Mgogoro NCCR Mageuzi: Timu Mbatia wachukua ofisi, wasema umefanyika uhaini ndani ya chama, Mbatia bado ni mwenyekiti

Ila CHADEMA imetapakaa Sana. Huyu Simbeye alikuwa CHADEMA miaka ya nyuma hapo. Kweli CHADEMA ni kiwanda Cha kutengeneza wanasiasa. Mpaka CCM walienda kununua huko baada ya kuona kwao ni magalasa. Keep it up CHADEMA.
Chadema yenyewe ilijengwa na wanasiasa kutoka nccr mageuzi yaani Selesini,Tundu Lisu,Komu,Malando,Lema n.k

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
Selasini ni Mdangaji kama wadangaji wengine.
Bei za mafuta zinashuka lini vile? Wakati Uhaini ukiendelea NCCR, CDM inaendelea na majadiliano. Nashauri Umakini uzingatiwe, hao jamaa walisema Wana mbinu nyingi sana zisotumika Bado.
 
Kitolewe tuu kile Kimbatia kwanza ni timu Sukuma gang na huwa Kasi yake ni kupondea awamu ya 6
 
Hivi vyama vinaendeshwa kama SACCOS na waliyovianzisha maana wanategemea viwalipe kufidia resources zao walizoinvest kwa miaka kadhaa

Mbatia hawatamtoa pale. Kama ni kung’oka ataondoka Selasini na wenzie.

Huu ndio upinzani wa Tanzania
 
Mlidhani Selasini ni mtu mwema?
Hivyo ni vipande vilivyo msaliti Yesu.
 
Wala hiyo siyo dharau, haiwezekani kumdharau mtu huku ukitumia nguvu nyingi batili kumhujumu! Ukiona nguvu nyingi za dola na ikiwa ni pamoja na kutumia fedha kurubuni watu na kuchochea uasi ujue chama hicho kina nguvu.
 
Hivi vibandiko vyako vya maneno mawili matatu, tena visivyokuwa na maana yoyote vimejaa sana humu tokea ujiunge JF.

Hivi huna hata uwezo wa kujifunza kuandika mambo ya maana na ukaeleweka?
Endelea kukariri!
 
Endelea kukariri!
Umri wote huo, umepoteza tu muda wako?

Vineno viwili, vitatu, tena visivyoongeza lolote katika unayochangia?

Si ajabu hata nyumbani upo hivi hivi, na wanao na mke walishazoea kutopata lolote la maana kutoka kwako!

Hopeless Kabisa.

Usinilaumu kwa lugha hii, lakini ukweli ni kwamba inaudhi kuwa na watu wa aina yako karibu.
 
“Kilichofanyika ni uhaini na uhuni ndani ya chama na hatuwezi kukubali kilichofanyika, chama kitakaa na kufanya maamuzi, kinachotusikitisha zaidi Msajili wa Vyama vya Siasa ameshiriki katika uhuni huu.
Kama vyama vyetu vya upinzani vinafanya uhuni sijui ndiyo itakuwaje sasa!?
 
Hahahahaha.

Hiki kisa kimenikumbusha zamani sana, NCCR yanajirudia tu. Yalitokea kama hayo huko Tanga kwenye mkutano wao wakazichapa, enzi za mwanzo mwanzo, nadhani walikuwa kina marehem Kassim Maguto. Mbatia siku hizo hata hajulikani kabisa, sijui kama alikuwa hata kishajiunga NCCR , mtanikumbusha wajuzi. Zilichapwa huko mpaka dola likaingilia kati.

Vijana wengi hawatalielewa jina hilo. Ni muda mrefu sasa.
 
I remember those days.
Mzee Mrema alikuwapo.Walizichapa wakatoana na ngeu.Maberu Marandu alijificha chini ya meza kuokoa nafsi yake.
 
I remember those days.
Mzee Mrema alikuwapo.Walizichapa wakatoana na ngeu.Maberu Marandu alijificha chini ya meza kuokoa nafsi yake.
Kweli kabisa. Si vijana wengi humu wanayoyaelewa hayo. Ndipo nadhani likazaliwa jina "mageuzi" mbele ya NCCR.

Yanajirudia tu. Yanyojitokeza hivi sasa huko NCCR yanathibitisha methali ya Kiswahili "Mtoto umleavyo ndivyo akuavyo".
 
subiri game bado
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…