya kukuelekeza kuwa hilo suala lako la rais
Mkristo Zanzibar ni kichekesho, ungekuwa na akili ungefanya utafiti niliokushauri.

Lakini nitakujibu swali lako kwa kuwa wewe huna uwezo wa kujua jibu la swali ulikouliza.
Rais wa nchi na jamii katika nchi yeyote iliyokuwa koloni inachukua uongozi katika nchi
kwa kushiriki katika siasa za ukombozi.

Umepata kuona au kusoma popote pale au angalau kusikia kuwa katika vyama vya
ukombozi Zanzibar, Hizbu, ASP na baadae Umma Party kama kulikuwa na Wakristo
wanapigania uhuru wa visiwa hivyo?

Au umepata kumuona Mkristo yeyote Zanzibar aliyekuwa na nguvu za kisiasa kiasi
aweze kugombea kuingoza nchi?

Mwisho kumbe lililokuchoma ni historia ya Ali Msham na duka la mafuta la Mama
Maria
Nyerere.

Kwani wewe ulipata kumsikia Mshume Kiyate katika historia ya TANU na historia ya
Nyerere kabla mimi sijamtaja?

dRI92Wy52vZELRmwqQbgZvtY6fjqAGp_GsKC1nwC9D2dAjXOmwLxFJtWLerfPTm5WOPG_N_N7tNsArsJ5OnSBwKRrk1iaONhXSvk4j4X1F-teVD4lhh8WBFM_IXCOp_b58FqnmSCKukcKcZ4W4IoSyj4fBnrJYb9463ZcYG_eV01bd1FFs5HULE57yNBDJVpfn7jkn_VIiK_hGAEPd6QBR3fpnXgix9ndGvtn3hA5xYVeW6ibkLIGlfq_62aDUSUBgiOPwhNMwId-M_rRWobR5t1dzVz2nvjsowP1ZuI7bKpvdZe8qkhVh_FQBn2hdRvITfJL37vgS6YGQ3xTXFqBxQ12e11Q_q4yPhxwSVO4eduXp91uxrCQ6-5OdRdz6qGjn3kZzwtlHS3JLB4CVK1f-Fb7r7D829ws4kejf2VdFJjKGL5F4ouQJ71SjofFqBaQC2UhXAg66j-TvJyQjE0SQulJV4kgrNBElnCnMJCTPWb3NTIYJAAZHFBPmoITcXepOV3F8NPr9oH4bDo2IhkBFKbj0vVjG2EwC_uyXlr3WXQoYmEHZ0tg6-66SbJikY3jTtdSznmGKRc8HYGrRUFv7H_vHlhsj6D361wfPNh6pQHnr8z=w360-h480-no

Mshume Kiyate na Nyerere 1964

Tuseme kwa kuwa hakupata kutajwa popote ndiyo Mshume Kiyate hakuwepo?
Mshume Kiyate alikuwapo na alikuwa rafiki mkubwa sana wa familia ya Nyerere.

Halikadhalika Mama Maria katika harakati za kupigania uhuru wa Tanganyika na yeye
alishiriki kama walivyoshiriki wazalendo wengine na akakumbnana na dhiki kama
zilizowapata wazalendo wengi katika TANU.

Hii biashara ya mafuta Mama Maria Nyerere aliifanya pia Mtaa wa Mchikichi karibu na
nyumba ya Mwalimu Bahia.

Huyu Mwalimu Bahia mimi ni shangazi yangu.
Mshume Kiyate, Ali Msham na Mwalimu Bahia si ''hekaya.''

Hawa walikuwapo na walishirikiana na Mwalimu Nyerere bega kwa bega katika kupigania
uhuru wa Tanganyika.

DSCN1793.JPG


Kulia Ali Msham aliyekaa ni Mwalimu Julius Nyerere 1955
Unasema Shakespeare sio wa kutishiwa wewe ? Sasa wewe una tofauti gani na Shigongo ?

Acha kumfananisha Shakespeare na vitu vya ajabu

Haya umezunguka kote huko faida yake ndio kuja na hizi hekaya , Je usingekuwa umezunguka ingekuwaje ?

Na wewe ni mwanazuoni ?

Unajitapa hapa na Hekaya zako kina Socrates sijui wasemaje

Endelea kuwafurahisha wanahekaya wenzako
Mimi sidanganyiki

Halafu kuna sifa moja mwanaume anayo ni uwezo wa kustahimili jambo ,nakuzunguka kote huko umekosa kujifunza hilo au ulikuwa unashangaa magorofa tu

Usitake kila mtu akubaliane na sumu zako
Hizo First Class pass zako zinasaidia nini uma kama hamna Legacy yoyote unayoacha zaidi ya kupigania udini ?

You are a disgrace to this Nation
 
Marehemu Shekilango alikuwa Waziri aliyepewa jukumu maalum na Rais Nyerere wakati huo ili awe mratibu kati ya Serikali ya Tanzania na Serikali mpya ya Uganda baada ya Idd Amin kuikimbia Uganda. Wakati huo Majeshi ya Tanzania yalikuwa bado yanasaidia ulinzi huko Uganda ingawa vita ilikuwa imekwisha malizika.

Ofisi ya kiraia ya Uratibu iliyokuwa kwenye Hoteli ya Nile Mansion ya wakati huo, iliongozwa na Waziri Shekilango; na mtumishi wa Serikali mwandamizi alikuwa Mr. Kilumanga aliyekuwa Afisa Mwandamizi bingwa wa Itifaki, aliyetokea Wizara ya Mambo ya Nje. Jeshi lilikuwa chini ya Afande Mayunga (Mtimkavu).

Waziri Shekilango, Mr. Kilumanga na maofisa wengine wakiwa kwenye ndege ya Jeshi la Tanzania walikuwa wakisafiri kutoka Entebbe Uganda kwenda Arusha kukutana na Rais Nyerere aliyekuwa Arusha wakati huo, ndege ikapata hitilafu ikiwa angani ikaanguka kwenye misitu ya Mlima Meru na wote waliokuwemo walifariki. Ilichukua muda kupata masalia ya ndege na maiti.

Wakati huo Sinza ilikuwa hajajengeka na kulikuwa na miti kwenye baadhi ya sehemu pia vilabu vya pombe za kienyeji. Kwa hiyo barabara mpya ilipojengwa ya kuunganisha Urafiki na Mwenge ikaitwa Shekilango kwa heshima ya Mheshimiwa Shekilango ambaye kifo chake akiwa kazini kilikuwa kimetoka kutokea.
 
Unasema Shakespeare sio wa kutishiwa wewe ? Sasa wewe una tofauti gani na Shigongo ?

Acha kumfananisha Shakespeare na vitu vya ajabu

Haya umezunguka kote huko faida yake ndio kuja na hizi hekaya , Je usingekuwa umezunguka ingekuwaje ?

Na wewe ni mwanazuoni ?

Unajitapa hapa na Hekaya zako kina Socrates sijui wasemaje

Endelea kuwafurahisha wanahekaya wenzako

Mimi sidanganyiki

Halafu kuna sifa moja mwanaume anayo ni uwezo wa kustahimili jambo ,nakuzunguka kote huko umekosa kujifunza hilo au ulikuwa unashangaa magorofa tu

Usitake kila mtu akubaliane na sumu zako
Hizo First Class pass zako zinasaidia nini uma kama hamna Legacy yoyote unayoacha zaidi ya kupigania udini ?

You are a disgrace to this Nation

Yamakagashi,
Ikiwa unapendezewa na ''hekaya,'' tutajadili kwa ushahidi wal si kwa hamaki.

Ikiwa mimi kuwarejesha wazee wangu katika historia ni udini ni bahati mbaya
sana kwako.

Nilikujua toka mwanzo kwa nini kifua chako kinafukuta kwa joto la hasad na chuki.

Kinafukuta kwa kuwa kila unapowasoma wazee wangu katika maandishi yangu
unauona ujasiri na uzalendo na mapenzi ya nchi.

Sasa turudi katika ''hekaya.
''Tuanze na hii hapa:

MJWTgR_JO-QlW5pRGZRJZX8D7K6Sew6ni04wCjPpG5I7akq3fpWs4xkfFePEgLmzIKVLuT_NS7c7u2g=w1366-h768-no

Guardian, Thursday 13 October 2016

Mohamed Said: FROM THE GUARDIAN: MWALIMU JULIUS NYERERE IN 1950s DAR ES SALAAM PART ONE

Ukimaliza njoo hapa chini:
Mohamed Said: TANZANIA: A NATION WITHOUT HEROES (ZMO) BERLIN

Seminar on
Fiftieth Anniversary of the African Independences

Organised by French Institute for Research in Africa
Nairobi 23th – 24th September 2013

Tanzania: A Nation Without Heroes
Speaker
Mohamed Said
Yamakagashi,
Umeniuliza swali nini tofauti yangu na Shigongo?
Tofauti yetu ni hii hapa chini naiweka tena kwa faida ya wasomaji wapya:
  1. PUBLICATIONS/RESEARCH PAPERS/ARTICLES
  2. The Life and Times of Abdulwahid Sykes 1924 –1968 The Untold Story of the Muslim Struggle against British Colonialism in Tanganyika, Minerva Press London, 1998 translated into Kiswahili as Maisha na Nyakati za Abdulwahid Sykes 1924-1968 Historia Iliyofichwa Kuhusu Harakati za Waislam Dhidi ya Ukoloni wa Waingereza, Phoenix Publishers, Nairobi, 2002.
  3. The Torch on Kilimanjaro, Oxford University Press, Nairobi, 2006
  4. Contributing author for an African anthology: The Mermaid of Msambweni and Other Stories, Oxford University Press 2007, Nairobi.
  5. Contributing author Dictionary of African Biography (DAB), Oxford University Press 2011, New York.
  6. Uchaguzi wa Busara, Abantu Publications 2008, Dar es Salaam.
  7. In Praise of Ancestors (1987) Africa Events (London).
  8. Abdulwahid Sykes: Founder of Political Movement (1988) Africa Events (London).
  9. Islam and Politics in Tanzania (1989) Al Haq International (Karachi)
  10. The Plight of Tanzanian Muslim (1993) Change (Dar es Salaam).
  11. Tanzania - The "Secular" Unsecular State (1995) Change (Dar es Salaam).
  12. The Question of Muslim Stagnation in Education in Tanzania - A Muslim Riddle (Paper presented at the Conference of the Global World of the Swahili Intercultural Dialogue on the Indian Ocean Zanzibar, February 20 - 23, 2003).
  13. Islamic Education and Intellectualism in Eastern Africa ‘Themes from the Pulpit in Tanganyika (Tanzania Mainland) 1800 – 2000’ (Paper presented at International Symposium on Islamic Civilisation in Eastern Africa Kampala, Uganda organised by the Islamic Conference Research Centre for Islamic History, Art and Culture (IRCICA), Istanbul and the Islamic University in Uganda, Mbale December 15th – 17th 2003).
  14. Sheikh Hassan bin Ameir - The Moving Spirit of Muslim Emancipation in Tanganyika (1950 – 1968) (Paper presented at Youth Camp Organised by Zanzibar University, World Assembly of Muslim Youth (WAMY) and Tanzania Muslim Students Association (TAMSA) 27th February – 4th March 2004).
  15. Islamic Movement and the Christian Lobby in Tanzania - the Experience of the late Prof. Kighoma Ali Malima (1938 – 1995) (Paper Presented to Tanzania Muslim Students Association (TAMSA) Sokoine University of Agriculture (SUA) Morogoro 11th April 2004).
  16. Terrorism in East Africa the Tanzanian Experience (Paper Presented at the Conference on Islam, Terrorism and African Development University of Ibadan, Nigeria 8th - 10th February 2006).
  17. Al Marhum Sheikh Kassim bin Juma bin Khamis (1940 – 1994) and the Pork Riots of 1993. (Paper Presented at the Regional Conference on Islam in Eastern Africa: Islam Encounter with the Challenges of the 21st Century 1st - 3rd August 2006, Kenyatta University, Nairobi.
  18. Muslim Bible Scholars of Tanzania – The Legacy of Sheikh Ahmed Deedat (1918 – 2005) Paper Presented at the International Symposium on Islamic Civilisation in Southern Africa Organised by The Organisation of Islamic Conference Research Centre for Islamic History, Art and Culture (IRCICA) The National AWQAF Foundation of South Africa (AWQAF SA 1 – 3 September 2006 University of Johannesburg.
  19. Tanzania: A Nation Without Heroes Seminar Organised by IFRA French Institute for Research in Africa and BIEA British Institute in East Africa 23rd and 24th September 2013 at IFRA Nairobi.
  20. Awards: Several Awards.
  21. Visiting Scholar: (2011)
  22. University of Iowa, Iowa City, USA
  23. Northwestern University, Chicago, Illinois, USA
  24. Zentrum Moderner Orient (ZMO), Berlin.
Kwa kuwa hupendi picha nakuwekea picha:

yjQISwvZ5krFAE3fjhHaCbnN8f3MSSlNkAZb_GyquPTaaUhWLIRPq5E8QU4SxkVGcZwlcir2I2RJgQjWMc3PrWKMnDpk8fsBQcXVHUwlLONvO7sLyNJ6rWz9Uh69WKHliPOJOPABwvXYbBPunn8kG3YMWRr4qBkrVK7pvF8EWPjHuKJHvInazidxy9GB1lD3KR-4npSi8eBFUJNVjgGvSoGhKb1iaSCWGj7eqs1MLP8F4OXNF3doBfNUKdESd3-AhB7lG6ZNpOVs6mT3JP8ZzpSZycRSYmK0h8muZCkeYu3cm2O38WOZZPz5YZUx7gdIKDzq3aFG3KxmrQECwZcCX1__B-A0jXm1lVfZVs_y1eNvTZVdCFnM_Y27nhqpz2Ycz3rcNfN4Wab__iPievnBnC0tItwx8xz12b6n4Df_R9KVZWuFrTNFhseFvm2Ylm6wwIopXAZ_X_KpVYmmAnHTeLEZO3duHO_HFC23OedEV_EjGDse7fP7gKLGsouUFWYlxg1Vb3cDYc7JsCNsLiim5B5R5kezQu6SBz5_ul1URR4I5WEOC78KUhWknwam4PybD5BbFDkUS_J2MTgBh3_L_rPzPjjBJyqSgfxgRiPebpKTZh5n6qFRMQ=w480-h360-no


Northwestern University, Evanston Chicago hapa nilizungumza ukumbi wa
Eduardo Mondlane kwa mwaliko wa chuo hicho.

Disgrace?
Me?

Msome Bergen (1981) kisha Sivalon (1992).
Kisha uwe na ujasiri wa kueleza Majlis uliyosoma.
 
Yamakagashi,
Yawezekana katika malezi yako hukufunzwa adabu kwa hiyo unadhani unaweza
kusema lolote na chochote hadharani kwa namna yoyote.

Inawezekana pia uwezo wako wa akili ni hafifu kiasi hujui tofauti ya kitabu cha Aesop
na kazi ya kisomi inayochapwa katika jarida la kisomi ikawa haya yote kwako ni sawa
kama unavyosema kuwa ni ''hekaya.''

Inawezekana nikakueleza kuwa majarida makubwa kama Cambridge Journal of African
History wamechapa mapitio ya kitabu changu yalioandikwa na wanahistoria mashuhuru
duniani kama John Iliffe, James Brennan na Jonathon Glassman ikawe wewe hulijui hilo
jarida wala huwajui hao wanahistoria.

Inawezekana dunia yako imezungukwa na ujinga.

Sasa tuje katika swali la kwa nini Mkristo hawi rais Zanzibar.
Unataka mimi nikujibu swali hilo.

Hakika swali hilo nimeliona na nililipuuza kwa kuwa si kawaida yangu kujibu maswali
ya vichekesho.

Lakini ili kuistua akili yako nami nitakuuliza swali unazijua takwimu za Zanzibar katika
mgawanyo wa watu na imani zao?

Unaijua historia ya Zanzibar?
Fanya utafiti jibu lako utalipata hapo.

Nimekuita mpuuzi kwa kuwa hakika wewe ni zaidi ya mpuuzi.

Hujui kitu lakini unajiaminisha kuwa unaweza kusimama na mimi katika historia ya
Tanganyika.

Mjinga tu ndiye asiweza kujipima na kujua uwezo wake.

Nakuwekea picha niliyopiga miaka 30 iliyopita nikifanya kipindi cha historia BBC
Glasgow Uskochi.

wQLwvqHnAkZvlnFj5VIOHASVbHZPbckL4k89SWZHgfVXtTAFoyCZVTTkwHvTJaTfelIsUiW5q9mlTqXotAJQ1kssRpMOgvRWl-LlATHM0e11iTzMKwTKR8PCM_NW1CtbNNi2Dr6AhqCu4y1C5fA0YXWNqSGWfx17MoXfJaeQ-yclQTHjXSgR-YFJMJH9GGxEgi5gABHV6omlPr12leVkc7IIBZHlBXLALyUf9ueedz6VcHYYsnswPgN2tBn8Vuxt1qyZpuLoZIgYOn7sn1_J8jCxHopecM7Ox4COiRxnvgmz8xUNPztaqfdjIsyX5Kd_dU3hmgILoJMWI0rJ_BGNX8ZhwQgmBb6P3ThKs-oIbwu5OlM01WCaR3YA0zvvclOSZ5NJDoXsTyw18y6X4kWyKWHkpP0WktfW1GBEDYm7rsRwJYA9fHg1F8iuBOQXLlBgVJh5ZcN9m9fH7DQc63llz_wxap2YLj-N-ZiSqu7Gq8qrY-gWLrwNWQbSpnjR4JRQVN5hpbFx_zj_ko4zqoXObGYqgdeEF7Q5RmCTdci1cNhhyzboJzAql79kXyHT60mSOtyxgRtQW9_OEYGgojBnP5BIFP3bljvvN7KcVZLtTgihs57UD5xjtF0-KLHC-lry_H29oRT-yCnCyZGzkkiVGSuAOne4a0Zo88B0PuW9CoY=w960-h692-no


Yamakagashi,
Hapo juu ndiko nilikotoka mimi na ni wakati huo nikiwa kijana mdogo nikiandika na magazeti mashuhuri Afrika kama New African, Africa Events na Africa Analysis.

Kuwa na adabu kidogo.
Si dhambi kuandika lolote au chochote IMA la muhimu Lowe/kiwete chenye ukweli uliotafitiwa kama ufanyavyo Mohammed Said. Kila mtu ana kwao, kama wewe imetokea bahati kwako kuwa wapigania uhuru wa Tanganyika ni "wazee wako wa Kariakoo", hiyo kwako ni neema sana na wala si dhambi.

Hilo lonakupa uhakika wa kujivuna kwa kile unachokiandika kwa kuwa umepewa na "wazee wako wa Kariakoo".
Endelea kufanya kazi zako kaka, unfold all folded papers and tell us untold stories.

Si lazima kila mtu apende unachoandika...ndio ubinaadamu huo, mtu anaweza kupendezwa au kuchukizwa na majina ya watu pengine kwa kushindwa kuyatamka tu kama Sykes, Schneider Schneider Schneider n.k.
 
Salumson,
Ahsante sana kaka.

Pokea zawadi ya X Mas:
ZUBERI MTEMVU: MPANGAJI MIKAKATI WA TANU NA MUASISI WA UPINZANI

o3yh0kDTiNcQlCSz2tfrbZqyvDxMlux2SVEVS9ZPocl0UoqwHRvOovD2nF06NGgWnC9L2hdZ3H9zIxwaNFQBDXoqAnGAs1siwu20fKYl1RaY6N_4FL2drI5PYgcYtDvaHyvmfBEnBH8MFtgU-1NdqLelBQiFYl0R12_0I0SwVlj4noN09YjLHxvbwL2ouyS_EZriHzzEN6kBPPnbob1C2IHRV1pQ7m5bbeNeqdxuGvEwBg5rW0Td8VGJF1MlIZiVt6RY2XxwZizK3ftSx-zjsV3z7XJ5S-9dD-N5WvBFMwtGgb4iVAzI-rfbF9hnsUJvpW8NZD7pcUTgNa6Tg3Ezm_t7p4uA_b0Mz0fY3QvniK0Jc4VU7cGwSSOvpF8-NWJk6IAV9bwxb9Ho71Y6zF3JGuu6tVwwAmfzU5H8eYYrXkqEX6muIiOHbC2HJ5eUEOO6H29b4vbRt61Xx5hNIkVOHB3CN9LbL8IdHcSwR8Puc9-IgMY-4jV8Z8ce4SwyDwntuI9bbpt6v7QthhAhQn104j_LQlq5V2FLFJXb3kT-oZsivOcJ9cVYBZdC5AfdsFw8ZzCBIoYAZO1C1Jtmb24anc9BpbzkeTP78p6Pm18XwQnCI04ZzA=w438-h692-no


IogchVui18NrygovxS4B2Uyzsa-IpdeG7bIax1lHOYLVrJbfLwo0rP3TKEoVdncdc4rtGtnj3lXAJJB2T8UMCuiYu33NvXGYxRgwstlfilgjEUEZ3wtZ87rOJ9x1lFrcpQ3mMjVxrVuOel2PvYaZDpiDxMxRcAE1JD9J2OarCBQKMAkQbZfosIpuSMpHz1h0brNFUE0pt5d5xp9Tce0zTb53rGpntSFmz-ncaXOBdvcHS-AlQQN_8KSYIIL9noZ5TorvOC2fEKFJclwMpINENByrJGjo_eV3AfebetH9n3oYxOU2v9tEZ28mgkOdOv-l6DWvKU59MhAIyMbLsOlqDT2vBhxk_SlOaXowwORnGgo02qwtu-SpJfML8I7Cn_VicTaT6osi6KiL-hmEdeJA5PyyTHkIYbQ3P7ettOpWeOxoNI-uvw75ngKCSci9w2trZCR9MmpxwaS60s3G46nXp1CaNPxFGQa_g9H4EDeGfEFIGESh3rXvmO-fXiAElrcEREpiF9QDg_XkJwiBr9b3p3WTgskGKaAHZNO7LoClLbsuZKzoJU9lk6zSGAZZfuULShGcbrxfnOZDmG_TCVUBSySEUSUZlZoljZA34_Hv_dUA_3ypmQ=w287-h220-no

Rai Oktoba 28 - Novemba 3, 1990
 
Kaka Joka Kuu,

Mzee Hussein Shekilango aliwahi kuwa Mbunge wa Korogwe na Baadaye alikuwa waziri Wa Nchi Ofisi Ya Waziri Mkuu anayeshughulikia mambo ya Utawala (Nafikiri utakuwa unawafahamu watumishi wa namna hii).Mzee Shekilango alikuwa mtu wa karibu sana na Rais Nyerere (RIP) na Waziri Mkuu wa wakati huo Mh.Edward Sokoine (RIP).

Ilikuwa mwezi May/1980 Mzee Shekilango pamoja na watumishi wengine wa serikali na Wanajeshi wa Jeshi la Ulinzi walipata ajali ya ndege huko Arusha na kufariki.Mzee Shekilango na ujumbe wake walikuwa wanasafiri kwa ndege ndogo kutoka Arusha kwenda Entebbe.Ikumbukwe kuwa kipindi hicho tulikuwa katika vita na Utawala wa Amin,na inasemekana Mzee Shekilango alikuwa ametumwa na Rais kwa kazi maalumu huko Uganda.

Sina Ufahamu ni nani alipendekeza Jina la Barabara ile ya Shekilango (Mwenge/sinza) lakini Shekilango anahesabiwa kama shujaa,kwa sababu alikufa kazini na katika shughuli za Vita vya Kagera.Mtoto wa Kiume wa Marehemu Shekilango alikuwa mmojawapo ya wanachama wa CCM 19 walioomba Ubunge wa Korogwe -Magharibi katika Uchaguzi Mkuu wa 2005.
Aliwahi kuwa RC wa DSM
 
Unasema Shakespeare sio wa kutishiwa wewe ? Sasa wewe una tofauti gani na Shigongo ?

Acha kumfananisha Shakespeare na vitu vya ajabu

Haya umezunguka kote huko faida yake ndio kuja na hizi hekaya , Je usingekuwa umezunguka ingekuwaje ?

Na wewe ni mwanazuoni ?

Unajitapa hapa na Hekaya zako kina Socrates sijui wasemaje

Endelea kuwafurahisha wanahekaya wenzako
Mimi sidanganyiki

Halafu kuna sifa moja mwanaume anayo ni uwezo wa kustahimili jambo ,nakuzunguka kote huko umekosa kujifunza hilo au ulikuwa unashangaa magorofa tu

Usitake kila mtu akubaliane na sumu zako
Hizo First Class pass zako zinasaidia nini uma kama hamna Legacy yoyote unayoacha zaidi ya kupigania udini ?

You are a disgrace to this Nation

Mzee wangu achana, nao ukweli mchungu unomuuma sana, tatizo ni elimu yetu ndo iliyozalisha vilaza kama hawa waliojificha katika kile wanachojiita wasomi, wasiotaka wala kupenda kufanya research.

Mzee wangu, endelea kutupa na kutupasha tusiyoyajua.
 
Ocean Road imekabidhiwa Obama kama shukran ya kuitembelea nchi yetu. Old Bagamoyo road ishabatizwa Mwai Kibaki. Siku hizi rair wa nje akija tunamzawadia barabara.

Usisahau JK na Mkapa bado hawajakabidhiwa barabara. Wao bado wanatesa na madaraja tu.
daraja la kikwete malagarasi na daraja la rufiji linaitwa mkapa
 
JINA SHEKILANGO


Jijini Dar es salaam kuna Barabara Mashuhuri kama 'Shekilango Road', ikianzia maungio ya Barabara ya Morogoro eneo la Nyumba za NHC mkabala na Kiwanda cha Urafiki, ikipitia Mitaa yote ya Sinza na kuishia Maungio ya Barabara ya Ali Hassan Mwinyi kituo cha Bamaga.

Ni watanzania wachache wajuao kuwa Barabara hiyo ya Shekilango imepewa jina Maalum kwaajili ya heshima ya Ndugu Hussein Ramadhani Shekilango, aliyekuwa Waziri wa Nchi katika Ofisi ya Waziri Mkuu, akishughulika zaidi na mambo ya Utawala, wakati wa Uongozi wa Rais Julius Nyerere na Makamo wake Aboud Jumbe Mwinyi.

Hussein Shekilango alichaguliwa na Wananchi wa kwao kuwa Mbunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wa Jimbo la Korogwe Mjini, Mkoani Tanga katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 1975, akiachia nafasi yake ya Zamani ya Meneja Mkuu wa Shirika la Usagishaji Nchini (NATIONAL MILLING CORPORATION).

Mwaka huo huo akachaguliwa na Rais Julius Nyerere kuwa Waziri wa Nchi katika Ofisi ya Waziri Mkuu (Utawala) akiwa chini ya Makamu wa Pili wa Rais na Waziri Mkuu, ndugu Rashid Mfaume Kawawa.

Mwaka 1977 yalifanyika Mabadiliko makubwa ya Baraza la Mawaziri Nchini, aliyekuwa Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kulinda Taifa, Ndugu Edward Moringe Sokoine aliteuliwa kuwa Waziri Mkuu akichukua nafasi ya Kawawa, Shekilango akabakishwa katika nafasi yake lakini akiwa na bosi mpya.

MATATIZO YA UGANDA


Mara baada ya Mapambano ya Vita vya Kagera, Mwanzoni mwa mwaka 1979 Vikosi vya Jeshi la Wananchi wa Tanzania vilifanikiwa kumng'oa Madarakani Dikteta Amin wa Uganda na kumpachika Ndugu Yusufu Lule kama Rais wa Muda wa Taifa hilo Jirani. Lule hakudumu sana madarakani kwa kuwa mwezi Juni, 1979 naye aling'olewa madarakani kwa kutofautiana na Baraza la Ushauri la Taifa la Nchi hiyo juu ya uteuzi wa nafasi za Mawaziri, na nafasi yake kuchukuliwa na Ngudu Godfrey Binaisa.

Miezi kadhaa baada ya kuchukua madaraka kwa Binaisa katika Serikali ya Uganda bado mambo ya kuendesha nchi hiyo hayakuonekana kwenda vizuri, Changamoto za kujenga upya nchi hiyo iliyoharibiwa na vita zilikuwa kubwa, huku Jeshi jipya la nchi hiyo likiwa na kashfa ya kufanya ukatili kwa wananchi na pia kushiriki kwenye uhalifu na uporaji. Ili kuimarisha mambo ya Kiutawala ya Nchi hiyo ilimbidi Rais Nyerere ambaye bado vikosi vya Jeshi lake vilikuwa havijaondoka Uganda, ampeleke Waziri Hussein Ramadhani Shekilango kwenda kusaidia mambo ya Kiutawala ya Nchi hiyo.

Mwezi Mei, 1980 ilizuka sintofahamu kubwa katika Utawala wa Uganda, Rais Godfrey Binaisa alimuondoa Jeshini Mnadhimu Mkuu wa Jeshi la Nchi hiyo (zamani akiitwa Chief of Staff) Ndugu David Oyite Ojok na kumteua kuwa Balozi wa Uganda Nchini Algeria, sababu kubwa ikitajwa kuwa ni nidhamu mbaya ya Jeshi la nchi hiyo hasa kwenye masuala ya Ukatili kwa wananchi na Uporaji.

Uamuzi huo wa Rais Binaisa haukumfurahisha Kiongozi huyo Namba 2 wa Jeshi la Nchi hiyo, hivyo alikataa Uteuzi mpya, na wanajeshi waliokuwa Watiifu kwake wakatangaza kumuondoa Madarakani Rais Binaisa aliyekuwa akilindwa na Jeshi la Wananchi wa Tanzania katika Hekalu la Rais la Entebbe.

Misururu mirefu ya Magari ikaonekana katika Jiji la Kamapala, ambapo Wanajeshi watiifu kwa David Ojok walikuwa wakiyapekuwa magari yote yaliyokuwa yakitoka na kuingia ndani ya jiji hilo ili kuhakikisha hakuna silaha, huku pia wakikiteka Kituo cha Redio cha Taifa cha Nchi hiyo.

Wanajeshi wafuasi wa Ojok waliweka vizuizi katika barabara zote za Jiji la Kampala na kuamua kuyalinda majengo yote nyeti ya Serikali likiwemo Jengo la Nile Mansion Hotel ambalo ndilo lililokuwa na Ofisi nyingi za Wizara nyeti za Serikali ya Nchi hiyo.

Kung'olewa kwa Binaisa kulifanywa na Tume maalum ya Watu sita, ambayo ilikuwa ni sehemu ya Baraza la Ushauri la Taifa lililomng'oa Rais Lule, huku matendo ya Tume hiyo pamoja na Ojok kwenye wiki hiyo yakihusishwa zaidi na Rais Milton Obote aliyekuwa ughaibuni, ambaye aling'olewa Madarakani na Amin mwaka 1971. Obote alikanusha kuhusika na matendo hayo ya Ojok yaliyokuwa yakiteteresha hali ya ustawi wa nchi hiyo japo haikubadili ukweli kuwa marafiki hao lao lilikuwa moja.

katika hali ya matatizo yote hayo, Waziri Hussein Ramadhani Shekilango pamoja na Balozi Kilumanga waliamua kupanda Ndege kwenda kumpa habari za namna hali halisi ya mambo ilivyo nchini humo Rais Nyerere ambaye alikuwa kwenye Ziara ya Kiserikali Mkoani Arusha. Safari hiyo ndiyo ikawa mwisho wa maisha yao.

Ilikuwa siku ya huzuni mno kwa kumpoteza Waziri huyo damu changa, Tarehe 11 Mei, 1980, ndege ya Kijeshi iliyowachukua Shekilango, Balozi Kilumanga pamoja na Wanajeshi wanne wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania ilianguka katika vilima vya Jiji la Arusha na Abiria wote kupoteza Maisha, wakiacha huzuni na majonzi mazito kwa Watanzania.

Msafara wa Rais ukakatisha ziara na shughuli ya Mapokezi ya Miili ya Mashujaa wetu hao ndiyo ikawa Ratiba rasmi, huku Rais Nyerere akionyesha kwa dhati namna alivyohuzunishwa kwa kumpoteza Waziri huyo Mchapa Kazi kwa Taifa. Majonzi zaidi yakiwa kwa Wanakorogwe waliopoteza Kijana wao Msomi wa Makerere aliyejitolea kuwatumikia kwa dhati.

Shekilango alizikwa Kijijini kwao Jitengeni, Korogwe, Mkoani Tanga, huku akisindikizwa na umati mkubwa wa watu, mpaka leo akibaki Mbunge kipenzi cha watu wa Korogwe na akisifika Serikalini kwa hatua yake ya kurudisha Madaraka Mikoani. Kwa kumuenzi kuna Shule yenye jina lake Jimboni Korogwe.

Mamlaka za Uongozi wa Jiji la Dar es salaam kwa kutambua mchango wa Shekilango kwa Taifa, ikaamua kuipa Barabara mpya iliyokuwa inajengwa wakati huo jina la Shekilango ili kumuenzi shujaa huyu.

Mola amlaze Pema Hussein Ramadhani Shekilango
 
Ata pale Sinza Africa Sana kuna shule inaitwa shekilango primary school ipo mkabala na mapambano shule ya msingi.
 
Vitu adimu kama hivi vinatakiwa vitunzwe vizuri kwa ajili ya siku za baadae. Safi sana mkuu.
 
Back
Top Bottom