BLACK MOVEMENT
JF-Expert Member
- Mar 11, 2020
- 4,548
- 11,901
Kutokana na Mabadiliko ya Tabia nchi, kumekuwepo na maeneo mengi sana ya nchi ambayo hupata mvua ndani ya mwezi na nusu tu na mvua hupotea mazima, au wanapata mvua miezi miwili pekee.
Arusha ni moja ya maeneo ambayo kwa miaka mitatu sasa wanapata mvua chini ya wastani na hivyo mazao hasa nafaka kama Mahindi yamekuwa yanahariboka kwa kunyauka.
Nini suluhisho kwa haya maeneo?
Ni kuwa sasa na vitalu vya miche ya mahindi na nafaka zingine kama mtama na hii miche itaoteshwa mapema mwezi mmoja kabla mvua hazijaanza na mvua zinapo anza kunyesha inakuwa ni kuhamishia shambani.
Wakati wengine ndio wanakimbizana na kuotesha mahindi chini wewe unakuwa unapiga mashimo ya kuotesha miche ya mahindi.
Hii njia ni nzuri kwa wakulima wadogo wenye hekari moja hadi 5 au 10 wanaweza kabisa kuotesha miche ya mahindi yenye mwezi mmoja.
Hii njia itasaidia sana kupunguza muda wa mahindi kukaa shambani, Kwa Arusha kama mvua zingeanza mwezi wa tatu kamili watu wangevuna sana ila mvua zimeanza mwezi wa 3 mwishoni na mwezi wa 5 zikapotea kabisa.
Kama hawa wakulima wangeotesha miche yenye mwezi moja maana yake shambani mahindi yangekaa na zile mvua zingekuwa ni za kuweka mbelewele na kubeba mahindi na hivyo watu wangepata Chakula cha kutosha.
Ni wakati sasa kwa wakulima kujaribu hii njia inawezekana kabisa kwa wakulima wadogo wa Tanzania, nyakati zinabadilika sana hivyo lazima na jamii ibadilike, ni ujinga una hekari moja unangoja mvua hadi zinyeshe ukapande mahindi wakati ukanda wako ni wa mvua za kusua sua.
Ni wakati sasa kwa Serikali na wakulima kuja na hizi njia za kutumia miche ya mahindi badala ya mahindi yenyewe kwa maeneo yanayo pata mvua za chini ya kiwango, hii itasaidia sana kuhakikisha upatikanaji wa chakula cha kutosha.
Hii njia inafaa kwa nafaka karibia zote ikiwemo viazi vitamu, Wengi hatujui kwamba viazi vitamu pia unaweza tumia miche badala ya cuttings au vijiti.
Karibu kwa maoni ya jinsi yakutekeleza wazo hili
Arusha ni moja ya maeneo ambayo kwa miaka mitatu sasa wanapata mvua chini ya wastani na hivyo mazao hasa nafaka kama Mahindi yamekuwa yanahariboka kwa kunyauka.
Nini suluhisho kwa haya maeneo?
Ni kuwa sasa na vitalu vya miche ya mahindi na nafaka zingine kama mtama na hii miche itaoteshwa mapema mwezi mmoja kabla mvua hazijaanza na mvua zinapo anza kunyesha inakuwa ni kuhamishia shambani.
Wakati wengine ndio wanakimbizana na kuotesha mahindi chini wewe unakuwa unapiga mashimo ya kuotesha miche ya mahindi.
Hii njia ni nzuri kwa wakulima wadogo wenye hekari moja hadi 5 au 10 wanaweza kabisa kuotesha miche ya mahindi yenye mwezi mmoja.
Hii njia itasaidia sana kupunguza muda wa mahindi kukaa shambani, Kwa Arusha kama mvua zingeanza mwezi wa tatu kamili watu wangevuna sana ila mvua zimeanza mwezi wa 3 mwishoni na mwezi wa 5 zikapotea kabisa.
Kama hawa wakulima wangeotesha miche yenye mwezi moja maana yake shambani mahindi yangekaa na zile mvua zingekuwa ni za kuweka mbelewele na kubeba mahindi na hivyo watu wangepata Chakula cha kutosha.
Ni wakati sasa kwa wakulima kujaribu hii njia inawezekana kabisa kwa wakulima wadogo wa Tanzania, nyakati zinabadilika sana hivyo lazima na jamii ibadilike, ni ujinga una hekari moja unangoja mvua hadi zinyeshe ukapande mahindi wakati ukanda wako ni wa mvua za kusua sua.
Ni wakati sasa kwa Serikali na wakulima kuja na hizi njia za kutumia miche ya mahindi badala ya mahindi yenyewe kwa maeneo yanayo pata mvua za chini ya kiwango, hii itasaidia sana kuhakikisha upatikanaji wa chakula cha kutosha.
Hii njia inafaa kwa nafaka karibia zote ikiwemo viazi vitamu, Wengi hatujui kwamba viazi vitamu pia unaweza tumia miche badala ya cuttings au vijiti.
Karibu kwa maoni ya jinsi yakutekeleza wazo hili
Upvote
4