Mgogoro NCCR Mageuzi: Timu Mbatia wachukua ofisi, wasema umefanyika uhaini ndani ya chama, Mbatia bado ni mwenyekiti

Mgogoro NCCR Mageuzi: Timu Mbatia wachukua ofisi, wasema umefanyika uhaini ndani ya chama, Mbatia bado ni mwenyekiti


Katibu wa Itikadi na Uenezi wa NCCR-Mageuzi, Edward Simbeye amezungumza na waandishi wa habari leo Mei 21, 2022 na kudai kuwa kilichofanywa na kundi lililojipa sura ya Halmashauri Kuu ndani ya chama hicho mapema leo ni uhaini.

Awali ilitolewa taarifa kuwa Halmashauri Kuu ya Chama cha NCCR-Mageuzi imemsimamisha Mwenyekiti wa chama hicho, James Mbatia na Makamu Mwenyekiti Bara, Angelina Mtahiwa kutojihusisha na shughuli zozote za chama hadi Mkutano Mkuu utakapoitishwa ili wajieleze kuhusiana na tuhuma inazowakubali.

Mjumbe wa Halmashauri Kuu na Mwenyekiti wa azimio hilo, Joseph Selasini alisema pamoja na kusimamishwa kwa viongozi hao pia wamelivunja Baraza la Wadhamini la NCCR na kuteua wajumbe wapya ambao watasajiliwa kwa mujibu wa taratibu zitakazowekwa.

Naibu Msajili wa Vyama vya Siasa Nchini, Sisty Nyahoza naye alikiri kupokea barua kutoka NCCR-Mageuzi kuwa kuna mabadiliko ya wajumbe wa bodi ya wadhami.

Baada ya tamko hilo ndipo muda mfupi baadaye Katibu Mkuu wa NCCR-Mageuzi, Martha Chiomba, alifunga ofisi za chama hicho zilizopo Ilala, Dar es Salaam, ili kumzuia James Mbatia.

Baada ya tukio hilo, wanachama wanaomuunga mkono Mbatia ndani ya chama hicho walifika ofisini hapo na kufanikiwa kuingia ndani kisha kuzungumza na Wanahabari wakisema waliotangaza kumsimamisha Mbatia hawana mamlaka n ahata akidi haikutimia.

Katibu wa Itikadi na Uenezi wa NCCR-Mageuzi, Edward Simbeye amesema:

“Kilichofanyika ni uhaini na uhuni ndani ya chama na hatuwezi kukubali kilichofanyika, chama kitakaa na kufanya maamuzi, kinachotusikitisha zaidi Msajili wa Vyama vya Siasa ameshiriki katika uhuni huu.

“Huwezi kuvunja Bodi ya Wadhamini au kumsimamisha Mwenyekiti kihuni.

“Msajili haoni hata haya, alijulishwa aliyekuwa Katibu Mkuu amesimamishwa inakuaje anapokea maamuzi yanayofanywa na watu kama hao.

“Sisty Nyahoza ndiye anaendesha haya makundi, anafadhili haya makundi na tuna uhakika, ukifika wakati tutaweka ushahidi hadharani. Huyu ndiye mhuni wa kwanza katika huu mchezo mchezo mchafu.

“Huyo aliyeitwa Katibu Mkuu (Martha Chiomba) alisimamishwa katika Kikao cha Kamati Kuu, anayekaimu ni Anthony Kom hakushiriki kwenye hicho kikao na hajui kama kuna hicho kikao walichofanya.

“Hao Wahuni walikuja kujaribu kufunga ofisi lakini tumewadhibiti na ndio maana tupo ofisini hapa, ofisi ipo chini ya wanachama. Tutaudhibiti uhuni wao, tumejipanga na tupo imara, hakuna ambaye ataweza kuivuruga NCCR Mageuzi.”


Pia Soma > NCCR Mageuzi yamsimamisha James Mbatia kufanya shughuli za Chama
Kosa la Mbatia ni kugoma kushiriki kikosi kazi cha kihuni
 
Wenyeviti wa hizi SACCOS kutoka Kaskazini wameona kama uenyekiti ni haki zao,Mbatia pamoja na Mbowe ni wenyeviti kwa muda mrefu hawana tofauti na raisi wa Uganda M7, hawa hawa ndio wanatoa mapovu majukwaani kudai demokrasia na katiba mpya wakati kwenye vyama vyao hakuna demokrasia wala mabadiliko ya katiba,ninachojiuliza wanang'ania uongozi kwa maslahi yapi? sio bure haiwezekani mtu miaka 20 baado upo palepale sijui wakipewa uraisi si ndio watajimilikisha nchi, wachaga acheni hizo bana, kuna maisha nje ya siasa na uenyekiti.
Wachaga wanaojihusisha na siasa ni wachache mno, hivi Lipumba ni mchaga?

Hashim Rungwe ni mchaga?

Chuki zako dhidi ya wachaga zinakuondolea ufahamu
 
Sisty nyahoza hii ndio.michezo yake

Kaishindwa chadema

Sasa anahamia NCCR MAGEUZI

CUF walifanikiwa kuivunja vunja vipande wanailia timing chadema mdogo mdogo n mwenyekiti anaonekana atajaa TU hiz safar za ikulu hiz asidhan wanachama wanafurahia maana hazina majibu tunayotaka

MUDA N MWL MZURI
Hivi inashindikana nini kumuua huyu mhuni?
 
Mbatia alifurahia wakati ule selasini anawananga Chadema huku akilindwa na spika ****** . acha na yeye akipate pate cha mtema kuni kutoka kwa mchaga mwenzie Selasini .
"Wema huwa hauna gharama mahususi , Ila pindi unapoutenda ubaya jua ubaya huo utarudi" by dizata vina .
Selasini ataenda ACT kwa wasaliti wenzake
 
Ila CHADEMA imetapakaa Sana. Huyu Simbeye alikuwa CHADEMA miaka ya nyuma hapo. Kweli CHADEMA ni kiwanda Cha kutengeneza wanasiasa. Mpaka CCM walienda kununua huko baada ya kuona kwao ni magalasa. Keep it up CHADEMA.
Walikuwa hukohuko NCCR kabla ya kwenda CHADEMA.
Sasa wamerudi nyumbani
 
I remember those days.
Mzee Mrema alikuwapo.Walizichapa wakatoana na ngeu.Maberu Marandu alijificha chini ya meza kuokoa nafsi yake.
Hizi kazi zinafanywa na vyombo vya dola kwa gharama ya kodi zetu,kufarakanisha Wapinzani ndiyo fani yao.
 
Mjumbe wa Halmashauri Kuu na Mwenyekiti wa azimio hilo, Joseph Selasini alisema pamoja na kusimamishwa kwa viongozi hao pia wamelivunja Baraza la Wadhamini la NCCR na kuteua wajumbe wapya ambao watasajiliwa kwa mujibu wa taratibu zitakazowekwa.

Naibu Msajili wa Vyama vya Siasa Nchini, Sisty Nyahoza naye alikiri kupokea barua kutoka NCCR-Mageuzi kuwa kuna mabadiliko ya wajumbe wa bodi ya wadhami.
Selasini ni muhuni na ndiyo maana CDM walimshtukia mapemaa !!
 
Umri wote huo, umepoteza tu muda wako?

Vineno viwili, vitatu, tena visivyoongeza lolote katika unayochangia?

Si ajabu hata nyumbani upo hivi hivi, na wanao na mke walishazoea kutopata lolote la maana kutoka kwako!

Hopeless Kabisa.

Usinilaumu kwa lugha hii, lakini ukweli ni kwamba inaudhi kuwa na watu wa aina yako karibu.
Umeshafura!
 
Kweli kabisa. Si vijana wengi humu wanayoyaelewa hayo. Ndipo nadhani likazaliwa jina "mageuzi" mbele ya NCCR.

Yanajirudia tu. Yanyojitokeza hivi sasa huko NCCR yanathibitisha methali ya Kiswahili "Mtoto umleavyo ndivyo akuavyo".
NCCR Mageuzi haikuanzishwa kama chama cha siasa bali lilikuwa kundi la wanaharakati waliokuwa wanadai kuanzishwa kwa mfumo wa vyama vingi vya siasa. Kama kumbukumbu zangu ni sahihi katibu mkuu wake alikuwa Mabere Marando.

Baada ya mfumo wa vyama vingi vya siasa kuruhusiwa ndipo kikajibadilisha kuwa chama cha siasa na Mzee Lyatonga Mrema alijiunga nacho baada ya kujiuzulu uwaziri. Lyatonga Mrema alichaguliwa kuwa Mwenyekiti wa NCCR na baadaye kugombea urais akiwa na Mkapa wa CCM, Mzee Mapesa wa UDP nk.
 
Back
Top Bottom