Mgogoro wa ndoa ya Dkt. Mwaka na mkewe kufikishwa Mahakamani

Mgogoro wa ndoa ya Dkt. Mwaka na mkewe kufikishwa Mahakamani

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2022
Posts
2,780
Reaction score
6,607
Sakata la ndoa ya mtaalamu wa tiba mbadala, Juma Mwaka maarufu Dk Mwaka na mkewe Queen Masanja, limechukua sura mpya baada ya shauri hilo kutua kwa wanasheria ambao wamepanga kulipeleka mahakamani.

Shauri hilo tayari limepita kwenye Baraza la Usuluhishi chini ya Ustawi wa Jamii na wakati wowote linatarajiwa kupelekwa mahakamani katika Kituo Jumuishi cha masuala ya familia Temeke, Dar es Salaam.

Akizungumza na HabariLEO kwa njia ya simu, Mwanasheria wa Queen, Zakia Msangi alisema shauri hilo liliondolewa katika Baraza la Kiislamu Tanzania (BAKWATA) na kulipeleka katika taasisi zinazosimamia masuala ya sheria. Msangi alisema mamlaka waliyopewa Bakwata ndio hayo hayo waliyopewa ustawi wa jamii ambao wana jukumu la kuwasikiliza wanandoa na kujaribu kusuluhisha.

Alisema wanandoa hao (Dk Mwaka na Queen) hawakuonesha kurudiana hivyo wamepewa fomu namba tatu kuashiria kwamba usuluhishi umekwama hivyo shauri lipelekwe mahakamani.


Chanzo: HabariLEO
 
Sakata la ndoa ya mtaalamu wa tiba mbadala, Juma Mwaka maarufu Dk Mwaka na mkewe Queen Masanja, limechukua sura mpya baada ya shauri hilo kutua kwa wanasheria ambao wamepanga kulipeleka mahakamani.

Shauri hilo tayari limepita kwenye Baraza la Usuluhishi chini ya Ustawi wa Jamii na wakati wowote linatarajiwa kupelekwa mahakamani katika Kituo Jumuishi cha masuala ya familia Temeke, Dar es Salaam.

Akizungumza na HabariLEO kwa njia ya simu, Mwanasheria wa Queen, Zakia Msangi alisema shauri hilo liliondolewa katika Baraza la Kiislamu Tanzania (BAKWATA) na kulipeleka katika taasisi zinazosimamia masuala ya sheria. Msangi alisema mamlaka waliyopewa Bakwata ndio hayo hayo waliyopewa ustawi wa jamii ambao wana jukumu la kuwasikiliza wanandoa na kujaribu kusuluhisha.

Alisema wanandoa hao (Dk Mwaka na Queen) hawakuonesha kurudiana hivyo wamepewa fomu namba tatu kuashiria kwamba usuluhishi umekwama hivyo shauri lipelekwe mahakamani.


Chanzo: HabariLEO
Wengi wanawake hudhani wakienda bakwata kuachana tu kumbe la tatizo kubwa hasa la baadhi ya wanawake wa kiisilamu hawako tayari kufuata mshariti ya ndoa, masharti hayo wao hudhani yanawabana
 
NA HUKO NDIKO MWANAMKE ATAKWENDA KUSHINDWA KAMA WASHINDWAVYO WALIO WENGI.
MAHAKAMA INAFANYA KAZI ZAKE KWA USHAHIDI, SIO HISIA NA MIHEMUKO.
WANAWAKE WENGI WANAFIKIRI UWEZO WAO WA KUONGEA AU KULIA UNATOSHA KUFANYA USHAWISHI MAHAKAMANI.
MSIJE SEMA MWANAUME KATOA HIKI AU KILE KUPATA UPENDELEO,
 
NA HUKO NDIKO MWANAMKE ATAKWENDA KUSHINDWA KAMA WASHINDWAVYO WALIO WENGI.
MAHAKAMA INAFANYA KAZI ZAKE KWA USHAHIDI,SIO HISIA NA MIHEMUKO.
WANAWAKE WENGI WANAFIKIRI UWEZO WAO WA KUONGEA AU KULIA UNATOSHA KUFANYA USHAWISHI MAHAKAMANI.
MSIJE SEMA MWANAUME KATOA HIKI AU KILE KUPATA UPENDELEO,
Na mwandiko wako mkubwa, Kama vile imeandikwa cha maana kumbe Hamna. Kwa taarifa Yako ndoa ikipita kwenye usuluhishi ikashindkana mahakamani inaenda kuvunjwa tu.. kupata hati ya kisheria ya kuachana.. hasa siku hizi mambo ya feminism yalivyo.. hapo wanaenda kutalikiana rasmii. Na hapo mwanamke ndo anatoa talaka
 
NA HUKO NDIKO MWANAMKE ATAKWENDA KUSHINDWA KAMA WASHINDWAVYO WALIO WENGI.
MAHAKAMA INAFANYA KAZI ZAKE KWA USHAHIDI,SIO HISIA NA MIHEMUKO.
WANAWAKE WENGI WANAFIKIRI UWEZO WAO WA KUONGEA AU KULIA UNATOSHA KUFANYA USHAWISHI MAHAKAMANI.
MSIJE SEMA MWANAUME KATOA HIKI AU KILE KUPATA UPENDELEO,
Hawezi kushindwa. Ndoa hakuna tena pale.
 
Kwahiyo Bakwata wameshindwa kutatua hili suala?
 
wengi wawanawake udhani wakienda bakwata kuachana tu kumbe la tatizo kubwa hasa la baadi ya wanawake wa kiisilamu hawako tayali kufuata mshariti ya ndoa masariti hayo wao udhani yanawabana
Ondoa neno hudhani; huo ndio ukweli. Dunia imebadilika; dunia ni kijiji; yanayotokea kwingineko dunia yanaifikia jamii kwa kasi ya mwanga. It is like this; you can't fool all people all time. Kuna siku wataamka tu penda usipende.
 
Na mwandiko wako mkubwa, Kama vile imeandikwa cha maana kumbe Hamna. Kwa taarifa Yako ndoa ikipita kwenye usuluhishi ikashindkana mahakamani inaenda kuvunjwa tu.. kupata hati ya kisheria ya kuachana.. hasa siku hiz mambo ya feminism yalivyo.. hpo wanaenda kutalikiana rasmii. Na hapo mwanamke ndo anatoa talaka
You are absolutely right! Kama imeshindikana kwa level ya mabingwa wa usuluhishi wa masuala ya ndoa, mahakama has nothing to do zaidi ya ku-endorse kuhitimisha ndoa ili kukamilisha sheria inavyotaka. That's it!
 
NA HUKO NDIKO MWANAMKE ATAKWENDA KUSHINDWA KAMA WASHINDWAVYO WALIO WENGI.
MAHAKAMA INAFANYA KAZI ZAKE KWA USHAHIDI,SIO HISIA NA MIHEMUKO.
WANAWAKE WENGI WANAFIKIRI UWEZO WAO WA KUONGEA AU KULIA UNATOSHA KUFANYA USHAWISHI MAHAKAMANI.
MSIJE SEMA MWANAUME KATOA HIKI AU KILE KUPATA UPENDELEO,
Au kinyume chake pia inawezekana
 
Nyie mashoga tumewastukieni na Kampeni yenu chafu.Ndugu mwana JF ukikutana na hiyo sloga tambua imeletwa na Shoga

Everything Everywhere Wrong With Everything Everywhere All at Once All At Once

 
Hapa Qadhi bingwa wa masuala ya ndoa na mirathi kakwama! Wanaenda kwenye mabaraza ya kisekula.
Hapo nadhani sasa mgao utapita ipasavyo jambo ambalo huyo jamaa hataki kulisikia
Mahakamani inakua ngumu kulazimisha kwamba unampenda mkeo ikiwa mmetengana. Ndoa haitaki ulaghai na ubabe ingawa watu wengi hawaliafiki hili
 
Hapo nadhani sasa mgao utapita ipasavyo jambo ambalo huyo jamaa hataki kulisikia
Mahakamani inakua ngumu kulazimisha kwamba unampenda mkeo ikiwa mmetengana. Ndoa haitaki ulaghai na ubabe ingawa watu wengi hawaliafiki hili
Ni jukumu la kila upande kuishawishi mahakama kwa vielelezo visivyo na shaka kwanini upande mwingine unastahili/haustahili sehemu ya mgao. Hapo ndipo shughuli ilipo.
 
Back
Top Bottom