Mgao ujao wa umeme…

Mgao ujao wa umeme…

Kivuli cha JPM ndio kipimo cha urais wa Samia. Marehemu aliwazoeza watu vibaya kwa kuwahakikishia ufanisi unaotokana na upendo hata kama ni kwa gharama za kutokuwa mkweli.

Wake ukawa ni uongozi unaofanana na mshumaa, unawawakia watu kwa gharama ya wenyewe kuteketea. JPM alikuwa ni POPULIST LEADER, Alisikiliza shida za wengi na akataka aonekane anao uwezo wa kutatua kila tatizo, kumbe utatuzi mwingine ukiambatana na ukweli ni bora zaidi kwa serikali yake na kwa mwananchi.
Hapa umeandika bila uhalisia....bali ni chuki binafsi kwa Hayati.

Tatizo hapa ni sababu za mgao wa umeme....

Mara ya kwanza ilikuwa ni ukame...

Sasa hivi ni matengenezo.


Cha ajabu huo mgao wenyewe unaweza usionekane kwasababu umeme unakatwa kila siku karibu mara 10....

Ni jambo la ajabu sana nchi yenye miaka sitini ya uhuru kuwa na mgao wa umeme....

Shida zingine ni za muhimu sana....umeme matumizi yake ni makubwa mno hasa kwa nchi zinazotaka kuendelea...

Kwenye serikali hii ya SAMIA inakosa mtu mwenye huruma na wananchi....
 
Hapa umeandika bila uhalisia....bali ni chuki binafsi kwa Hayati.

Tatizo hapa ni sababu za mgao wa umeme....

Mara ya kwanza ilikuwa ni ukame...

Sasa hivi ni matengenezo.


Cha ajabu huo mgao wenyewe unaweza usionekane kwasababu umeme unakatwa kila siku karibu mara 10....

Ni jambo la ajabu sana nchi yenye miaka sitini ya uhuru kuwa na mgao wa umeme....

Shida zingine ni za muhimu sana....umeme matumizi yake ni makubwa mno hasa kwa nchi zinazotaka kuendelea...

Kwenye serikali hii ya SAMIA inakosa mtu mwenye huruma na wananchi....
Sina chuki kwa JPM, alipokuwa hai nilikuwa ni mmoja wa waliomuunga mkono kwa dhati kabisa. Alipofariki nikajifunza mengi kuhusiana na aina ya watu wake wa karibu na mienendo yao, ninapotoa maoni kumhusu ninajitahidi sana nimtendee haki.

Umeme wa Tanzania umeingizwa na siasa ukizingatia nishati hii ni pesa tupu. Hivyo wapigaji wakubwa wanaingiza mikono yao katika masuala yanayogusa maisha ya nchi.

Mama kazunguka kuitangaza nchi kimataifa hivyo alipaswa kufahamu muunganiko unaokuwepo kati ya uwekezaji mpana na uwepo wa nishati ya uhakika. Ni wizara nyeti sana lakini makundi ndani ya CCM yanaifanya ionekane kama vile ni wizara isiyoweza kuongozwa ikaongozeka.
 
Inadaiwa mgao wa umeme unakuja. Inadaiwa unaanza tarehe 1 mwezi ujao wa Februari.

Sababu ya huo mgao eti ni matengenezo ya mitambo yao ya wapi wapi huko sijui…

Sasa kwa akili zangu hizi za kidato cha nne, ni kama vile sielewi elewi.

Mbona nchi zingine huwa hakuna migao inayosababishwa na matengenezo ya mitambo ya umeme?

Au zipo? Kama zipo, basi sawa. Ila kwa nchi nizijuazo mimi, kamwe hata mara moja sijawahi sikia eti kutakuwepo na mgao au migao ya umeme kwa sababu mitambo ya kuzalisha au kusambaza umeme inafanyiwa ukarabati.

Hao wenzetu wao mitambo yao huwa haihitaji ukarabati? Kama huwa inahitaji ukarabati, wanawezaje kuepuka migao ya umeme?

Kwa nini sisi kila mitambo inapohitaji ukarabati [ kama ni kweli inahitaji huo ukarabati] basi kunakuwepo na mgao?

Manake hili si jambo geni. Limekuwepo siku zote. Sasa miaka yote hii hawa watu hawajaweza tu kubuni namna ya kuikarabati hiyo mitambo bila kuleta usumbufu wa migao?

Tanesco….and whoever else involved….seriously????

NB: Halafu nani anaamini huu mgao utakuwa ni wa siku 10 tu????? Mimi siamini….
Wenye Tanzania na CCM walisharudi; wewe ulikuwa hujui hilo? Siku hizi nchi inakwenda kwa maneno na ahadi lukuki huku matendo yakiwa zero.
 
Imebaki siku moja!

Ila baadhi ya watu wanadai tayari mgao ushaanza na wengine wanasema kuwa mgao umekuwepo kwa muda sasa!

🖕
 
Back
Top Bottom