Mgawanyiko na mpasuko ndani ya CHADEMA, sasa wadhihirika bayana na unaelekea pabaya usipodhibitiwa mapema kisiasa

Mgawanyiko na mpasuko ndani ya CHADEMA, sasa wadhihirika bayana na unaelekea pabaya usipodhibitiwa mapema kisiasa

Mr-Njombe

Member
Joined
Aug 29, 2022
Posts
64
Reaction score
122
Mwanzoni viongozi waandamizi wa chadema hususani ngazi ya taifa walikua wakijipiga kifua sana hadaharani kwamba hakuna mgawanyiko wala mpasuko wowote ndani ya chadema, ispokua kilichokua kinajitokeza ni uhuru wa viongozi na wanachama wa chadema kutoa maoni na mitazamo yao dhidi ya waliyo kua wakiyaona ndani ya chama chao.

Lakini kwasasa, ni wazi waliokua wanakana kutofautiani ndio hao hao wanalumbana waziwazi na kupambana kugombania nafasi na fursa za uongozi wa ngazi za juu chadema.

Unafiki wao wa kiwango cha juu, wanaupambanua wenyewe bila kificho kwasasa, kwa kutuhumiana masuala ya rushwa, kudanganya umma au kusema uongo.

Ni mategemeo ya wengi kwamba unafiki zaidi miongoni mwa viongozi waandamizi wa chadema, unatarajiwa kuibuka na kujidhihirisha bayana kadiri siku za uchaguzi zinavyokaribia.

Vita ya maneno ni kali mno, na kuna mashaka na hofu kubwa sana katika kila upande, na ni kwamba vita hii isipodhibitiwa kisaisa mapema inaweza kuleta madhara ya kijamii na kisiasa miongoni mwa wahusika na chadema wakapata hasara na huzuni.

Una maoni gani?
 
Mwanzoni viongozi waandamizi wa chadema hususani ngazi ya taifa walikua wakijipiga kifua sana hadaharani kwamba hakuna mgawanyiko wala mpasuko wowote ndani ya chadema, ispokua kilichokua kinajitokeza ni uhuru wa viongoz...
Kwa hatua iliyofikia they have come to the end of the road for these two bulls' camps to be together.

Kuna msemo : pema usipopema ukipema si pema tena.

Kamwe baada ya uchaguzi haiwezekani tena hizi kambi mbili kuwa kitu kimoja na wote wanajua hilo.

Lissu amekwishaamua liwalo na liwe.
 
Mwanzoni viongozi waandamizi wa chadema hususani ngazi ya taifa walikua wakijipiga kifua sana hadaharani kwamba hakuna mgawanyiko wala mpasuko wowote ndani ya chadema...
Gentleman,
chadema is no more within Tanzanian political scene :pulpTRAVOLTA:
 
Back
Top Bottom