Mfumo wa ajira nchini umeshindikana, bila connection hutoboi!

Mfumo wa ajira nchini umeshindikana, bila connection hutoboi!

Thee MF

New Member
Joined
Sep 26, 2016
Posts
2
Reaction score
18
Mfumo wa Ajira Nchini kwetu umeshindikana kabisa hasa kwa tusio na Koneksheni kabisaa!

Mfano: nimewahi kuitwa kwenye interview nyingi tu za serikalini ila zote zinafanywa kwa ushahidi tu ili wale wasahili walipwe kwa kupoteza muda wetu.

Viongozi wanakazia eti vijana mjiajiri wanasahau kama Kuji-ajiri pia kunataka Pesa tena muda mwingine ni pesa ndefu kuliko mshahara uliokuwa una vizia kwenye Ajira zao.

Nina rafiki zangu wamesomea Mambo ya tourism 😂 sasa sijui wafuge simba wao au wanunue land cruiser la Million 100 wabebe wazungu.

Mwingine kasomea shipping pale TPA temeke sasa yeye ajiajiri vipi wakati hao TPA wenyewe wameporwa kazi
Kibaya Zaidi niliwahi kuomba nafasi za mafunzo ya JKT ila nikakosa kwa sababu za hovyo sana ila kuna dogo alilazimishwa na dingi ake ila dogo hataki kabisa ni vile tu ana koneksheni zimempa hiyo nafasi ambayo sisi tumenyimwa kwa makusudi apewe dogo asiye itaka tena analalamika tangu kafika mpaka anaondoka, tena kuna muda alitaka kutoroka asiandikishwe ila karudishwa na kiongozi wa pale pale!

Wale walioenda kwenye usahili wa SENSA wanakumbuka balaa la pale na figisu za makusudi!

Wiki kadhaa hapa kulikuwa na usahili wa TAKUKURU. Kuna jamaa angu alifika usahili wa ORAL akaulizwa "Arusha kilitokoea nini juzi kati?" Khee, imagine maswali kama hayo mtu umempandisha basi umemsubirisha masaa!! Umempima vipimo, umemvua nguo alafu unamuuliza Arusha kimetokea nini majuzi kati? Au Tarehe ya kufa Lowasa? Khaaa!

Mi sio adui wa kujiajiri ila kuna vitu haviingii akili na vingine viko nje ya uwezo wetu

Mfano: Wengi tumesomeshwa either na wazazi na ndugu au na serikali (mikopo) ila tulio someshwa na ndugu na wazazi HUWEZI kuwaambia nipeni izo milioni 6 nikafungue biashara sitaki degree haina uhakika wa Ajira!! Mzazi gani au ndugu gani atakubali? Tunabaki kwenye kifungo icho mpaka tunakuja kuteseka mtaani!

Pia baadhi ya ajira za kujiajiri zinataka ukaze roho mfano washkaji uliosoma nao msingi wakafeli wakawa bodaboda au bajaji au car washer! Umewaacha karibu miaka kumi alafu unarud mtaani unamuomba 'deiwaka' aisee inataka moyo!

Mi nanyoa watu Saloon ila bosi wangu nilimuacha shule ya msingi jina lake halikuwa kwenye Listi ya form 1, mimi nina degree langu geto lina mhuri wa mwanasheria! Tuna pambana na Koneksheni huku tuna pambana na ndugu wenye wivu wanao nadhani degree ndio Pesa.

Huku tuna kaza sura kwa aibu tunazopata mitaani 2025 mgombea anasimama anasema MKINICHAGUA NAWAPA UBWABWA!

inbound728898474250464900.png
 
Binafsi nakuelewa sana. Ila tafsir ya maisha wakat mwingine ni ngumu sana kuielewa. Any way tuishi na ndio maisha.

Kuna tuliobahatika japo kufanya kazi za mkataba Serikalin na tukafanya haswaaa kwa bidii sana. Ni ngumu kujisifia ila nilipewa sifa na watu kuwa utendaji wangu wenda ulizidi mara dufu ya Bosi wangu, na hizo sifa ni za Nje tuu, za ndani nilizijua mimi ikiwepo na kuongeza mapato ya ofsi mara dufu. Kiufupi kabla sijaja Mkoa haukuwahi kufikia lengo la Makusanyo ya mapato uliopewa kwa kipindi kirefu tu, Ila baada ya mimi kuanza kazi pale nilijaribu njia tofauti na zikalipa sana tuu, Sasa mkoa ulikuwa unaweza kufikia lengo na nyongeza ya robo au nusu ya kiwango tulichokuwa tumepangiwa.

My friends nilifanya kadri y uwezo wangu wote na ilinisaidia maana ilinijenga sana kiakili, Pamoja na kukosa ajira katika taasisi ile. Saiv nipo tuu Mtaani na najaribu kufanya kinachowezekana japo mambo ni magumu mnoo. Mwaka wa Sita Sasa toka nihitimu Shahada yangu ya kwanza ila Mwanga sioni kabisaa. Wazee kijijini huko kila siku kupiga simu na kuuliza vipi serikal imekukumbuka? Simply kuhusu ajira nishakata Tamaa
 
Mfumo wa Ajira Nchini kwetu umeshindikana kabisa hasa kwa tusio na Koneksheni kabisaa!

Mfano: nimewahi kuitwa kwenye interview nyingi tu za serikalini ila zote zinafanywa kwa ushahidi tu ili wale wasahili walipwe kwa kupoteza muda wetu.

Viongozi wanakazia eti vijana mjiajiri wanasahau kama Kuji-ajiri pia kunataka Pesa tena muda mwingine ni pesa ndefu kuliko mshahara uliokuwa una vizia kwenye Ajira zao.

Nina rafiki zangu wamesomea Mambo ya tourism 😂 sasa sijui wafuge simba wao au wanunue land cruiser la Million 100 wabebe wazungu.

Mwingine kasomea shipping pale TPA temeke sasa yeye ajiajiri vipi wakati hao TPA wenyewe wameporwa kazi
Kibaya Zaidi niliwahi kuomba nafasi za mafunzo ya JKT ila nikakosa kwa sababu za hovyo sana ila kuna dogo alilazimishwa na dingi ake ila dogo hataki kabisa ni vile tu ana koneksheni zimempa hiyo nafasi ambayo sisi tumenyimwa kwa makusudi apewe dogo asiye itaka tena analalamika tangu kafika mpaka anaondoka, tena kuna muda alitaka kutoroka asiandikishwe ila karudishwa na kiongozi wa pale pale!

Wale walioenda kwenye usahili wa SENSA wanakumbuka balaa la pale na figisu za makusudi!

Wiki kadhaa hapa kulikuwa na usahili wa TAKUKURU. Kuna jamaa angu alifika usahili wa ORAL akaulizwa "Arusha kilitokoea nini juzi kati?" Khee, imagine maswali kama hayo mtu umempandisha basi umemsubirisha masaa!! Umempima vipimo, umemvua nguo alafu unamuuliza Arusha kimetokea nini majuzi kati? Au Tarehe ya kufa Lowasa? Khaaa!

Mi sio adui wa kujiajiri ila kuna vitu haviingii akili na vingine viko nje ya uwezo wetu

Mfano: Wengi tumesomeshwa either na wazazi na ndugu au na serikali (mikopo) ila tulio someshwa na ndugu na wazazi HUWEZI kuwaambia nipeni izo milioni 6 nikafungue biashara sitaki degree haina uhakika wa Ajira!! Mzazi gani au ndugu gani atakubali? Tunabaki kwenye kifungo icho mpaka tunakuja kuteseka mtaani!

Pia baadhi ya ajira za kujiajiri zinataka ukaze roho mfano washkaji uliosoma nao msingi wakafeli wakawa bodaboda au bajaji au car washer! Umewaacha karibu miaka kumi alafu unarud mtaani unamuomba 'deiwaka' aisee inataka moyo!

Mi nanyoa watu Saloon ila bosi wangu nilimuacha shule ya msingi jina lake halikuwa kwenye Listi ya form 1, mimi nina degree langu geto lina mhuri wa mwanasheria! Tuna pambana na Koneksheni huku tuna pambana na ndugu wenye wivu wanao nadhani degree ndio Pesa.

Huku tuna kaza sura kwa aibu tunazopata mitaani 2025 mgombea anasimama anasema MKINICHAGUA NAWAPA UBWABWA!
KAMA UKOO WAKO HAKUNA HATA MUWAJILIWA KATAA UKOO NA WEWE UNAENDA KUWA MKOSA AJIRA
 
Zamani kutokana na stori za hapa na pale nasikia ilikua unapokaribia kuhitimu elimu ya chuo kikuu, ajira zilikua zinakufata chuoni makampuni tofauti tofauti yakijinadi kwa namna yake kwako, kitu kilichopelekea wazee wetu waamini katika elimu.

Kwa kizazi chetu saivi mambo yamebadilika sisi ndo tunaujua uhalisia.
 
Kila kitu ni connection mdau hata issue nyingine za kuingiza hela kama biashara mpaka mtu akuguse mkono !! Unaweza kuwa na mtaji na akili unazo ila Inabidi upewe address kijana nenda hivi au vile inaweza kuwa ushauri au mawazo ila sehemu yeyote lazima watu wahusike! Wakikunjia roho huendi mwanangu (wapo wanaoenda ila ni asimilia ndogo sana )

Labda hilo wazo uwe umeliibua wewe mwenyewe ila vinginevyo hautasogea 😀😀 hiyo ndiyo maana ya msemo watu ni mali !!
Mwenyewe mwenyewe huendi ! Jichanganyeni na watu
 
Binafsi nakuelewa sana. Ila tafsir ya maisha wakat mwingine ni ngumu sana kuielewa. Any way tuishi na ndio maisha.

Kuna tuliobahatika japo kufanya kazi za mkataba Serikalin na tukafanya haswaaa kwa bidii sana. Ni ngumu kujisifia ila nilipewa sifa na watu kuwa utendaji wangu wenda ulizidi mara dufu ya Bosi wangu, na hizo sifa ni za Nje tuu, za ndani nilizijua mimi ikiwepo na kuongeza mapato ya ofsi mara dufu. Kiufupi kabla sijaja Mkoa haukuwahi kufikia lengo la Makusanyo ya mapato uliopewa kwa kipindi kirefu tu, Ila baada ya mimi kuanza kazi pale nilijaribu njia tofauti na zikalipa sana tuu, Sasa mkoa ulikuwa unaweza kufikia lengo na nyongeza ya robo au nusu ya kiwango tulichokuwa tumepangiwa.

My friends nilifanya kadri y uwezo wangu wote na ilinisaidia maana ilinijenga sana kiakili, Pamoja na kukosa ajira katika taasisi ile. Saiv nipo tuu Mtaani na najaribu kufanya kinachowezekana japo mambo ni magumu mnoo. Mwaka wa Sita Sasa toka nihitimu Shahada yangu ya kwanza ila Mwanga sioni kabisaa. Wazee kijijini huko kila siku kupiga simu na kuuliza vipi serikal imekukumbuka? Simply kuhusu ajira nishakata Tamaa
Pole sana mkuu
 
Pole sana kijana, ajira ni mtihani mkuu.
Binafsi sijahangaika saana na kuapply hizo mbanga ila eanaoapply wanaipatapata.
Ukiachana na koneksheni basi walau na wewe uwe na kitu tofauti cha kuoffer la sivyo utaula wa chuya na hizi gentleman GPA zetu.
 
Kwa mifumo ilivyo as is..., na kwa teknolojia na automation iliyopo usitegemee kutakuja kuwa na ajira zenye ujira wa kutosha bila kufanya mabadiliko na complete overhaul....

Nguvu kazi sio deal tena.....; watoa huduma wamekuwa wengi kuliko uhitaji....; Sasa kama demand ni kubwa kuliko uhitaji na mwenzako ana advantage ya connection unategemea nini kwenye dunia ambayo humans are corrupt ?
 
Back
Top Bottom