Mfunze Mwanao kujiajiri, mwambie maisha hayaanzi akiajiriwa, wasomi wakiwa wengi ajira zinakuwa chache

Hakuna kilicho haribika,mleta mada amezungumzia nini kifanyike na wewe umezungumzia ni kwa namna gani kifanyike,labda kama umekusudia kumkosoa tu.

Na maneno tupu yanaathari pia maana hata hiyo sumu aliyoisema mleta mada imetokana na hayohayo maneno,wazazi wanaaminisha sana watoto kuwa asome ili aajiriwe,unakuta mzazi hana ajira rasmi lakini anahangaika kumsomesha mwanae akiamini ataajiriwa na kufanikowa.

Na mwingine ni mfanya biashara Mkubwa na yeye anahangaika kumsomesha mwanaeashule ya gharama hadi nje ya nchi mwisho wa siku mtoto akirudi anakuja kupika makande.Maana hawajui huko chuoni walifuata nini.

Hivyo inabidi kubadilika maana hali imebadilika ili tuendane na mazingira.
Maisha hayaanzi baada ya kuajiriwa au kumaliza chuo Bali haya tunayoishi ndio maisha.
 
Watu ni wengi sana .


Ulichosema ni sahihi , Wazazi wengi bado wameshikilia imani kubwa ya Soma mwanangu uajiriwe na serikali uwe na maisha mazuri.


Watoto wanaposoma, nakuishia kua Waalimu wa HKL ,hajira hamna, wengi wao huwa hawana tena Fikra Mpya kichwan.



Wazazi wawahimize wanao kusoma si kwaajili ya Kuajiriwa tu Bali kujiajiri ..nikweli nawazi hapa Duniani kazi za kuajiriwa zinakupa Mahitaji muhimu tu, lkn nyingi hazifanyi vijana wengi kua vile walivyopanga kua.


Na vijana vilevile waache kushikilia Akili zao , Akili ukiishikilia hautafanya kitu chochote.


Unakuta kijana anayepata Mkopo 80% , hata kufikiria nn afanye ambacho kinaweza zalisha hiyo pesa , hamna...yeye kichwan ni Nguo, mademu na Anasa...sababu anajua ukimaliza, anaajiriwa

Baadae wakirudi kitaani ,kulia hakuishi !!.
 
Tanzania ipi mkuu? Kama hi hi ya JPM naomba utupe vigezo hivyo mkuu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu mama amekusudia kukosoa tu.

Huyo mama sina jema kwake,ana matatizo.

Sidhani kama uzi wangu haukuwa na makosa wmbayo wana JF wengine hawakuona,lakini ni makosa ya kawaida yasiyobadili maana ya uzi mzima.

Ila huyo bi mkubwa akishupalia jambo hatari.

Maneno yana athari kubwa tu kwa sababu watoto wengi wanatamani kuajiriwa kutokana na kuambiwa na wazazi wao hivyo ilhali wazazi wanauza nyanya tu.

Kama vitendo ndo vinaathiri kwa nini watoto hawa nao wasitake kuuza nyanya kama wanavyomuona baba yao kwa vitendo?

Hiiyo mama ni mtu wa kupuuzwa.
Sent using Jamii Forums mobile app
 
Umegonga vitu vya msingi sana.

Wadau kibao mtu akipokea pesa ananunua masimu ya nguvu na kujivinjari huku akisahau kuwa sasa hivi mtu anaitaka ajira kuliko sjira inavyomtaka mtu.
Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sasa kama wewe utaipata hiyo nafasi wakati sisi tupo maofisini ?

Ndo mana tunakuambia ukajiajiri ili umiliki hayo maghorofa kama sisi wa maofisini.

Au ulitaka uambiwe kaa nyumbani tu ulale ?

Sent using Jamii Forums mobile app

Ndio muanze nyie kuonyesha mifano ya hawa mnayoandika humu. Anzeni nyie kujiajiri ili watoto wenu waige waone kumbe inawezekana.
Wengi wenu wenye ajira hamjawahi ata kufungua banda la kuonesha mpira ila ndo mko mstari wa mbele vijana wajiajiri vijana wajiajiri


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Chuki binafsi .......she is intelligent woman I like her mature comments

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Maneno yana nafasi katika mabadiliko.

Sio lazima vitendo,al muhimu wapo waliojiajiri inatosha kuangalia kwao.

Lakini kumbuka kuwa unaambiwa ujiajiri kwa faida yako mwenyewe na sio kwa faida ya anayekuambia.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Genuine Entrepreneurs humu JF ni wachache sanaaaana na hua tunakutana nao huko PM tunaongea mambo ya msingi na wala hawanaga mambo ya kuji-brag na kujifanya eti 'they made it'.

Wengi wanaopiga kelele hapa wanafanya tu wishfull thinkings.
 
Ujumbe umefika kaka
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…