Mfanyakazi wangu ametapeliwa bidhaa zenye thamani ya Tsh. 300,000 Goba njia nne kwenye sheli

Mfanyakazi wangu ametapeliwa bidhaa zenye thamani ya Tsh. 300,000 Goba njia nne kwenye sheli

Isijekua huyo aliyekuambia ametapeliwa ndio amekutapeli
 
Mfanyakazi aligeuka kilaza sijui mjinga.
Mteja amepiga simu anataka bidhaa tukakubaliana na bei, nikamkabidhi bidhaa apeleke wampe laki tatu, akaondoka wakamwambia wako sheli walikuwa ni wadada kwenye kigari kidogo kufika akawapa mzigo wakamwambia wametuma hela hata ajajisumbua kuuliza kama nimetumiwa hela wala nini, anarudi mikono mitupu ananiambia aliwaamini kwa sababu ni wadada.
Hapa kuna utata,walijuaje kama atakayepeleka mzigo ni dada wa kuuza duka,je ungepeleka mwenyewe ina maana wasingekulipa?Hapa ninahisi inawezekana walituma kweli ila wamekosea namba au baada ya kuona ni mdada wakajiongeza kumpiga kitu kizito.Wadada wa mjini kwakweli sio wa kuwaamini,halafu unaweza kukuta ni hawa walioweka avatar za sura nzuri nzuri humu JF......
 
📌📌📌kubali tu kugawana UMASIKINI na wananchi wenzako HAKUNA NAMNA!!!

KWA UTITIRI HUU WA JOBLESS,DASLAM INAWATU WENGI SANA ILA NUSU YAO NI WAZURURAJI UNATEGEMEA NINI.
 
Neno tapeli limetoka kwenye kifaransa na chanzo chake ni wimbo wa hemed maneti vijana jazz wimbo matapeli

Kuna mkongo alipigwa za uso pale posta kwenye picha ya sanamu ya bismark sasa akaanza kulalamika komatitapeli komatitapeli jamaa wakajua jamaa mkongo kashapigwa tayari na wabongo ndipo wakatoa wimbo wanaitwa matapeli

Komatitapeli shemapeli kupekupe kumbamba weeeeba

Comment t'appelez(What's your name)

Je m'appelle (My name is)
Niliacha kusoma French form 2
 
Back
Top Bottom