Wanajamii,
Unapoomba passport au ya ID, ni kawaida kuulizwa kwenye form Jina lako la Kwanza, la katikati na la Ukoo. Sasa Tatizo ni kwamba Passport au ID vikitolewa, kunakuwa hakuna utenganisho huu, bali Mambo ya Ndani na NIDA wanaamua kuunganisha jina lako la kwanza na la katikati kama jina lako la kwanza (given name).
Yaani, kama ulijaza form namna hii;
Jina la kwanza: Musa
Jina la katikati: Salum
Jina la Ukoo: Zengezenge
Passport au NIDA vitatoka Vikoonyesha hivi
Jina/Given name: Musa Salum
Jina la Mwisho: Zengezenge
Sasa mara kadhaa katika shughuli zako, nimekataliwa katakata kwamba mwenye jina sio mimi, baada ya kuandika jina langu la kwanza kama Musa, la la ukoo kama Zengezenge. Nikaambiwa mtu wanaemtaka jina lake la Kwanza ni Musa Salum. Nilijaribu kujiteteta lakini nikaambiwa system imenikataa!
Tatizo ni kwamba hata unapojaza form ambapo unatakiwa utoe forst name, middle name na surname, ni lazima uandike jina la kwanza kama majina mawili ili uendane na Passport au ID. Ukiandika moja unaambiwa huyu sio wewe. Sasa unajiuliza nikijaza jina la kwanza Musa Salum, jina la kati nijaze nini?
Na kumbuka mpangilio wa majina sasa unakuwa tofauti kwenye Passport /NIDA ID na kwenye cheti cha kuzaliwa.
Sasa hili ni jambo ambalo linapaswa kurekebishwa haraka. Kama Tanzania wanaona hakuna nafasi ya kuweka jina la kati kwenye Passport au ID basi wasiweke kabisa badala ya kuliunganisha na jina la kwanza na kufanya kila mtazania awe na majina mawili ya kwanza au given name.