Mfahamu Wilfred Mwabulambo, aliyecharazwa bakora na Mwl. Julius K Nyerere

Mfahamu Wilfred Mwabulambo, aliyecharazwa bakora na Mwl. Julius K Nyerere

Kwa wasiomfahamu Mwambulambo, ni huyo jamaa mwenye nusu kipara aliyekuwa akijipima ubavu na Mohammed Ali wakati akiwa katibu mkuu wa wizara ya vijana na utamaduni mwaka 1977 au 1978 hivi. Alimwambia Ali usiniletee ujinga hapa; mimi siyo Joe Frazier wala George Foreman, nitakuzaba hapa hapa airport kavukavu.

View attachment 1474029
Anaonekana ni version kama ya mjukuu wangu John Malecela hivi, ila yeye mfupi kidogo. Ni kati ya majina ambayo yalikuwa yanasumbua sana kwenye mitihani wakati tukiwa shule ya msingi. Ilikuwa katika kila mtihani swali lipo linalohusiana na jina la Mwabulambo. Kwa hiyo kila wakati mwanafunzi ulitakiwa uje huyu mtu ana cheo gani Serikalini!
 
Ilikuwaje hiyo? Hebu tupe stori.
Ninachojua ni kwamba JKT walikuwa wanajiunga baada ya kumaliza kidato cha sita.
Pia jeshini kitu kinachoitwa mgomo hakipo kwani kule ni amri na utii.
Pia Mambo ya jeshi humalizwa kijeda


MGOGORO KATI YA MWL NYERERE NA WANAFUNZI WA CHUO KIKUU CHA DAR ES SALAAM ULIOLETA AZIMIO LA ARUSHA.

Chanzo: 430/

MWALIMU aliwahi kuelezea aina ya Vijana aliotaka kuwaona ,alisema alitaka "Vijana jeuri na wenye kujiamini sio Vijana akina " ndiyo bwana"...... Vijana wenye ujasiri wa kuhoji mfumo wa jamii usioshahabiana na matakwa na matarajio ya jamii : Vijana waasi wa mifumo kandamizi.
Alisema " Ni kazi bure na kwa kweli ni ubatili mtupu ,kuwa na Taifa lenye "Silaha" nyenzo za maendeleo za kisasa lakini Vijana wake ni waoga.( Joseph Mihangwa).
Mawaidha haya yalijenga jeuri ya kujiamini kwa Vijana wa kitanzania miaka hiyo ya 1960 hadi kung'atuka kwa Mwalimu Nyerere mwaka 1985, Ni jeuri hiyo aliyowajengea ,ambayo Siku moja ilimtoa jasho Mwalimu mwenyewe pale wanafunzi wa Vyuo Vikuu walipogomea mpango wake wa Jeshi la kujenga Taifa(JKT) mwaka 1966 na kulazimika kuwatimua Chuo hapo Oktoba ,1966.
Mapema Februari 1966, Serikali ilichapisha muswada wa Sheria kwa madhumuni ya kuanzisha program na jeshi la kujenga Taifa (JKT) kwa lazima, kwa Vijana wote waliomaliza elimu ya kidato cha sita na Vyuo vya elimu ya juu ,kikiwemo Chuo Kikuu pekee cha Dar es salaam wakati huo.
Mpango huo uliendeshwa na kusimamiwa na wanafunzi wa kijeshi kutoka Israel ,uliwataka Vijana kutumikia jeshi la kujenga Taifa kwa miaka miwili, ambapo miezi sita ya kwanza ilikuwa kwa mafunzo ya kijeshi kambini na miezi 18 mingine ya kutumikia jeshi nje ya kambi kama watumishi wa umma. Walitakiwa pia kukatwa asilimia 60 ya mishahara yao kama mchango katika kulitumikia Taifa.
Chuo Kikuu cha Dar es salaam kilichoanzishwa mwaka 1961 baada tu ya Uhuru ,kilitoa wasomi wake wa kwanza mwaka 1964 ambao walionekana tishio kwa nafasi za vigogo madarakani kwa sababu ya elimu yao. Ni vigogo hao walioasisi wazo la jeshi la kujenga Taifa JKT ,kwa Vijana ,lakini kwa nia njema ya kuimarisha uzalendo.
Kabla ya program hii ,JKT iliyoanzishwa mwaka 1964 ,ilikuwa kwa Vijana wa kujitolea. Hadi oktoba 1966 ,ni Vijana 25 tu wa kujitolea waliokuwa wamejiunga. Na pale mpango huo ulipochukua mkondo wa kuwaingiza wasomi kwa lazima, Muswada wake haukupokelewa vyema na wasomi nchini na baadhi ya wabunge.
Wabunge wasomi kama kina Nicholaus Kuhanga na wengine , wakati wakijadili muswada huo, walisema, ;"Kuwakata Vijana asilimia 60 ya mishahara yao kuwa ni ujamaa ni uongo, Wabunge na viongozi wa Serikali wanasahau kwamba , ni wao haohao wanaomiliki majumba yenye thamani kubwa na magari ya kifahari kinyume na itikadi ya ujamaa, wanapaswa kuonyesha kwanza kwamba wao ni wajamaa kabla ya kuwataka Vijana hawa masikini kuwa wajamaa "(Hansard,Septemba 22----Oktoba 11,1966,UK,249).
Muswada huu ulizua ukinzani mpana katika jamii hadi maofisini ,ambapo kuliripotiwa kisa kimoja na wakati wa mjadala bungeni. Juu ya mabishano makali ya maofisa wawili ; mmoja Msomi na mwingine asiye msomi , wakiapizana; yule asiyesoma akisema, " Kusoma si hoja hata muwe na digrii ,mtatufanya nini wakati tuna kila kitu, majumba ,magari ,vipusa (wasichana warembo) na madaraka tunayo?(Hansard, kama hiyo hapo juu) .
Mara tu muswada huo ulipopita ,wanafunzi waliwasilisha Serikalini madai yao ya kutaka muda wa JKT upunguzwe Kutoka miaka miwili hadi miezi sita na makato ya asilimia 60 ya mishahara yaondolewe .
Kukataliwa kwa madai hayo kulitafsiriwa kama nia mbaya ya Serikali dhidi yao, Ziara za mara kwa mara za viongozi wa Serikali Chuoni hapo kuzungumza na wanafunzi hazikubadili hisia za wanafunzi hao
Mambo yalitibuka zaidi pale aliyekuwa Naibu Waziri wa Ulinzi na JKT wa wakati ule, Richard Wambura ,alipowahutubia wanafunzi ,Oktoba 18,1966, kwa hotuba ambayo ilitafsiriwa kuwa mpango wa JKT ulikuwa wa hila kwa lengo la kuwaonea na kuwanyanyasa Vijana kwa kuwa tu wao ni wasomi ,Baada ya hotuba hiyo, wanafunzi waliitisha mkutano wa dharura ambapo ziliundwa Kamati mbili ,moja ya kwenda kuonana na Rais Ikulu kuelezea malalamiko yao, na ya pili, kwenda Polisi kuomba kibali cha kufanya maandamano.
Kamati iliyokwenda kuonana na Rais ilitoa taarifa kuwa Mwalimu Nyerere hakuwa na uhakika juu ya kile kilichokuwa kikiendelea ; akayatupilia mbali malalamiko yao. Na ile iliyokwenda Polisi, ilitaarifu juu ya kukataliwa kibali, Hivyo ,Oktoba 21, 1966 ,uongozi wa wanafunzi ukaitisha kikao kingine cha dharura ,safari hii wakaazimia kuandamana bila kibali cha Polisi, kwenda Ikulu kukabiliana uso kwa uso na Mwalimu Nyerere.
Waliandaa mabango yenye ujumbe mbalimbali, Kwa kutaja baadhi tu, yalisomeka :"TUMECHOKA KUTUMIKIA WABENZI(mafisadi) "
"AFADHALI WAKATI WA UKOLONI", " KUMBUKA YA INDONESIA", "ATOKOMEZWE KAWAWA NA MPANGO WAKE WA JKT" na mengine mengi.
Hili la "KUMBUKA YA INDONESIA", liliikumbusha Serikali jinsi Serikali ya Rais Suharto wa nchi hiyo ilivyoangushwa kwa maandamano ya wanafunzi mwaka 1965.
Lakini hili la " AFADHALI WAKATI WA UKOLONI", inadhaniwa hadi leo kuwa bango hili halikuwa na ridhaa ya wanafunzi hao, bali lilipandikizwa na watu wa Usalama wa Taifa ili kuchokoza hasira ya Mwalimu Nyerere aweze "kuwaadabisha " waandamanaji hao. Na hili ndilo kweli lililomchoma zaidi Nyerere.
Huko Ikulu Oktoba 22, bila ya wanafunzi hao kujua ,Mwalimu aliitisha kikao cha dharura cha Baraza la Mawaziri kuamua jinsi ya kukabiliana na waandamanaji watarajiwa, Iliazimiwa kuwa ,maandamano hayo yaongozwe na Polisi kuingia Ikulu siku hiyo, Oktoba 22, 1966.
Maandamano hayo hayakuwahusisha Vijana wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam pekee ,bali walijiunga wengine wengi kutoka Chuo cha Uganga cha Muhimbili ; Chuo Cha Ualimu Chang'ombe, Chuo cha Biashara (CBE) ,Shule ya Sekondari ,Aghakhan na Vijana " wapita njia" wengine.
Ikulu waandamanaji hao walilakiwa na Mwalimu mwenyewe ,Makamu wa pili wa Rais Rashidi Mfaume Kawawa na Mawaziri.
Mwalimu akamkaribisha msemaji mkuu wa waandamanaji kuelezea malalamiko yao ; naye bila kusita kwa Lugha ya kiingereza fasaha ,akatamka masharti yao kwa sauti ya ukali ,akisema;
"......Serikali inajaribu kutupa mzigo wa kugharamia mpango huu(JKT) mabegani mwa wanafunzi masikini, .......Ama tulipwe haki zetu zote za mishahara ; ama wale wote wanaopata mishahara ya juu nao watumbukizwe katika utaratibu huu uonekane kweli ni wa kujitolea na si mpango wa kunyonya wasomi Vijana pekee."
Akaendelea :" kwa hiyo Mheshimiwa ,kama utaratibu huu pamoja na mawazo ya viongozi wa juu hayakubadilika ,hatukubali mpango wa JKT kwa moyo.
Miili yetu inaweza kwenda ,Lakini mioyo yetu itabaki nje ya mpango huu" akatamka kwa kujiamini na kwa kushangiliwa na wenzake. Kisha akamaliza kwa kishindo ,akasema "Na vita hii baina ya wanasiasa na watu wenye elimu itaendelea daima, Aksante".
Akawa amemchokoza Mwalimu.
Mwalimu alianza kujibu risala hiyo, kwanza kwa upole na kwa sauti tulivu ,akasema
"Nilitarajia haya mapema ,nimeyaelewa malalamiko yenu , sisi Serikali tumeupata ujumbe wenu; natafuta njia ya kuelezea kidogo ; maneno yenu mliyotuambia viongozi wenu tumeyasikia," akasema akiangaza macho huku na kule kukazia hoja"
Sauti yake ikaanza kupanda kidogo; "Sasa mimi nimeyakubali masharti yenu, naweza kuwahakikishia kwamba sitamlazimisha mtu yoyote.
Mnayosema ni sawa ; kwamba hata miili yenu ikienda JKT ,mioyo yenu haitakuwa huko ............Sitampeleka hata mmoja wenu JKT ambaye moyo wake haupendi (makofi) maana huko si gerezani.
Lakini hata hivyo mpango wa JKT utaendelea kuwa ni wa lazima kwa kila mwanafunzi ambaye hatimaye atafanya kazi serikalini, kwa hiyo ni juu yenu kuamua,.......", akatahadharisha , kisha akaendelea.
" Mnayosema juu ya mishahara yetu ni ya kweli ,ni mikubwa mno (shangwe na makofi), mimi na ninyi tumo katika kundi la wanyonyaji . Je, hayo ndiyo mambo nchi iliyoyapigania ? Je, juhudi yote tuliyofanya ni kwa sababu ya kuneemesha kikundi cha wanyonyaji huku juu? Akahoji kwa ukali, kisha akawaeleza juu ya mapinduzi yanayotakiwa ,akasema:
"Siku nikayoweza kumlipa mfanyakazi wa Tanzania Mshahara wa shilingi mia tano kwa mwezi ,tutakuwa tumefanya mapinduzi makubwa sana ; hapo tutaweza kusimama juu ya mlima Kilimanjaro na kutangaza Mapinduzi ya Tanzania kwa faraja na fahari kubwa."
Kuthibitisha kwamba alikuwa hatanii juu ya mishahara mikubwa ,Mwalimu alisema ," Mshahara wangu mnajua ni kiasi gani! Shilingi elfu tano kwa mwezi ; ni kiasi kikubwa mno!!Mshahara mkubwa mno sawa na pato la Mkulima wa kawaida kwa miaka 25;
Naupunguza kwa asilimia ishirini kuanzia sasa hivi, .........Nchi hii ya hovyo ; mishahara minene mno" akasema kwa kucharuka na kufoka, katikati ya ukimya uliokosa shangwe wala makofi.
Akarejea kwenye hoja ya siku hiyo, akasema " Mimi nimeyakubali maneno yenu mnayosema .....Na ninyi ,mimi nawaomba mwende Nyumbani kwenu.... Rashidi (yaani Kawawa) ni jukumu lako kuhakikisha kwamba wanakwenda kwao."
Alikuwa amewafukuza wanafunzi wote 415 : mara wakazingirwa na Polisi ,wakaanza kushughulikiwa na FFU kwa ulinzi na kudhibitiwa.
Oktoba 28,1966 Chama cha wanafunzi (USUD) ,kupitia barua iliyotiwa sahihi na Kaimu Rais wa chama hicho ,kilimwomba Mwalimu awasamehe wanafunzi waliofukuzwa kwa sababu tu ya "Kuchambua jamii waliyomo"
Barua nyingine ya Oktoba 30,1966 iliweka bayana kuwa malalamiko ya wanafunzi hayakutendewa haki kwa kupotoshwa kwamba walitaka kupindua Serikali wakati haikuwa hivyo, bali kuitahadharisha Serikali juu ya matabaka yaliyokuwa yakijengeka nchini.
Mwalimu hakujibu barua zote ,Wala hoja za Washauri wake wa karibu akiwamo msaidizi wake ,Mama Joan Wickens.
Alikaa kimya akiwaza na kuwazua hoja za wanafunzi aliowatimua na hatima ya nchi. Kwa kipindi chote kati ya Novemba 1966.
Na januari 1967 ,Mwalimu alikuwa akiandika itikadi na Sera mpya ya kisiasa na kiuchumi kudhibiti matabaka yaliyokuwa yameanza kujitokeza Nchini.
Aliandika Sera ya ujamaa na kujitegemea iliyotafsiriwa vyema katika Hati(blue print) iliyopewa jina la " Azimio la Arusha" na kutangazwa Februari 5,1967 kuwa dira ya maendeleo ya nchi.
Aliyekuwa mlezi wa wanafunzi wa Chuo ,Profesa T.O. Ranger ,katika barua yake aliyomwandikia Msaidizi wa Rais Mama Joan Wickens ,Kumb: C3/SA.13 ya tarehe 2/3/1967.
Kumuomba amshawishi Mwalimu awarejeshe wanafunzi hao 23, alisema haikuwa halali kwa wanafunzi hao kutumika kama chambo kwa Serikali iliyokuwa imepoteza dira na yenye kujaa mafisadi wasiojali maslahi ya umma.
Wanafunzi hao walirejeshwa mwaka 1969 pamoja na adhabu ya kuchapwa viboko kwa mkono wa Mwalimu mwenyewe.
Azimio la Arusha na Siasa ya Ujamaa na Kujitegemea vilipokelewa kwa nderemo na vifijo na jamii ya wasomi kama mkombozi wa wanyonge ,kuanzia hap.
Na nchi kuamua kufuata siasa za mrengo wa kisoshalisti ,wanafunzi Vijana wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam walifunga fungate ya uswahiba na Serikali Fungate iliyokuja kukatwa na Sera za soko huria kwa kuzika Azimio la Arusha na kuanza Kwa Azimio la Zanzibar la mwaka 1992.
Hivyo kuibuka kwa matabaka kipindi kile kulipata dozi kupitia kuanzishwa kwa Azimio la Arusha , na mpango wa JKT tunaona bado unaendelea mpaka leo kama njia nzuri na mahsusi ya kuwajenga Vijana kimaadili zaidi na kizalendo wakati wa kulitumikia taifa letu.
Pichani chini Siku Mwalimu Nyerere alipokuwa akiongea na wanafunzi wa Chuo Kikuu.
Na. Fredy Nyaluchi
 
Tunaona kuna mabadiliko kakubwa, wanafunzi wa vyuo vikuu ambao tunaamini ndipo kisima cha kupika udadisi wa mambo sasa hawafanyi kazi hiyo tena, ni wazee wa Ndiyo Mzee - As a results Taifa linakosa vijana wenye mtazamo chanya wa kulisogeza mbele.
 
Nyerere Aliwatunuku Vijana Wake Wenye Jeuri Ya Kizalendo...

- Wilfred Mwabulambo alicharazwa bakora sita za ‘kumtuliza Malkia’

Mtu mzima unapoona jirani yako amekuja juu kulaumu kuwa mtoto wako wa kiume amekutwa akimshikashika kifuani binti wa nyumba ya jirani, basi, mzazi hapo unaweza kuchukua hatua hapo hapo. Mwingine anaweza hata kumzaba vibao mwanawe.

Lakini jioni akikaa chumbani na mkewe, kwa furaha atamwambia mkewe;

“ Naona mwanetu sasa amekua...!”

Kitendo kile cha Mwabulambo kumpinga Mzee wake Ikulu kingeweza kuwa na athari ya mahusiano ya kidiplomasia kati yetu na Uingereza.

Bakora zile sita yumkini zilikuwa za ‘ Funika Kombe..’

Nyerere naye alionekana kukerwa na Mwingereza. Valangati lile la akina Sitta na Mwabulambo kwenye Ubalozi wa Uingereza kulikuwa na lazima ya kidiplomasia kulilaani, lakini, kwenye miwani mingine ya Nyerere, aliwaona watoto wake kuwa

“ Sasa wamebalehe kisiasa”

Kwamba wana jeuri ya kizalendo kuipigania nchi yao.

Si ajabu Mwabulambo baada ya kuhitimu tu, ajira yake ya kwanza ikawa Ikulu.

Je, hali ikoje kwa viongozi wetu vijana wa sasa?

Mwingine amepata kunijibu, kuwa kuna baadhi ya viongozi vijana wa sasa wenye kuona fahari ya kupakatwa na wakubwa na hata kuinanga Tanzania waliyozaliwa na kukulia wakiwa kwenye sebule za waliotutawala
 
Bongo Hapo Zamani:

Nyerere Aliamuru Mwanafunzi Mwenye Hasira Kali Atandikwe Bakora Sita...!

Ndugu zangu,

Mwandishi Mtafiti, Saida Yahya - Othman anasimulia tukio hili la mwaka 1965. Ni kwenye juzuu ya kwanza kati ya tatu ( The Making Of A Philosopher Ruler, Ukurasa 241-242.)

Wanafunzi wale wa Mlimani walijipanga na kufanya maandamano hadi Ubalozi wa Uingereza bila kuomba kibali.

Pale Ubalozini wakafanya purukushani kubwa ikiwamo kuchoma moto bendera ya Malkia.

Jambo hilo lilimshtua Julius na akaamuru waswekwe ndani kwa muda na baadae akawaita Ikulu ya Magogoni kuzungumza nao.

Akawaambia waende wenyewe kwa Mheshimiwa Balozi kumwomba radhi.

Kwamba kimsingi ni Waziri wa Mambo ya Nje ndiye alipaswa kufanya hivyo, lakini, kwa vile ni yeye, Julius,ndiye Rais wa Jamhuri na pia Waziri wa Mambo ya Nje, kwenye macho ya umma ingeonekana ni Rais ndiye aliyekwenda kumpigia goti Balozi.

Wanafunzi wale wakakubaliana na Julius Nyerere, kasoro mmoja, ( Mwandishi hamtaji ni nani).

Huyu alimpinga Julius hapo hapo. Nyerere naye akaamuru acharazwe bakora sita za matakoni.

Kwa huruma inaandikwa kuwa Nyerere alimwita tena Ikulu mwanafunzi yule kumwelezea kwanini aliamuru achapwe bakora!

Kisa hiki kilikuwa maarufu pale Mlimani na nimepata kusimuliwa na Msomi wa Mlimani wa wakati huo, anayependa kujitambulisha kiuandishi kama born again pagan- BAP.
 
Samuel Sitta ndiye aliyekuwa kiongozi wa kina Mwabulambo, yeye hakuchapwa kwasababu alikubali kwenda kumuomba msamaha balozi
Huu ulikuwa mgomo Mwingine Sita alicharazwa fimbo Tena na Mwalimu mwenyewe. Hii aliwambia wainamishe vichwa, wakiwa ukumbini, anaupinga anyoshe Kidole. Samuel Sita akanyosha kumbe amenyosha peke yake, akachukuliwa akala bakora. Siku anamaliza mtihani wa mwisho Chuo kikuu aliiywa Ikulu na Mwalimu akalamba ajira
 
1965 Mwanasheria Mkuu wa Serikali alikuwa Joseph Sinde Warioba, leo nasoma tena hapa kuwa 1965 Warioba alikuwa Kiongozi wa Maandamano haramu
 
Sasa hivi wanaandamana kwa ajili ya boom tu si mengineyo
Inaonekana wanafunzi wa vyuo wa zaman walikua na uelewa sana na mambo ya kimataifa....wa sa hivi hata ramani yenyewe ya dunia sidhani kama wanaielewa vizuri!
 
Ilitakiwa iwepo movie ya Mwalimu Nyerere. Imagine kuna movie ya Idi Amin lakini siyo Mwalimu Nyerere.
Hapa ndo Wizara inayosimamia utamaduni na michezo inapotakiwa kufanya jambo. Hii kitu inabidi iratibiwe na serikali
 
ikithibitika kala rushwa atapata viboko12 siku anaingia jela na 12 siku anatoka akamuonyeshe mkewe
🙏🙏


Hayo ndiyo miongoni mwa mapungufu ya Mwalimu Nyerere, ----Je ina maana wala rushwa ni wanaume tu??🤣
 
Zidumu fikra za mwenyekiti
Mwalimu nae alikua anapenda kisifiwa sifiwa tu, ukimkosoa ilikua ni nongwa, hana tofauti yoyote na walimu wa kemia.
Mkeo watoto, wageni, lazima wakusifie sifie nyumbani kwako, mara utasikia ''Baba /Mama asante kwa chakula'' ''uzomile kusuma tata''

asipo shukuru hutamfurahia, wala kumheshimu si ajabu usimruhusu aje kwako siku nyingine! Eti kwa Nyerere imekuwa nongwa!
 
MWANAFUNZI WA CHUO KIKUU WILFRED MWABULAMBO ALICHARAZWA VIBOKO KWA KUMGOMEA RAIS NYERERE!

Wanafunzi wanapogoma au kufanya maandamano, dola hujibu mapigo kwa njia anuai. Ipo mifano ya wanafunzi waliosimamisha au kufukuzwa chuo, kuswekwa korokoroni na kuchukuliwa hatua mbalimbali za kinidhamu kwa kujihusisha kwao na maandamano yasiyo na kibali cha dola.

Ni vigumu mtu kuamini kwamba kati ya hatua zinazoweza kuchukuliwa kuwadhibiti wanafunzi wa chuo kikuu wanaoonekana kuwa watukutu ni kuwaadabisha kwa bakora! Amini usiamini, hapa nchini imewahi kufika pahala serikali, tena chini ya Mwalimu Nyerere kuwatandika viboko wanafunzi waliokosa utiifu kwa viongozi wa serikali.

Mfano wa hili ni kwenye mgomo wa wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam dhidi ya tamko la uhuru wa walowezi wa Zimbabwe (Unilateral Declaration of Independence-UDI) la mwaka 1965 chini ya Ian Smith.

Ikumbukwe kuwa baada ya Ian Smith na genge lake la walowezi kujitangazia uhuru na kutwaa mamlaka ya kuiongoza Rhodesia ya Kusini (Sasa Zimbabwe), Umoja wa Afrika uliitisha kikao cha dharura , ambapo viongozi wa nchi za Kiafrika waliafikiana kwa kauli moja kuipa shinikizo Uingereza (Waliokuwa wakoloni wa Rhodesia ya Kusini kabla ya kuwaachia walowezi) kubatilisha utawala wa Smith na kuukabidhi uhuru kwa wazalendo.

Azimio la Umoja wa Nchi Huru za Afrika liliweka bayana kwamba kama Uingereza haikutekeleza matakwa hayo ifikapo 15 Disemba 1965 basi nchi zote za Kiafrika zingefuta mahusiano ya kidiplomasia na nchi hiyo.

Uingereza ilipochelea kutekeleza azimio la OAU, Tanzania ilikuwa kati ya nchi za mwanzo kabisa za Kiafrika kufanya uamuzi mzito wa kuvunja mahusiano ya kidiplomasia na Uingereza. Kwenye hotuba yake Bungeni kuhusu suala hili, Mwalimu Nyerere aliweka wazi msimamo wa Tanzania. “Sera za Tanzania na Afrika kuhusiana na suala la Rhodesia ya Kusini mara zote zimekuwa na zitaendelea kuwa na lengo moja tu. Lengo hilo lilikuwa na litaendelea kuwa kupatikana kwa uhuru wa wengi. Kuhusu hili, kila hatua tuliyochukua na kila hotuba tuliyotoa vimelenga kulifanikisha lengo hilo. Hatuna zaidi ya hilo” alisema Mwalimu.

Kwa upande wa wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, kama yalivyofanya makundi mbalimbali barani Afrika, wao waliamua kufanya maandamano makubwa kuipinga serikali ya kimabavu ya UDI chini ya Ian Smith ili kuonyesha mshikamano na wapigania uhuru wa Zimbabwe.

Joseph Sinde Warioba aliyekuwa kiongozi wa Chama cha Wanafunzi Tanzania (National Union of Tanzania Students ) na mmoja wa vinara wa mgomo huo wa mwaka 1965 anatujuza yaliyotokea; “Walowezi wa Zimbabwe walipojitangazia uhuru tuliamua kufanya maandamano kwenye mitaa ya jiji la Dar es Salaam bila kibali. Mwalimu aliagiza tukamatwe na wengi tuliwekwa mahabusu makao makuu ya polisi. Baadaye tulipelekwa Ikulu kuonana naye”.

“Kwenye mkutano wetu alitueleza kwa upole kwamba hatukukamatwa kwa sababu ya kuipinga serikali ya Walowezi wa Zimbabwe bali ni kwa sababu tumevunja sheria kwa kuandamana bila kibali na kwamba tumefanya uharibifu”
“Alisema hakuna hatua zaidi zitazochukuliwa dhidi yetu lakini akatutaka tuiombe msamaha serikali ya Uingereza kwa uharibifu wa mali tulioufanya (Wanafunzi waandamanaji walikwenda ubalozi wa Uingereza na kuharibu mali za ubalozi).

Alisema kuomba msamaha ni utaratibu uliopaswa kutekelezwa na Waziri wa Mambo ya Nje lakini kwa sababu kwa wakati huo yeye aliishikilia nafasi hiyo, angeomba msamaha, ingetafsiriwa kwamba ni Rais aliyeomba msamaha na si Waziri wa Mambo ya Nje. Hivyo, akatutaka tuombe msamaha kwa niaba yake”

“Baada ya hapo Mwalimu akauliza kama yupo mwenye pingamizi. Mwanafunzi mmoja akasema kwamba analo pingamizi na papohapo Mwalimu akamuamuru kamishna wa polisi amchukue na kumcharaza bakora sita. Ni katika hatua hiyo tuligundua kwamba alikuwa na hasira na sisi. Mazungumzo yote yale ya upole yalikuwa ni njia ya kuficha hasira zake dhidi ya tulichokifanya”

“Baadaye Mwalimu alimuita tena Ikulu yule kijana aliyecharazwa bakora na kumfafanulia kwamba alikuwa ametenda yale kutokana na msukumo wa hasira. Alisema alikuwa ametenda kwa misingi ya ualimu”

“Kama tulivyo wengi, Mwalimu aliweza kupandwa na hasira na kufanya makosa. Lakini moja ya sifa zake ilikuwa ni kwamba hakuona soni kuyakubali mapungufu yake”.

Kijana aliyecharazwa bakora alikuwa ni Wilfred N. J. Mwabulambo. Yeye na Jaji Joseph Warioba, miaka kadhaa baadaye walikuja kuwa viongozi wakubwa serikalini. Wilfred Mwabulambo ambaye sasa ni marehemu amewahi kushika nafasi mbalimbali za Uongozi, zikiwemo ukatibu mkuu kwenye Wizara mbalimbali na pia kuwa Katibu Mkuu Kiongozi. Jaji Joseph Sinde Warioba ambaye ameshawahi shika nafasi mbalimbali Kama vile Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Waziri Mkuu na Makamu wa Rais.

Pichani ni Rais Nyerere akiwa na Wilfred Mwabulambo, Picha hii inatajwa kupigwa mwanzoni mwa miaka ya 90 wakati Mwabulambo akiwa Kiongozi Serikalini.

1001526_699319653446404_771184154_n.jpg

Picha na Maelezo husika ni kwa Hisani ya Ndugu Ado Shaibu Ado wa Watanzania Mashuhuri.​


Nilipata kusikia hata Marehemu Samweli Six naye alipata kuchwapwa bakora na Mwalimu Nyerere walipogomea kitu fulani walipokuwa chuo kikuu.
 
Mkeo watoto, wageni, lazima wakusifie sifie nyumbani kwako, mara utasikia ''Baba /Mama asante kwa chakula'' ''uzomile kusuma tata''

asipo shukuru hutamfurahia, wala kumheshimu si ajabu usimruhusu aje kwako siku nyingine! Eti kwa Nyerere imekuwa nongwa!
Hakuna mtu aliyekatazwa asisifiwe na wala hakuna asiependa kusifiwa pale anapofanya vizuri, ila unapo kubali kusifiwa pia ukubali kukosolewa pale unapokosea,
Mwenyekiti alikua hakubali kukosolewa pale anapokua hayupo sahihi mpaka watu wakampachika jina la "haambiliki" fikra zake zilikua hazikosolewi mpaka ikaanzishwa slogan ya "zidumu fikra za mwenyekiti" na wengi waliomkosoa walikua wanaishia matatizoni kama sio uhamishoni.
Mwenyekiti aliweka mazingira ya kuogopwa zaidi, watu hawakuthubutu hata kukaa pamoja na kuzungumzia mustakbali wa mambo kama yalikua yanaenda ndivyo sivyo, kila mtu alikua na wasiwasi na mwenzie kwa jinsi mzee alivyowatengezea watu uoga kutokana na vitisho vyake.
 
Hakuna mtu aliyekatazwa asisifiwe na wala hakuna asiependa kusifiwa pale anapofanya vizuri, ila unapo kubali kusifiwa pia ukubali kukosolewa pale unapokosea,
Mwenyekiti alikua hakubali kukosolewa pale anapokua hayupo sahihi mpaka watu wakampachika jina la "haambiliki" fikra zake zilikua hazikosolewi mpaka ikaanzishwa slogan ya "zidumu fikra za mwenyekiti" na wengi waliomkosoa walikua wanaishia matatizoni kama sio uhamishoni.
Mwenyekiti aliweka mazingira ya kuogopwa zaidi, watu hawakuthubutu hata kukaa pamoja na kuzungumzia mustakbali wa mambo kama yalikua yanaenda ndivyo sivyo, kila mtu alikua na wasiwasi na mwenzie kwa jinsi mzee alivyowatengezea watu uoga kutokana na vitisho vyake.
Ndiyo Rais kamili anatakiwa kuwa ivo!! siyo unamtomasa tomasa km mkeo! Watu wengine tumeumbwa ivo kutisha! sasa nijikatae? km nikisimama tu unajinyea we ni jinga, joga, nikufanyeje sasa? huna hoja za akili ili kunipiku halafu unalaumu akili zangu? are you mad? udhaifu mkubwa sana huo!

Hata Wazungu Ulaya, USA na Dunia, walimuogopa. kwa hoja, kwa muonekano, kwa mipangilio, misimamo nk, walimjua/mtamani hata watoto wadogo huko! hadi wakaamini siyo Mwafrica ni mzungu mwenzao! ila rangi tu.

Hakubali makosa kweli? hakuna Rais mwafrica Duniani, aliye wahi kuachia madaraka kiu-rahisi km Nyerere. wengine wakaiga. watanzania walimuhitaji lkn alikataa! tena alikiri ''kuwa yeye siyo Malaika, walifanya makosa mengi kiuongozi'' mojawapo ya makosa ni kubinafsisha mashamba ya Mkonge bila management ya kutosha!

akasema ''chukueni mazuri yetu mabaya yetu muyaache''! sasa weye unaangalia mabaya tu, Hata kwenye familia yako huwezi kukubali kila jambo unaloshauriwa na mkeo! mwanao, mgeni, utapotea! na wale utakao acha mawazo yao lazima wakupachike majina km. Kitama kwigwa, dingi jeuri, mkoloni,nk

Siyo kila ushauri una maana, mfano ukimfumania mkeo, ukitaka afe kwa stress au akuue usichukue hatua yeyote! ivoivo kwa Nyerere! ukiwa na madhambi yako yatakukimbiza kutoka kwenye upeo wa macho yake! au ukajilopokea tu ''siyo mimi mzee ni majungu tu ya watu'' ndiyo Rais anatakiwa awe.

kwa jinsi alivo kuwa mpole, mpenda watu, hkn mpaka leo raia jasho wa chini aliye thubutu kupanda ndege ya jeshi au ya Rais kwenda anakotaka. lkn yeye alitoa Bure tena kwa msisitizo! raia/ wanafunzi, Kamunyonge, nyasho, kipawa, wanajua.

Rais Imara sana Africa, alizungukwa na maadui wengi wenye nguvu na Misomi, Kama wa Rhodesia, Mreno-Msumbiji, Makaburu, NATO, lazima ajilinde binafsi then nchi, asiwe goi goi! na alisimama kidete kuwatetea weusi wanyonge Duniani, bila kupepesa macho mbele ya weupe! leo nani mwenye Guts hizo Africa?

Tatizo mlivo wazembe mlitaka awe mzembe mzembe! wa kupigwa na povu la sabuni kwishne? na visununu vyenu ivo visivyoisha, kubali aliweza na wengi wanamkubali.

Rais imara,... hata Mungu mwenye enzi, hawezi kumfurahisha kila mtu. wenye kulalama wapo tuu!!!

Walio jaribu kuwa km Nyerere walipotea bure na faster km upepo, mfano Nkwame nkrumah, juzijuizi tu Gadaffi. lkn Nyerere wetu alipangua waliotaka afe, wewe ulitaka afe!,
Hao walioona wenzao wanapotezwa na wakanyamaza ukiwemo wewe! ni madhaifu wakubwa, waoga,wajinga ndiyo wakulaumiwa, kwa nini wasiwatetetee wenzao! mbona yeye alipinga dhuruma ya Mikoloni bila uoga? na alijua watamunyongelea kwa mbali. aliona bora auliwe tu kuliko wengine kuumia akiwaona kwa macho! Mungu awape nini? mjifunzege kuwa na shukrani!
cc2a0ecebf22589590612e8e1043b9e1.jpg

Angalia Bure Yetu Madege caribou tulipanda kwa raha zote na popote TZ, Shule bure mpaka chuo na posho juu, Hosp bure, Mafunzo ya raha huko JKT bure Madisco, yakisindikizwa na jkt jazz band bure weeee! Government warrant tulipata popote, NH bure, hatukutegemea baba zetu kusoma na kujenga majumba tunayorithi leo! nyie wachawi mnataka nini sasa? inawezekana chuki zenu dhidi ya wanyonge ziliwafanya msifaidi, mlitaka nyie tu, nani Rais alifanya hayo Africa? wewe sema Mungu kakupiga kofi tu! na kwa msimamo huu atakupiga sana.
 
Hayo ndiyo miongoni mwa mapungufu ya Mwalimu Nyerere, ----Je ina maana wala rushwa ni wanaume tu??🤣
Komesha rushwa ni mapungufu? wanaume wenge kasoro! wanawake ni wapole, waaminifu na wachapakazi!
 
Back
Top Bottom