Mfumo wa wengi wape ni mfumo wa ajabu sana

Mi napendekeza wanaolipa kodi kwa Tin number au Paye kiwe ni kigezo cha kwanza.

Cha pili kiwe ni kufaulu angalau asilimia 60 katika intavyuu ndogo ya kuqualify kupiga kura. Katika intavyuu kutakuwa na swali kama anatambua vyama vingine vya siasa? Ana uelewa wa sera moja mbili tatu??
 
Amini amini nakwambia trump bi bora kuliko yule mwanamama Harris. Yule mwanamama ni mweupe sana sana we fuatilia interview zake hata hakuna alikuwa anajibu na nyingi ziko edited.
Siwezi kubisha.

Hata ukienda milembe vichaa huzidiana ukichaa kuna wenye uhafadhali kuzidi wengine lakini wote ni vichaa.
 
Ulichosema kina mantiki.

Tia nyama zaidi karibu
 
Dahhh.....
Hizi headings zingine miwe mnajaribu kuzinyima ukali wa maneno mkuu, maana mie nimekuja nduki nikijua mambo yetu yaleeee.....😋😋
Mwehu wewe😀
 
Siwezi kubisha.

Hata ukienda milembe vichaa huzidiana ukichaa kuna wenye uhafadhali kuzidi wengine lakini wote ni vichaa.
Kuna muda mambo hayaendi hadi watu wanaweza kupigia kura dikteta. Watu waliichoka democratic na kumpa ushindi trump maana alikuwa anazungumzia mambo yaliyo wachosha. Mfano illegal immigrants sasa ni kilio hadi EU
 
Kuna muda mambo hayaendi hadi watu wanaweza kupigia kura dikteta. Watu waliichoka democratic na kumpa ushindi trump maana alikuwa anazungumzia mambo yaliyo wachosha. Mfano illegal immigrants sasa ni kilio hadi EU
Marekani bila wahamiaji sio marekani tena iwe ni legal au illegal
 
Kama watunga sheria tu wengine hata la saba hawakumaliza, kwanini wapiga kura wawe na vigezo hivyo
Ndio maana nimezungumzia suala la meritocracy system huwezi weka mtu kama msukuma au babu tale akatunga sheria za kuleweka zaidi tu ni uozo
 
Ndio maana nimezungumzia suala la meritocracy system huwezi weka mtu kama msukuma au babu tale akatunga sheria za kuleweka zaidi tu ni uozo
Mimi nachoona ni kufanya reform ya elimu watu wapate elimu bora maana ukiwaacha wachache ndio wachague mwisho nao watakiwa corrupt na kuchagua kwa maslahi yao peke yao kwanza.
 
Kwa hiyo unaona bora tuongozwe na utashi wa kikundi fulani kinachoangalia maslahi yao binafsi?
 
Mimi nachoona ni kufanya reform ya elimu watu wapate elimu bora maana ukiwaacha wachache ndio wachague mwisho nao watakiwa corrupt na kuchagua kwa maslahi yao peke yao kwanza.
Ndio maana nikasema watu wengi walioathirika na mfumo mbovu wa elimu haipaswi kutumika wengi wape maana watakuwa hawajui lolote la maana.

Mabadiliko ya mfumo wa elimu ni ya lazima.
 
Kwa hiyo unaona bora tuongozwe na utashi wa kikundi fulani kinachoangalia maslahi yao binafsi?
Hapana maslahi ya Taifa.

CCM haina sifa hii.
 
Kwa hiyo unaona bora tuongozwe na utashi wa kikundi fulani kinachoangalia maslahi yao binafsi?
China ya CCP na CCM ya vyote ni vikundi vidogo tu katika population nzima ya nchi lakini vimejitodautisha.

Kipi ni kikundi kinachojali maslahi ya taifa na kipi kinajali maslahi binafsi na utofauti huo umechorwa na mstari wa meritocracy system.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…