Mfanyabiashara kuongoza Shirika la Umma Rais Samia unaenda kusiko

Viongozi wote wana biashara ndani ya serikali
Ku moonlight hilo ruksa toka siku nyingi.
Kufuga kuku, ng'ombe na hata vishamba(siyo ranchi), mbona hio limeruhusiwa toka enzi za Sokoine.
Tunachosema, kwa sasa inawezekana kama alivosema ndugu yangu johnthebaptist, tutegemee Bakhressa aendeshe shirika la Reli, Manji apewe National Housing na angekuwepo Reginald Mengi angepewa TAMISEMI kabisa!
 
Kuna ubaya gani mfanyabiashara kuwa kiongozi serikalini?. Naona kama mawazo yako ni ya kijamaa mpaka yamepitiliza.

Mwalimu Nyerere alihubiri huo ujamaa wakati yeye anatunzwa na serikali kwa kila kitu. Kina Chediel Mgonja na Profesa Machunda walikufa kimaskini sana baada ya kuamua kuuiga ujamaa wa Nyerere.
 
1. Anaye kidhi yukoje? Anakuaje?
2. Kuna chuo cha kufundisha urais?
3. Umempa muda gani hadi uhitimishe kuwa hakidhi vigezo?

Samia ni rais kwa mujibu wa katiba iliyopo, sio kwa bahati! Hakuomba Ndugu Magufuli afe, ni mipango ya Mungu tu!
Nongwa zinatutesa sana watanzania, mawazo ya kimaskini pia ni tatizo. Maadam yeye hana basi na majirani zake wote wakose vile vile.

Hiyo ni mindset ya kishirikina.
 
Huwa nawashangaa sana mnapokuwa mnaongelea issue za vetting, hicho kitu hakipo hata hao wanaojiita tiaies hamna kitu.
 
Huwa nawas

Huwa nawashangaa sana mnapokuwa mnaongelea issue za vetting, hicho kitu hakipo hata hao wanaojiita tiaies hamna kitu.
Kiutawala vetting ipo, na haiwezi kukwepwa.
La sivyo kuna siku tutajikuta tuna Rais toka Madagascar!
 
Kiutawala vetting ipo, na haiwezi kukwepwa.
La sivyo kuna siku tutajikuta tuna Rais toka Madagascar!
Hakuna vetting mkubwa akishakupendekeza maana yake ww ushapita Kwan huoni haya yanayotendeka nchin unataka uwe na elimu ya PHD ndio utambue?
 
Hakuna vetting mkubwa akishakupendekeza maana yake ww ushapita Kwan huoni haya yanayotendeka nchin unataka uwe na elimu ya PHD ndio utambue?
Unielewe mkuu, sisemi kuwa ipo, haifuatwi.
Kada ya wateuliwa inajieleza the level that we have sunk!
 
Usipindishe mada, nimeleta mada mbele ya jamvi kuonyesha kuwa si vema mfanyabiashara mkubwa kupewa vyombo vya serikali, ni conflict of interests popote atakapokuwa serikalini.

Serikali imeruhusu mtu binafsi kufungua biashara yoyote iliyo halali, na ujamaa ulipote kitambo.

Hivi tukiamua leo Manji, mfanyabiashara mkubwa ,ateuliwe kuwa mkuu wa TRA, itakuwaje?
 
Mpaka leo hujaona madhara ya kumpa nafasi kubwa ya uongozi mtu ambaye hajui biashara inafanyika vipi?. Tupunguze hizi fikra za kijamaa vichwani mwetu.

Unajua kwamba JPM alikuwa ni kiongozi mzuri lakini asiye na uzoefu wowote wa masuala ya kibiashara?. Hasara yake unaifahamu vyema lakini?.

Tuna utajiri mkubwa wa fukwe yenye urefu wa kilomita 1424 lakini hatujawahi kuwa na mkurugenzi wa TPA mwenye uzoefu wa masuala ya uchumi, na ndio sababu licha ya kuwa na faida za kijiografia kulinganisha na majirani zetu bado hatujaweza kufaidika nayo.

Hata haya mawazo mengi yenye kuupinga uwekezaji wa DP World pale bandarini chanzo chake ni kuwa na akili za kijamaa katika ulimwengu ambao inatubidi tupigane kibepari.

Tuna safari ndefu ya kwenda kama mpaka leo mwaka 2023 tunaziamini sana zile fikra za Mwalimu Nyerere, dunia sio rafiki tena.
 
Stupid fish
 
A selfish point of view.
Mwalimu alisema kama watu hawana uelewa/ujuzi wa kuendesha migodi, tutulie wanatu wasome na waelimike ili biashara ya madini wajue jinsi ya kuiendesha.
Madini yaachwe ardhini, hayaozi.

Wakajitokeza wajinga kama ninyi na kuvuna rare earh ore na kupeleka nje pata madini ya dhahabu na rare metals.
Tukapoteza si biashara tu bali ajira na ujuzi muhimu.
Katika nchi nyingine watu kama ninyi mlio madarakani ni risasi tu kwa kujifikiria na kuwa corrupt.
 
Hata Mkapa aliyewapa barrick hizo dhahabu nae ni mjinga pia?. Huwezi kumkwepa mtu mwenye exposure katika utendaji wa kazi, anakuja na uelewa mpana wa nini anachotaka kukifanya tofauti na mtu ambaye hajawahi hata kufuga kuku.

Utakapompa shirika mtu kama Rostam au Mo Dewji ni tofauti na litakavyoendeshwa na mtu mshamba tu aliyemaliza mlimani na hajafanya chochote cha maana.

Shirika nyeti kama bandari limekuwa likishindwa kuinuka kimataifa na kuisaidia nchi kwa sababu ya hizi akili za kijamaa zenye kupitwa na wakati. Lazima vichwani tupanuke ili kujua nini haswa kinachoendelea huko nje.
 
Kati ya mambo Mkapa alikuja kukiri ni kuuza/kubinafsisha mali za umma bila kutumia akili.
Alikuwa muungwana sana kukiri hivyo.
 
Kiranja wa Malaika alimsafishia njia, sasa anapiga tu. Hao ni wasaidizi wa upigaji.
 
Kati ya mambo Mkapa alikuja kukiri ni kuuza/kubinafsisha mali za umma bila kutumia akili.
Alikuwa muungwana sana kukiri hivyo.
Kuna mahali tulikosea katika kushughulika na hii dhana nzima ya mabadiliko ya kimfumo kutoka kwenye ujamaa kuingia katika ubepari.

Lakini makosa yetu hayawezi kuufuta ukweli kwamba ni afadhali sana uchumi wa kibepari kuliko zile akili za nchi nzima kuvaa sare sare maua kama vile watoto mapacha.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…