Vin Diesel
JF-Expert Member
- Mar 1, 2011
- 9,088
- 6,384
Wakigoma Mkuu wa Mkoa wa dar ataenda kuongea nao na watarudi barabarani....mmesahau mara hii?
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Nimemisskusikia habari za migomo.Wakuu habari
Habari za kuaminika za kutoka chanzo changu ninachokiamini kabisa zinanitaarifu niwaambie wale wanaotaka kusafiri siku hizi za karibuni wajiandae haswa
Madereva wote wa mabus wa Tanzania nzima kwa umoja wao wameadhimia kugoma kutoa huduma hiyo muda wowote kuanzia sasa (hapa sitasema siku)
Lengo kubwa la mgomo huu ni kutokana na kauli tata zinazopishana zinazotolewa na vyombo vinavyosimamia usalama wa barabarani,ambapo baadhi ya kauli ya viongozi wa usalama zimekuwa zikipishana kila kukicha
siku chache zilizopita alisikika afisa mmoja mkubwa wa jeshi la polis kitengk cha usalama barabarani akitumia vyombo vya habari akiweka katazo kuwa gari halitakiwi kusimama kwenye zebra endapo hakuna mtu bali lipunguze mwendo tu na ukisimama bila kuwepo mtu kwenye kivuko utakuwa umetenda kosa na utawajibishwa
Afisa wa pili mwingine wa juu kabisa alitumia vyombo vya habari kuwaonya madereva wasiosimama kwenye zebra hata kama hakuna mtu.Jambo lilozua utata mkubwa kwani madereva hawajui wafuate kauli ipi
kauli iliyoleta hasira zaidi ni hivi juzi ambapo kiongozi mwingine alinukuliwa akisema "madereva wanapaswa kuogopa kama shetani au kama simba"
Hayo ni baadhi yatakayopelekea kuanza mgomo huu mkubwa kabisa licha ya kuwa yapo mengi pamoja na yale ya kukosekana alama za barabarani na ubovu wa barabara huku lawama zote zikielekezwa kwa madereva pindi ajali zinapotokea
Narudia tena wasafiri wajiandae kisaikolojia
Na hiyo itakuwa ni kinyume cha sheria,Yaani nisimame kwenye zebra bila ya kuwa na mtu, tunafanyana machizi?
Mbona sababu za kijinga sana.
Sheria inasemaje?
Wakuu habari
Habari za kuaminika za kutoka chanzo changu ninachokiamini kabisa zinanitaarifu niwaambie wale wanaotaka kusafiri siku hizi za karibuni wajiandae haswa
Madereva wote wa mabus wa Tanzania nzima kwa umoja wao wameadhimia kugoma kutoa huduma hiyo muda wowote kuanzia sasa (hapa sitasema siku)
Lengo kubwa la mgomo huu ni kutokana na kauli tata zinazopishana zinazotolewa na vyombo vinavyosimamia usalama wa barabarani,ambapo baadhi ya kauli ya viongozi wa usalama zimekuwa zikipishana kila kukicha
siku chache zilizopita alisikika afisa mmoja mkubwa wa jeshi la polis kitengk cha usalama barabarani akitumia vyombo vya habari akiweka katazo kuwa gari halitakiwi kusimama kwenye zebra endapo hakuna mtu bali lipunguze mwendo tu na ukisimama bila kuwepo mtu kwenye kivuko utakuwa umetenda kosa na utawajibishwa
Afisa wa pili mwingine wa juu kabisa alitumia vyombo vya habari kuwaonya madereva wasiosimama kwenye zebra hata kama hakuna mtu.Jambo lilozua utata mkubwa kwani madereva hawajui wafuate kauli ipi
kauli iliyoleta hasira zaidi ni hivi juzi ambapo kiongozi mwingine alinukuliwa akisema "madereva wanapaswa kuogopa kama shetani au kama simba"
Hayo ni baadhi yatakayopelekea kuanza mgomo huu mkubwa kabisa licha ya kuwa yapo mengi pamoja na yale ya kukosekana alama za barabarani na ubovu wa barabara huku lawama zote zikielekezwa kwa madereva pindi ajali zinapotokea
Narudia tena wasafiri wajiandae kisaikolojia
kwa awamu hii unapoint kubwa mkuu, tutasafiri hata kwa makarandingaMakampuni yatakayo goma yatafutiwa leseni, gari za jeshi zitaingia kazini
Hebu tukumbushe mumu ilikuaje hiyo mei12011?Mmh,isije kuwa kama ya mei 1/2011...
hii point sana ama kwa hakika unasafiri mara kwa maraKusema ukweli hiki chombo cha usalama barabarani kimekuwa kero na sasa hakijulikani kinafanya kazi gani, kuna mengi ya kujiuliza je haya matamko yanalenga kuwachanganya madereva ili askari wapate kuchukua rushwa kwa wingi zaidi au wanalenga kulinda usalama wa watumiaji wa barabara na vyombo vya moto.
Ukitazama kwa makini, utagundua wengi wa askari wa kikosi hicho wapo kifedha zaidi na siyo kazi, nitatoa mfano mmoja kati ya mingi inayoonekana wazi ambayo vyombo vya uchunguzi vinaweza kufanyia kazi na kuja na majibu.
Ukiwa kwenye bus linaloanza safari kwenye terminal, (mathalani UBT) anakuja askari anatangaza kufunga mikanda, bus linaondoka na abiria waliokaa kwenye viti tu, bus likifika nje linaongeza abiria kama kumi wanakaa kwenye mfuniko wa injini na wengine kusimama mlangoni, bus hilo litakwenda mpaka karibu na mpaka wa Dar na Pwani kabla ya Maili Moja, dereva wa bus atatoa fedha na kumpa kijana (wakala) atangulize kwa askari Maili Moja ili asibughudhiwe kwenye ukaguzi, na kama siku hiyo kuna askari mtata basi abiria hao wanahamishiwa kwenye taxi au bus jingine dogo wanatangulizwa mbele ambako bus litawakuta na kuwapakia tena, bus hilo likifika Ruvu JKT pub kuna askari pale wanapewa chao kisha linaendelea na safari, bus likifika Ruvu darajani abiria wanapakiwa kwenye pikipiki watangulie baada ya mizani ili kukwepa uzito wa bus kusomeka umezidi kwenye mizani, bus litawachukua abiria hao baada ya kuvuka mizani ya vugwaza ambapo hapo napo kuna askari wa kikosi hicho, nadhani napo pale askari na madereva wanajuana kwa vilemba vyao, bus litaendelea na safari mpaka njiapanda ya JK Msolwa, napo askari wanajifanya wanakagua lakini kwa kupita upande wa dereva na kupenda mikono kisha bus linaendelea na safari.
Tunaona waziwazi yanayofanywa na askari wa kikosi hicho na kujiuliza maswali mengi;
Wanafanya kwa maslahi ya kwao binafsi?
Wanatumwa na kiongozi wao kukusanya pesa kwa maslahi ya viongozi?
Au wanacheza igizo kumridhisha Rais kuwa wapo kazini kumbe wana agenda yao?
Binafsi naona askari wengi kwenye hizo check points wapo kibiashara zaidi, naomba Mkuu wa kikosi hicho ajitokeze hadharani aonyeshe mikanda ya usalama wanayojifunga wale abiria wanaokaa juu ya mfuniko wa injini na kusimama mlangoni kwenye mabasi huku askari wake wakiyatazama yanapita wakati askari hao ndiyo waliotangaza kila abiria afunge mikanda ya usalama.
sio vizuri dereva kuitwa shetaniHii kwetu sote ni hatari kubwa sana.