Mfahamu Mugo wa Kibiru au Chege(Cege) wa Kibiru, Nabii aliyetabiri ujio wa mzungu/mkoloni Afrika Mashariki

Mfahamu Mugo wa Kibiru au Chege(Cege) wa Kibiru, Nabii aliyetabiri ujio wa mzungu/mkoloni Afrika Mashariki

pingli-nywee

JF-Expert Member
Joined
Sep 16, 2015
Posts
11,923
Reaction score
13,350
Hii ni kwa waafrika wote wafia dini za kuja kwa meli na manabii wa uongo, ambao hadi leo hii hawajatabiri jambo lolote la kweli kuhusu Afrika.

Mugo wa Kíbirú alikuwa nabii aliyeishi kabla na wakati mkoloni alipowasili Kenya. Nabii Mugo alitabiri ujio wa mkoloni Afrika Mashariki, miaka mingi kabla ya tukio lenyewe.

Utabiri wa Mugo wa Kíbirú ulikuwa hivi; Kwamba kutawasili watu wenye ngozi inayofanana na chura mweupe, 'kiengere' kwa kikikuyu.

Kwamba kwa kuwatazama tu watu watakuwa wanaona damu kwenye mishipa miilini mwao. Vyura hivyo vitakuwa vimevalia nguo zenye rangi nyingi, mithili ya vipepeo(kííuhuruta) na itakuwa upumbavu kuwashambulia kwa mikuki.

Kwasababu watakuja na vijiti vya ajabu(bunduki), ambavyo vitakuwa vinatoa moto(risasi).

Kisha akatabiri ujio wa reli na treni ya mkoloni. Akasema watakuja na joka kubwa la chuma, ambalo litakuwa linatembea kwenye barabara ya chuma. Likitema watu kila mara linaposimama, huku likiongozwa na kichwa kinachotoa moshi.

http://shujaastories.com/stories/mugo-wa-kibiru/
 
Nabii Mugo wa Kíbirú aliyeishi Kariara, Gatuzi la Múrang'a karibu na mji wa Thíka alitabiri ujio wa mkoloni 'in detail'. Akatabiri kwamba joka la chuma(treni) la mkoloni litakuwa na barabara ambayo itatoka Bahari ya Hindi hadi Ziwa Victoria. Akatabiri kwamba wakoloni watakuwa wanabeba moto kwenye mifuko yao(viberiti). Mugo wa Kibiru alitabiri pia mwisho wa ukoloni, baada ya miaka 68 nchini Kenya. Ambapo alisema kwamba mti mtakatifu wa wakikuyu, Múgumo, ambao ulikuwa Thika utakapoanguka utaashiria mwisho wa ukoloni. Jambo ambalo lilimtia kiwewe mkoloni hadi akauvingira mti huo kwa chuma na kuujazia mchanga ili usije ukaanguka. Ila mti huo mkubwa mwishowe ulipigwa na radi na ukaanguka na kunyauka muda mfupi kabla ya nchi ya Kenya kupata uhuru. Mabaki ya mti wenyewe na 'fortification' ya chuma, kazi ya mkoloni, pale Múgumo Garden, Thíka.
 
Hii ni kwa waafrika wote wafia dini za kuja kwa meli na manabii wa uongo ambao hadi leo hii hawajatabiri jambo lolote la kweli kuhusu Afrika. Mugo wa Kibiru alikuwa nabii aliyeishi kabla na wakati mkoloni alipowasili Kenya. Nabii Mugo alitabiri ujio wa mkoloni Afrika Mashariki miaka mingi kabla ya tukio lenyewe. Utabiri wa Mugo wa Kibiru ulikuwa hivi; Kwamba kutawasili watu wenye ngozi inayofanana na chura mweupe aina ya 'kiengere'(kikikuyu). Kwamba kwa kuwatazama tu watu watakuwa wanaona damu kwenye mishipa miilini yao. Vyura hivyo vitakuwa vimevalia nguo zenye rangi nyingi kama vipepeo(kiiuhuruta) na itakuwa upumbavu kuwashambulia kwa mikuki. Kwasababu watakuja na vijiti vya ajabu(bunduki) ambavyo vitakuwa vinatoa moto(risasi). Kisha akatabiri ujio wa reli na treni ya mkoloni. Ambayo alisema itakuwa ni joka kubwa la chuma ambalo litakuwa linatembea kwenye barabara ya chuma likitema watu kila mara linaposimama. Huku likiongozwa na kichwa ambacho kinatoa moshi. http://shujaastories.com/stories/mugo-wa-kibiru/
Hapa JamiiForums mambo ya utabiri hayaruhusiwi kabisaaa
 
Jombaa, nimekuekea link hapo, isome vizuri na ukipenda fanya risechi yako ya ziada kwenye vyanzo vingine na kwenye kumbukumbu za kihistoria. Hizi sio hadithi za abunuwasi, tizama hiyo video hapo juu pia. Kumbukumbu ipo ya mabeberu na walivoingiza baridi kuhusu utabiri wa Mugo wa Kíbirú. Ukipenda zuru Kenya ufike mji wa Thika, Múgumo Gardens, ujionee mwenyewe kwa macho yako ushahidi wa mti huo ambao ndio ulimalizia utabiri wake na kila kitu kilivyotokea kama alivyotabiri.
 
Naam kwa wanaotaka kujua dini yake ipo mpaka leo
Mimi mwenyewe mfuasi wa Mungu wake.
Tunajiita Alkebulans

Sent using Jamii Forums mobile app
Siku hizi Alkebulan(Mother of Mankind) imevurugwa na watoto wake hawana imani kabisa kwamba nabii anaweza akawa mtu mwenye ngozi nyeusi. Wapo radhi kuchukiana na kuuana kwasababu ya dini za watu wa ngozi nyeupe na pua ndefu. Tena dini ambazo hazina nafasi ya mtu mweusi. Poor Alkebulans.
 
Siku hizi Alkebulan(Mother of Mankind) imevurugwa na watoto wake hawana imani kabisa kwamba nabii anaweza akawa mtu mwenye ngozi nyeusi. Wapo radhi kuchukiana na kuuana kwasababu ya dini za watu wa ngozi nyeupe na pua ndefu. Tena dini ambazo hazina nafasi ya mtu mweusi. Poor Alkebulans.
So sad. Hizi hizi dini zilizotumika kutugeuza slaves leo hii zinatufanya slaves wa fikra.
Kama tulivopigania Uhuru wa ukoloni physically Tunabidi tupigane na huu ukoloni mpya lakini this time sio kwa mapanga na maandamano lakini kwa kalamu na karatasi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ngúgí wa Thiong'o, 1967. "It's (Mau Mau movement)
origins can, so the people say,
be traced to the day the
whiteman came to the country,
clutching the book of God in
both hands, a magic witness that the whiteman was a
messenger from the Lord. His tongue was coated with sugar: his
humility was touching. For a
time, people ignored the voice
of the Gikuyu seer who once
said: there shall come a people
with clothes like the butterflies"- page 10 - A Grain of Wheat
Unanikumbusha literature kitabu cha Ngugi wa Thiong'o "the river between " A level. Mwandishi alimtaja huyo Mugo wa Kibiru.
 
Nakumbuka tulimsoma miaka ya zamani ktk kitabu cha The River between nafikiri by Ngugi wa Thing'o ila tulikuwa tunamwita Mugo wa kibiro

Akina Waiyaki n.k,

Kwny Maumau kuna Dedan Kimathi, Waruihu Itote, na jamaa mmoja alizikwa akiwa hai simkumbuki jina
 
Nakumbuka tulimsoma miaka ya zamani ktk kitabu cha The River between nafikiri by Ngugi wa Thing'o ila tulikuwa tunamwita Mugo wa kibiro

Akina Waiyaki n.k,

Kwny Maumau kuna Dedan Kimathi, Waruihu Itote, na jamaa mmoja alizikwa akiwa hai simkumbuki jina
Ndio yeye tu, linatamkwa Kebiro, ila linaandikwa hivyo Kíbirú, 'í' linatamkwa kama 'e' na 'ú' kama 'o'. Gray Leakey(mkoloni) ndiye aliyezikwa akiwa hai, juu chini na wapiganaji wa Mau Mau. Yaani alizikwa miguu juu kichwa chini kikiangalia Ml. Kenya.
 
Waafrika ni kizazi kiovu sana mpaka leo.

Binadam angekua na uwezo wa kuona mambo yanayofanywa na waafrika muda wote angesema dunia pasuka niingie au dunia simama nishuke njiani nipande sayari ya Mars. Watu wanalogana usiku kucha. Watu wanazini bila kuheshimu ndoa. Watu wajabaka watoto wadogo na kuwa ingilia watoto kinyume na maumbile ,watu wamekaa maofisini wanawaza kuiba tu. Watu wanatoa makafara watoto wao ,wazazi wao n.k .ili wafanikiwe. Hizi ni mbinu chafu sana za kupata mafanikio. Watu wanapata mali kwa njia za chuma ulete. Kuna watu wana masharti mabaya sana ya kulinda utajiri wao huu duniani.
Hii haijitaji kulaumu dini za Mkoloni mana zimejitahidi kupinga hayo maovu na imani zisizofaa.



Mtawala wa kwanza wa dunia hii ni muafrika lakini aliiyawala kikatili sana na akatumia vipaji vyake vyote kuwaangamiza wanadamu wenzake. Lakini sio hivyo tu bali akaweza kupinga suala la Mungu anayetawala Dunia nzima. Nimrodi alikua Muafrika aliyeinyoosha dunia nzima kidikteta na kuwaamrisha wanajeshi wake wamshambulie hata Mungu kwa kuelekeza mishale yake angani ili Mungu akitokea impate. Ulikua ni utawala uliojawa na wendawazimu.

Wazungu wana mapungufu yao lakini mapungufu ya waafrika ni manaya zaidi mana hawajifunzi wala kubadilika.

Wamisionari walikua ni watu wema sana kuliko wapigania uhuru walivyowabadili vitabu vya historia na kuwaandika baada ya Uhuru.

Dini hasa zilikua ni dini na zilisaidia sana kuleta uhuru kwa kuwaonyesha binadamu mema na mabaya.
Waafrika hawajawahi kuwa na mfumo wa pamoja wa kupinga mabaya ndio maana walikua na matendo ya kihuni na kishenzi kabisa wao kwa wao. Tangu enzi na enzi jamii za wafugaji walikua wanatanua utajiri wao kwa wizi . Kwa hiyo suala la kuvamia na kuiba rasilimali za watu wengine halikuanzishwa na Mkoloni bali lilifanywa na waafrika kwa karne na karne. Waliiba mpaka wanawake na kuvamia ardhi zenye rutuba.

Wakoloni hawakua na nguvu ya kuvamia bila kushirikiana na waafrika wenzetu walioshawishiwa na kukubali kuwakaribisha.

Hakuna Mahali wamisionari walivamia kwa nguvu bali walitumia ushawishi. Ni jambo la maana kabisa kumtawala binadam kwa ushawishi. Dini zao zilijaa ushawishi.
Lakini pia tukumbuke kuwa Afrika mpaka leo kuna watu wanakula binadamu wenzao kama wanyama hasa kule Congo kwa wale mbilikimo. Afrika mpaka miaka hii bado serikali zenye mifumo ya kikoloni zililala Albino wanauawa na kukatwa viungo kwa ajili ya matambiko ya dini za asili.
Ni bora Dini za mabeberu zinazokataza ubaguzi. Waafrika mpaka leo kuna makabila hawaoani . Kuna makabila wanabaguana mpaka kwa rangi na maumbo yao .Waafrika bado wanabaguana kwa lugha zao na koo zao. Waafrika bado wanahitaji kuletewa ukombozi mana wameshindwa kujikomboa.

Hivi karne hii ni kitu dini inazuiaje kiwanda kama kile Cha magari cha Nyumbu kuendelea wakati kilianzishwa kipindi viwanda kama vya magari ya TATA vinaanzishwa?
Hapo dini inahusikaje hapo zaidi ya ubinafsi wa mwafrika?

Nigeria kwa Mfano kitu gani kinawashinda serikali kuwahakikishia wananchi wake maisha mazuri wakati wana akiba kubwa ya mafuta na gesi na madini badala yake wanashindana kwa uchawi na kudhulumiana .

Wanaendekeza mifumo ya kizungu kwenye serikali lakini maisha ya kawaida wanaishi kwa ubinafsi na mifumo ya kiasili.
Wakoloni walikuja kama leo zilivyo simu hulazimishwi kuzinunua lakini unajikuta tu umenunua na anayeacha kununua anapitwa na taarifa nyingi sana.
Shetani anayewadanganya wanaharakati wa kupigania ujinga wa zamani wa mwafrika wananganya watu kuwa Dini ndiyo adui wa Mwafrika bila kujua kuwa adui wa mwafrika ni mwafrika mwenyewe na ubinafsi wake .
Wanachodhindwa kujua ni kwamba Dini ya mkoloni ni ile ile ya Mwafrika lakini inajaribu kwenda na wakati. Wafrika hawana dini zinazofanana. Kila kabila lilikua na dini zake. Palikua na dini za kweli na dini za uongo kama ilivyokua wakoloni.

Sio makabila yote walikua wanatambika kwa kuchinja wanyama na kumwaga damu zao kama ishara ya kutakasa. Walifanya hayo wafugaji zaidi. Kwa hiyo hao wafugaji kamwe wasingeweza kuwashawishi wakulima mana walikua ni maadui wakubwa kutokana na migogoro isiyokwisha. Lakini ukweli ni kwamba imani za matambiko ya wanyama yalitoka kule kwa Ibrahimu ambaye pia alikua baba wa baadhi ya makabila yaliyopo Afrika.
Kuzuia dini ya uzao wa Ibrahimu isiendelee ni vitendo vya kikatili mana kuna wajukuu zake wapo kila mahali kwa kila rangi duniani.

China Ukristo na uislam umeanza kuingia na sasa maendeleo yao yanapaa.
Ulaya watakapoitupa dini ya Ibrahimu wachina wataipokea na watautawala ulimwengu kwa kila kitu. Korea Kusini dini ya Ibrahimu imeingia siku nyingi na imeenea kwa kasi na maendeleo yao ni makubwa sana.
Ulaya na Amerika pia waliipokea dini mapema na sasa wanaasi mana kizazi cha sasa hakijui habari ya imani za kidini matokeo yake wanaanza mpaka kuoana watu wa jinsia moja.
 
Waafrika ni kizazi kiovu sana mpaka leo.

Binadam angekua na uwezo wa kuona mambo yanayofanywa na waafrika muda wote angesema dunia pasuka niingie au dunia simama nishuke njiani nipande sayari ya Mars. Watu wanalogana usiku kucha. Watu wanazini bila kuheshimu ndoa. Watu wajabaka watoto wadogo na kuwa ingilia watoto kinyume na maumbile ,watu wamekaa maofisini wanawaza kuiba tu. Watu wanatoa makafara watoto wao ,wazazi wao n.k .ili wafanikiwe. Hizi ni mbinu chafu sana za kupata mafanikio. Watu wanapata mali kwa njia za chuma ulete. Kuna watu wana masharti mabaya sana ya kulinda utajiri wao huu duniani.
Hii haijitaji kulaumu dini za Mkoloni mana zimejitahidi kupinga hayo maovu na imani zisizofaa.



Mtawala wa kwanza wa dunia hii ni muafrika lakini aliiyawala kikatili sana na akatumia vipaji vyake vyote kuwaangamiza wanadamu wenzake. Lakini sio hivyo tu bali akaweza kupinga suala la Mungu anayetawala Dunia nzima. Nimrodi alikua Muafrika aliyeinyoosha dunia nzima kidikteta na kuwaamrisha wanajeshi wake wamshambulie hata Mungu kwa kuelekeza mishale yake angani ili Mungu akitokea impate. Ulikua ni utawala uliojawa na wendawazimu.

Wazungu wana mapungufu yao lakini mapungufu ya waafrika ni manaya zaidi mana hawajifunzi wala kubadilika.

Wamisionari walikua ni watu wema sana kuliko wapigania uhuru walivyowabadili vitabu vya historia na kuwaandika baada ya Uhuru.

Dini hasa zilikua ni dini na zilisaidia sana kuleta uhuru kwa kuwaonyesha binadamu mema na mabaya.
Waafrika hawajawahi kuwa na mfumo wa pamoja wa kupinga mabaya ndio maana walikua na matendo ya kihuni na kishenzi kabisa wao kwa wao. Tangu enzi na enzi jamii za wafugaji walikua wanatanua utajiri wao kwa wizi . Kwa hiyo suala la kuvamia na kuiba rasilimali za watu wengine halikuanzishwa na Mkoloni bali lilifanywa na waafrika kwa karne na karne. Waliiba mpaka wanawake na kuvamia ardhi zenye rutuba.

Wakoloni hawakua na nguvu ya kuvamia bila kushirikiana na waafrika wenzetu walioshawishiwa na kukubali kuwakaribisha.

Hakuna Mahali wamisionari walivamia kwa nguvu bali walitumia ushawishi. Ni jambo la maana kabisa kumtawala binadam kwa ushawishi. Dini zao zilijaa ushawishi.
Lakini pia tukumbuke kuwa Afrika mpaka leo kuna watu wanakula binadamu wenzao kama wanyama hasa kule Congo kwa wale mbilikimo. Afrika mpaka miaka hii bado serikali zenye mifumo ya kikoloni zililala Albino wanauawa na kukatwa viungo kwa ajili ya matambiko ya dini za asili.
Ni bora Dini za mabeberu zinazokataza ubaguzi. Waafrika mpaka leo kuna makabila hawaoani . Kuna makabila wanabaguana mpaka kwa rangi na maumbo yao .Waafrika bado wanabaguana kwa lugha zao na koo zao. Waafrika bado wanahitaji kuletewa ukombozi mana wameshindwa kujikomboa.

Hivi karne hii ni kitu dini inazuiaje kiwanda kama kile Cha magari cha Nyumbu kuendelea wakati kilianzishwa kipindi viwanda kama vya magari ya TATA vinaanzishwa?
Hapo dini inahusikaje hapo zaidi ya ubinafsi wa mwafrika?

Nigeria kwa Mfano kitu gani kinawashinda serikali kuwahakikishia wananchi wake maisha mazuri wakati wana akiba kubwa ya mafuta na gesi na madini badala yake wanashindana kwa uchawi na kudhulumiana .

Wanaendekeza mifumo ya kizungu kwenye serikali lakini maisha ya kawaida wanaishi kwa ubinafsi na mifumo ya kiasili.
Wakoloni walikuja kama leo zilivyo simu hulazimishwi kuzinunua lakini unajikuta tu umenunua na anayeacha kununua anapitwa na taarifa nyingi sana.
Shetani anayewadanganya wanaharakati wa kupigania ujinga wa zamani wa mwafrika wananganya watu kuwa Dini ndiyo adui wa Mwafrika bila kujua kuwa adui wa mwafrika ni mwafrika mwenyewe na ubinafsi wake .
Wanachodhindwa kujua ni kwamba Dini ya mkoloni ni ile ile ya Mwafrika lakini inajaribu kwenda na wakati. Wafrika hawana dini zinazofanana. Kila kabila lilikua na dini zake. Palikua na dini za kweli na dini za uongo kama ilivyokua wakoloni.

Sio makabila yote walikua wanatambika kwa kuchinja wanyama na kumwaga damu zao kama ishara ya kutakasa. Walifanya hayo wafugaji zaidi. Kwa hiyo hao wafugaji kamwe wasingeweza kuwashawishi wakulima mana walikua ni maadui wakubwa kutokana na migogoro isiyokwisha. Lakini ukweli ni kwamba imani za matambiko ya wanyama yalitoka kule kwa Ibrahimu ambaye pia alikua baba wa baadhi ya makabila yaliyopo Afrika.
Kuzuia dini ya uzao wa Ibrahimu isiendelee ni vitendo vya kikatili mana kuna wajukuu zake wapo kila mahali kwa kila rangi duniani.

China Ukristo na uislam umeanza kuingia na sasa maendeleo yao yanapaa.
Ulaya watakapoitupa dini ya Ibrahimu wachina wataipokea na watautawala ulimwengu kwa kila kitu. Korea Kusini dini ya Ibrahimu imeingia siku nyingi na imeenea kwa kasi na maendeleo yao ni makubwa sana.
Ulaya na Amerika pia waliipokea dini mapema na sasa wanaasi mana kizazi cha sasa hakijui habari ya imani za kidini matokeo yake wanaanza mpaka kuoana watu wa jinsia moja.
Vipi mbona huongelei middle east inavyochafuka damu kwasababu ya ibrahim?
Mbona huongelei Urusi?
Hujasikia China wanawatenga na kuwatesa waislam?

Make no mistake, Dini haijaleta maendeleo
Watu ndo wanaleta maendeleo
Na maendeleo yanapokuja watu wanaacha dini(mf. Ulaya na America) kwasababu wanajua ilikuwa ni tool Ya kizamani tu iliyotumiwa kutawala
na baada ya miaka 500-1000 ijayo hakutakuwa na dini duniani

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Vipi mbona huongelei middle east inavyochafuka damu kwasababu ya ibrahim?
Mbona huongelei Urusi?
Hujasikia China wanawatenga na kuwatesa waislam?

Make no mistake, Dini haijaleta maendeleo
Watu ndo wanaleta maendeleo
Na maendeleo yanapokuja watu wanaacha dini(mf. Ulaya na America) kwasababu wanajua ilikuwa ni tool Ya kizamani tu iliyotumiwa kutawala
na baada ya miaka 500-1000 ijayo hakutakuwa na dini duniani

Sent using Jamii Forums mobile app
Dini inaaminika kutokana na usahihi waka na maadili ,haki,n.k.
Mashariki ya kati kuna vurugu lakini hazisababishwi na dini bali watawala wanaotawala kwa mgongo wa dini. Matokeo yake wanafanya dhulma kwa mgongo wa dini.

Dini za Mashariki ya Kati zina usahihi wa matukio yanayotaja nyakati tangu kuumbwa kwa Dunia .
Dini za imani ya Ibrahim zimebeba kumbukumbu kubwa ya matukio ya binadam ukilinganisha na imani ya kiafrika.

Dunia haina miaka 500 ijago. Hapatakuwa na kitu kinachoitwa dunia inayoishi viumbe hai.
Yatabaki magofu tu na jangwa kavu lisilo na maji.

Ulifuatilia sana utagundua hata sayari ya Mars iliwahi kuishi viumbe vikatoweka na kubaki Jangwa lisilo na kitu.
Kumbuka sayansi tuliyonayo kwa sasa inatumika kwa kasi kubwa sana.

Itafikia mahali binadamu wanachomwa sindano kama kuku wa kisasa ili waweze kukua kwa haraka na kisha kufa.
Wazungu wanajua kuwa dunia haina muda mrefu tena ndio maana wanafanya tafiti nyingi kwenye sayari nyingine.

Kwa sasa duniani karibu kila kitu ni zao la mzungu. Hata mimea na mazao ya asili yamenza kutoweka. Fikiri miaka 150 ijayo patakua na zao gani duniani. Kemikali zitatumika zaidi mpaka kuzalisha wanyama.
Wanaume watakua hawana uwezo wa Kuzalisha . Wanawake watashika mimba kwa shida sana.
Watoto wengi watakua wa maabara.
Wakati huo huo mazingira yatakuwa yameharibika vibaya mno.
Ndoa za jinsia moja zitafanyika kila mahali.Wanawake watakua wengi sana .
 
Dini inaaminika kutokana na usahihi waka na maadili ,haki,n.k.
Mashariki ya kati kuna vurugu lakini hazisababishwi na dini bali watawala wanaotawala kwa mgongo wa dini. Matokeo yake wanafanya dhulma kwa mgongo wa dini.

Dini za Mashariki ya Kati zina usahihi wa matukio yanayotaja nyakati tangu kuumbwa kwa Dunia .
Dini za imani ya Ibrahim zimebeba kumbukumbu kubwa ya matukio ya binadam ukilinganisha na imani ya kiafrika.

Dunia haina miaka 500 ijago. Hapatakuwa na kitu kinachoitwa dunia inayoishi viumbe hai.
Yatabaki magofu tu na jangwa kavu lisilo na maji.

Ulifuatilia sana utagundua hata sayari ya Mars iliwahi kuishi viumbe vikatoweka na kubaki Jangwa lisilo na kitu.
Kumbuka sayansi tuliyonayo kwa sasa inatumika kwa kasi kubwa sana.

Itafikia mahali binadamu wanachomwa sindano kama kuku wa kisasa ili waweze kukua kwa haraka na kisha kufa.
Wazungu wanajua kuwa dunia haina muda mrefu tena ndio maana wanafanya tafiti nyingi kwenye sayari nyingine.

Kwa sasa duniani karibu kila kitu ni zao la mzungu. Hata mimea na mazao ya asili yamenza kutoweka. Fikiri miaka 150 ijayo patakua na zao gani duniani. Kemikali zitatumika zaidi mpaka kuzalisha wanyama.
Wanaume watakua hawana uwezo wa Kuzalisha . Wanawake watashika mimba kwa shida sana.
Watoto wengi watakua wa maabara.
Wakati huo huo mazingira yatakuwa yameharibika vibaya mno.
Ndoa za jinsia moja zitafanyika kila mahali.Wanawake watakua wengi sana .
mkuu bila dini hao watawala wasingeweza kushawishi vita...achana na viongozi kuna watu binafsiwanajilipua,wanajiunga na makundi ya ugaidi kwasababu dini imekolea...kama ni kitu kizuri kwanini hiyo abrahamic religion ilivyoingia middle east isingeleta amani?it is always muslims vs Jews and Christians. kwahyo bila dini hayo yasingekuwepo.

Na kuhusu miaka 500 ijayo trust me dunia itakuwepo labda ungesema miaka millioni500 ijayo...umeangalia movie sana zimekuharibu.
 
Back
Top Bottom