Mgogoro NCCR Mageuzi: Timu Mbatia wachukua ofisi, wasema umefanyika uhaini ndani ya chama, Mbatia bado ni mwenyekiti

Mgogoro NCCR Mageuzi: Timu Mbatia wachukua ofisi, wasema umefanyika uhaini ndani ya chama, Mbatia bado ni mwenyekiti

Umeshafura!
Hiyo CCM ya watu wa aina yako mnaidhalilisha sana. Hicho chama kilikuwa ni chama chenye heshima kubwa sana duniani, mmekigeuza kuwa dimbwi la uchafu kwa watu wa aina yako kuwa ndio wenye sauti huko.
Iliyobaki ni vimipasho tu, hakuna lolote la maana linaloweza kujadiliwa huko. Halafu unaleta tabia hiyo hiyo hadi hapa ukumbini!
 
Hiyo CCM ya watu wa aina yako mnaidhalilisha sana. Hicho chama kilikuwa ni chama chenye heshima kubwa sana duniani, mmekigeuza kuwa dimbwi la uchafu kwa watu wa aina yako kuwa ndio wenye sauti huko.
Iliyobaki ni vimipasho tu, hakuna lolote la maana linaloweza kujadiliwa huko. Halafu unaleta tabia hiyo hiyo hadi hapa ukumbini!
Umejideula!
 

Katibu wa Itikadi na Uenezi wa NCCR-Mageuzi, Edward Simbeye amezungumza na waandishi wa habari leo Mei 21, 2022 na kudai kuwa kilichofanywa na kundi lililojipa sura ya Halmashauri Kuu ndani ya chama hicho mapema leo ni uhaini.

Awali ilitolewa taarifa kuwa Halmashauri Kuu ya Chama cha NCCR-Mageuzi imemsimamisha Mwenyekiti wa chama hicho, James Mbatia na Makamu Mwenyekiti Bara, Angelina Mtahiwa kutojihusisha na shughuli zozote za chama hadi Mkutano Mkuu utakapoitishwa ili wajieleze kuhusiana na tuhuma inazowakubali.

Mjumbe wa Halmashauri Kuu na Mwenyekiti wa azimio hilo, Joseph Selasini alisema pamoja na kusimamishwa kwa viongozi hao pia wamelivunja Baraza la Wadhamini la NCCR na kuteua wajumbe wapya ambao watasajiliwa kwa mujibu wa taratibu zitakazowekwa.

Naibu Msajili wa Vyama vya Siasa Nchini, Sisty Nyahoza naye alikiri kupokea barua kutoka NCCR-Mageuzi kuwa kuna mabadiliko ya wajumbe wa bodi ya wadhami.

Baada ya tamko hilo ndipo muda mfupi baadaye Katibu Mkuu wa NCCR-Mageuzi, Martha Chiomba, alifunga ofisi za chama hicho zilizopo Ilala, Dar es Salaam, ili kumzuia James Mbatia.

Baada ya tukio hilo, wanachama wanaomuunga mkono Mbatia ndani ya chama hicho walifika ofisini hapo na kufanikiwa kuingia ndani kisha kuzungumza na Wanahabari wakisema waliotangaza kumsimamisha Mbatia hawana mamlaka n ahata akidi haikutimia.

Katibu wa Itikadi na Uenezi wa NCCR-Mageuzi, Edward Simbeye amesema:

“Kilichofanyika ni uhaini na uhuni ndani ya chama na hatuwezi kukubali kilichofanyika, chama kitakaa na kufanya maamuzi, kinachotusikitisha zaidi Msajili wa Vyama vya Siasa ameshiriki katika uhuni huu.

“Huwezi kuvunja Bodi ya Wadhamini au kumsimamisha Mwenyekiti kihuni.

“Msajili haoni hata haya, alijulishwa aliyekuwa Katibu Mkuu amesimamishwa inakuaje anapokea maamuzi yanayofanywa na watu kama hao.

“Sisty Nyahoza ndiye anaendesha haya makundi, anafadhili haya makundi na tuna uhakika, ukifika wakati tutaweka ushahidi hadharani. Huyu ndiye mhuni wa kwanza katika huu mchezo mchezo mchafu.

“Huyo aliyeitwa Katibu Mkuu (Martha Chiomba) alisimamishwa katika Kikao cha Kamati Kuu, anayekaimu ni Anthony Kom hakushiriki kwenye hicho kikao na hajui kama kuna hicho kikao walichofanya.

“Hao Wahuni walikuja kujaribu kufunga ofisi lakini tumewadhibiti na ndio maana tupo ofisini hapa, ofisi ipo chini ya wanachama. Tutaudhibiti uhuni wao, tumejipanga na tupo imara, hakuna ambaye ataweza kuivuruga NCCR Mageuzi.”


Pia Soma > NCCR Mageuzi yamsimamisha James Mbatia kufanya shughuli za Chama
haya sasa ndo vyama tulivyovitegemea vituvushe unadhani kwa hali hii tutavushwa na hivi vyama au tutafute mbadala?je kwa kuendekeza hizo vurugu wananchi kweli watavielewa?shida ni kuwa viongozi wengi kama siyo wote wanafikiri kuwa wananchi hawaelewi lolote kuhusu haya yanayoendelea katika vyama.inapofikia wakati wananchi kuchukua maamuzi juu yao kwenye box la kura wanaanza kuwalaumu kuwa kura zinaibiwa sivyo haziibiwi bali wananchi hawataki malumbano kwa hayo hayana tija kabisa.mwananchi anataka kuona maisha yake yanabadilika,anaishi na kula vzr,huduma muhimu za kijamii anazipata bila kero,vijiji kuna umeme na maji ya kutosha,barabara nzuri na zinapitika wakati wote,bei za mazao ziwe na tija,anapata fursa ya kuchagua wapi anauza mazo yake kwa bei anayotaka na si kupangiwa bila ya bughuza nk.lkn vurugu kwenye vyama kwa mwananchi hayo kwake si tija.
 
Ni kwanini hatutaki kujenga DEMOKRASIA yenye TAASISI imara na endelevu?
Ukiangalia CCM tangia uhuru hawaanini kama wakishindwa uchaguzi chama kingine kinaweza kutawala;

CHADEMA Mwenyekiti kashikilia madaraka tangu enzi hizo mpaka leo;

NCCR Mageuzi Mbatia tangia nikiwa mdogo hatoki kwenye hicho kiti,;

CUF Lipumba baada ya kukisambaratisha chama mwendo ni sifasifa zisizoeleweka!;

ACT ya Zitto nayo haieleweki maana kimekuwa chama cha kutunga uongo na mwelekeo wa kujenga chama na kukikomaza haupo!;

TLP Mrema aliiacha hoi kabisa, haijulikani kama hiki chama kipo Dunia hii;

ADC ya Limbu nayo sijui ilitokomea shimo gani!;

Mzee wa kubeba HOTPOT na MASAHANI ya ubwabwa kabaki kuongea upupu na na lawama tele bila kuendeleza chama chake;!

Nchi yetu imekumbwa na wasomi wa kusaka vyeo kwa kusifiasifia viongozi ili wapate vyeo au nafasi mbalimbali kwenye taasisi!
 
Wenyeviti wa hizi SACCOS kutoka Kaskazini wameona kama uenyekiti ni haki zao,Mbatia pamoja na Mbowe ni wenyeviti kwa muda mrefu hawana tofauti na raisi wa Uganda M7, hawa hawa ndio wanatoa mapovu majukwaani kudai demokrasia na katiba mpya wakati kwenye vyama vyao hakuna demokrasia wala mabadiliko ya katiba,ninachojiuliza wanang'ania uongozi kwa maslahi yapi? sio bure haiwezekani mtu miaka 20 baado upo palepale sijui wakipewa uraisi si ndio watajimilikisha nchi, wachaga acheni hizo bana, kuna maisha nje ya siasa na uenyekiti.
Kwani kiongozi wa mapinduzi bwana serasini ni mtu wa wapi mkuu!?
 
Hahahahaha.

Hiki kisa kimenikumbusha zamani sana, NCCR yanajirudia tu. Yalitokea kama hayo huko Tanga kwenye mkutano wao wakazichapa, enzi za mwanzo mwanzo, nadhani walikuwa kina marehem Kassim Maguto. Mbatia siku hizo hata hajulikani kabisa, sijui kama alikuwa hata kishajiunga NCCR , mtanikumbusha wajuzi. Zilichapwa huko mpaka dola likaingilia kati.

Vijana wengi hawatalielewa jina hilo. Ni muda mrefu sasa.
Faiza,nimeenda google kusearch jina la Kassim Maguto nilichoambulia ni hii post yako. Naomba kumfahamu huyu mtu kwa chochote unachojua. Maguto alikuwa jirani yetu wakati nipo Mdogo,alikuwa rafiki wa Baba angu. Alipenda sana watoto na mimi alinipenda Haswa.

Leo nimemkumbuka Maguto,najua alikuwa kwenye Siasa,najua alikuwa NCCR MAGEUZI lakini sijui alikuwa nani haswa. Alikuwa akirudi toka safari zake anaweka mlima wa pipi na zawadi kedekede alafu watoto wote mtaani wanapanga foleni kupokea zawadi. Nimemkumbuka mke wake Bi mjumbe.
 
Faiza,nimeenda google kusearch jina la Kassim Maguto nilichoambulia ni hii post yako. Naomba kumfahamu huyu mtu kwa chochote unachojua. Maguto alikuwa jirani yetu wakati nipo Mdogo,alikuwa rafiki wa Baba angu. Alipenda sana watoto na mimi alinipenda Haswa.

Leo nimemkumbuka Maguto,najua alikuwa kwenye Siasa,najua alikuwa NCCR MAGEUZI lakini sijui alikuwa nani haswa. Alikuwa akirudi toka safari zake anaweka mlima wa pipi na zawadi kedekede alafu watoto wote mtaani wanapanga foleni kupokea zawadi. Nimemkumbuka mke wake Bi mjumbe.
Maguto akija Dar, stop ya kwanza ni njumbani kwetu Kariakoo, hapo ilikuwa station yake ya kuanza mishe zingine na kuja kula mchana na usiku. Alikuwa na family friend.

Maguto alikuwa mdhamini wa NCCR. Siyajuwi sana maisha yake kisiasa isipokuwa nafahamu kuwa alikuwa ni UWT mwenye heshima kubwa sana Ikulu na nafahamu kuwa alikuwa ndiyo mtu pekee kwa heshima yake ya kustaafu (kama UWT wanastaafu} aliyepewa ulaji mrefu sana na Ikulu, alikuwa na kibali cha kuwezesha kusafirisha chuma chakavu nje ya nchi.

Ukiona au ukimsikia tajiri yoyote kasafirisha chuma chakavu nje ya nchi, ujuwe ni kwa kibali cha Kassim Maguto. Mume wangu akifanya biashara hiyo ya chuma chakavu ndiyo wakashikana sana kama chanda na pete.

Biashara nyingine aliyokuwa akiifanya Kassim Maguto ni ya kufuga nyoka na kuuza sumu za nyoka nje ya Tanzania. Alikuwa kila akiniona ananambia tafuta soko Canada, ni utajiri huu. Yeye alikuwa anauza Afrika Kusini tu na wao Afrika Kusini ndiyo walikuwa wanasafirisha tena nchi zingine.

Hayo kwa uchache.

Nafahamiana nae kama Family friend siyo kama mwana siasa.
 
Maguto akija Dar, syop ya kwanza ni njumbani kwetu Kariakoo, hapo ilikuwa station yake ya kuanza mishe zingine na kuja kula mchana na usiku. Alikuwa na family friend.

Maguto alikuwa mdhamini wa NCCR. Siyajuwi sana maisha yake kisiasa isipokuwa nafahamu kuwa alikuwa ni UWT mwenye heshima kubwa sana Ikulu na nafahamu kuwa alikuwa ndiyo mtu pekee kwa heshima yake ya kustaafu (kama UWT wanastaafu} aliyepewa ulaji mrefu sana na Ikulu, alikuwa na kibali cha kuwezesha kusafirisha chuma chakavu nje ya nchi.

Ukiona au ukimsikia tajiri yoyote kasafirisha chuma chakavu nje ya nchi, ujuwe ni kwa kibali cha Kassim Maguto. Mume wangu akifanya biashara hiyo ya chuma chakavu ndiyo wakashikana sana kama chanda na pete.

Biashara nyingine aliyokuwa akiifanya Kassim Maguto ni ya kufuga nyoka na kuuza sumu za nyoka nje ya Tanzania. Alikuwa kila akiniona ananambia tafuta soko Canada, ni utajiri huu. Yeye alikuwa anauza Afrika Kusini tu na wao Afrika Kusini ndiyo walikuwa wanasafirisha tena nchi zingine.

Hayo kwa uchache.

Nafahamiana nae kama Family friend siyo kama mwana siasa.
Asante sana,Mie alikuwa jirani yangu huko Mlandizi,kwa namna nilivyomuona na kumbukumbu nilizonazo sikumuona sana kama mwanasiasa,sio hizi type za kina Tundu Lisu.
Hivi Umenisaidia kujua kumbe alikuwa ni mdhamini wa Chama.Kwenye msiba wake nakumbuka Mbatia alikuja. Kuhusu Biashara wala UWT hakuna nalolijua,ila nina hakika kipindi cha mwisho cha uhai wake hakuwa vizuri kiuchumi,aliyumba. Zile zawadi za utotoni ziliisha.
Utakuwa unawajua watoto wake kina Farhad na Jamila?
Hivi sasa ninamuwaza nimekumbuka jambo,aliwahi kuniambia nikipata pesa Starehe zipo Hong Kong. Asante kwa kumbukumbu nzuri,haya nayokwambia hapa ni mambo nipo nasoma Shule ya Msingi miaka ya 2000,ndio nagundua nilipaswa nikupe Shikamoo.
 
Asante sana,Mie alikuwa jirani yangu huko Mlandizi,kwa namna nilivyomuona na kumbukumbu nilizonazo sikumuona sana kama mwanasiasa,sio hizi type za kina Tundu Lisu.
Hivi Umenisaidia kujua kumbe alikuwa ni mdhamini wa Chama.Kwenye msiba wake nakumbuka Mbatia alikuja. Kuhusu Biashara wala UWT hakuna nalolijua,ila nina hakika kipindi cha mwisho cha uhai wake hakuwa vizuri kiuchumi,aliyumba. Zile zawadi za utotoni ziliisha.
Utakuwa unawajua watoto wake kina Farhad na Jamila?
Hivi sasa ninamuwaza nimekumbuka jambo,aliwahi kuniambia nikipata pesa Starehe zipo Hong Kong. Asante kwa kumbukumbu nzuri,haya nayokwambia hapa ni mambo nipo nasoma Shule ya Msingi miaka ya 2000,ndio nagundua nilipaswa nikupe Shikamoo.
Pesa alikuwa nazo mpaka uzeeni, lakini ni mzee mwenye hakima sana, alikuwa hajioneshi kabisa. Kazi hizo nazokwambia ni baada ya kustaafu, uzeeni ndio kapewa kama zawadi.

Yule na katika kitengo cha mwanzo cha ujasusi kilichoingia Uganda wakati wa Idia Amin, kabla hata ya vita kuanza yeye yupo Uganda anafanya mamboi chini kwa chini.

Yule siyo mdhamini tu, ndiyo waanzilishi wa NCCR, vyma hivi vyote vya siasa vilianzishwa na watu wa Ikulu, asikudanganye mgtu, hakuna upinzani Tanzania.

Ukiigeuka system ndiyo yanakupata ya kina Tundu Lissu na wengne walioyeyuka tu.
 
Back
Top Bottom