Uchaguzi 2020 Mgombea Urais wa chama kimoja aweza muunga mkono mgombea urais wa chama kingine tofauti bila ridhaa ya Mkutano Mkuu wa chama chake?

Uchaguzi 2020 Mgombea Urais wa chama kimoja aweza muunga mkono mgombea urais wa chama kingine tofauti bila ridhaa ya Mkutano Mkuu wa chama chake?

YEHODAYA

JF-Expert Member
Joined
Aug 9, 2015
Posts
36,902
Reaction score
52,001
Kuna maajabu yanayovunja katiba za vyama kwenye uchaguzi huu mkuu.

Tumeona Lisu Makamu mwenyekiti taifa wa CHADEMA na mgombea uraisi kupitia Chadema akitoa tamko kuwa anamuunga mkono Mgombea uraisi wa Zanzibar Maalim Seif wa Act wazalendo.

Pia tumeona Maalim SEIF Mwenyekiti wwa ACT wazalendo taifa akimuunga mkono Tundu Lissu.

Sina shida na kuungana mikono hata kuungana miguu ruksa.

Ninachohoji kwa mujibu wa katiba za vyama vyao hayo maamuzi yalitakiwa kufanywa na kamati kuu na mikutano mikuu yao sio wao kujiamulia kwenye majukwaa!

Ninaomba ufafanuzi kuhusu hili kutoka kwa wataalamu wa sheria na katiba liko sahihi? kama haliko sahihi nini kinatakiwa kufanyika?
Kwa mfano Membe ni Mgombea uraisi wa ACT wazalendo aliyepitishwa na vikao halali kuanzia kamati kuu hadi mkutano mkuu. Na kapoteza pesa zake za kuchukua fomu na gharama za kuzunguka nchi nzima kutafuta wadhamini na akaanza kugharimia kampeni zake leo mwenyekiti wa ACT-Wazalendo Maalim Seif anasema hamtambui anamtambua Lissu.

Pia upande wa Zanzibar kuna mgombea uraisi kupitia Chadema Vikao vya chama vya kamati kuu na mkutano mkuu walimptisha Said Issa Mohamed kuwa mgombea uraisi wa Zanzibar kaingia gharama za kuchukua fomu na kuzunguka nchi nzima ya zanzibar kutafuta wadhamini leo Makamu mwenyekiti wa Chadema Taifa Tundu LIsu anasema hamtambui anamtambua Maalim Seif wa ACT wazalendo kinyume cha katiba ya chadema na maamuzi ya kamati kuu na mkutano mkuu wa Chadema.
 
Ukisikia udikteta ndio huu sasa.

Kwa mujibu wa katiba za Chadema na ACT - Wazalendo maamuzi yote makubwa na muhimu yanatolewa na vikao halali vya chama kama kamati kuu, halmashauri kuu, mkutano mkuu nk.

Kitendo cha Tundu Lisu kusimama jukwaani na kutangaza kumuunga mkono maalim Seif huko Zanzibar na Zitto Kabwe kule Kigoma ni uvunjifu wa katiba ya Chadema.

Kadhalika Maalim Seif kutangaza kumuunga mkono Tundu Lisu ilhali mgombea halali wa ACT - Wazalendo ni Bernad Membe nao ni udikteta na dharau.

Natoa tu angalizo kwa wapiga kura mkiwachagua hawa yawezekana kabisa tukawa tumeukaribisha udikteta nchini kitu kinachoweza kuliangamiza taifa siku za usoni.

Mtu asiyeheshimu katiba ya chama chake hataiheshimu katiba ya nchi na hizo ndio sifa za madikteta huko duniani.

Nawatakia Tuesday yenye baraka.

Maendeleo hayana vyama!
 
mmepata pa kukojolea sio. hili litakaa sawa, jadilini maendeleo ya nchi
 
We yanakuhusu nini ?? Ya mwenyekiti wenu mbona hamuyaonii ??
 
Mkuu tulia hivyohivyo, naleo kwa taarifa yako Zitto atakua Tabora kusafisha uchafu aliotema jana POMBE, tunaomba muwe wavumilivu maana mmetutesa miaka 5, sisi tumeanza kupiga sindano hata miezi 2 bado mnaanza kulia, tulieni kabisa msipige kelele, NEC&CCM walijifanya wajanja kwa sheria zao uchwara ili ACT&CDM wasiungane, sasa tunawaonyesha nini maana ya akili kubwa.
 
Ukisikia udikteta ndio huu sasa.

Kwa mujibu wa katiba za Chadema na ACT - Wazalendo maamuzi yote makubwa na muhimu yanatolewa na vikao halali vya chama kama kamati kuu, halmashauri kuu, mkutano mkuu nk...
Umenena vyema mkuu.

Ila wafuasi wa Mbowe ni ngumu kukuelewa! Wapo kiushabiki hawataki kuaangalia reality.
 
Ukisikia udikteta ndio huu sasa.

Kwa mujibu wa katiba za Chadema na ACT - Wazalendo maamuzi yote makubwa na muhimu yanatolewa na vikao halali vya chama kama kamati kuu, halmashauri kuu, mkutano mkuu nk...
Umeshawahi kumkemea Meko kwa udikteta wake?

Siasa ni sayansi bwashee na maendeleo yana vyama, just relax!
 
Back
Top Bottom