Mfahamu T.O Kihombo 2006 aliyepata Degree yake ya Kwanza baada ya Miaka 11

Na hii ndio ilitakiwa kufanyika tangu zamani ili kuondoa udanganyifu uliopo kwenye sekta ya Elimu.
 
Na kuna uwezekano mkubwa kuwa hawa wanafunzi waliongoza kitaifa katika mitihani ya darasa la saba, kidato cha nne na kidato cha sita huwa wanapotezwa [ ⚰️ ] kwa sababu wanazozijua wenyewe watawala na sio vyema kuelezea kila kitu hadharani.

Mimi binafsi nimepitia misukosuko mingi, mpaka kuja kuelewa kuwa niliongoza kidato cha nne ndio nafsi ilitulia na hii imenichukua takribani miaka miwili [ 2 ] tangu [ 2018 mpaka 2020 ] nilipoamua kufuatilia na kufahamu ukweli.

Nilienda mpaka Wizara ya Elimu na Sayansi pale Dodoma wakaniambia niende Mahakamani, yaani nilichoka!

Nikaenda tena Baraza la Mitihani yaani NECTA, wakaniambia wanafahamu wanachokifanya na hiyo sio bahati mbaya, Duuh niliishiwa pozi! Yaani hawa watu ni wa HOVYO sana tena sana! Hakuna kipimo cha kuelezea uchafu uliopo pale NECTA.

Nikaandika barua kwa ofisi ya Rais yaani IKULU, kuelezea haya masahibu yaliyonikuta. Lakini sijajibiwa mpaka leo!

Nikatoka hapo, nikaenda Wizara ya Mambo ya Ndani kuchukua CLEARANCE CERTIFICATE ili niweze kurudi kule nilipokuwa nafanya kazi, nchi jirani.

Na nikapata na wasaa wa kuzungumza na Askari waliokuwa zamu pale POLICE HQ, waliishia kuniambia "HIYO NDIO TANZANIA DOGO" [ 😁😁😁 ]. Aah, this is too funny wallah!

Maana mimi nilitakiwa kwenda kufanya kazi moja kwa moja London - Uingereza nikitokea Kigali - Rwanda.

Hapo ndipo nilipojua kuwa kuna kitu kinaitwa "vetting process" na majibu baada "interview" yalisoma "vetting disclosure". Yaani hamna kitu hapo!

Maana yake, matokeo yanayosoma kwenye vyeti vya sekondari yaani matokeo ya kidato cha nne na matokeo ya kidato cha sita ni tofauti kabisa na matokeo halisi. Kwa hiyo ilinipasa kurudi TANZANIA moja kwa moja mpaka Baraza la Mitihani yaani NECTA na kufuatilia matokeo yangu halisi, ndio nikafahamu kuwa niliongoza kidato cha nne lakini vyeti hawawezi kubatilisha labda ikitokea wametangaza wanafunzi bora waliofanya vizuri kitaifa kwa miaka iliyopita. Aisee!

Kwa hiyo sasa hivi nipo na nitakuepo mpaka sikukuu za mwisho wa mwaka. Kitakachofuata ni kwenda kujenga nchi za watu, maana kwa TANZANIA hali halisi ndio iko hivyo.
 
Wakuue ili iweje sasa! Kwa madhumuni yapi haswa?

Kwa kutunga vijihadithi hamjambo nyinyi!

Washindwe kukuua muda wote huo wasubiri mpaka upate A ya chemistry ndio wakuue?

Kweli?
 
UNACHO KISEMA NI PROPAGANDA NA KUTOA SHUTUMA KWA HAYATI BABA WA TAIFA NA KWA MKOA WA MARA.

Kama huju maana na chanzo cha JAMHURI YA CHUI
Kulikuwa na jamaa mmoja anaitwa Nyamaghanya
alikuwa jembe kweli na ni shujaa wa kweli wa mkoa wa mara nakumbuka mwaka 1982 alitangaza jamhuri ya watu wa chui nami nikiwa miongoni mwa wakazi wa nchi yake makao makuu yakatangazwa kuwa ni GIBASO na mishahara ya watumishi wake ni ng'ombe alikuwa na jeshi hodari sana likiitwa Esaiga ya gesambiso na vijana wa kati ambao walikuwa hodari wa kupiga mishale ndipo mchongameno akaamua kumwaga jeshi lake toka zenji kuja kumsaka shujaa wa wanamara wakashindwa kumkamata ikabidi watumie mbinu ya kupitia kwa mke wake mdogo ndipo akauwawa au akajiua mwenyewe kwenye mashimo ya gwisalaa hakukamatwa wala hakuzikwa mwili wake ulifichwa ili kukwepesha mauaji zaidi toka jeshi lake
Nyamhanga aliteremsha Bendera ya Tanzania na kupandisha ngozi ya chui na kutangaza rasmi kuwa hiyo si tena Tanzania , kuanzia siku hiyo majeshi yalikusanywa nchi nzima kama vile kulikuwa na vita ya Kagera.

Mapambano yaliendelea kwa siku zipatazo 7 hivi kabla ya Nyamhanga kupitia chini ya nyuma ya mtungi na kupotelea bondeni.

Kama ilivyokuwa kwa Hitira kuna habari za kutatanisha kuhusu huyu bwana baada ya vita kwisha. Kuna wengine wanasema yalitupwa mabomu mengi sana huko alikokimbilia na wengine wanasema alitorokea nje ya nchi.

Kuna Simulizi nyingi tu ambazo siwezi kuziandika hapa hasa kwa sababu zinahusiana na ushirikina wake, nami sina imani na ushirikina.

Sasa maswali fikirishi kama huo ulikuwa ni mpango wa NYERERE ni kwanini alete wanaheshi kuja kumvamia na kumpoteza kabisa?

Ndugu acha kutengeneza propaganda za chuki
 
mbunge Agnes Marwa karudia form 4 mara 4, hawa watu wa namna hii huwa wana kismart sana na mambo mablimbali wanakuja kufanikiwa katika mambo mengi na wakipata nafasi hawaichezei
 
Na hii ndio ilitakiwa kufanyika tangu zamani ili kuondoa udanganyifu uliopo kwenye sekta ya Elimu.
Ndugu, nilituma hiyo taarifa kuonesha kuwa wizi au udanganyifu wa matokeo ubafanywa na shule zote za kishua na za Kayumba.

Kinachoshangaza ni maelezo yako, kuwa mtu anatangazwa kuwa ameongoza halafu mtu huyo matokeo yake kwenye TSM9 kama ulivyokomaa nayo kuwa yanaandikwa tofauti na yalivyotangazwa. Sasa swali linakuja, kama wanaotangaza matokeo (NECTA) ndio hao wanaojaza matokeo kwenye hizo TSM9 wanafanyaje kindezi namna hiyo? Yaani watamke jina la uongo halafu maksi kwenye makaratasi wajaze za ukweli..nini kinawazuia wasidanganye mazima,.kwenye makaratasi na kwa taarifa zao kwa umma?
 
Huyu jamaa ni mwongo na ni mpenda Sifa
NECTA siku zote huwaga wanatoa Grade tu sio maksi na kama mtu wakawanza ameongoza mathalani ana one point 7 hii haizuhi mwanafunzi mwingine kuwa na one point 7 ila hapa utpfauti unabakia kuwa wakwanza alikuwa na alama zipi kwa wastani wake ukilinganisha na huyu mwingine ambaye hata kumi Bora hajaingia lakini ki grade wanalingana na yule aliyekuwa wakwanza

Pia swala la matokeo yaliyo tajwa kutofautiana na na yale yaliyoko kwenye cheti au mfumo sio kweli hakuna udanganyifu wa hivyo leo hii mtu anatajwa kwenye matokeo ukiangalia net utakuta hivyo hivyo na hata kwenye cheti huwa hivyo hivyo

Kwa maelezo yake huyu jamaa Mandela, ni upotoshaji na pia anapandikiza chuki kwa watanzania kuhusu watu wa MARA

Hii nchi inamisingi yake ambayo imetukuka toka enzi na enzi na pia hilo Baraza la mitiani NECTA limepata heshima kubwa ndani na nje ya Tanzania kwa waledi na ufanisi ulio tukuka
 
Wakuue ili iweje sasa! Kwa madhumuni yapi haswa?

Kwa kutunga vijihadithi hamjambo nyinyi!

Washindwe kukuua muda wote huo wasubiri mpaka upate A ya chemistry ndio wakuue?

Kweli?
Mimi sijasema kuwa huwa wanawauwa! Mimi nimesema huwa wanawapunguza [ ⚰️ ] ! Hiyo ya kuwauwa umesema wewe!
 
Hao watu wa Mara unaowazungumzia unamaanisha people from Mara region au umeamua kutumia code tu?nieleweshe please
Usifanye kama hauelewi kitu kinachozungumziwa hapa!

Mimi nasema kuna JAMHURI YA WATU WA CHUI au kwa jina jingine wanaitwa SERENGETI au kwa jina jingine wanaitwa RAMADHANI yaani RAMA! Sasa hayo ya kumaanisha PEOPLE FROM MARA REGION unayasema wewe, sio mimi!

Na nilijaribu kuelezea kwa kifupi kuhusu JAMHURI YA WATU WA CHUI au SERENGETI au RAMADHANI.

Na nikasema ukitaka kuifahamu TANZANIA vizuri inabidi ufahamu vizuri Chama Tawala kinavyofanya kazi - kwa sababu hiki chama, mizizi yake imejikita tangu UHURU wa TANGANYIKA na hata baada ya MUUNGANO wa TANGANYIKA na ZANZIBAR hiki Chama Tawala kina historia yake.

Baada ya hapo unatakiwa kufahamu ni nani alikuwepo nyuma ya mafanikio ya hiki Chama Tawala. Tangu kinaitwa TANU mpaka kilivyo ungana na ASP ya ZANZIBAR na kuitwa CHAMA CHA MAPINDUZI yaani CCM. Ukifahamu haya yote ndio utakuwa umeifahamu TANZANIA kwa ujumla wake na nani yupo nyuma ya MAFANIKIO na MADHAIFU ya hili taifa linaloitwa TANZANIA.

Sasa inabidi tuelekeze mawazo yetu na mitazamo yetu kwa kile kinachojadiliwa hapa!

Jaribu kutuonesha orodha ya wanafunzi bora waliofanya vizuri kitaifa ya kidato cha sita mwaka 2006, ambapo ELIAS KIHOMBO aliongoza?

Jaribu tena, kutuonesha orodha ya wanafunzi bora waliofanya vizuri kitaifa ambapo huyo MARTIN CHEGERE ameongoza kwa darasa la saba, kidato cha nne na kidato cha sita! Huyu mwanafunzi ndio aliyehojiwa mpaka Channel-5.

Hao wote haikutokea bahati mbaya! Eti wamejitangaza kuwa waliongoza sekondari na mwingine aliongoza msingi na sekondari! La hasha! Sio bahati mbaya! Kila kitu huwa kimepangwa na hii ndio ilikuwa inafanyika kwa miaka ya nyuma.

Lakini ukweli ni kuwa, hawa wanafunzi wote hawajawahi kuongoza! Kama hizo orodha zipo tuoneshe! Hapo mjadala ndipo ulipoanzia na ukazaa mambo mengine, ambayo hayajapata majibu mpaka muda huu.

Kama hizo orodha zipo tuoneshe? Hilo ndilo swali la msingi, mengine ni mbwembwe tu na kujaribu kuhamisha mada!

Halafu ukimaliza hapo! Jaribu tena kutizama matokeo ya wanafunzi bora waliofanya vizuri kitaifa kidato cha nne mwaka 2007. Huku unafanya ulinganisho na yale matokeo ya wanafunzi waliomaliza kidato cha nne mwaka 2007 kwa shule ya UHURU SECONDARY SCHOOL.

Hapo ndio utaelewa tunachozungumzia ni nini kwenye hii mada, halafu uwe na tabia ya kupitia kile walichojadili wenzio ili kupata mtazamo mzima wa kile kilichokuwa kinajadiliwa.
 
Mimi sijamsema Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.

Huyu ni baba wa Taifa na ana nafasi yake katika taifa hili, kwa hiyo sio vyema kumuweka hadharani!

Kuna namna yake ya kujadili viongozi hasa viongozi wa Taifa, ili kutunza haiba na heshima aliyoliletea Taifa la TANZANIA.

Ukiendekeza sana mambo haya, utashangaa yaliyomtoa khanga manyoya.
 
Mimi na wewe hatufahamu kwa nini wanafanya hivyo. Halafu kwa nini tuandikie mate na wino upo!

Tuchukue hizi sampuli za orodha ya wanafunzi bora waliofanya vizuri kitaifa kwa miaka kadhaa iliyopita, ndio utaelewa ni nini ninachosema au kujadili kwa uwazi bila hata ya kuogopa.

Hili swali zuri sana! Sasa twende na orodha ya wanafunzi bora waliofanya vizuri kitaifa kwa miaka yote ya nyuma, kuanzia 2015 kushuka chini halafu uangalie na matokeo ya hao wanafunzi kwenye website ya NECTA.

Angalia orodha ya wanafunzi bora kwa vidato vyote yaani kidato cha nne na kidato cha sita ya mwaka 2015. Halafu uangalie na matokeo ya hao wanafunzi kwenye website ya NECTA. Nasema hivyo, kwa sababu matokeo yanayosoma kwenye website ya NECTA ndio matokeo yanayosoma kwenye vyeti vya wanafunzi.

Angalia tena, orodha ya wanafunzi bora kwa vidato vyote yaani kidato cha nne na kidato cha sita ya mwaka 2012. Halafu uangalie na matokeo ya hao wanafunzi yanayosoma kwenye website ya NECTA.

Angalia tena, orodha ya wanafunzi bora kwa vidato vyote yaani kidato cha nne na kidato cha sita ya mwaka 2010. Halafu uangalie na matokeo ya hao wanafunzi yanayosoma kwenye website ya NECTA.

Angalia tena, orodha ya wanafunzi bora kwa vidato vyote yaani kidato cha nne na kidato cha sita ya mwaka 2008. Halafu uangalie na matokeo ya hao wanafunzi yanayosoma kwenye website ya NECTA.

Angalia tena, orodha ya wanafunzi bora kwa vidato vyote yaani kidato cha nne na kidato cha sita ya mwaka 2007. Halafu uangalie na matokeo ya hao wanafunzi yanayosoma kwenye website ya NECTA.

Angalia tena, orodha ya wanafunzi bora kwa vidato vyote yaani kidato cha nne na kidato cha sita ya mwaka 2006. Halafu uangalie na matokeo ya hao wanafunzi yanayosoma kwenye website ya NECTA.

Hapa nadhani tutaelewana sasa. Makosa huwa ni kwa Baraza la Mitihani yaani NECTA na kituo cha mtihani yaani shule, sio mwanafunzi na hii inatokana na kupika matokeo ya wahitimu wa shule za msingi na shule za sekondari.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…