Eiyer
JF-Expert Member
- Apr 17, 2011
- 28,259
- 20,891
Kwanini mnapenda sana kupindisha maandiko ninyi?Kumtambulisha “Babiloni Mkubwa”
KITABU cha Ufunuo kina majina ambayo yana maana ya mfano. (Ufunuo 1:1) Kwa mfano, kinataja mwanamke ambaye jina “Babiloni Mkubwa” limeandikwa katika paji la uso wake. Kinasema kwamba mwanamke huyo ameketi juu ya “umati na mataifa.” (Ufunuo 17:1, 5, 15) Kwa kuwa hakuna mwanamke halisi anayeweza kufanya hivyo, lazima Babiloni Mkubwa awe mwanamke wa mfano. Kwa hiyo, kahaba huyo wa mfano anawakilisha nini?
Kwenye Ufunuo 17:18, mwanamke huyohuyo wa mfano anatajwa kuwa “lile jiji kubwa lililo na ufalme juu ya wafalme wa dunia.” Jina “jiji” linarejelea kikundi cha watu. Kwa kuwa ‘jiji hilo kubwa’ linaongoza “wafalme wa dunia,” lazima yule mwanamke anayeitwa Babiloni Mkubwa awe shirika lenye uvutano ulimwenguni pote. Linaweza kuitwa milki ya ulimwengu. Milki ya aina gani? Ya kidini. Ona jinsi maandiko mengine katika kitabu cha Ufunuo yanavyotusaidia kufikia uamuzi huo.
Milki inaweza kuwa ya kisiasa, ya kibiashara, au ya kidini. Mwanamke anayeitwa Babiloni Mkubwa si milki ya kisiasa kwa sababu Neno la Mungu linasema kwamba “wafalme wa dunia,” au wanasiasa wa ulimwengu huu, “walifanya uasherati” naye. Uasherati wake ni mapatano ambayo amefanya na watawala wa dunia na ndiyo sababu anaitwa “kahaba mkubwa.”—Ufunuo 17:1, 2; Yakobo 4:4.
Babiloni Mkubwa hawezi kuwa milki ya kibiashara kwa sababu “wanabiashara wa dunia,” watamlilia atakapoharibiwa. Isitoshe, wafalme na wanabiashara watamwangalia Babiloni Mkubwa wakiwa “mbali.” (Ufunuo 18:3, 9, 10, 15-17) Kwa hiyo, ni wazi kwamba Babiloni Mkubwa, si milki ya kisiasa wala ya kibiashara, bali ni milki ya kidini.
Hilo linathibitishwa na ile taarifa ya kwamba Babiloni Mkubwa anapotosha mataifa yote kwa ‘mazoea yake ya kuwasiliana na pepo.’ (Ufunuo 18:23) Kwa kuwa mazoea yote ya kuwasiliana na pepo hutokana na dini na roho waovu, haishangazi kwamba Biblia inamwita Babiloni Mkubwa “makao ya roho waovu.” (Ufunuo 18:2; Kumbukumbu la Torati 18:10-12) Pia, milki hiyo inapinga vikali dini ya kweli, ikiwatesa “manabii” na “watakatifu.” (Ufunuo 18:24) Kwa kweli, Babiloni Mkubwa anachukia sana dini ya kweli hivi kwamba anawatesa kikatili na hata kuwaua “mashahidi wa Yesu.” (Ufunuo 17:6) Hivyo, ni wazi kwamba mwanamke huyo anayeitwa Babiloni Mkubwa anawakilisha milki ya ulimwenguni pote ya dini ya uwongo, inayotia ndani dini zote zinazompinga Yehova Mungu
Rejea
Biblia inafundisha nini hasa? @ jw.org chini ya kichwa machapisho>vtabu
Dhambi hii itawatafuna nawaambieni...
Ufunuo inatoa fasiri ya mwanamke ni nani na imesema wazi kuwa ni mji mkuu,wewe unakuja na maana yako kuwa ni milki ya kidini,unatoa wapi hii? Unataka kusema kuwa malaika hakuwa anajua alichokuwa akisema? Tena alikuwa anatoa TAFSIRI siyo kwamba alikuwa anazungumza kwa mafumbo kwasababu tayari Yohana alikuwa ameshapewa mafumbo na alikuwa anataka ufafanuzi.....
Hii dhana ya mwanamke kuwa kanisa au milki ya kidini haikubaliani kabisa na unabii huu.Siyo kila mahali anapotamkwa mwanamke kwenye unabii ni kanisa.....
Kanuni ya kufasiri unabii inaeleweka,kuna maeneo Mungu ametoa ufafanuzi wa mafumbo na kuna sehemu hajatoa,kule alikotoa kwanini mnakataa maana hiyo na kutafuta yenu?
Sijui ni kwanini mnaendelea kujidanmganya....