KERO Mfereji wenye maji yenye kinyesi unatumiwa kumwagilia bustani za mbogamboga Kibaha Maili Moja, Wataalamu wetu mko wapi?

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua
Miaka ya zamani kidogo wachina waliokuwa wakifanyia kazi kwenye mgodi wa makaa ya mawe wa Kiwira kule Kyela walikuwa wakiishi sehemu panaitwa Kayuki (Siku hizi hiyo kambi yao ni shule ya sekondari)...wale jamaa walikuwa wakimwagilia Spinachi ambayo inafahamika kama Chinese kwa kinyesi cha binadamu...na ilistawi sana...wanyakyusa wa Ushirika wakasema hatuli kabisa Chinese...ile mbolea ikishaingia kwenye mizizi inakuwa converted kuwa chakula cha mmea kwa utaratibu wa osmosis kama ulimfuatilia mwalimu wako wa bayoloji, muhimu osha vizuri kabla ya kuila....
 
Kinyesi ni mbolea
 
Sasa ni zaidi ya mika sita mboga kwaajili ya familia yangu nazalisha mwenyewe nyumbani kwangu. Baada ya kuuziwa mboga iliyopulizwa dawa kuua wadudu iitwayo SnowCrone kabla ya kuchumwa....
 
Nadhani kwa kuwa hatujasikia kama kuna mlipuko wa Kipindupindu hapo maeneo ya Kibaha tuamini hizi mboga ni salama!
After then haziliwi zikiwa mbichi,zinaoshwa na harafu zinapikwa ili kuua bacteria.
 
Nilivyoona neno mfereji nimeshtuka kweli!
 
Kinyesi hakina shida
Hata kuku na bata wanakula!
Kama hayo maji yana chemicals zenye sumu huo ndio uchafu mbaya!

Maji ya kinyesi si hatari kwa afya

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
nilitaka kumueleza hili umeniwahi.
huwa kuna process za kuua wadudu wapatikanao ndani ya kinyesi. zamani bustani za magereza dar mboga zao zilikua zimenawiri walikua wakitumia hii kitu.
 
Wachina wachafu sana. Humo kuna mavipindupindu, mataifodi, ma amoeba, ma minyoo ma tetenus na magonjwa mengine kibao kibao. Mbolea ya binadamu haifai kwa mbolea, na nchi zingine ukitaka kutumia mbolea ya wanyama lazima uichome na utumie majivu yake.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…