MDUDU KANTANGAZE ( Tuta absoluta) AZIDI KUUA KILIMO CHA NYANYA TANZANIA.
Leo nimeona habari iliyotolewa na ITV kuhusu zaidi za ekari mianane za Nyanya katika kijiji cha Ngarenanyuki wilaya ya Arumeru mkoani Arusha kuteketezwa na Kantangaze na hivyo nimeamua kuandika machache kuhusu huyu mdudu wenda yakawasaidia wengi.
CHIMBUKO
Chimbuko la Kantangaze ni America ya Kusini miaka ya 80's. Kutoka huko alienea sehemu za Ulaya hususani Spain na katika hali ya Kimediterania. Mpaka sasa mataifa yaliyo Kaskazini mwa Africa mfano Tunisia yameshashambuliwa vikali. Nchi Tanzani mdudu huyu kwa mara ya kwanza aliripotiwa mwaka 2014 ambapo kati ya mwaka 2014 - 2015 na maeneo ya kwanza kuathirika sana ambayo ni Ngabobo, Ngarenanyuki na King'ori wilayani Arumeru ambayo ni maarufu kwa uzalishaji nyanya yalipata hasara kubwa.Mdudu huyu husambazwa kwa kasi sana hususani kupitia mazao yaliyoharibiwa sokoni na kutumia mbegu zenye masalia.Hivyo hupaswi akufikie ndo umfahamu.
MUONEKANO
Tuta absoluta hutaga mayai kati ya 250 mpaka 300 katika kipindi cha uhai wake ambao ni kati ya siku 28-30.Akiwa mkubwa- huonekana katika umbo la kipepeo ( moth) mdogo mwenye ukubwa wa mm 6 hivi. Kipepeo huyo huwa na rangi ya Kijivu chenye Ukahawia ( grey-brown).
Akiwa Kiwavi ( Caterpillar)- Kiwavi mchanga sana huwa na rangi ya Njano ( Yellowish).Kadiri anavyokuwa hubadilika na rangi ya njano yenye ukijani ( yellow-green) na michirizi myeusi ( black bands) huota nyuma ya kichwa. Akikua huwa na rangi ya waridi ( pink).
Pupa:- Pupa wake ana rangi ya kahawia isiyokolea ( light brown).
UHARIBIFU
Hushambilia sana nyanya.Pia ana uwezo wa kuharibu viazi mviringo.Hatua ya ukuaji ya Tuta absoluta inayoshambia mmea ni KIWAVI ( Caterpillar) .Kiwavi huchimba majani, mashina na sehemu ya taji la tunda la nyanya. Pia huchimbua matunda ya nyanya yaliyo na ukijani na kufanya uingiaji wa vijidudu wengine kama fangasi na bakteria uwe rahisi. Kiwahi husababisha madoadoa yaliyokauka ( blotches ) katika majani ya mnyanya ambapo huwa anaishi. Lakini pia kiwavi anaweza kuishi nje ya majani na mashina mfano aridhini kwa muda. Maambukizi yakizidi jani hufa kabisa na mmea kunyauka.Pia huharibu mashina.
JINSI YA KUMZUIA
-Kilimo cha mzunguko ( crop rotation) kwa kutumia mazao yasiyo shambuliwa( mazao yasiyo jamii ya nyanya au viazi mviringo ). Mfano msimu huu ukilima nyanya/viazi msimu ujao unalima mahindi. Masalia ya wadudu hao yatakosa chakula na kufa kabisa maana hayana uwezo wa kula mahindi).
-Kuondoa mazao yote shambani kipindi cha kuvuna.
-Kuondoa na kuteketeza kabisa mimea iliyoathiriwa shambani
( Hizi njia zikitumiwa sehemu iliyo closed mfano greenhouse huwamaliza kabisa. Lakini sehemu iliyo wazi hizi njia huwapunguza kiasi cha kutosababisha hasara ( economic loss). Pia kama pembeni kuna mimea ya Solanaceae family itoe isije kuwa hifadhi.
Njia nyinginezo ni:Kulima vizuri, umwagiliaji mzuri na matumizi mazuri ya mbolea.
KUTUMIA KEMIKALI ( Insectides)
Japo zinatofautiana uwezo kemikali hizi ukizipa zaweda kuwa msaada mkubwa.
Cypermethrin, duduall-yenye mchanganyiko wa Cypermethrin na Profenofos au Chloropyrphos. Hizi ndizo zimeonekana kuwa na uwezo wa kuwaua.
Pia Deltamethrin na Pyrethroids zaweza kutumiwa japo uwezo wake umethibi
kuwa mdogo.
Nyinginezo ni Mwarubaini, spinosin,indoxacarb, methamidophos, abamectin, emamectin benzoate na cryomazin.
Pia unaweza kutumia mtego ( bait). Huwa na sex hormone iliyotengenezwa , harufu yake huvutia vidume. Vikija kwenye huo mtego hufa maana huwa na dawa. Hivyo unapunguza wingi wao na kasi ya kuzaliana.
Leo nimeona habari iliyotolewa na ITV kuhusu zaidi za ekari mianane za Nyanya katika kijiji cha Ngarenanyuki wilaya ya Arumeru mkoani Arusha kuteketezwa na Kantangaze na hivyo nimeamua kuandika machache kuhusu huyu mdudu wenda yakawasaidia wengi.
CHIMBUKO
Chimbuko la Kantangaze ni America ya Kusini miaka ya 80's. Kutoka huko alienea sehemu za Ulaya hususani Spain na katika hali ya Kimediterania. Mpaka sasa mataifa yaliyo Kaskazini mwa Africa mfano Tunisia yameshashambuliwa vikali. Nchi Tanzani mdudu huyu kwa mara ya kwanza aliripotiwa mwaka 2014 ambapo kati ya mwaka 2014 - 2015 na maeneo ya kwanza kuathirika sana ambayo ni Ngabobo, Ngarenanyuki na King'ori wilayani Arumeru ambayo ni maarufu kwa uzalishaji nyanya yalipata hasara kubwa.Mdudu huyu husambazwa kwa kasi sana hususani kupitia mazao yaliyoharibiwa sokoni na kutumia mbegu zenye masalia.Hivyo hupaswi akufikie ndo umfahamu.
MUONEKANO
Tuta absoluta hutaga mayai kati ya 250 mpaka 300 katika kipindi cha uhai wake ambao ni kati ya siku 28-30.Akiwa mkubwa- huonekana katika umbo la kipepeo ( moth) mdogo mwenye ukubwa wa mm 6 hivi. Kipepeo huyo huwa na rangi ya Kijivu chenye Ukahawia ( grey-brown).
Akiwa Kiwavi ( Caterpillar)- Kiwavi mchanga sana huwa na rangi ya Njano ( Yellowish).Kadiri anavyokuwa hubadilika na rangi ya njano yenye ukijani ( yellow-green) na michirizi myeusi ( black bands) huota nyuma ya kichwa. Akikua huwa na rangi ya waridi ( pink).
Pupa:- Pupa wake ana rangi ya kahawia isiyokolea ( light brown).
UHARIBIFU
Hushambilia sana nyanya.Pia ana uwezo wa kuharibu viazi mviringo.Hatua ya ukuaji ya Tuta absoluta inayoshambia mmea ni KIWAVI ( Caterpillar) .Kiwavi huchimba majani, mashina na sehemu ya taji la tunda la nyanya. Pia huchimbua matunda ya nyanya yaliyo na ukijani na kufanya uingiaji wa vijidudu wengine kama fangasi na bakteria uwe rahisi. Kiwahi husababisha madoadoa yaliyokauka ( blotches ) katika majani ya mnyanya ambapo huwa anaishi. Lakini pia kiwavi anaweza kuishi nje ya majani na mashina mfano aridhini kwa muda. Maambukizi yakizidi jani hufa kabisa na mmea kunyauka.Pia huharibu mashina.
JINSI YA KUMZUIA
-Kilimo cha mzunguko ( crop rotation) kwa kutumia mazao yasiyo shambuliwa( mazao yasiyo jamii ya nyanya au viazi mviringo ). Mfano msimu huu ukilima nyanya/viazi msimu ujao unalima mahindi. Masalia ya wadudu hao yatakosa chakula na kufa kabisa maana hayana uwezo wa kula mahindi).
-Kuondoa mazao yote shambani kipindi cha kuvuna.
-Kuondoa na kuteketeza kabisa mimea iliyoathiriwa shambani
( Hizi njia zikitumiwa sehemu iliyo closed mfano greenhouse huwamaliza kabisa. Lakini sehemu iliyo wazi hizi njia huwapunguza kiasi cha kutosababisha hasara ( economic loss). Pia kama pembeni kuna mimea ya Solanaceae family itoe isije kuwa hifadhi.
Njia nyinginezo ni:Kulima vizuri, umwagiliaji mzuri na matumizi mazuri ya mbolea.
KUTUMIA KEMIKALI ( Insectides)
Japo zinatofautiana uwezo kemikali hizi ukizipa zaweda kuwa msaada mkubwa.
Cypermethrin, duduall-yenye mchanganyiko wa Cypermethrin na Profenofos au Chloropyrphos. Hizi ndizo zimeonekana kuwa na uwezo wa kuwaua.
Pia Deltamethrin na Pyrethroids zaweza kutumiwa japo uwezo wake umethibi
kuwa mdogo.
Nyinginezo ni Mwarubaini, spinosin,indoxacarb, methamidophos, abamectin, emamectin benzoate na cryomazin.
Pia unaweza kutumia mtego ( bait). Huwa na sex hormone iliyotengenezwa , harufu yake huvutia vidume. Vikija kwenye huo mtego hufa maana huwa na dawa. Hivyo unapunguza wingi wao na kasi ya kuzaliana.