Mgogoro NCCR Mageuzi: Timu Mbatia wachukua ofisi, wasema umefanyika uhaini ndani ya chama, Mbatia bado ni mwenyekiti

Mgogoro NCCR Mageuzi: Timu Mbatia wachukua ofisi, wasema umefanyika uhaini ndani ya chama, Mbatia bado ni mwenyekiti

Ila CHADEMA imetapakaa Sana. Huyu Simbeye alikuwa CHADEMA miaka ya nyuma hapo. Kweli CHADEMA ni kiwanda Cha kutengeneza wanasiasa. Mpaka CCM walienda kununua huko baada ya kuona kwao ni magalasa. Keep it up CHADEMA.
Chadema yenyewe ilijengwa na wanasiasa kutoka nccr mageuzi yaani Selesini,Tundu Lisu,Komu,Malando,Lema n.k

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
Selasini ni Mdangaji kama wadangaji wengine.
Bei za mafuta zinashuka lini vile? Wakati Uhaini ukiendelea NCCR, CDM inaendelea na majadiliano. Nashauri Umakini uzingatiwe, hao jamaa walisema Wana mbinu nyingi sana zisotumika Bado.
 

Katibu wa Itikadi na Uenezi wa NCCR-Mageuzi, Edward Simbeye amezungumza na waandishi wa habari leo Mei 21, 2022 na kudai kuwa kilichofanywa na kundi lililojipa sura ya Halmashauri Kuu ndani ya chama hicho mapema leo ni uhaini.

Awali ilitolewa taarifa kuwa Halmashauri Kuu ya Chama cha NCCR-Mageuzi imemsimamisha Mwenyekiti wa chama hicho, James Mbatia na Makamu Mwenyekiti Bara, Angelina Mtahiwa kutojihusisha na shughuli zozote za chama hadi Mkutano Mkuu utakapoitishwa ili wajieleze kuhusiana na tuhuma inazowakubali.

Mjumbe wa Halmashauri Kuu na Mwenyekiti wa azimio hilo, Joseph Selasini alisema pamoja na kusimamishwa kwa viongozi hao pia wamelivunja Baraza la Wadhamini la NCCR na kuteua wajumbe wapya ambao watasajiliwa kwa mujibu wa taratibu zitakazowekwa.

Naibu Msajili wa Vyama vya Siasa Nchini, Sisty Nyahoza naye alikiri kupokea barua kutoka NCCR-Mageuzi kuwa kuna mabadiliko ya wajumbe wa bodi ya wadhami.

Baada ya tamko hilo ndipo muda mfupi baadaye Katibu Mkuu wa NCCR-Mageuzi, Martha Chiomba, alifunga ofisi za chama hicho zilizopo Ilala, Dar es Salaam, ili kumzuia James Mbatia.

Baada ya tukio hilo, wanachama wanaomuunga mkono Mbatia ndani ya chama hicho walifika ofisini hapo na kufanikiwa kuingia ndani kisha kuzungumza na Wanahabari wakisema waliotangaza kumsimamisha Mbatia hawana mamlaka n ahata akidi haikutimia.

Katibu wa Itikadi na Uenezi wa NCCR-Mageuzi, Edward Simbeye amesema:

“Kilichofanyika ni uhaini na uhuni ndani ya chama na hatuwezi kukubali kilichofanyika, chama kitakaa na kufanya maamuzi, kinachotusikitisha zaidi Msajili wa Vyama vya Siasa ameshiriki katika uhuni huu.

“Huwezi kuvunja Bodi ya Wadhamini au kumsimamisha Mwenyekiti kihuni.

“Msajili haoni hata haya, alijulishwa aliyekuwa Katibu Mkuu amesimamishwa inakuaje anapokea maamuzi yanayofanywa na watu kama hao.

“Sisty Nyahoza ndiye anaendesha haya makundi, anafadhili haya makundi na tuna uhakika, ukifika wakati tutaweka ushahidi hadharani. Huyu ndiye mhuni wa kwanza katika huu mchezo mchezo mchafu.

“Huyo aliyeitwa Katibu Mkuu (Martha Chiomba) alisimamishwa katika Kikao cha Kamati Kuu, anayekaimu ni Anthony Kom hakushiriki kwenye hicho kikao na hajui kama kuna hicho kikao walichofanya.

“Hao Wahuni walikuja kujaribu kufunga ofisi lakini tumewadhibiti na ndio maana tupo ofisini hapa, ofisi ipo chini ya wanachama. Tutaudhibiti uhuni wao, tumejipanga na tupo imara, hakuna ambaye ataweza kuivuruga NCCR Mageuzi.”


Pia Soma > NCCR Mageuzi yamsimamisha James Mbatia kufanya shughuli za Chama
Kitolewe tuu kile Kimbatia kwanza ni timu Sukuma gang na huwa Kasi yake ni kupondea awamu ya 6
 
Hivi vyama vinaendeshwa kama SACCOS na waliyovianzisha maana wanategemea viwalipe kufidia resources zao walizoinvest kwa miaka kadhaa

Mbatia hawatamtoa pale. Kama ni kung’oka ataondoka Selasini na wenzie.

Huu ndio upinzani wa Tanzania
 

Katibu wa Itikadi na Uenezi wa NCCR-Mageuzi, Edward Simbeye amezungumza na waandishi wa habari leo Mei 21, 2022 na kudai kuwa kilichofanywa na kundi lililojipa sura ya Halmashauri Kuu ndani ya chama hicho mapema leo ni uhaini.

Awali ilitolewa taarifa kuwa Halmashauri Kuu ya Chama cha NCCR-Mageuzi imemsimamisha Mwenyekiti wa chama hicho, James Mbatia na Makamu Mwenyekiti Bara, Angelina Mtahiwa kutojihusisha na shughuli zozote za chama hadi Mkutano Mkuu utakapoitishwa ili wajieleze kuhusiana na tuhuma inazowakubali.

Mjumbe wa Halmashauri Kuu na Mwenyekiti wa azimio hilo, Joseph Selasini alisema pamoja na kusimamishwa kwa viongozi hao pia wamelivunja Baraza la Wadhamini la NCCR na kuteua wajumbe wapya ambao watasajiliwa kwa mujibu wa taratibu zitakazowekwa.

Naibu Msajili wa Vyama vya Siasa Nchini, Sisty Nyahoza naye alikiri kupokea barua kutoka NCCR-Mageuzi kuwa kuna mabadiliko ya wajumbe wa bodi ya wadhami.

Baada ya tamko hilo ndipo muda mfupi baadaye Katibu Mkuu wa NCCR-Mageuzi, Martha Chiomba, alifunga ofisi za chama hicho zilizopo Ilala, Dar es Salaam, ili kumzuia James Mbatia.

Baada ya tukio hilo, wanachama wanaomuunga mkono Mbatia ndani ya chama hicho walifika ofisini hapo na kufanikiwa kuingia ndani kisha kuzungumza na Wanahabari wakisema waliotangaza kumsimamisha Mbatia hawana mamlaka n ahata akidi haikutimia.

Katibu wa Itikadi na Uenezi wa NCCR-Mageuzi, Edward Simbeye amesema:

“Kilichofanyika ni uhaini na uhuni ndani ya chama na hatuwezi kukubali kilichofanyika, chama kitakaa na kufanya maamuzi, kinachotusikitisha zaidi Msajili wa Vyama vya Siasa ameshiriki katika uhuni huu.

“Huwezi kuvunja Bodi ya Wadhamini au kumsimamisha Mwenyekiti kihuni.

“Msajili haoni hata haya, alijulishwa aliyekuwa Katibu Mkuu amesimamishwa inakuaje anapokea maamuzi yanayofanywa na watu kama hao.

“Sisty Nyahoza ndiye anaendesha haya makundi, anafadhili haya makundi na tuna uhakika, ukifika wakati tutaweka ushahidi hadharani. Huyu ndiye mhuni wa kwanza katika huu mchezo mchezo mchafu.

“Huyo aliyeitwa Katibu Mkuu (Martha Chiomba) alisimamishwa katika Kikao cha Kamati Kuu, anayekaimu ni Anthony Kom hakushiriki kwenye hicho kikao na hajui kama kuna hicho kikao walichofanya.

“Hao Wahuni walikuja kujaribu kufunga ofisi lakini tumewadhibiti na ndio maana tupo ofisini hapa, ofisi ipo chini ya wanachama. Tutaudhibiti uhuni wao, tumejipanga na tupo imara, hakuna ambaye ataweza kuivuruga NCCR Mageuzi.”


Pia Soma > NCCR Mageuzi yamsimamisha James Mbatia kufanya shughuli za Chama
Mlidhani Selasini ni mtu mwema?
Hivyo ni vipande vilivyo msaliti Yesu.
 
Unaziita SACCOS Halafu unataka zifanye demokrasia. Acha dharau na kiburi. Zingekuwa SACCOS mngefanya uchafuzi wa 2019 na 2020. Mngewaingilia CHADEMA kwenye viti maalum?. Acheni dharau wakati mkizidiwa mnawamiminia Risasi na kuwabambikizia kesi za ugaidi. Acha dharau maana Rais wa nchi ana jua thamani ya hivi vyama ndio maana anaongea nao ikulu.
Wala hiyo siyo dharau, haiwezekani kumdharau mtu huku ukitumia nguvu nyingi batili kumhujumu! Ukiona nguvu nyingi za dola na ikiwa ni pamoja na kutumia fedha kurubuni watu na kuchochea uasi ujue chama hicho kina nguvu.
 
Hivi vibandiko vyako vya maneno mawili matatu, tena visivyokuwa na maana yoyote vimejaa sana humu tokea ujiunge JF.

Hivi huna hata uwezo wa kujifunza kuandika mambo ya maana na ukaeleweka?
Endelea kukariri!
 
Endelea kukariri!
Umri wote huo, umepoteza tu muda wako?

Vineno viwili, vitatu, tena visivyoongeza lolote katika unayochangia?

Si ajabu hata nyumbani upo hivi hivi, na wanao na mke walishazoea kutopata lolote la maana kutoka kwako!

Hopeless Kabisa.

Usinilaumu kwa lugha hii, lakini ukweli ni kwamba inaudhi kuwa na watu wa aina yako karibu.
 
“Kilichofanyika ni uhaini na uhuni ndani ya chama na hatuwezi kukubali kilichofanyika, chama kitakaa na kufanya maamuzi, kinachotusikitisha zaidi Msajili wa Vyama vya Siasa ameshiriki katika uhuni huu.
Kama vyama vyetu vya upinzani vinafanya uhuni sijui ndiyo itakuwaje sasa!?
 
Hahahahaha.

Hiki kisa kimenikumbusha zamani sana, NCCR yanajirudia tu. Yalitokea kama hayo huko Tanga kwenye mkutano wao wakazichapa, enzi za mwanzo mwanzo, nadhani walikuwa kina marehem Kassim Maguto. Mbatia siku hizo hata hajulikani kabisa, sijui kama alikuwa hata kishajiunga NCCR , mtanikumbusha wajuzi. Zilichapwa huko mpaka dola likaingilia kati.

Vijana wengi hawatalielewa jina hilo. Ni muda mrefu sasa.
 
Hahahahaha.

Hikikisa kimenikumbusha zamani sana, NCCR yanajirudia tu. Yalitokea kama hayo huko Tanga kwenye mkutano wao wakazichapa, enzi za mwanzo mwanzo, nadhani walikuwa kina marehem Kassim Maguto. Mbatia siku hizo hizo hata hajulikani kabisa, sijui kama alikuwa hata kishajiunga NCCr, mtanikumbusha wajuzi. Zilichapwa huko mpaka dola likaingilia kati.

Vijana wengi hawatalielewa jina hilo. Ni muda mrefu sasa.
I remember those days.
Mzee Mrema alikuwapo.Walizichapa wakatoana na ngeu.Maberu Marandu alijificha chini ya meza kuokoa nafsi yake.
 
I remember those days.
Mzee Mrema alikuwapo.Walizichapa wakatoana na ngeu.Maberu Marandu alijificha chini ya meza kuokoa nafsi yake.
Kweli kabisa. Si vijana wengi humu wanayoyaelewa hayo. Ndipo nadhani likazaliwa jina "mageuzi" mbele ya NCCR.

Yanajirudia tu. Yanyojitokeza hivi sasa huko NCCR yanathibitisha methali ya Kiswahili "Mtoto umleavyo ndivyo akuavyo".
 

Katibu wa Itikadi na Uenezi wa NCCR-Mageuzi, Edward Simbeye amezungumza na waandishi wa habari leo Mei 21, 2022 na kudai kuwa kilichofanywa na kundi lililojipa sura ya Halmashauri Kuu ndani ya chama hicho mapema leo ni uhaini.

Awali ilitolewa taarifa kuwa Halmashauri Kuu ya Chama cha NCCR-Mageuzi imemsimamisha Mwenyekiti wa chama hicho, James Mbatia na Makamu Mwenyekiti Bara, Angelina Mtahiwa kutojihusisha na shughuli zozote za chama hadi Mkutano Mkuu utakapoitishwa ili wajieleze kuhusiana na tuhuma inazowakubali.

Mjumbe wa Halmashauri Kuu na Mwenyekiti wa azimio hilo, Joseph Selasini alisema pamoja na kusimamishwa kwa viongozi hao pia wamelivunja Baraza la Wadhamini la NCCR na kuteua wajumbe wapya ambao watasajiliwa kwa mujibu wa taratibu zitakazowekwa.

Naibu Msajili wa Vyama vya Siasa Nchini, Sisty Nyahoza naye alikiri kupokea barua kutoka NCCR-Mageuzi kuwa kuna mabadiliko ya wajumbe wa bodi ya wadhami.

Baada ya tamko hilo ndipo muda mfupi baadaye Katibu Mkuu wa NCCR-Mageuzi, Martha Chiomba, alifunga ofisi za chama hicho zilizopo Ilala, Dar es Salaam, ili kumzuia James Mbatia.

Baada ya tukio hilo, wanachama wanaomuunga mkono Mbatia ndani ya chama hicho walifika ofisini hapo na kufanikiwa kuingia ndani kisha kuzungumza na Wanahabari wakisema waliotangaza kumsimamisha Mbatia hawana mamlaka n ahata akidi haikutimia.

Katibu wa Itikadi na Uenezi wa NCCR-Mageuzi, Edward Simbeye amesema:

“Kilichofanyika ni uhaini na uhuni ndani ya chama na hatuwezi kukubali kilichofanyika, chama kitakaa na kufanya maamuzi, kinachotusikitisha zaidi Msajili wa Vyama vya Siasa ameshiriki katika uhuni huu.

“Huwezi kuvunja Bodi ya Wadhamini au kumsimamisha Mwenyekiti kihuni.

“Msajili haoni hata haya, alijulishwa aliyekuwa Katibu Mkuu amesimamishwa inakuaje anapokea maamuzi yanayofanywa na watu kama hao.

“Sisty Nyahoza ndiye anaendesha haya makundi, anafadhili haya makundi na tuna uhakika, ukifika wakati tutaweka ushahidi hadharani. Huyu ndiye mhuni wa kwanza katika huu mchezo mchezo mchafu.

“Huyo aliyeitwa Katibu Mkuu (Martha Chiomba) alisimamishwa katika Kikao cha Kamati Kuu, anayekaimu ni Anthony Kom hakushiriki kwenye hicho kikao na hajui kama kuna hicho kikao walichofanya.

“Hao Wahuni walikuja kujaribu kufunga ofisi lakini tumewadhibiti na ndio maana tupo ofisini hapa, ofisi ipo chini ya wanachama. Tutaudhibiti uhuni wao, tumejipanga na tupo imara, hakuna ambaye ataweza kuivuruga NCCR Mageuzi.”


Pia Soma > NCCR Mageuzi yamsimamisha James Mbatia kufanya shughuli za Chama
subiri game bado
 
Back
Top Bottom