HIMARS
JF-Expert Member
- Jan 23, 2012
- 70,791
- 98,334
Baada ya kutangaza kugoma kufungua maduka yao wiki iliyopita, hatimaye Kariakoo ikasimama.
Mkuu wa Mkoa akaenda, akashindwa wafanyabiashara wakamtaka Rais, Ripoti ikatoka kutoka Dodoma kuwa Mkutano utafanyika Dodoma siku ya Alhamis, chini ya Waziri Mkuu, wafanyabiashara wakagoma.
Likatoka tamko kuwa Jumatano watakutana Ofisi ya Waziri Mkuu, wakagoma Waziri Mkuu akaenda Kariakoo, akaongea nao ila hawakuelewana. Jumanne mgomo ukaendelea kama kawaida.
Polisi wakapewa majina ya watu kuwa ndo wanaoshinikiza, watu hao wakaitwa Msimbazi kutoa maelezo.
Leo mkutano ukawa ufanyika kati ya Viongozi wa Wafanyabiashara na Serikali Anatouglu, wafanyabiashara wakaugomea kwamba hawaamini viongozi wao wanataka wao wenyewe watoe maoni yao.
Pametokea mvutano ila mwisho Serikali imekubali kupeleka Kikao cha Wazi Mnazi Mmoja. Wafanyabiashara wameonesha umoja na wameweza.
Kamwe msikubali maoni yenu yapelekwe kifichoni na watu wachache.
Mkuu wa Mkoa akaenda, akashindwa wafanyabiashara wakamtaka Rais, Ripoti ikatoka kutoka Dodoma kuwa Mkutano utafanyika Dodoma siku ya Alhamis, chini ya Waziri Mkuu, wafanyabiashara wakagoma.
Likatoka tamko kuwa Jumatano watakutana Ofisi ya Waziri Mkuu, wakagoma Waziri Mkuu akaenda Kariakoo, akaongea nao ila hawakuelewana. Jumanne mgomo ukaendelea kama kawaida.
Polisi wakapewa majina ya watu kuwa ndo wanaoshinikiza, watu hao wakaitwa Msimbazi kutoa maelezo.
Leo mkutano ukawa ufanyika kati ya Viongozi wa Wafanyabiashara na Serikali Anatouglu, wafanyabiashara wakaugomea kwamba hawaamini viongozi wao wanataka wao wenyewe watoe maoni yao.
Pametokea mvutano ila mwisho Serikali imekubali kupeleka Kikao cha Wazi Mnazi Mmoja. Wafanyabiashara wameonesha umoja na wameweza.
Kamwe msikubali maoni yenu yapelekwe kifichoni na watu wachache.